Magufuli, Pesa hizi zinatoka wapi?

Magufuli, Pesa hizi zinatoka wapi?

wewe unaamini matapeli wa kisiasa wa ccm hawana tofauti ni wale wale anaropoka tuu bajeti ilishapitishwa
 
Tuwe realistic na kuongea kwa figure labda itasaidia mjadala uwe na mshiko zaidi. Mleta mada ungeongea kwa takwimu ingekuwa rahisi kuchanganua na kupata majibu.

..je, watoto wa primary kuanzia std I-VII ni wangapi Tanzania?
..Gharama ya kusomesha mtoto mmoja kwa mwaka ni kiasi gani?
Then tutajua gharama halisi ya kusomesha watoto wa primary Tanzania.
Likewise tufanye kwa watoto wa f I-IV (waliopo boarding + day) ili tujue ni kiasi gani kwa watoto wote kuanzia std I hadi form IV wanahitaji kwa ajili ya tuition.

Mimi naona mleta mada umekuja blindly bila takwimu, ndio maana watu watakushambulia kwa sababu mada haijakamilika.
 
Nanona umeongelea negative Points, sasa unadhani angefanyeje ili elimu iwe bora? Je unfahmu badget ya elimu kwa mwezi hapa TZ? na je unafahamu incomes ya Tanzania kwa siku, chukulia tu hapo badari unadhani panapatikana kiasi gani kwa siku?
Ufisadi ukikomeshwa mambo mengi tu yatafunguka ingawa ni kazi ngumu sana.
Cha muhimu nikuona ahadi zake zitafika wapi. Ndio maana siasa si kama mpira ukiwa simba basi utakua simba milele hata kama wachezaji wakihama lakini siasa ni kitu kingine, Sera ndio zinazo fuatwa kama zinatekelezwa na pia kuangali uchapakizi wa huyo mtoa sera. Binafsi Magufuli nimemkubali lakini ningependa kuona viti vingi vya upinzani hapo bungeni.
Bahati mbaya sana unasahau hoja na kumtetea mtu. Sina tatizo na Magufuli, nina tatizo na utekelezaji ambao unaashiria kutofuata taratibu na kanuni za nchi. Ukipitia posts zangu hapo nyuma utaona nimeorodhesha vipaumbele vya nchi yetu. Kipaumbele kwenye bajeti ya sasa hivi si elimu bure kutoka nursery mpaka sekondari au chuo kikuu. Haya mambo yanahitaji mipango. Ahadi hii ni endelevu ambayo anatakiwa aitekeleze miaka yote atakapokuwa madarakani. Si barabara kama ukijenga na kumaliza gharama zimekwisha. Inahitaji wadau wa elimu waweze kutambua mahitaji halisi ni kiasi gani. Tukumbuke shule zinatofautiana Kijiografia na kimahitaji pia. Wengine wanapata maji ya bomba na wengine hawapati. Maji yatawafikia vipi kama watapewa bajeti yenye kufanana. Lini amefanya uchambuzi? Amefuta ada peke yake au na michango? Ninafaham kipato cha nchi na bajeti ya elimu naifaham fika. Kufanya maamuzi kwa kukurupuka kutatugharimu. Hata kama tulimchagua tusiogope kuongea yale yenye kuitakia nchi yetu mema.
 
ukweli ni kwamba watanzania wengi hatufatilii vitu hii sera ya elimu bure ilishapitishwa mda mrefu na kuingizwa katika sera ya elimu ya mwaka 2014 iliyotolewa mwaka jana kabla ya hapo shule ya msingi ilikua bure na mimi nimesoma bure na ndo maana Mr President analisema hilo kwa kujiamini........still loading elimu kutolewa bure mpaka chuo kikuu haikuwa rahisi kama Waziri Mkuu Mstaafu/mgombea kupitia ukawa Edward Lowassa alivyokua ana ahidi elimu bure mpaka chuo kikuu
Inawezekana ndio lakini inahitaji ifanyike kwa hatua.
Tusubiri na kila mmoja afanye kazi katika nafasi yake tujenge nchi yetu kwa pamoja
Tanzania ni kubwa kuliko vyama vyetu na itikadi zetu
KwaPamojaTunaweza #HapaKaziTu
 
Hapo nime mention short term na long term solutions kwa faida ya wengine.Ila naomba tumuachie,kwa kuwa sisi hatuko kwenye chungu.Ila nikuhakishishie kwamba kwenye short term solutions peke yake tutapata pesa nzuri tu.

Hata hivyo labda na washauri wake walipo-spread costs over four quaters,wameona they can manage with what they will get and what they have, kwa kuwa tunatumia a quarter system, hulipi kila kitu mara moja kama nilivyo kwisha sema.

Rais ana nia nzuri,lets be patient and see what he can do.At most tumtie moyo.

Hatuwezi kuendelea kuishi kwa dhana ya CCM ni ile ile. Tunataka namba safari hii. Hicho ni kiashiria cha kuzidi kuiboronga elimu. Cha kushangaza wadau wa elimu wamefumba macho. Hawaulizi hii kauli inakwenda mpaka wapi na pia pesa zitatoka wapi na kugawanywa namna gani. Ni miezi miwili kufika January 2016. Kuandaa mfumo na utaratibu wa kuzifikia shule zote nchi hii ni kitu kisichowezekana. Utafika mwezi January tutasoma malalamiko mengi kutoka katika shule mbalimbali. Utekelezaji wa sera yoyote unahitaji mipango thabiti.
 
kuna watu hawana kumbukumbu kabisa, sijui akili yao ikoje? mara hii mmesahau kuwa bajeti ya 2015/16 wizara ya elimu ilisema shule ya msingi hadi sekondari bure? rejea kwenye kumbukumbu za bunge na wizara ya elimu utapata majibu yote hayo.
 
kuna watu hawana kumbukumbu kabisa, sijui akili yao ikoje? mara hii mmesahau kuwa bajeti ya 2015/16 wizara ya elimu ilisema shule ya msingi hadi sekondari bure? rejea kwenye kumbukumbu za bunge na wizara ya elimu utapata majibu yote hayo.

ni wachache sana wenye uwezo wa kukumbuka na kufatilia vitu ndio maana wanakaa kutia soga badala ya kufanya kazi hiyo sera ya elimu bure ilikua inasubiri tu mda lakni ilikuwepo.....
 
Tatizo la vijana wa leo wanasoma kava la kitabu na kudhani wamemaliza kitabu chote. Hela ndani ya nchi yetu si tatizo....bali tatizo lilikuwa usimamizi wa rasilimali tulizo nazo. Hauhitaji kuwaza au kufikiria sana km mnywa viroba kuhusu gharama za kuwezesha alichokisema mh. Dr JPM
 
Pamoja na vyanzo, issue hapa siyo karo! Michango, michango, michango! Atuambie amefuta michango na karo!
 
Si ameshafuta Safari zote za nje! Makongamano! Think this despot J kikwete used 50 million USD by only himself plying the world; doing his business! The money is enough to educate our boys and girls!!

By the way Mr. JPM remove this ambassador at the Beijing Embassy!

Magufuli alikuwa mwamasishaji Mkuu Wa JK kwenda kuomba nje barabara zitengenezwe na alijisifia kwa hilo,na kumshauri JK asiache kufanya safari kwani safari hizo zina faida kubwa hata wapinzani wanapata sehemu nzuri ya kufanya maandamano,huku kukurupuka kutatuumiza wengi
 
kuna watu hawana kumbukumbu kabisa, sijui akili yao ikoje? mara hii mmesahau kuwa bajeti ya 2015/16 wizara ya elimu ilisema shule ya msingi hadi sekondari bure? rejea kwenye kumbukumbu za bunge na wizara ya elimu utapata majibu yote hayo.

Hapa kuna ishu umeiongeza. Kwahiyo unachosema magufuli alieleza kitu ambacho tayari kilikuwa kinatekelezwa na hizo ni kelele tu. Tuwekee bajeti ya Wizara ya Elimu na hii itatusaidia saana. Lakini kwa kukumbusha ni kwamba kwenye Hotuba ya Kikwete mwaka 2014 mwezi Desemba Kikwete alisema wamekamilisha sera ya Elimu na Elimu itakuwa bure kuanzia mwaka 2016. Ninakuwekea Sera ya Elimu ukipenda nitakupa na Hotuba ya Kikwete, tupitie na bajeti halafuu tuone tunasimama wapi. Km Magufuli si mkweli au amekurupuka
 
Mkuu acha dharau unauliza fedha zinatoka wapi?

Serikali ina vyanzo vingi vya pesa tofauti na tunavyoelewa sisi kwa hiyo kitu cha msingi hapo ni kupokea utekelezaji wa ahadi zake na usihoji fedha imetoka wapi unadhani itakuwa imetoka wapi?

Wakati wa kampeni alijua fedha zitatoka wapi na ndiyo maana alisema, Yule wa mazingaombwe ya kumaliza matembe nchi nzima naye alijua atapata wapi wakandarasi wa kujenga na kulipwa ili kumaliza matembe yote jamhuri nzima ya Tanzania.

Ushauri wangu tumhoji anaposhindwa kutekeleza ahadi na tusihoji anapotimiza ahadi.
 
Ame dist111 Rolandi BabuM hoja kuu hapa siyo wapi zitoka hizo hela bali mfumo wa kiserikali (Kama utafuatwa) fedha zote zinazotumika zinatakiwa ziwe zimepitishwa na Bunge wakati wa kikao chake cha Bajeti. Sasa kwenye Bunge la bajeti lililopita lilipitisha na bajeti hiyo ya kulipia ada wanafunzi watakao kuwa wanaingia kidato cha kwanza?

Chai itafutwa fedha zake ziende ELIMU BADO UNA SWALI?
 
Mkuu acha dharau unauliza fedha zinatoka wapi??????!!!!!!! Serikali ina vyanzo vingi vya pesa tofauti na tunavyoelewa sisi kwa hiyo kitu cha msingi hapo ni kupokea utekelezaji wa ahadi zake na usihoji fedha imetoka wapi unadhani itakuwa imetoka wapi?????? Wakati wa kampeni alijua fedha zitatoka wapi na ndiyo maana alisema, Yule wa mazingaombwe ya kumaliza matembe nchi nzima naye alijua atapata wapi wakandarasi wa kujenga na kulipwa ili kumaliza matembe yote jamhuri nzima ya Tanzania. Ushauri wangu tumhoji anaposhindwa kutekeleza ahadi na tusihoji anapotimiza ahadi.


Nchi ya bila kuhoji si nchi ya Kidemokrasia. Tunatambua Serikali ina vyanzo vingi na hivyo vyanzo vilishapangiwa matumizi na Bunge tukufu la JMT. Wakati wa Kampeni si wakati wa utekelezaji. Kutekeleza ni suala jema, atuambie anatoa hizo fedha kwenye mipango ipi? Na kama anasema anatoa kwenye kubana matumizi atuambie atabana matumizi kwa kiasi na kiasi gani kitapatikana. Lakini kumbuka kuandaa mfumo wa makusanyo na kusambaza pesa kwenye shule zote ndani ya miezi miwili, inawezekana? Halafu deni lililoachwa na watangulizi wake si deni la familia za watangulizi bali ni deni la Watanzania. Lazima tulipe ili tuweze kukopesheka. Tunazitengenezea shule matatizo ifikapo mwezi January.
 
Nchi ya bila kuhoji si nchi ya Kidemokrasia. Tunatambua Serikali ina vyanzo vingi na hivyo vyanzo vilishapangiwa matumizi na Bunge tukufu la JMT. Wakati wa Kampeni si wakati wa utekelezaji. Kutekeleza ni suala jema, atuambie anatoa hizo fedha kwenye mipango ipi? Na kama anasema anatoa kwenye kubana matumizi atuambie atabana matumizi kwa kiasi na kiasi gani kitapatikana. Lakini kumbuka kuandaa mfumo wa makusanyo na kusambaza pesa kwenye shule zote ndani ya miezi miwili, inawezekana? Halafu deni lililoachwa na watangulizi wake si deni la familia za watangulizi bali ni deni la Watanzania. Lazima tulipe ili tuweze kukopesheka. Tunazitengenezea shule matatizo ifikapo mwezi January.

Mkuu shule haiwezi kuendeshwa kwa ada ya 20, 000/= hata kama zitalipwa kama unavyotaka, bado serikali ilikuwa inatuma fedha kwa ajili ya uendeshaji wa shule kama huamini naomba umuulize headmaster wa shule iliyoko jirani yako hasa yule mwenye ndevu nyingi atakupa ufafanuzi A level nako ilkuwa 70,000/= lakini michango kibao kwahiyo ada itafutwa michango iko palepale ambayo kwa mwanafunzi wa A level inafikia laki sita mpaka saba upo hapo???? Kama hilo hulijui tuulize sisi tunaosomesha tutakuambia na mfano wa hiyo shule nenda SENGEREMA SEC SCHOOL HUO NI MFANO WA SHULE ZOTE ZA SERIKALI ADA NI NDOGO SANA ILA MAHITAJI YA MWANAFUNZI UTAKOMA NI BORA ULIPE ADA MAHITAJI YA MWANAFUNZI WAKULIPIE.
 
Kwa mimi ninavyojua wanasiasa wa nchi zilizoendelea wakitoa ahadi kama hii hutimizwa ila inapangiwa mkakati kama elimu bure chama kilichoshinda 2015 hiyo system ingeanza labda 2018 baada ya kujipanga na kuwekea bajeti ya kutosha
 

Mkuu shule haiwezi kuendeshwa kwa ada ya 20, 000/= hata kama zitalipwa kama unavyotaka, bado serikali ilikuwa inatuma fedha kwa ajili ya uendeshaji wa shule kama huamini naomba umuulize headmaster wa shule iliyoko jirani yako hasa yule mwenye ndevu nyingi atakupa ufafanuzi A level nako ilkuwa 70,000/= lakini michango kibao kwahiyo ada itafutwa michango iko palepale ambayo kwa mwanafunzi wa A level inafikia laki sita mpaka saba upo hapo???? Kama hilo hulijui tuulize sisi tunaosomesha tutakuambia na mfano wa hiyo shule nenda SENGEREMA SEC SCHOOL HUO NI MFANO WA SHULE ZOTE ZA SERIKALI ADA NI NDOGO SANA ILA MAHITAJI YA MWANAFUNZI UTAKOMA NI BORA ULIPE ADA MAHITAJI YA MWANAFUNZI WAKULIPIE.

Ni kweli serikali ilikuwa inatoa fedha na kila mtu anafaham pesa hiyo haitoshi. Lakini kwa mujibu wa kitabu cha sera ya Elimu, wanafunzi wa Sekondari walioandikishwa wanafikia takribani 2,000,000. Okay zidisha na elfu 20. Unapata 40,000,000,000. Ni bilioni 40. Kuna wale wa A-level pia. Tunazungumzia zaidi bilioni 50. Pia kubwa zaidi itakuwa ni udanganyifu kufuta ada na kuacha michango nyingine. Lakini hili bado hajasema hizi pesa anazitoa wapi tukiwa tunamaliza nusu ya bajeti?
 
Si ameshafuta Safari zote za nje! Makongamano! Think this despot J kikwete used 50 million USD by only himself plying the world; doing his business! The money is enough to educate our boys and girls!!

By the way Mr. JPM remove this ambassador at the Beijing Embassy!
Mkuu why balozi wa Beijing hahhh? Anakula raha hatumikii wanaomlipa mshahara au?
Mkuu Raisi JPM akifuta swala la wabunge wa kuteuliwa na manaibu katibu ktk wizara na katibu wa kudumu
Wabunge wa kuteuliwa angelenga Walemavu Walimu Wauuguzi Vijana Watoto kila chama kitoe mwakalishi mmoja au wawili mchezo kwisha tutanufaika na kodi yetu huu utitiri wa wabunge wa kuchaguliwa na kuteuliwa unaifilisi nchi. Ama sivyo awaambie wabunge wa kuteuliwa wajitegemee kwa kila jambo tuone nani atabaki walipwe msharahara kwa mahudhurio bungeni nukta!
 
Back
Top Bottom