Magufuli, Pesa hizi zinatoka wapi?

Magufuli, Pesa hizi zinatoka wapi?

Tutaongeza kodi maana hakuna namna nyingine

Kwahiyo ndugu wananchi kazeni mikanda maana bei za bidhaa zinaweza kupanda maradufu

Natania tu jamani nikipata nauli nitakuja kukwambia fedha zitatoka wapi.
 
Si ameshafuta Safari zote za nje! Makongamano! Think this despot J kikwete used 50 million USD by only himself plying the world; doing his business! The money is enough to educate our boys and girls!!

By the way Mr. JPM remove this ambassador at the Beijing Embassy!

Pole woooote wenye imani na jpm????
 
Tusiongee kinadharia hapa, aseme gharama ya shule zote za serikali ni kiasi gani na kiasi anachotarajia kupata ni kiasi gani kutokana na kubana matumizi. Kufanya kazi kwa headlines hakutatusaidia.
Your a great thinker ?
 




kutakuwa hakuna misamaha ya kodi.. pesa zitapatikana huko...
safari za nje zimekatwa pesa zitapatikana...
tutakusanya marejesho ya mikopo kwa wanafunzi waliomaliza na kuanza kazi... pesa itapatikana

TULIENI DAWA IWAINGIE MIAKA 5 IJAYO NI KAZI TU
 
Kwani Lowasa pia si alisema hayo.. Yeye angezitoa wapi hizo hela??

Elimu ni kitu cha muhimu sana ndio maana leo hii w?tanzania wengi wanashabikia vyama vya siasa kama wanavyo shabikia mpira, Na hatuwezi kupata maendeleo kama hatuna elimu nzuri.
Afya pia ni muhimu sana kwani umaskini unasababishwa na magonja na kukosekana huduma nzuri mahospitalini. Ukiwa mgonjwa leo hii utamaliza akiba yote uliojiwekea na kurudi kwenye umaskini.

Hela zipo nyigi saaaana lakini asilikia kubwa zinaishia kwa mafisadi kwa hiyo kazi ya kwanza inabidi abane na kutokomeza ufisadi. Sasa ndio amenza kazi tuone.
Wakati wa Lowassa kujibu maswali haya umekwisha. Hatutekelezi sera zake. Tunatekeleza ilani ya CCM.
Elimu bora ni muhimu, lakini kufuta michango bila maelezo ya kina kwamba zile pesa walizokuwa wanachangia wanafunzi za Maabara nani atapeleka. Madawati na afya, je Magufuli kajipanga? Anatoa wapi? Huwezi kuleta hadithi ya kuwa watu wakakusanye pesa, wanaenda kukusanya wapi? Ni asilimia ngapi ya safari zitafutwa. Safari km za ofisi ya CAG kukagua balozi huwezi kufuta. Safari za UN na AU za kiusalama huwezi kufuta. Amefuta safari zipi? Hizi porojo za kwenye vyombo vya habari si mahitaji ya Watanzania
 
Suals la manunuzi ili lifanikiwe inatakiwa kubadili vipengele katika sheria ya manunuzi.kwani sheria tulizonazo zingine ni ' copy and paste' na zingine zinamwelekeo wa kifisadi.mfano manunuzi kwa sheria za Tanzania ,lazima kununua bidhaa na huduma kwa mtu wa kati.ikiwa idara au taasisi ya serikali inataka kununua magari au ndege inatakiwa kununua kutoka kwa agent(wakala),na sio kiwandani. Angalia karatasi inaweza kuwa shs.6'000/- kiwandani na wakala akawa anauzaTshs.10'000/-,bado taasisi inalazimika kununua kutoka kwa wakala.sheria hairuhusu kununua kiwandani.ukiangalia shetia za manunuzi zimefuata shetia za manunuzi za UN,au Worl Bank ambao huwa wanafanya hivi kwa manufaa ya USA.chukulia IRAQ tenda nyingi za ujenzi na huduma zilichukuliwa na makampuni !!!.
 
Pesa yenyewe usifikiri ni nyingi iliyokuwa inapatikana kama ada. Kumbuka kila mwanafunzi alikuwa analipa elfu 20 tu. Piga hesabu kama wanafunzi wako milioni moja kwa mwaka watalipa ngapi.

Kwahiyo Masolex analipa ile ada ya 20, 000 tu ile michango mingine ya madawati, mlinzi, maji, chakula, uniform, emergency ambayo ni zaidi ya 350, 000 tunalipa wenyewe.

CCM kweli ina wenyewe na nimeamini tutaisoma number
 
Mjomba yenu Mamvi Lowasa alipokuwa anawaingiza chaka kwamba elimu mpaka chuo kikuu bure mbona hamkuwahi kumuuliza hizo pesa atazitoa wapi?
Mwacheni Hon President afanye yake.

Mtoa mada amezingatia current budget. Hajasema kuwa haiwezekani. Kabla ya kujibu kiushabiki na kivyama zaidi soma content yote ya uzi. Mtoa mada anajua inawezekana elimu kuwa bure, lakini January ni almost miez miwili na hivyo bajeti kuu itakayohusika ni ile iliyopo. Nafikiri Mh Dr Magufuli, pamoja na kuahidi kwenye kampeni, angelianza jambo hili slowly angalau mwez July, wasiwasi asije akakwama kwenye mambo mengine!
 
Kuna umuhimu gani kuwa na vikao vya bajeti vya kupanga pesa za maendeleo na pesa za matumizi ya serikali?

Pesa za kulipia elimu ya bure amempa nani au ni mamlaka ipi imeidhinisha pesa hizo zitumike ?

Umeumia sana mme wako kufungiwa safari za nje😀😀
 
ukweli ni kwamba ada ikitolewa afu michango mingine ikabakizwa bado haijamsaidia mtanzania.
jiulize elfu 20 unajisifu umefuta ada? sekondari ni elfu 70 sasa michango mingine ndo ishu, ulinzi, mpishi, dawati, nk haya yanawkewaga ela kubwa kuliko ata ada yenyewe
 
Hapo nime mention short term na long term solutions kwa faida ya wengine.Ila naomba tumuachie,kwa kuwa sisi hatuko kwenye chungu.Ila nikuhakishishie kwamba kwenye short term solutions peke yake tutapata pesa nzuri tu.

Hata hivyo labda na washauri wake walipo-spread costs over four quaters,wameona they can manage with what they will get and what they have, kwa kuwa tunatumia a quarter system, hulipi kila kitu mara moja kama nilivyo kwisha sema.

Rais ana nia nzuri,lets be patient and see what he can do.At most tumtie moyo.
Naomba ieleweke sina tatizo kwa watoto kusoma bure. Hii ni November na January elimu ni bure. Hayo makusanyo yote uliyotaja mengine yanahitaji mipango na hata kubadilishwa kwa sheria. Mf suala la misamaha ya kodi. Tatizo amekurupuka kudhani ukiahidi leo lazima kesho uanze kutekeleza bila kujua pesa anatoa wapi. Unazungumzia madini, kuna kampuni zinatangaza kupunguza wafanyakazi kutokana na kupungua kwa bei ya dhahabu, kubuni vyanzo vipya; si suala la miezi miwili. Angekuja na hesabu hapa kwa hiyo mipango yake mipya atakusanya kiasi gani na mahitaji ya shule ni kiasi gani. Tumechoka kusikiliza porojo zisizokuwa na evidence. Hizi shule, mambo yatakuwa magumu zaidi. Hao walimu watapata hizo fedha kufidia umbwe litakalojitokeza?
 
UKAWA kweli wamechanganyikiwa na hawaamini kilichotokea! EL aliposema atatoa elimu ya bure toka chekechea hadi vyuo vikuu mbona hawakumuuliza hizo pesa atapata wapi?
 
pesa ipo.Kikwete tu safari za nje ametumia zaidi yq Trillion 4.5
 
Mjomba yenu Mamvi Lowasa alipokuwa anawaingiza chaka kwamba elimu mpaka chuo kikuu bure mbona hamkuwahi kumuuliza hizo pesa atazitoa wapi?
Mwacheni Hon President afanye yake.
Tuwe wakweli nchi ni ya kwetu na ccm ni ya kwangu na magufuli ni rahisi wetu mamvi alisema pesa itatokana na kuondoa safari za nje na kuondoa mashangingi/gari ambazo serikali inagharamia pesa ndefu.Leo tumeona raisi wetu anapita mulemule banyani mbaya lkn tukubali sisi tulikukuwa wa maisha club kidumu chama chetu.
 
Wakati wa Lowassa kujibu maswali haya umekwisha. Hatutekelezi sera zake. Tunatekeleza ilani ya CCM.
Elimu bora ni muhimu, lakini kufuta michango bila maelezo ya kina kwamba zile pesa walizokuwa wanachangia wanafunzi za Maabara nani atapeleka. Madawati na afya, je Magufuli kajipanga? Anatoa wapi? Huwezi kuleta hadithi ya kuwa watu wakakusanye pesa, wanaenda kukusanya wapi? Ni asilimia ngapi ya safari zitafutwa. Safari km za ofisi ya CAG kukagua balozi huwezi kufuta. Safari za UN na AU za kiusalama huwezi kufuta. Amefuta safari zipi? Hizi porojo za kwenye vyombo
vya habari si mahitaji ya Watanzania

Nanona umeongelea negative Points, sasa unadhani angefanyeje ili elimu iwe bora? Je unfahmu badget ya elimu kwa mwezi hapa TZ? na je unafahamu incomes ya Tanzania kwa siku, chukulia tu hapo badari unadhani panapatikana kiasi gani kwa siku?
Ufisadi ukikomeshwa mambo mengi tu yatafunguka ingawa ni kazi ngumu sana.
Cha muhimu nikuona ahadi zake zitafika wapi. Ndio maana siasa si kama mpira ukiwa simba basi utakua simba milele hata kama wachezaji wakihama lakini siasa ni kitu kingine, Sera ndio zinazo fuatwa kama zinatekelezwa na pia kuangali uchapakizi wa huyo mtoa sera. Binafsi Magufuli nimemkubali lakini ningependa kuona viti vingi vya upinzani hapo bungeni.
 
Back
Top Bottom