Magufuli, Pesa hizi zinatoka wapi?

Magufuli, Pesa hizi zinatoka wapi?

bnhai

JF-Expert Member
Joined
Jul 12, 2009
Posts
2,846
Reaction score
2,402
Mh Rais umetutangazia kuwa elimu itakuwa bure kuanzia January 2016. Lakini hujatueleza kuwa pesa hizo za elimu zinatoka sehemu gani katika bajeti yetu na ukizingatia Bunge lilishapitisha bajeti yetu. Je, zinapunguza pesa kutoka afya? Miundombinu au wapi?

Ni kweli umetoa ahadi nyingi za katika ilani ya CCM lakini utekelezaji wa "hapa kazi tu" bila mipango unaweza kuyumbisha maeneo mengine muhimu ya serikali.

Tafadhali angalia usikwame mapema kama vikao vya Ngurudoto.
 
Hujasikia ameamua kuwabana zaidi wafanyabiashara wakubwa plus kufuta safar za vigogo nje ya nchi! Wataka nn tena, kama amekulenga sema
 
Safari za nje na ile budget ya chai inatosha kabisa kulipia ada zote.

Akiongeza na kuondoa mashangingi yote, then posho ya vikao maana wahusika wanalipwa % zaidi kwenye mishahara yao plus misamaha ya kodi basi hadi lap top watanunuliwa ����
 
Na wewe naye si usubiri upate kushangaa uwa zipo na ujiulize kumbeeeee
 
Tusiongee kinadharia hapa, aseme gharama ya shule zote za serikali ni kiasi gani na kiasi anachotarajia kupata ni kiasi gani kutokana na kubana matumizi. Kufanya kazi kwa headlines hakutatusaidia.
 
Si ameshafuta Safari zote za nje! Makongamano! Think this despot J kikwete used 50 million USD by only himself plying the world; doing his business! The money is enough to educate our boys and girls!!

By the way Mr. JPM remove this ambassador at the Beijing Embassy!
 
Nchi ina pesa nyingi sana ila wachache walijitengenezea wigo kutumia sheria na kuwa exclude wananchi ili wao wajichotee kodi zetu.

Yeye anaifahamu serikali na njia zake zote za uchumi, tumpe tu muda tuone.
 
Pesa yenyewe usifikiri ni nyingi iliyokuwa inapatikana kama ada. Kumbuka kila mwanafunzi alikuwa analipa elfu 20 tu. Piga hesabu kama wanafunzi wako milioni moja kwa mwaka watalipa ngapi.
 
Mjomba yenu Mamvi Lowasa alipokuwa anawaingiza chaka kwamba elimu mpaka chuo kikuu bure mbona hamkuwahi kumuuliza hizo pesa atazitoa wapi?
Mwacheni Hon President afanye yake.
 
Ame dist111 Rolandi BabuM hoja kuu hapa siyo wapi zitoka hizo hela bali mfumo wa kiserikali (Kama utafuatwa) fedha zote zinazotumika zinatakiwa ziwe zimepitishwa na Bunge wakati wa kikao chake cha Bajeti. Sasa kwenye Bunge la bajeti lililopita lilipitisha na bajeti hiyo ya kulipia ada wanafunzi watakao kuwa wanaingia kidato cha kwanza?
 
Last edited by a moderator:
kwanza ada yenyewe ni shilingi 20000 kwa mwaka kwa sekondar za olevel na 70000 kwa wale wa a level...bado kiuhalisia ni gharama ndogo sana...kwa serikali na mbaya zaidi wanafunz hawa walikua hawailipi hii ada kwa wakat...hili linawezekana...ww unalipa ada ya secondary 5m feza boys ndio maana unaona ni gharama sana
 
Kama aatatekeleza hata 1/4 ya ahadi zake zote nchi itakua mbali sana na tutamuona mwanamume wa kweli.
 
Kwani Lowasa pia si alisema hayo.. Yeye angezitoa wapi hizo hela??

Elimu ni kitu cha muhimu sana ndio maana leo hii w?tanzania wengi wanashabikia vyama vya siasa kama wanavyo shabikia mpira, Na hatuwezi kupata maendeleo kama hatuna elimu nzuri.

Afya pia ni muhimu sana kwani umaskini unasababishwa na magonja na kukosekana huduma nzuri mahospitalini. Ukiwa mgonjwa leo hii utamaliza akiba yote uliojiwekea na kurudi kwenye umaskini.

Hela zipo nyigi saaaana lakini asilikia kubwa zinaishia kwa mafisadi kwa hiyo kazi ya kwanza inabidi abane na kutokomeza ufisadi. Sasa ndio amenza kazi tuone.
 
Binafsi nahisi hayo maswali yangemuhusu zaidi yule aliyetaka Elimu iwe bure kuanzia chekechea hadi Chuo Kikuu kitu ambacho hata marekani haifanyi
Kwa hili la Pesa kwa mtazamo wangu ni kama tayari lilisha fikia mwisho anachofanya ni kula mkia tu..Sijui kama unajua ada ya mwanafunzi wa Sekondari wa bweni... tayari ni kidogo (kama 7%) ya gharama halisi
Mimi nafikiri tungemuomba hapa aangazie macho michango mingine...

Nikupe mfano rahisi;
Haya maposhoposho meeeengi yakitengenezewa mfumo rasmi nakuingizwa kwenye mishahara, yatawafikia watu wengi zaidi na serikali itakusanya mabilioni ya paye na pia kuongeza ufanisi kwani mishahara itapanda kwa bajeti ilele...

Ni swala la kuamua tu...hela zipo ni kuziwekea tu utaratibu....
 
Unafuta elfu 20 mwanafunzi analipa Tuition laki 3 kwa mwaka.Mdanganyika ni mdanganyika tu
 
Back
Top Bottom