Magufuli bila madaraka yukoje?

Magufuli bila madaraka yukoje?

Wakati naandika makala ambayo itatoka kwenye gazeti moja la leo kuhusu Magufuli na kwanini hana chaguo jingine lolote isipokuwa kujiuzulu nilijadiliana na ndugu yangu mmoja na tukajikuta tunakabiliwa na swali ambalo hatukuweza kulipatia jibu: Hivi nje ya madaraka Dr. Magufuli anaweza kukumbukwa vipi katika kusimamia sheria nchini na kupigania maslahi ya wananchi?

Hapa sizungumzii mambo ambayo alikuwa anauliza kama mbunge kwa ajili ya jimbo lake tu nazungumzia kitaifa ana jambo lolote ambalo tunaweza kusema alilisimamia kitaifa nje ya yale ambayo amewahi kuyafanya akiwa na madaraka?

Yawezekana ujasiri wa Magufuli hautokani na msimamo au mtazamo uliosahihi bali unatokana na kuwa na madaraka kwamba kwake madaraka na siyo kanuni ya kuongozwa na uadilifu ni chombo kwake cha kutimiza mambo mbalimbali?

Je amewahi kusimama akiwa Mbunge kuhoji na kutaja uwajibikaji wa serikali kwenye jambo gani ambalo lilikuwa na taswira au matokeo ya kitaifa?

Ni wazi kwamba amekuwa Waziri toka wakati wa Mkapa na wakati wote wa Kikwete yawezekana madaraka yamemjengea pazia ambalo ni kwa hilo tu anaweza kuonekana? Je Magufuli bila ya madaraka ni nani? Bila kuwa na cheo - yaani akiwa Mbunge wa kawaida anaweza kupigania sheria isimamiwe Bungeni bila kucompromise? Je akiwa MBunge wa kawaida yuko tayari kubanwa na mawaziri na wabunge wengine?

Katika kujitahidi kupata majibu binafsi nilifikia mahitimisho yafuatayo - mengine nimeandika kwenye makala hiyo:

a. Dr. Magufulu hawezi kuwa mpiganaji wa raslimali za taifa bila ya madaraka. Madaraka ni kinga kwake ya kuweza kufanya mambo mbalimbali.

b. Dr. Magufuli hana historia ya kujivunia ya kujitofautisha kuwa ni mtetezi wa raslimali za wananchi nje ya ofisi yake. Kwa kiasi kikubwa anakumbukwa kwa mamboa ambayo yamemjengea sifa ya kuwa ni "askari wa mwamvuli" wakati wa Mkapa lakini bila kuwa na uwaziri ni mtu ambaye yuko very docile.

Haya mawili yanajibu maswali mawili - kwa uzuri na kwa ubaya:

a. Itakuwa vigumu sana kwa Magufuli kujiuzulu on principle hasa baada ya kutofautiana na RAis na Waziri Mkuu wake na vile vile kwa viongozi hao wawili kuonesha wazi kuwa hawana imani na uwezo, nia na sababu ya maamuzi ya waziri wao. Kwa vile hawezi kukaa bila ya madaraka na kupigania anachoamini ataendelea kuwa waziri na tushangae akiwa mkimya mno kwani alichofanyiwa juzi si kidogo kwa kipimo chochote.

b. Endapo atakuja kutaka kupewa madaraka makubwa zaidi nchini; kuna watu wanaweza kujikuta wanakimbia nchi kwani ni wazi kuwa anaweza kutumia madaraka aliyonayo kufikitia masuluhisho ya mambo kadha wa kadha kuliko baadhi ya viongozi wengine ambao wamebakia kuja na sura za huruma na upole wakikwepa kusimamia sheria.

my two cents plus the other fifty
Kumbe ..................!!
 
Enzi za mwanakijiji hizo,pesa ni mwanaharamu sana.hata yuda alimsariti bwana yesu kwa vipande 30 tu.namkumbuka mwanakijiji kipindi kile namsoma kwenye Tanzania daima
 
"Kumkoma Nyani Giladi"......Hiyo ndiyo ilikuwa misemo yao lakini sasa inamrudia na yeye!
 
N
Wakati naandika makala ambayo itatoka kwenye gazeti moja la leo kuhusu Magufuli na kwanini hana chaguo jingine lolote isipokuwa kujiuzulu nilijadiliana na ndugu yangu mmoja na tukajikuta tunakabiliwa na swali ambalo hatukuweza kulipatia jibu: Hivi nje ya madaraka Dr. Magufuli anaweza kukumbukwa vipi katika kusimamia sheria nchini na kupigania maslahi ya wananchi?

Hapa sizungumzii mambo ambayo alikuwa anauliza kama mbunge kwa ajili ya jimbo lake tu nazungumzia kitaifa ana jambo lolote ambalo tunaweza kusema alilisimamia kitaifa nje ya yale ambayo amewahi kuyafanya akiwa na madaraka?

Yawezekana ujasiri wa Magufuli hautokani na msimamo au mtazamo uliosahihi bali unatokana na kuwa na madaraka kwamba kwake madaraka na siyo kanuni ya kuongozwa na uadilifu ni chombo kwake cha kutimiza mambo mbalimbali?

Je amewahi kusimama akiwa Mbunge kuhoji na kutaja uwajibikaji wa serikali kwenye jambo gani ambalo lilikuwa na taswira au matokeo ya kitaifa?

Ni wazi kwamba amekuwa Waziri toka wakati wa Mkapa na wakati wote wa Kikwete yawezekana madaraka yamemjengea pazia ambalo ni kwa hilo tu anaweza kuonekana? Je Magufuli bila ya madaraka ni nani? Bila kuwa na cheo - yaani akiwa Mbunge wa kawaida anaweza kupigania sheria isimamiwe Bungeni bila kucompromise? Je akiwa MBunge wa kawaida yuko tayari kubanwa na mawaziri na wabunge wengine?

Katika kujitahidi kupata majibu binafsi nilifikia mahitimisho yafuatayo - mengine nimeandika kwenye makala hiyo:

a. Dr. Magufulu hawezi kuwa mpiganaji wa raslimali za taifa bila ya madaraka. Madaraka ni kinga kwake ya kuweza kufanya mambo mbalimbali.

b. Dr. Magufuli hana historia ya kujivunia ya kujitofautisha kuwa ni mtetezi wa raslimali za wananchi nje ya ofisi yake. Kwa kiasi kikubwa anakumbukwa kwa mamboa ambayo yamemjengea sifa ya kuwa ni "askari wa mwamvuli" wakati wa Mkapa lakini bila kuwa na uwaziri ni mtu ambaye yuko very docile.

Haya mawili yanajibu maswali mawili - kwa uzuri na kwa ubaya:

a. Itakuwa vigumu sana kwa Magufuli kujiuzulu on principle hasa baada ya kutofautiana na RAis na Waziri Mkuu wake na vile vile kwa viongozi hao wawili kuonesha wazi kuwa hawana imani na uwezo, nia na sababu ya maamuzi ya waziri wao. Kwa vile hawezi kukaa bila ya madaraka na kupigania anachoamini ataendelea kuwa waziri na tushangae akiwa mkimya mno kwani alichofanyiwa juzi si kidogo kwa kipimo chochote.

b. Endapo atakuja kutaka kupewa madaraka makubwa zaidi nchini; kuna watu wanaweza kujikuta wanakimbia nchi kwani ni wazi kuwa anaweza kutumia madaraka aliyonayo kufikitia masuluhisho ya mambo kadha wa kadha kuliko baadhi ya viongozi wengine ambao wamebakia kuja na sura za huruma na upole wakikwepa kusimamia sheria.

my two cents plus the other fifty

Ni kweli kabisa! Rais Magufuli ni aina ya watu wachache wanoelewa ukubwa wa dhamana inayoendana na nafasi ya utendaji ya uteuzi au uchaguliwa. Kwa makala hii Mwanakijiji amenishangaza sana juu ya uwezo wake wa kuona kwa undani, na kuweza kupambanua kwa kina na usahihi uhalisia wa tabia ya kiongozi wetu wa awamu ya tano.

Who cant follow, cannot learn how to lead. Kitendo cha kutambua madaraka ya Rais na implications zake kulimsaidia kufanya uamuzi sahihi wa kutojiuzulu, ambayo ingehasisha hili tunalolizungumza sasa.

Kuna aina ya viongozi ambao wanatafuta nafasi za uongozi na wanapozipata wanashindwa kujua dhamana, na mamlaka yanayoambatana na nafasi hizo. Hao ni aina ya viongozi ambao utamsikia anailaumu serikali, bila kutambua kwamba yeye ni sehemu ya hiyo serikali, na uamuzi husika uko mikononi mwake, na unamuwezesha kuwa sehemu ya suluhisho na siyo muendelezo wa tatizo/changamoto zinazo wakabili aliojukumishwa kuwahudumia: Kwa sababu ya madaraka aliyopewa kwa mujibu wa sharia, kutokana na nafasi anayoishikilia, pia ndani ya mipaka na ukomo wa kiongozi anayemzidi au aliyemkasimisha madaraka husika

Aina ya watu kama Mh. Magufuli wana uwezo wa kutambua uzito wa madaraka wanayokabidhiwa, na uhalisi wa kisheria unaowathibitisha katika madaraka hayo. Kwa sababu hiyo, wana uwezo mkubwa sana wa kufanya mambo makubwa kupitia nafasi zao za uongozi, kwa kuwa wanajua kwa uhakika uwezo unaoendana na nafasi husika. Kwa mantiki hiyohiyo, watu wa aina hiyo wanajua kwa uhakika, kwamba mara nafasi zao za uongozi zinapokoma, na mamlaka na uwezo wa kuathiri mifumo ya Taasisi wanazoziongoza inafikia ukomo pia. Hivyo ni kwelii nje ya nafasi za madaraka utawakuta watu wa namna hii, wakijishughulisha na mambo ya kawaida tu, kwa kuwa wanajua hawana dhamana ya madaraka husika. Nchi ikimpata kiongozi wa aina hii, ambaye hana nia ya kujijengea himaya ya kiuchumi (Kwa sababu hana nia ya kujijengea mamlaka yanayotokana na nguvu binafsi za kiuchumi): Nchi hiyo inakwenda mbali na kwa haraka sana.

Historia ya nchi yetu itakapoandikwa, Rais Magufuli atakuwa na nafasi ya pekee sana kutokana na jinsi Mungu alivyomuumba. Na Mzee Mwanakijiji aliweza kuona au kuonyeshwa moja kwa moja essence ya kiongozi wetu huyu.

Mungu mlinde na kumbariki Rais JPM, Mungu ibariki Tanzania, na wale wote wenye mapenzi mema na Watanzania.

NB: Viongozi wanaoamini kwamba chimbuko la mamlaka yao ni uwezo wao binafsi wa kiuchumi, na siyo dhamana ya madaraka ya kisheria waliyonayo; mara zote huharibu. JPM anautambua uzito, mamlaka, na uwezo unaoambatana na madaraka. Ni very focused: Atafanikiwa!
 
Mzee Mwanakijiji alipokuwa ktk ubora wake Enzi hizo. .. alikuwa msemakweli daima
 
Tuangalie kwa ufupi. Huyu bwana alipoingia bungeni ulikuwa wakati wa Msekwa ambapo bunge lilikuwa mhuri tu na haikuwa rahisi sana kujua wapiganaji kwa uwazi hasa ukiwa ndani ya chama. Halafu akawa waziri jambo lililombana zaidi.

Kurudi kwake bungeni tena bila kupingwa ni ishara ya kuwa wapiga kura wake walikubali kazi yake, na hiyo inamjengea hoja kuwa japo si msemaji ni mtendaji. Kama ni kweli au si kweli wananchi wa Chato wanamajibu sahihi.

J.P Magufuli ni kiongozi ambaye ametuonyesha mengi yaliyowashinda wenzake.mambo. Anaifahamu vizuri kazi yake na yupo tayari kusimamia sheria zetu wenyewe hata kama ni za kurithi kutoka kwa mkoloni.
Kukubalika kwake kunatokana na kufuata kanuni, sheria na mipango. Kwanfano aliposimamia ujenzi wa bara bara, ile ni sehemu ya kutumia na kuendeleza rasilimali za taifa. Alipotuonyesha kuwa tumelala na watu wanavua samaki karibu na kigamboni alisimamia rasilimali za taifa.

J.P.M anaposema ujenzi haramu ndani ya hifadhi za bara bara anasimamia matumizi ya kile kidogo tulicho nacho kwa manufaa yetu sote,kwa kuzingatia sheria tulizozikubali sisi wenyewe na kumkabidhi azisimamie.

Kitendo cha viongozi wa juu kumsema mbele ya mikutano ni ukiukaji wa kanuni za uwajibikaji wa pamoja 'collective responsibility'. Sijui kama PM au Rais wameshindwa kuwasiliana naye faragha hadi kusimanga hadharani.

Viongozi wanajali kura zaidi na si sheria walizoapa kuzisimamia ' cheap popularity'. Utamaduni uliotufikisha mahali wizi, ubadhirifu na ufujaji ni sehemu ya uongozi.

La kushangaza,ni kitendo cha J.P kutojiuzulu. Kanuni za utawala bora zinasema kunapokuwa na tofauti za mitazamo wazi kiongozi anatakiwa ajiuzulu.
Magufuli anaweza kuwa kiongozi mzuri hata kama si msemaji wa wazi kama
mbunge, sijui anasubiri nini na kama anataka kuwa malaika ndani ya kundi la wahalifu.

Kiongozi anayeamini katika kanuni na sheria tunamhitaji katika nchi hii kwa sasa. Nchi yetu haihitaji kiongozi wa kuwafurahisha watu bali mwenye 'discipline, vision, goals and action'.
Mpwa kumbe una maono kiasi hiki.
 
Mzee Mwanakijiji alipokuwa ktk ubora wake Enzi hizo. .. alikuwa msemakweli daima
Kwa kweli huyu mtu ni hazina, kama wapinzani wangemsikiliza wangefika mbali mno. Ona alivyomuona Magu vizuri as mtendaji anaejua kusimamia kazi na majukumu aliyopewa. JPM sio mwanasiasa, sio mwanaharakati, sio mpiga dili bali ni mtu anayebebwa na kazi yake nzuri anayofanya kwa moyo wote.
 
vp ndugu, huku kumbukwa kwenye Ufalme? Endelea utakumbukwa kama wakina Taratibu. Changamkia fursa Mkuu.
 
Kiongozi anayeamini katika kanuni na sheria tunamhitaji katika nchi hii kwa sasa. Nchi yetu haihitaji kiongozi wa kuwafurahisha watu bali mwenye 'discipline, vision, goals and action'.
Hatimae tukampata, Allah alisikia kilio chako, pamoja sasa haupo upande wake
 
Mzee Mwanakijiji alipokuwa ktk ubora wake Enzi hizo. .. alikuwa msemakweli daima
Watu wa Chadema wanazani kusema ukweli ni kuwasema viongozi wa serikali ya CCM.. ila akiwasema wa upinzani inaonekana msaliti.. Ukweli ni ukweli hauna upinzani au CCM.. Sasa ukawa na vibaraka wao.. Wao wanaona ukiwasema serikali ya CCM NDIO UKWELI ILA UKIWA SEMA CHADEMA AU UPINZANI BASI MSALITI
 
Hawezi kujiuzulu kwa vile hajavunja sheria.

Wajiuzulu wale wasio na uthubutu wa kuifanyia jamii ya Wanzania chochote, hasa kwenye kutoa maamuzi magumu kama Mwakyembe na mawaziri wengine. Hawa wamewafanyia nini Watz tangu wachaguliwe hadi leo? au ndio mpaka wapewe order ya nini cha kufanya ndio wafanye? ili wasionekane wamekosea? Waoga?
kati ya mawaziri waliokuwa wanamsifu Kikwete ndani ya utawala wake yumo
 
b. Endapo atakuja kutaka kupewa madaraka makubwa zaidi nchini; kuna watu wanaweza kujikuta wanakimbia nchi kwani ni wazi kuwa anaweza kutumia madaraka aliyonayo kufikitia masuluhisho ya mambo kadha wa kadha kuliko baadhi ya viongozi wengine ambao wamebakia kuja na sura za huruma na upole wakikwepa kusimamia sheria.

my two cents plus the other fifty


Duh.. prophetic one might say...
 
Wakati naandika makala ambayo itatoka kwenye gazeti moja la leo kuhusu Magufuli na kwanini hana chaguo jingine lolote isipokuwa kujiuzulu nilijadiliana na ndugu yangu mmoja na tukajikuta tunakabiliwa na swali ambalo hatukuweza kulipatia jibu: Hivi nje ya madaraka Dr. Magufuli anaweza kukumbukwa vipi katika kusimamia sheria nchini na kupigania maslahi ya wananchi?

Hapa sizungumzii mambo ambayo alikuwa anauliza kama mbunge kwa ajili ya jimbo lake tu nazungumzia kitaifa ana jambo lolote ambalo tunaweza kusema alilisimamia kitaifa nje ya yale ambayo amewahi kuyafanya akiwa na madaraka?

Yawezekana ujasiri wa Magufuli hautokani na msimamo au mtazamo uliosahihi bali unatokana na kuwa na madaraka kwamba kwake madaraka na siyo kanuni ya kuongozwa na uadilifu ni chombo kwake cha kutimiza mambo mbalimbali?

Je amewahi kusimama akiwa Mbunge kuhoji na kutaja uwajibikaji wa serikali kwenye jambo gani ambalo lilikuwa na taswira au matokeo ya kitaifa?

Ni wazi kwamba amekuwa Waziri toka wakati wa Mkapa na wakati wote wa Kikwete yawezekana madaraka yamemjengea pazia ambalo ni kwa hilo tu anaweza kuonekana? Je Magufuli bila ya madaraka ni nani? Bila kuwa na cheo - yaani akiwa Mbunge wa kawaida anaweza kupigania sheria isimamiwe Bungeni bila kucompromise? Je akiwa MBunge wa kawaida yuko tayari kubanwa na mawaziri na wabunge wengine?

Katika kujitahidi kupata majibu binafsi nilifikia mahitimisho yafuatayo - mengine nimeandika kwenye makala hiyo:

a. Dr. Magufulu hawezi kuwa mpiganaji wa raslimali za taifa bila ya madaraka. Madaraka ni kinga kwake ya kuweza kufanya mambo mbalimbali.

b. Dr. Magufuli hana historia ya kujivunia ya kujitofautisha kuwa ni mtetezi wa raslimali za wananchi nje ya ofisi yake. Kwa kiasi kikubwa anakumbukwa kwa mamboa ambayo yamemjengea sifa ya kuwa ni "askari wa mwamvuli" wakati wa Mkapa lakini bila kuwa na uwaziri ni mtu ambaye yuko very docile.

Haya mawili yanajibu maswali mawili - kwa uzuri na kwa ubaya:

a. Itakuwa vigumu sana kwa Magufuli kujiuzulu on principle hasa baada ya kutofautiana na RAis na Waziri Mkuu wake na vile vile kwa viongozi hao wawili kuonesha wazi kuwa hawana imani na uwezo, nia na sababu ya maamuzi ya waziri wao. Kwa vile hawezi kukaa bila ya madaraka na kupigania anachoamini ataendelea kuwa waziri na tushangae akiwa mkimya mno kwani alichofanyiwa juzi si kidogo kwa kipimo chochote.

b. Endapo atakuja kutaka kupewa madaraka makubwa zaidi nchini; kuna watu wanaweza kujikuta wanakimbia nchi kwani ni wazi kuwa anaweza kutumia madaraka aliyonayo kufikitia masuluhisho ya mambo kadha wa kadha kuliko baadhi ya viongozi wengine ambao wamebakia kuja na sura za huruma na upole wakikwepa kusimamia sheria.

my two cents plus the other fifty
we we jamaa ni nabii
 
Back
Top Bottom