Magufuli bila madaraka yukoje?

Magufuli bila madaraka yukoje?

Let freedom reign!
By Mzee Mwanakijiji, February 1, 2017
My fellow citizens, let freedom reign, from the sparkling snow-capped mount Kilimanjaro, to the green valleys of Southern Highlands, from the golden sands of the coast of the Indian ocean to the praised shores of Lake Tanganyika!

Let Freedom Ring! May our nation dare to rise to be all it can be, may we as a people and as a nation ascend to the heights that our forebearers never dreamed of, may we build a nation that is freer, modern, and yet very African!

Yes, may we one day, pass to the next generation of Tanzanians, a nation that has finally taken its rightful place among the nations of the world!

If our esteemed leaders won't lead now to fulfill such an ambition of ours, they'll find themselves following later! For Freedom never ceases to ring!

Huwezi kuamini kwamba haya maandishi yalielekezwa kwa awamu ya tano chini ya Jakaya Mrisho Kikwete! Leo wakosoaji wananyanyaswa wazi wazi, Mzee Mwanakijiji anasifia uongozi, uhuru (freedom)...where art thou gone?
hasante sana mkuu.
 
/.
Mkuu , labda niongelee kwa nafsi yangu kuwa nipo na nafuatilia mjadala kila nikipata fursa

Levictus alitaka kujua kama niliyoandika 2011 bado nasimama nayo. Nimemjibu bandiko 237 nikimujumuisha mpwa wangu Judi wa Kishua

Nilisema hivi, tunahitaji nidhamu nchini na kwamba nidhamu inaanzia kwa mtu kwanza kabla ya kusambaa.

Nidhamu ni utartaibu unaofuatwa kwa kuzingatia taratibu.

Kuna tofauti ya nidhamu na woga. Ninasimama katika nidhamu kwani ndicho tunahitaji

Nikasema sote tunataka mapambano dhidi ya uovu na waouvu wanaoifasidi nchi

Nimerejea kwa hili kwasababu kuu moja.
Wapo wenzetu wanaoamini wale wanaosimamia nidhamu na mapambano ya ufisadi n.k.

Halafu wapo (nikiwemo) tunaoamini katika nidhamu na mapambano ya ufisadi kwa udhati, kwa nidhamu bila kupepesa macho, bila mahaba, bila kuonea au kuhurumia.

Nitoe mifano. Jana Rais alikuwa Unguja katika ziara inayosemwa ya kiserikali.
Wasoma risala walizungumzuia habari za CCM. Shughuli ilikuwa ya CCM kwa kila mantiki.

Sasa kama mikutano ya siasa imepigwa marufuku mbona huu wa ''ccm' umeruhusiwa?

Je, hapo kuna nidhamu ya kutekeleza yale yanayosemwa?
Wapo wapi wanaokemea maandamano na mikutano ya siasa?

Je, huo si uoga? Tofauti ya nidhamu na uoga ipo wapi?

La pili, tumesikia Rais akisema kitendo cha mtu fulani kukataa kutoa mkono kwa Rais wa Zanzibar asingeweza kusaini makaratasi ya mtu huyo kwenda kutibiwa.

Kwamba mzozo wa mambo yao binafsi unaingiaje katika haki zao kisheria

Aliyekataa kutoa mkono ana haki ya kufanya hivyo kama binadamu

Hakuna sheria ya nchi inayolazimisha wawili hao kupeana mikono kwa namna yoyote

Haki ya kutibiwa nje ni ya kisheria , si favor wala hisani.

Kama ni ku sign karatasi Rais wa ZNZ hana chaguo, ni wajibu wake kisheria na kikatiba
Ndivyo nidhamu inavyotaka, kwamba kuheshimu taratibu

Katika hali kama hii inawezekanaje kuwaambia wananchi kuhusu nidhamu ya kazi?

Hivi kuna karani gani atakayepeleka faili bila kuogopa kumuudhi Rais?

Je,atakuwa ametendewa haki? Je, karani atakuwa ametimiza wajibu wake kwa nidhamu?

Tunaposema kiongozi asimamie nidhamu tuna maana hiyo kuwa nidhamu kila eneo bila chuki , husda au upendeleo.

Ukiangalia Taifa kwanza, utaona sote tunazungumzia umuhimu wa nidhamu na mapambano ya ufisadi, ufujaji na wizi.

Ukiangalia kwa jicho la 'uchama' mahaba n.k. utaiona nidhamu kwa mtu, utaona mapambano ya ufisadi kwa mtu.

Utaweza ku trade nidhamu kwa woga. Utaufumbia macho ufisadi kwa kuuita ujasiriamali.

Nasimama na bandiko langu la 2011 kwa asilimia zote.
 
mlitakiwa kusoma bandiko hili la mwaka 2011 ili kumjua na kumuelewa magufuli

mwanakijiji ni nabii wa haya mambo

swala eti anamsifia magufuli ni kwa sababu , hakuna wa kusifiwa upinzani!!

mwanakijiji ni muumizwa wa kuondolewa kwa akina slaa,

mrudi nyuma angalieni mlianguakia wapi, mtalaumu sana. na the fact kuwa Magufuli ndio rais, mtaongea kwa kinyongo kila siku kwa miaka 10 ijayo!!!

badala ya kuweka hoja za msingi, hoja zenu ni kumshambulia na kurudi nyuma kufuatilia MKJJ alisema nini


tukirudia misimamo yetu ya nyuma, nani atapona humu??

tujadili hoja hasa kwa nyie wakongwe, heshima zenu za ukongwe na mawazo yenu yanahitajika sana

ila inabidi kuwa na uhuru wa mawazo, na uwezo wa kukataa hata unachokipenda, uwezo wa kukosoa hata pale utakapoona aibu, uhuru huu wengi wenu hamna!! hamuwezi kusifia wala kukosoa kwa akili huru, pasi kuongozwa na emotion na madonda ya moyoni ambayo ndio haya yanafanya ndugu mgombane na kutengeneza mipasuko

iko wapi JF ya kujadili hoja kwa hoja, pasi kutajana eti ulisema hivi jana, ulisema hivi juzi, unasema hivi leo....why??


tunaiharibu JF

Fact ni kuwa Magufuli kuna mazuri mengi anafanya! halina ubishi hili
Fact ni kuwa juzi alikosea kusema 'siasa hazitakiwi' hili nalo halina ubishi

Fact ni kuwa upinzani mpaka leo, hauna hoja ya kuisumbua serikali kwa mambo ya msingi ya kuleta maendeleo, akili hii...haiko upinzani, hamna, na haileti faida kwa mtanzania wa kawaida.

Fact ni kuwa kosa hili la Magu limewaamsham at least iobekane kuna uhai......ila mmesahau hamna la kusema, hamna hoja, msijifiche huko!

mbali ya hoja ya UKUTA hamna lingine lililo mioyoni mwa watu ambao wapinzani wanaweza kuisumbua serikali...hamna, hakuna, halipo na naona halitakuwepo

we need brain kwa wapinzani...zimepotea sana na hata wale niliowategemea kama akina zitto wote kimya!
 
Ahsante, nilikuwa nasubiri swali hili. Jibu ni yes nasimama na hayo niliyosema

Nikukumbushe msemo unaosema 'absolute power corrupts absolutely'

Kwa maana rahisi ya Kiswahili , nguvu zozote au nguvu za kiutawala, nguvu hizo huondoa uadilifu.

Je, tunahitaji kiongozi atakayeleta nidhamu, jibu ni yes
Tunahitaji kiongozi wa kupambana na uovu, wizi na ufisadi, jibu ni ndiyo

Nidhamu(discipline) huanza kwa mtu kabla ya kwenda nje. Nidhamu si woga au hofu, ni mpangilio, utaratibu, utii wa taratibu na kuzifanya kwa taratibu kwa kuzingatia utaratibu

Je, tuna nidhamu tunayohitaji, jibu ni hapana! Woga, kutisha, matumizi ya nguvu , matumizi mabaya ya nguvu (abuse of power) hayo si nidhamu. Tofauti ya nidhamu na woga au hofu ni nyembamba na mara nyingi watu hawawezi kutofautisha

Je, kuna mapambano ya uovu, yes yapo. Mapambano ya uovu ni across the board, kwamba hakuna anayepewa favor au kusalimika. Nidhamu ndiyo iongoze mapambano hayo bila kubagua au kuchagua nani mhalifu sana, nani mhalifu kidogo

Fisadi wa bilioni 36 na karushwa ka 5,000 huwezi kuweka katika madaraja. Mimba ni mimba tu hakuna ka mimba na li mimba.

Fisadi wa bilioni 36 anapoambia akamalizie kazi, huku fisadi wa mshahara hewa wa milioni 40 akiwekwa magereza, ni double standards na hiyo si nidhamu tunyaohitaji wala mapambano tunayotaka.

Kwanini tumefika hapo kinyume na matarajio tuliyoonyesha huko nyuma? Jibu ni rahisi absolute power corrupts absolutely na culture iliyojengeka ndani ya CCM miaka nenda rudi ya 'get away'

Ninasimama na kauli zangu 100% , sikubaliani na utekelezaji kwasababu haupo katika muktadha wa hoja yangu. Umekwenda kombo !

Judi wa Kishua mpwa nijaalie, za siku
I respect every line of your argument
 
Wakati naandika makala ambayo itatoka kwenye gazeti moja la leo kuhusu Magufuli na kwanini hana chaguo jingine lolote isipokuwa kujiuzulu nilijadiliana na ndugu yangu mmoja na tukajikuta tunakabiliwa na swali ambalo hatukuweza kulipatia jibu: Hivi nje ya madaraka Dr. Magufuli anaweza kukumbukwa vipi katika kusimamia sheria nchini na kupigania maslahi ya wananchi?

Hapa sizungumzii mambo ambayo alikuwa anauliza kama mbunge kwa ajili ya jimbo lake tu nazungumzia kitaifa ana jambo lolote ambalo tunaweza kusema alilisimamia kitaifa nje ya yale ambayo amewahi kuyafanya akiwa na madaraka?

Yawezekana ujasiri wa Magufuli hautokani na msimamo au mtazamo uliosahihi bali unatokana na kuwa na madaraka kwamba kwake madaraka na siyo kanuni ya kuongozwa na uadilifu ni chombo kwake cha kutimiza mambo mbalimbali?

Je amewahi kusimama akiwa Mbunge kuhoji na kutaja uwajibikaji wa serikali kwenye jambo gani ambalo lilikuwa na taswira au matokeo ya kitaifa?

Ni wazi kwamba amekuwa Waziri toka wakati wa Mkapa na wakati wote wa Kikwete yawezekana madaraka yamemjengea pazia ambalo ni kwa hilo tu anaweza kuonekana? Je Magufuli bila ya madaraka ni nani? Bila kuwa na cheo - yaani akiwa Mbunge wa kawaida anaweza kupigania sheria isimamiwe Bungeni bila kucompromise? Je akiwa MBunge wa kawaida yuko tayari kubanwa na mawaziri na wabunge wengine?

Katika kujitahidi kupata majibu binafsi nilifikia mahitimisho yafuatayo - mengine nimeandika kwenye makala hiyo:

a. Dr. Magufulu hawezi kuwa mpiganaji wa raslimali za taifa bila ya madaraka. Madaraka ni kinga kwake ya kuweza kufanya mambo mbalimbali.

b. Dr. Magufuli hana historia ya kujivunia ya kujitofautisha kuwa ni mtetezi wa raslimali za wananchi nje ya ofisi yake. Kwa kiasi kikubwa anakumbukwa kwa mamboa ambayo yamemjengea sifa ya kuwa ni "askari wa mwamvuli" wakati wa Mkapa lakini bila kuwa na uwaziri ni mtu ambaye yuko very docile.

Haya mawili yanajibu maswali mawili - kwa uzuri na kwa ubaya:

a. Itakuwa vigumu sana kwa Magufuli kujiuzulu on principle hasa baada ya kutofautiana na RAis na Waziri Mkuu wake na vile vile kwa viongozi hao wawili kuonesha wazi kuwa hawana imani na uwezo, nia na sababu ya maamuzi ya waziri wao. Kwa vile hawezi kukaa bila ya madaraka na kupigania anachoamini ataendelea kuwa waziri na tushangae akiwa mkimya mno kwani alichofanyiwa juzi si kidogo kwa kipimo chochote.

b. Endapo atakuja kutaka kupewa madaraka makubwa zaidi nchini; kuna watu wanaweza kujikuta wanakimbia nchi kwani ni wazi kuwa anaweza kutumia madaraka aliyonayo kufikitia masuluhisho ya mambo kadha wa kadha kuliko baadhi ya viongozi wengine ambao wamebakia kuja na sura za huruma na upole wakikwepa kusimamia sheria.

my two cents plus the other fifty
Shikamoo MM.
Hii uliandika miaka 6 iliyopita, Kweli una maono
 
mlitakiwa kusoma bandiko hili la mwaka 2011 ili kumjua na mumuelewa magufuli

mwanakijiji ni nabii wa haya mambo

swala eti anamsifia magufuli ni kwa sababu , hakuna wa kusifiwa upinzani!!

mwanakijiji ni muumizwa wa kuondolewa kwa akina slaa,

mrudi nyuma angalieni mlianguakia wapi, mtalaumu sana. na the fact kuwa Magufuli ndio rais, mtaongea kwa kinyongo kila siku kwa miaka 10 ijayo!!!

badala ya kuweka hoja za msingi, hoja zenu ni kumshambulia na kurudi nyuma kufuatilia MKJJ alisema nini


tukirudia misimamo yetu ya nyuma, nani atapona humu??

tujadili hoja hasa kwa nyie wakongwe, heshima zenu za ukongwe na mawazo yenu yanahitajika sana

ila inabidi kuwa na uhuru wa mawazo, na uwezo wa kukataa hata unachokipenda, uwezo wa kukosoa hata pale utakapoona aibu, uhuru huu wengi wenu hamna!! hamuwezi kusifia wala kukosoa kwa akili huru, pasi kuongozwa na emotion na madonda ya moyoni ambayo ndio haya yanafanya ndugu mgombane na kutengeneza mipasuko

iko wapi JF ya kujadili hoja kwa hoja, pasi kutajana eti ulisema hivi jana, ulisema hivi juzi, unasema hivi leo....why??


tunaiharibu JF

Fact ni kuwa Magufuli kuna mazuri mengi anafanya! halina ubishi hili
Fact ni kuwa juzi alikosea kusema 'siasa hazitakiwi' hili nalo halina ubishi

Fact ni kuwa upinzani mpaka leo, hauna hoja ya kuisumbua serikali kwa mambo ya msingi ya kuleta maendeleo, akili hii...haiko upinzani, hamna, na haileti faida kwa mtanzania wa kawaida.

Fact ni kuwa kosa hili la Magu limewaamsham at least iobekane kuna uhai......ila mmesahau hamna la kusema, hamna hoja, msijifiche huko!

mbali ya hoja ya UKUTA hamna lingine lililo mioyoni mwa watu ambao wapinzani wanaweza kuisumbua serikali...hamna, hakuna, halipo na naona halitakuwepo

we need brain kwa wapinzani...zimepotea sana na hata wale niliowategemea kama akina zitto wote kimya!
Umeongea fact sana!
Kiukweli sio JF tu, social media imeshindwa kujenga viongozi wetu. Wengi tumetumia vibaya nafasi Hii ku-bully others na kufanya intimidation au assassination ya sifa za watu hasa viongozi.
Kuna sehemu nyingi JPM na viongozi wetu wengine wameteleza, kama binadamu wanayajua hayo tena baada ya kusoma reactions za watu au feedback kwa njia nyingine zozote.
Shida ipo kwa watu wanao-abuse nafasi Hii kwa kutaka kumtishia kiongozi, unapomuwekea conditions au ultimatum, kwamba he was suppose kufanya hivi, au mtoe x, etc.
Bullying kwa kiongozi wa juu kabisa wa Nchi ni kukaribisha trouble, he will never bend na sote tunakuwa losers.
Nadhani JF inapaswa Kurudi kwenye level yake ya kuanalyse issues na kuwekea mizania ili actors angalau wajisahihishe! maana what is the use ya kufanya hiki kuwa ni kijiwe cha kutusi au kushambulia viongozi au watu wengine!
 
Mwanakijiji wa wakati aliyetumia mali na muda wake mwingi kuandika article zilizotulia sana na kupendwa na Watanzania wengi waliobahatika kuzisoma kabla hajaamua kuhamisha goli.

Duh.. na wewe inaonekana umesoma kichwa cha habari tu; kinyume na mliobadilika sisi wengine kanuni zinatukataza kubadilika!
 
Wakati naandika makala ambayo itatoka kwenye gazeti moja la leo kuhusu Magufuli na kwanini hana chaguo jingine lolote isipokuwa kujiuzulu nilijadiliana na ndugu yangu mmoja na tukajikuta tunakabiliwa na swali ambalo hatukuweza kulipatia jibu: Hivi nje ya madaraka Dr. Magufuli anaweza kukumbukwa vipi katika kusimamia sheria nchini na kupigania maslahi ya wananchi?

Hapa sizungumzii mambo ambayo alikuwa anauliza kama mbunge kwa ajili ya jimbo lake tu nazungumzia kitaifa ana jambo lolote ambalo tunaweza kusema alilisimamia kitaifa nje ya yale ambayo amewahi kuyafanya akiwa na madaraka?

Yawezekana ujasiri wa Magufuli hautokani na msimamo au mtazamo uliosahihi bali unatokana na kuwa na madaraka kwamba kwake madaraka na siyo kanuni ya kuongozwa na uadilifu ni chombo kwake cha kutimiza mambo mbalimbali?

Je amewahi kusimama akiwa Mbunge kuhoji na kutaja uwajibikaji wa serikali kwenye jambo gani ambalo lilikuwa na taswira au matokeo ya kitaifa?

Ni wazi kwamba amekuwa Waziri toka wakati wa Mkapa na wakati wote wa Kikwete yawezekana madaraka yamemjengea pazia ambalo ni kwa hilo tu anaweza kuonekana? Je Magufuli bila ya madaraka ni nani? Bila kuwa na cheo - yaani akiwa Mbunge wa kawaida anaweza kupigania sheria isimamiwe Bungeni bila kucompromise? Je akiwa MBunge wa kawaida yuko tayari kubanwa na mawaziri na wabunge wengine?

Katika kujitahidi kupata majibu binafsi nilifikia mahitimisho yafuatayo - mengine nimeandika kwenye makala hiyo:

a. Dr. Magufulu hawezi kuwa mpiganaji wa raslimali za taifa bila ya madaraka. Madaraka ni kinga kwake ya kuweza kufanya mambo mbalimbali.

b. Dr. Magufuli hana historia ya kujivunia ya kujitofautisha kuwa ni mtetezi wa raslimali za wananchi nje ya ofisi yake. Kwa kiasi kikubwa anakumbukwa kwa mamboa ambayo yamemjengea sifa ya kuwa ni "askari wa mwamvuli" wakati wa Mkapa lakini bila kuwa na uwaziri ni mtu ambaye yuko very docile.

Haya mawili yanajibu maswali mawili - kwa uzuri na kwa ubaya:

a. Itakuwa vigumu sana kwa Magufuli kujiuzulu on principle hasa baada ya kutofautiana na RAis na Waziri Mkuu wake na vile vile kwa viongozi hao wawili kuonesha wazi kuwa hawana imani na uwezo, nia na sababu ya maamuzi ya waziri wao. Kwa vile hawezi kukaa bila ya madaraka na kupigania anachoamini ataendelea kuwa waziri na tushangae akiwa mkimya mno kwani alichofanyiwa juzi si kidogo kwa kipimo chochote.

b. Endapo atakuja kutaka kupewa madaraka makubwa zaidi nchini; kuna watu wanaweza kujikuta wanakimbia nchi kwani ni wazi kuwa anaweza kutumia madaraka aliyonayo kufikitia masuluhisho ya mambo kadha wa kadha kuliko baadhi ya viongozi wengine ambao wamebakia kuja na sura za huruma na upole wakikwepa kusimamia sheria.

my two cents plus the other fifty
watu mnaona mbali
 
Sijawahi kubadilika kuhusu fisadi yoyote nchi hii na wala sina sababu ya kufanya hivyo ila wewe wanaokufahamu na mabandiko yako wanakushangaa sana.

Duh.. na wewe inaonekana umesoma kichwa cha habari tu; kinyume na mliobadilika sisi wengine kanuni zinatukataza kubadilika!
 
Kwa CCM uongozi sio utumishi bali ni ajila, sasa mnapotegemea magufuri ajiuzulu mimi nawashangaa, mtu kutoka CCM atajiuzulu tu pale atakapokumbwa na kashfa kubwa na shinikizo la umma kuwa kubwa, hapo ndipo unapoweza kusikia kiongozi kutoka CCM anajiuzulu na si vinginevyo, CCM ingekuwa kwao uongozi ni utumishi basi hata Mkwere hasingegombea hii term ya pili ili aangalie afya yake kwanza maana ni mgonjwa, na hilo haliitaji vipimo vya maabara, kwa macho tu anaoneka afya iko mushkeli licha ya kunywa kikombe kwa babu Loliondo.
Dah hahaha vipi bado mgonjwa au macho hayaoni tena
 
Back
Top Bottom