Magufuli bado hajanishawishi

Magufuli bado hajanishawishi

WanaJF,

Kwaa muda wa siku kama 24 sasa tangu rais atembelee wizara ya fedha na baadae Mhimbili. Na shughuli hii ya bandari watanzania wengi wamepofuka macho na hawataki kabisa uhoji chochote kuhusu rais au maamuzi yake kana kwamba mheshimiwa rais amekuwa Mungu.

Leo hii kwenye uzi wa mtu fulani nimetoa maoni yangu kuwa Matumizi ya fedha za umma bila kufuata sheria ya manunuzi ni upendeleo kwa kampuni husika na uvunjifu washeria. Watu wameniwakia mbaya.

Sasa nimeanzisha uzi huu ili tuwekane sawa na mnaotapika tapikeni.

Barabara hii ya Mwenge - Morocco, mimi najua ilishafanyiwa usanifu na upembuzi yakinifu muda mrefu. Na mwaka jana wajapan kupitia shirika lao la JICA walionyesha interest ya kughalimia ujenzi huu na hivyo wakatoa hela, kuhuisha (update the ESIA and RAP) na tulitegemea mwaka huu ujenzi uanze. Je mpango huo wa ufadhili wa JICA ulikuwa wa update ya study tu? Na kama ilikuwa na ujenzi pia mpango huo umefutwaje?

Suala la pili, huyu mkandarasi anayejenga amepataje kazi? Tuelekezane vizuri.

Sheria ya manunuzi ya umma inasemaje kuhusu manunuzi ya kiwango hiki cha pesa 4 billion.

sheria inaongelea mchakato,mchakato mchakato, tumechoshwa na michakato inayotumia fedha. Moja ya vitengo tunavyotaka vifutwe ni hiki cha manunuzi!Barabara kasanifu engineer then wewe sio hata engineer ndio unafanya mauzo na manunuzi ya kazi ya kihandisi upuuzi mtupu. mwisho wa michakato tutaenda kisayansi
 
Kungekuwa na pesa, barabara ingekuwa imeishajengwa muda mrefu. Maana ni kwamba kila kitru kilikuwa tayari kasoro pesa tu.
 
Kwani humjui mh.magufuri?kazi zake ni za kutotumia akiri na anataka kufanya jambo kwa asila sana mwisho wa kazi unakuta kila kitu ni kibovu.si unaona swala la barabara.


swissme

LUWASSA! LUWASSA! nakupenda kwa moyo wote! UTAJIBEBA KATIKA MIAKA 5 IJAYO!
 
Nikiri kwamba kaanza vizuri sana lakini bado hajanishawishi, watanzania tunahitaji maisha bora na yenye uhakika, tunataka uchumi wa nchi ukae vizuri, tunataka vifaa vya ujenzi vishuke bei, tunataka pembejeo za kilimo zishuke bei, tunataka vyakula vishuke bei, tunataka mafuta yashuke bei ili kushusha gharama za usafiri, tunataka umeme wa uhakika na wa kiwango cha chini, tunataka maji ya uhakika, tunataka elimu ya uhakika ikiwemo kuboresha maslahi ya walimu, tunataka madawati na majengo kwa uhakika, tunataka huduma bora za afya nchi nzima, hapo nitaanza kukuunga mkono.
Fanya kazi acha majungu. Mahaba niue.com
 
Nikiri kwamba kaanza vizuri sana lakini bado hajanishawishi, watanzania tunahitaji maisha bora na yenye uhakika, tunataka uchumi wa nchi ukae vizuri, tunataka vifaa vya ujenzi vishuke bei, tunataka pembejeo za kilimo zishuke bei, tunataka vyakula vishuke bei, tunataka mafuta yashuke bei ili kushusha gharama za usafiri, tunataka umeme wa uhakika na wa kiwango cha chini, tunataka maji ya uhakika, tunataka elimu ya uhakika ikiwemo kuboresha maslahi ya walimu, tunataka madawati na majengo kwa uhakika, tunataka huduma bora za afya nchi nzima, hapo nitaanza kukuunga mkono.
ndo kwanza ameanza ni kweli si vizuri kusema ameweza kuuvunja mfupa uliowashinda wengi ila kwa sasa at least we can see a bright future of tanzania hakika nchi itabadilika na si yeye tu KAZI TUFANYE SOTE tanzania yetu sote yeye katuonyesha mfano na sisi wa chini pia tupige kazi kama wewe mvuvi piga nyavu kisawawasa kama mkulima piga jembe kisawasawa kama konda kula vichwa yaan sasa ni kazi tuu kama uko ofisini mambo ya facebuku tupa kule umiza kichwa hapo ulipo ufanye nini ili kusaidia uchumi wa nchi kwa ujumla
 
Unataka kumpa nini mwanaume mwenzio ili akushawishi, wewe ndio unahitaji - unataka na sio watanzania. Watz wenye akili timamu wanajua maendeleo ni mchakato na muda ni rasilimali muhimu katika kufikia malengo. Sidhani kama JPM anahitaji kukushawishi wewe, kwa ulivyoandika wewe ni wakufuata na utapata. Magufuli ana stop bleeding kwanza iliuhai uendelee kuwepo halafu ata fix tatizo linalosababisha bleeding.

Nikiri kwamba kaanza vizuri sana lakini bado hajanishawishi, watanzania tunahitaji maisha bora na yenye uhakika, tunataka uchumi wa nchi ukae vizuri, tunataka vifaa vya ujenzi vishuke bei, tunataka pembejeo za kilimo zishuke bei, tunataka vyakula vishuke bei, tunataka mafuta yashuke bei ili kushusha gharama za usafiri, tunataka umeme wa uhakika na wa kiwango cha chini, tunataka maji ya uhakika, tunataka elimu ya uhakika ikiwemo kuboresha maslahi ya walimu, tunataka madawati na majengo kwa uhakika, tunataka huduma bora za afya nchi nzima, hapo nitaanza kukuunga mkono.
 
mkuu..ndio maana fisiemu itatutawala milele sababu inajua sana kucheza na akili za wadaanganyika.Mind games hizi watu washajaa tayari inasikitisha sana mie nakwambia ipo siku tutachekwa sana.
lisa mie huo upaja wako tu mmmh niko hoi
 
sheria inaongelea mchakato,mchakato mchakato, tumechoshwa na michakato inayotumia fedha. Moja ya vitengo tunavyotaka vifutwe ni hiki cha manunuzi!Barabara kasanifu engineer then wewe sio hata engineer ndio unafanya mauzo na manunuzi ya kazi ya kihandisi upuuzi mtupu. mwisho wa michakato tutaenda kisayansi

Duuuuh
Kula like 1000000000000
 
.. bei za vifaa vya ujenzi, vyakula, n.k. kushuka no way. kadiri majipu yanavyotubuliwa ndivyo kodi halali watakazolipa zitahamishiwa kwa walaji. Pia ajira zitapungua sana... waajiri wanaotubuliwa majipu watapunguza sana ajira na wawekezaji pia wataanza kusita kuwekeza /serikali yenyewe tu imeshaagiza ashirika yapunguze ajira. Ila huduma kama elimu, afya, maji & miundo mbinu zinaweza kuboreka iwapo hiyo kodi itatumika vizuri.
 
Nikiri kwamba kaanza vizuri sana lakini bado hajanishawishi, watanzania tunahitaji maisha bora na yenye uhakika, tunataka uchumi wa nchi ukae vizuri, tunataka vifaa vya ujenzi vishuke bei, tunataka pembejeo za kilimo zishuke bei, tunataka vyakula vishuke bei, tunataka mafuta yashuke bei ili kushusha gharama za usafiri, tunataka umeme wa uhakika na wa kiwango cha chini, tunataka maji ya uhakika, tunataka elimu ya uhakika ikiwemo kuboresha maslahi ya walimu, tunataka madawati na majengo kwa uhakika, tunataka huduma bora za afya nchi nzima, hapo nitaanza kukuunga mkono.

binafsi mimi naona hajaanza vibaya. in fact anatekeleza sera za upinzani (hususani UKAWA).

mimi nadhani tuendelee kumpa benefit of the doubt still.

kuna mawaziri (waandamizi na wengine walikuwamo kwenye kinyang'anyiro cha kugombea urais within CCM - sihitaji kuwataja mnawajua!)....akiwarudisha hao kwenye cabinet - hasa hasa yule jamaa - basi nitajua kuwa haya yote ya sasa ni maigizo ya kiini macho na kwamba awamu ya nne ndiyo bado inatawala.
 
Nikiri kwamba kaanza vizuri sana lakini bado hajanishawishi, watanzania tunahitaji maisha bora na yenye uhakika, tunataka uchumi wa nchi ukae vizuri, tunataka vifaa vya ujenzi vishuke bei, tunataka pembejeo za kilimo zishuke bei, tunataka vyakula vishuke bei, tunataka mafuta yashuke bei ili kushusha gharama za usafiri, tunataka umeme wa uhakika na wa kiwango cha chini, tunataka maji ya uhakika, tunataka elimu ya uhakika ikiwemo kuboresha maslahi ya walimu, tunataka madawati na majengo kwa uhakika, tunataka huduma bora za afya nchi nzima, hapo nitaanza kukuunga mkono.

Kila mtu ana threshold yake. Kuwa mvumilivu tu na yako itafika utafurahi kama wwngine wanavyofurahi sasa. Just contain yourself.
 
Hatuwezi kukwepa ukweli juu ya mfumuko wa bei sokoni, Hivi ni kwa nini kama mchele unatoka hapa hapa nchini ila unakuwa bei juu sana?
 
Mkuu, Magufuli sasahivi hafanyi kazi ya kushawishi watu bali anatumbua majipu tu.Kazi ya kushawishi alishaifanya wakati wa kampeni. Hivyo kama bado unataka akushawishi subiri mwaka 2020. Hata hivyo ninakutahadharisha kuwa kama wewe ni jipu usicheze mbali maana jamaa muda si mrefu atakufikia tu.
 
Back
Top Bottom