realoctopus
JF-Expert Member
- May 11, 2014
- 3,232
- 1,983
Anatekeleza ilani ya ukawa,ccm hawakuwa na ilani kama hii.Mfano safari za nje za kila mara kufutwa ccm walikuwa nayo kwenye ilani yao?
Sidhani kama kushawishi ni moja ya majukumu ya rais.
Nikiri kwamba kaanza vizuri sana lakini bado hajanishawishi, watanzania tunahitaji maisha bora na yenye uhakika, tunataka uchumi wa nchi ukae vizuri, tunataka vifaa vya ujenzi vishuke bei, tunataka pembejeo za kilimo zishuke bei, tunataka vyakula vishuke bei, tunataka mafuta yashuke bei ili kushusha gharama za usafiri, tunataka umeme wa uhakika na wa kiwango cha chini, tunataka maji ya uhakika, tunataka elimu ya uhakika ikiwemo kuboresha maslahi ya walimu, tunataka madawati na majengo kwa uhakika, tunataka huduma bora za afya nchi nzima, hapo nitaanza kukuunga mkono.
Hahahaa, eti Vyakura vishuke bei,fanya edit andiko lake ndo tuchangie
Vyakura = Vyakula
masrai = maslahi
elim =elimu
walim = walimu
Vinginevyo mawazo yako ni mzuri na ya msingi pia, Hapa unawakilisha matarajio ya Watanzania walio wengi, Lakini kumbuka kuwa huu sio mwanzo mbaya! muheshimiwa ameanza vizuri, tumpe support na tumuombee.
Hivi kule ICJ mlijibiwa nini.......??
Fanya edit na wewe, husirudie tena kukurupuka!
Hahaha....kweli nyani aoni kundule
Kwahiyo unataka haya yote afanye kwa siku hizi 26 alizokaa ikulu? Mjue nyie ukawa mmelaaniwa kazi yenu ni kugombania maiti basi.Nikiri kwamba kaanza vizuri sana lakini bado hajanishawishi, watanzania tunahitaji maisha bora na yenye uhakika, tunataka uchumi wa nchi ukae vizuri, tunataka vifaa vya ujenzi vishuke bei, tunataka pembejeo za kilimo zishuke bei, tunataka vyakula vishuke bei, tunataka mafuta yashuke bei ili kushusha gharama za usafiri, tunataka umeme wa uhakika na wa kiwango cha chini, tunataka maji ya uhakika, tunataka elimu ya uhakika ikiwemo kuboresha maslahi ya walimu, tunataka madawati na majengo kwa uhakika, tunataka huduma bora za afya nchi nzima, hapo nitaanza kukuunga mkono.
Nikiri kwamba kaanza vizuri sana lakini bado hajanishawishi, watanzania tunahitaji maisha bora na yenye uhakika, tunataka uchumi wa nchi ukae vizuri, tunataka vifaa vya ujenzi vishuke bei, tunataka pembejeo za kilimo zishuke bei, tunataka vyakula vishuke bei, tunataka mafuta yashuke bei ili kushusha gharama za usafiri, tunataka umeme wa uhakika na wa kiwango cha chini, tunataka maji ya uhakika, tunataka elimu ya uhakika ikiwemo kuboresha maslahi ya walimu, tunataka madawati na majengo kwa uhakika, tunataka huduma bora za afya nchi nzima, hapo nitaanza kukuunga mkono.
Nyi ndo wale asante bwana, wewe baada ya kujenga hoja unashikili ku-support tu huna mchango wowote, watanzania wanakufa kwa njaa vyakula ni ghali mno na hapa ndio kuna matarajio ya watanzania 95% au unataka kuniambia wewe ukihisi njaa utaenda kula vumbi linalotifuliwa pale morocco kuelekea mwenge barabara inayojengwa??
Mkuu umeuwaa..! mimi naungana na wewe kuna mambo magufuli alitakiwa siku 1 tu baada ya kushika madaraka afanye kwa haraka sana ili apate hizo sifa.
Siku ile eti amesema hela za viburudisho ambazo zimechangwa eti zinunuliwe vitanda pale muhimbili tu wakati Tz kuna mahospital yameenea kama madanguro watu hawana huduma yeyote. kuna watu Tz hawajuwi ata iyo hospitali ya muhimbili ipo nchi gani.
Alafu hizi hela nyengine ambazo zimeokolea kwa nini serikali haikuagiza vyakula au kununu chakula kama mchele na vitu vyengine wakauz kwenye mashirika yao kwa bei nafuu ili wafanya biashara wengine walazimike kuuza vyakula vyao bei ya chini ili Mtanzania wa kawaida aanze kufaidika tena hata yule mtu wa chini kabisa.
Juzi nimeskia atapunguza wafanyakazi katika taasisi za umma ili awe na watendaji kidogo hapa mimi sina neno ila je ametengeneza kwanza hizo ajira huko nje? ili hao wafanyakazi wakiachishwa hapo waende kufanya kazi nyengine huko nje? manake hii ni sawa na kusema kipindupindu kinauwa watu wajikinge na kuweka usafi haliyakuwa serikali miundo mbinu na takataka na maji machafu serikali haikuimarisha kabla katika miji yote. Nchi nzima ni uchafu mtupu. South Africa walijenga kwanza nchi yao, miji yao na kuboresha miundo mbinu watu wake automatically walilazimika kufanya usafi.
Leo nimesoma pesa zilizookolewa kwenye sherehe za uhuru zijengwe barabara pale morocco na hadi mwenge ni sawa lakini ivi Watanzania kwani wanakula barabara? Tatizo sugu la Tz ni chakula watu wanakufa njaa watu karib 90% wanahangaika na mlo 1 wa chakula tunataka bidhaa za chakula kwa haraka sana ndio zishuke ili tumpe credit magufuli hili liwe jambo la kwanza.
Alafu ivi kuna shida gani siku 1 asitamke pale kivukoni watu wavuuke bure. Hii hoja kwamba ameokoa hizo fedha na zimo ndani ya mfuko wa serikali hazimshawishi mtanzania yeyote yule madam hakuna faida kwa mtanzania mmoja mmoja. itakuwa ni fedha zinaandikwa katika magazeti na mitandao ya kijamii tu.
nimekusoma mkuu wewe ni Genius!!point zako zimeenda chuo kikuu..tunataka bei za vyakula vishuke na sio barabara na vitanda.usanii mtupu huu wa kutafta sifa kwenye media.Mind games hizi zinachezwa
Nikiri kwamba kaanza vizuri sana lakini bado hajanishawishi, watanzania tunahitaji maisha bora na yenye uhakika, tunataka uchumi wa nchi ukae vizuri, tunataka vifaa vya ujenzi vishuke bei, tunataka pembejeo za kilimo zishuke bei, tunataka vyakula vishuke bei, tunataka mafuta yashuke bei ili kushusha gharama za usafiri, tunataka umeme wa uhakika na wa kiwango cha chini, tunataka maji ya uhakika, tunataka elimu ya uhakika ikiwemo kuboresha maslahi ya walimu, tunataka madawati na majengo kwa uhakika, tunataka huduma bora za afya nchi nzima, hapo nitaanza kukuunga mkono.