Kweli wewe utampigia Magufuli kwani ndiye mwenye mabadiliko ya kweli. M4C Magufuli for Change.
Hiyo ndio sababu yangu ya Msingi. Na naamini anaweza kufanya anachoiwazia nchi hii kupitia ahadi hiyo.
Naamini akifanikiwa hilo, Tanzania itakua sehemu salama ya kuishi binadamu.
Huwezi kuchoshwa na umaskini kama huna mikakati ya kupambana na ufisadi.... Tusidanganyane.. Tanzania inamwitaji Magufuli kuliko Magufuli anavyooiitaji Tanzania.!
Atakemeaje wakati hata yeye ni wale wale
Asante Dr. Magufuli. Wewe ndo kiongozi tunayekuhitaji. Wewe huangalii sura ya mtu. Hapa kazi tu. Lowassa na wenzake longolongo tu.Mahakama ya mafisadi ni moja ya vipaumbele vya Magufuli akishaapishwa tu
Tambua hizo mahakama unazosema zinasheria zilizopitwa na wakati, anaposema atafungua Mahakama ya Mafisadi ina maana ataanza na mchakato wa sheria zake,adhabu zitakazoendana na makosa husika.
Haiwezekani mtu aibe bilioni kadhaa, halafu unakua na sheria ya kumfunga miezi mitatu.
sinta mpigia kura yangu magufuli kwa sababu anaonekana ni mtu wa visasi. Anaapa mungu akisema ' haki ya mungu ngoja niwe rais "
ULISHAONA CHAMA CHA KUITOA CCM MADARAKANI? KWELI UNAOTA MCHANA. SUBIRI 48hrs utapata jibu.the rest is history!
kinachotia moyo kwa sasa ni kuwa over 65% ya registered voters wanataka kuuondoa mfumo chovu wa kijani...na this time utaondoka tu.
Mjumbe ni wewe?Hataweza Kupambana na Ufisadi katika katiba ya Zamani pia amezungukwa na mafisadi wengi mno akiwa CCM hajawahi kukemea bora hata James Lembel kuliko Magufuli.