Magufuli anasalitiwa

Tofauti na hao marais wengine mama samia kaingia kwa kura za magufuli. Watu walimpigia magufuli kura kwa asilimia 84.6. Hii ni awamu ya magufuli sema mungu kampenda. Huyu mama kutuletea mambo za fikra zao za laisez faire upwani za kipigaji hakika tunaumia sana roho.
Magufuli alikuwa na baadhi ya mapungufu kama binadamu wengine. Kwa muono wangu, huyu alipaswa kurekebisha mapungufu ya Magufuli na kuendeleza mengine yote kwani anasimamia ilani ileile.

Juzijuzi hapa kuna kauli ya kutisha imetolewa kuwa ikibidi sheria zipindishwe ili kuwavuta waporaji wanaoitwa wawekezaji.

Where this nation is headed to, only God knows. Nchi inapoteza dira ndani ya muda mfupi sana.
 
Kama walikuwa wana Mapinduzi ya kweli, na wanaonewa basi dhamira y kweli itainuka tena hata baada ya kizazi chao, na kwa kuwa ule mfumo wa kitanzania wa kuvumilia ya waliopita na mapungufu yao nao unaelekea ktik nyumba ya milele, na kuingia kizazi cha kuhoji yaliyopita, japo waliong'oa Meno ya Ulimboka hawatafutwi , aliompoteza ghafla pale kizota hawaulizwi. Basi watakaokuja nao walikula na wanaoshangilia sasa hata kam sio wao kizazi chao.

Hizi ibada tunazofanya ni za nini ikiwa kusamehe ni bidhaa adimu?

Maana imeandikwa
"Kisasi ni chake Bwana atalipa"
 
Utawala wa damu, ambao haukuwa na baraka za Muumba!! mwisho wake ndiyo huwa hivi.
Na bado...mtatajana wote!! Tumeanza na huyo mtoboa watu misumari kwenye miguu..bado yule serial killer na yeye ataingia tu kwa 18 za Jamhuri...damu ya mtu huwa haimwagiki bure - never..hii siyo mimi bali ni sheria katika ulimwengu wa roho.
 
Nahuzunika sana kuona ndoto za Mwanamapinduzi wa kweli, JPM zinafifishwa siku hadi siku.
Lakini ninachofurahi ni kwamba, Damu ya Mwanamapinduzi huwa haipotei bure.
Si mbali si siku nyingi watapatikana wanamapinduzi wengi na wenye moyo mmoja na ujasiri usiomithilika. Hao ndio watakaoipambania Tanzania na kutimiza ndoto za Mwanamapinduzi, JPM.
Mungu mkubwa.
 
Ni jambo la kusikitisha kuona mwendo wa kimapinduzi wa magufuli unasalitiwa na wanamapinduzi wanaangalia hawana cha kufanya. Ni hakika mrithi kikatiba wa magufuli sio mwanamapinduzi kwa hivyo tutegemee mwendo wa maendeleo wenye upendeleo kwa umma kusimama.
Makada waliyokua wanasimamia mapambano dhidi ya rushwa dhuluma kwa wanyonge ukwepaji wa kodi na maduhuri ya serikali sasa rais katoa taa kijani waburuzwe na kubambikiwa makosa kama wabakaji kusudi kuwaondoa kwenye nafasi zao.
Tumeona furaha ya mabwanyeye wa kimachame kote kutokana na jinsi sabaya alivyovunja mitandao yao ya uhalifu iliyokua na makao makuu hai. Kwa mfano wizi wa magari ili kuuzwa kama spear used. Utengenezaji fedha bandia ukwepaji kodi na kadhalika.
Hawajaishia hapo sasa wanadai kila kiongozi mwenye ujasiri aina ya sabaya aburuzwe kotini. Wanataja majina na tunaogopa hii serikali ya samia isiyo kua ya kimapinduzi ya chama cha mapinduzi huenda wakawa kwenye kazi ya kuvuruga mwendo wa kimapinduzi wa magufuli.
Kudadadeeki lazima mtaota vibiyongo safari hii maana mama Samia hana muda mchafu wa kusikiliza majungu yenu na kumramba miguu.
 
Pole sana.

Tulionya hamkusikia na sasa mmeshachelewa.

Sasa hivi wanalialia tu kama wakimbizi ndani ya chama chao
 
Ndugu yang kila nabii na kitabu chake. Mzee Mwinyi alipoingia madarakan aliwatema viongozi wengi waliokuwepo ktk serikali ya Nyerere, hakuna mtu aliesema Mwinyi kamhujumu Nyerere. Mkapa alipoingia hivyo hivyo aliwatema viongozi wengi waliokuwepo ktk serikali ya Mwinyi, hakuna aliemlaumu kwa hilo. Kikwete halikadhalika alifanya the same kama watangulizi wake na yeye akaja na watu wake kuongoza serikali yake japo wapo wachache wa Mzee Mwinyi na Mkapa waliokuwepo, hakuna aliempigia kelele au kumlaumu. Hayati Magufuli pia alipoingia alipanga safu yake aliyoona ndio bora na itakayomsaidia kuifikisha Tanzania ilipofika pia na yeye hakulaumiwa. Sasa ni zamu ya mama na yeye ana haki au uhuru wa kupanga au kuchagua anaowataka yeye ktk serikali yake kulingana na nguvu aliyopewa na katiba kwahiyo haina haja ya kumlaumu na kuona kwamba sio mzalendo au anamfanyia hujuma marehemu. Tumuombee dua mama atufikishe salama huko tunapoelekea maana yeye ndio dereva na sisi ni abiria wake.
Mtalia sana nyinyi MATAGA
 
Ni jambo la kusikitisha kuona mwendo wa kimapinduzi wa magufuli unasalitiwa na wanamapinduzi wanaangalia hawana cha kufanya. Ni hakika mrithi kikatiba wa magufuli sio mwanamapinduzi kwa hivyo tutegemee mwendo wa maendeleo wenye upendeleo kwa umma kusimama.
Makada waliyokua wanasimamia mapambano dhidi ya rushwa dhuluma kwa wanyonge ukwepaji wa kodi na maduhuri ya serikali sasa rais katoa taa kijani waburuzwe na kubambikiwa makosa kama wabakaji kusudi kuwaondoa kwenye nafasi zao.
Tumeona furaha ya mabwanyeye wa kimachame kote kutokana na jinsi sabaya alivyovunja mitandao yao ya uhalifu iliyokua na makao makuu hai. Kwa mfano wizi wa magari ili kuuzwa kama spear used. Utengenezaji fedha bandia ukwepaji kodi na kadhalika.
Hawajaishia hapo sasa wanadai kila kiongozi mwenye ujasiri aina ya sabaya aburuzwe kotini. Wanataja majina na tunaogopa hii serikali ya samia isiyo kua ya kimapinduzi ya chama cha mapinduzi huenda wakawa kwenye kazi ya kuvuruga mwendo wa kimapinduzi wa magufuli.
Punguani mkubwa, kama sabaya alikua bwanako kamtoe rumande jambawazi mkubwa yule

Sent from my SM-G973U using JamiiForums mobile app
 
Hujui hata maana ya neno mwanamapinduzi?
Magufuli hajawahi hata kufikiriwa kuwa mwanamapinduzi acha ujinga wako!
Yaani watu wa aina ya kina sabaya bado wapo miongoni mwetu wa kuwatetea kweli?
Mtu mweusi ana safari ndefu sana aisee!
Mbona hujabambikiwa wewe hayo makosa????
Umesahau kuwa ndege wa rangi moja huruka pamoja?
 
Ni mtazamo tu ila hata wakiweka mabarabara ya lami kulikobakia na kujenga Airport kila kona bado ni nchi moja inajengwa
 
Nahuzunika sana kuona ndoto za Mwanamapinduzi wa kweli, JPM zinafifishwa siku hadi siku.
Lakini ninachofurahi ni kwamba, Damu ya Mwanamapinduzi huwa haipotei bure.
Si mbali si siku nyingi watapatikana wanamapinduzi wengi na wenye moyo mmoja na ujasiri usiomithilika. Hao ndio watakaoipambania Tanzania na kutimiza ndoto za Mwanamapinduzi, JPM.
Mungu mkubwa.
Watajitahidi kumfubaza Magufuli, lakini nakuhakikkshia ukifika uchaguzi watalazimika kujinasibisha na Magufuli. Hii ni kwa sababu wapiga Kura wa kweli ni wananchi wa kawaida ambao wanampenda. propaganda na harakati za mitandaoni zilizotekwa na kakikundi kadogo hazitapiga kura
 
Mzee amelala mwacheni Apumzike hayo mambo Yenu pambanieni kwenye jamii zenu bila kumhusisha mzee Huyu
 
Ni jambo la kusikitisha kuona mwendo wa kimapinduzi wa magufuli unasalitiwa na wanamapinduzi wanaangalia hawana cha kufanya. Ni hakika mrithi kikatiba wa magufuli sio mwanamapinduzi kwa hivyo tutegemee mwendo wa maendeleo wenye upendeleo kwa umma kusimama.
Makada waliyokua wanasimamia mapambano dhidi ya rushwa dhuluma kwa wanyonge ukwepaji wa kodi na maduhuri ya serikali sasa rais katoa taa kijani waburuzwe na kubambikiwa makosa kama wabakaji kusudi kuwaondoa kwenye nafasi zao.
Tumeona furaha ya mabwanyeye wa kimachame kote kutokana na jinsi sabaya alivyovunja mitandao yao ya uhalifu iliyokua na makao makuu hai. Kwa mfano wizi wa magari ili kuuzwa kama spear used. Utengenezaji fedha bandia ukwepaji kodi na kadhalika.
Hawajaishia hapo sasa wanadai kila kiongozi mwenye ujasiri aina ya sabaya aburuzwe kotini. Wanataja majina na tunaogopa hii serikali ya samia isiyo kua ya kimapinduzi ya chama cha mapinduzi huenda wakawa kwenye kazi ya kuvuruga mwendo wa kimapinduzi wa magufuli.
Subiri wakifikishwa mahakamani ukawatolee utetezi wa kimapinduzi. Hizo hela umekula za kuwasafirisha hao madhalimu ni bora urudishe, maana unakula haramu.
 
Back
Top Bottom