Sikonge
JF-Expert Member
- Jan 19, 2008
- 11,633
- 6,229
Acid,
Tupo pamoja sana na nafurahi ingawa kwa shingo upande unakubali.
Haya mambo ya kuandika mikataba kwa sasa ninavyofahamu baadhi ya nchi za Ulaya wanayafundisha vyuoni.
Kuna Mtanzania mmoja alishawahi kuajiriwa kufanya kazi ya kufundisha Shirika kubwa la Serikali kama Tanroads kwa Tanzania. Wazungu walichukia sana kupewa shule na Mpingo na hasa inapokuja kuwa wengi wao tayari walikuwa Wahandisi waliobobea ila hawajui kuwekeana/kuandika mikataba.
Jamaa (wakandarasi) walikuwa wakitumia makosa wanayoyafanya kwenye UPEMBUZI yakinifu. Kwa mfano katika sehemu wanayojenga, mkandarasi anakuta swamp na kwenye makaratasi haipo. Hili linakuwa kosa la TANROADS kwa sababu hawakuliweka kwenye maelezo. Sasa jamaa wanajenga pale kwa kukausha maji kwanza. Na wakimaliza kujenga, kama gharama yake imeongezeka kwa dola 5,000 basi wao ndiyo sehemu ya kujidai maana wataandika bei wanayotaka. Wanaweza kuandika hata Dola 500,000. Inabidi muwe mmekubaliana mapema kuwa kikitokea kitu cha ajabu njiani, nini kifanyike na mkataba ubadilike vipi. Ni bora zaidi kama watu wa SOIL ENGINEERING watafanya kazi yao vizuri basi wataokoa hizi ajali.
Kwa Tanzania nina uhakika uzembe ni mwingi sana na wanapokuja wajuzi wa kuandikiana mikataa na kuiba, tutalizwa sana. Kuna kampuni fulani la Ki-German ni Washenzi sana. Wana wanasheria kama 12 hivi na Wahandisi kama 3. Wao hushinda kama Mkandarasi mkuu na hapo huchukua wafanyakazi wa chini wengi. Sasa wao wanachukua pesa Serikalini na hawawalipi nyie. Huwa wanakuja Wahandisi wao na wanatafuta makosa madogomadogo. Wakiyaona tu, wanaandika kwenye report na kupiga picha. Ukimaliza kazi HAWAKULIPI HELA. Sasa jifanye unaenda Mahakamani, mhhhh ...... hapo unakutana na ile timu ya Wanasheria 12, unakuwa chali.
Ndiyo maana ni rahisi sana kwa Mkandarasi TAJIRI sana leo, kesho ukasikia KAFILISIKA.
Magufuli atengeneze timu ya Wanasheria wakali wa TANROADS ili wawe wanasaidia kwenye mikataba na kusimamia mikataba pia. Unaweza kuwafanyia unyama Wakandarasi kama wamezoea kuiibia serikali huku ukipeleka onyo kwa wengine kuwa "mnaweza kufilisika sasa hivi kama mtajifanya mwatoa sana hongo........."
Tupo pamoja sana na nafurahi ingawa kwa shingo upande unakubali.
Haya mambo ya kuandika mikataba kwa sasa ninavyofahamu baadhi ya nchi za Ulaya wanayafundisha vyuoni.
Kuna Mtanzania mmoja alishawahi kuajiriwa kufanya kazi ya kufundisha Shirika kubwa la Serikali kama Tanroads kwa Tanzania. Wazungu walichukia sana kupewa shule na Mpingo na hasa inapokuja kuwa wengi wao tayari walikuwa Wahandisi waliobobea ila hawajui kuwekeana/kuandika mikataba.
Jamaa (wakandarasi) walikuwa wakitumia makosa wanayoyafanya kwenye UPEMBUZI yakinifu. Kwa mfano katika sehemu wanayojenga, mkandarasi anakuta swamp na kwenye makaratasi haipo. Hili linakuwa kosa la TANROADS kwa sababu hawakuliweka kwenye maelezo. Sasa jamaa wanajenga pale kwa kukausha maji kwanza. Na wakimaliza kujenga, kama gharama yake imeongezeka kwa dola 5,000 basi wao ndiyo sehemu ya kujidai maana wataandika bei wanayotaka. Wanaweza kuandika hata Dola 500,000. Inabidi muwe mmekubaliana mapema kuwa kikitokea kitu cha ajabu njiani, nini kifanyike na mkataba ubadilike vipi. Ni bora zaidi kama watu wa SOIL ENGINEERING watafanya kazi yao vizuri basi wataokoa hizi ajali.
Kwa Tanzania nina uhakika uzembe ni mwingi sana na wanapokuja wajuzi wa kuandikiana mikataa na kuiba, tutalizwa sana. Kuna kampuni fulani la Ki-German ni Washenzi sana. Wana wanasheria kama 12 hivi na Wahandisi kama 3. Wao hushinda kama Mkandarasi mkuu na hapo huchukua wafanyakazi wa chini wengi. Sasa wao wanachukua pesa Serikalini na hawawalipi nyie. Huwa wanakuja Wahandisi wao na wanatafuta makosa madogomadogo. Wakiyaona tu, wanaandika kwenye report na kupiga picha. Ukimaliza kazi HAWAKULIPI HELA. Sasa jifanye unaenda Mahakamani, mhhhh ...... hapo unakutana na ile timu ya Wanasheria 12, unakuwa chali.
Ndiyo maana ni rahisi sana kwa Mkandarasi TAJIRI sana leo, kesho ukasikia KAFILISIKA.
Magufuli atengeneze timu ya Wanasheria wakali wa TANROADS ili wawe wanasaidia kwenye mikataba na kusimamia mikataba pia. Unaweza kuwafanyia unyama Wakandarasi kama wamezoea kuiibia serikali huku ukipeleka onyo kwa wengine kuwa "mnaweza kufilisika sasa hivi kama mtajifanya mwatoa sana hongo........."