Magufuli aanza kulewa madaraka?

Wanapowekeana mikataba na wakandarasi kuna kipengele cha kuwaweka ndani kama hawajatimizima masharti yaliyowekwa?

Na mkuu wa mkoa atamjuaje mkandarasi aliyefanya kazi chini ya viwango?

Kama kazi haijatendwa kama inavyotakiwa basi sheria ifuate mkondo wake na adhabu stahili zitolewe na sio kuwaweka watu ndani kama hakuna vyombo vya sheria.
Mkuu wa mkoa anamjua through senior engineer's reports ( if they are doing their jobs ) kila halmashauri ina mhandisi mshauri wa ujenzi sambamba na meneja wa mkoa wa tanroads mwenye dhamana ya kusimamia maendeleo ya barabara na miradi husika mkoani kwake
 
Miaka ya 80 mwishoni, jengo la IFM pale Dar lilikuwa likijengwa na kampuni fulani ya Wahindi nimeisahau.

Waliposhindwa kufanya kazi kwa kujengwa polepole, walikuja kufukuzwa na mkataba ulikuwa wazi kuwa anayekuja hapo kujenga, basi anachukua kila kitu. Waliacha kila kitu pale na kuondoka weupeee!!!! Masharti yalisema hivyo na wao walijua.

Sasa kama TANROADS wanaandikiana mikataba mibovu na Wakandarasi na hawaweki masharti ya:
1. Nini kitokee mara kazi ikiwa chini ya kiwango.
2. Nini kitokee mara kazi ikichelewa kumalizwa,
hilo linakuwa kosa lao wao TANROADS.

Kwangu mie naanza kumuona Magufuli kama kichaa fulani asiyefaa kukaa wizarani hapo. Hivi huyu akiwa Rais kweli, si ataanza kutuambia mambo ya ajabu yafanyike? Tunataka kichaa ila siyo wa hivi. Tunataka kichaa ambaye kama sheria ni MPIRA basi anauchezea kwenye mstari wa chaki huku kukiwa kumebaki milimita chache sana kuvuka mstari ili asije akavuna Dowans nyingine.

Akitaka kuonekana kweli ana Mafenesi mawili makubwa kati ya miguu, afuatilie kazi za TANROADS. Awabane watu wake kujua kwa nini wameruhusu kazi za uzembe zifanyike na siyo kuwabana Wakandarasi. Kuna haja hizi Wizara ziwe zinawekwa wajenzi kweli kwa mfano hapa angelifaa Prof. Mwandosya awe Waziri.

Magufuli, anza kulia na watu wako kwa uzembe wao na waache Wakandarasi waishi wakitumbua hela zao maana nyie wenyewe Serikali ya CCM mliwaruhusu na kuwapa. Huyu jamaa tangu aanze kusifiwa sasa kaanza kuwa kama mlevi kweli. Utaendaje kuchoma nyavu za wavuvi walizozinunua hapahapa Tanzania na ni Made in Tanzania badala ya kukibana KIWANDA?
 
ni miezi miwili tu sasa toka ateuliwe kushika huo wadhifa mi nadhani anastahili kupewa muda zaidi. Kutekeleza mipango yote ndani ya muda kama huu ni ndoto za mchana, tusiwe watu wa kukosoa tu.




.
 
watanzania tumezoea longolongo nyingi kazini, tunahitaji viongozi kama hawa ili watu wanyoke, safi Dr.Magufuli, ikiwezekana watandikwe na bakora kabisa
 
"dr magufuli aagiza makandarasi kukamatwa
na john maduhu
mwanza
waziri wa ujenzi,dr john magufuli ameagiza wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya kuwaweka ndani mkandarasi wazembe wanaopewa kazi na kushindwa kuzifanya kwa wakati.
amesema kwa kuwa makandarasi hao wanaonekana kuwa kikwazo njia pekee ya kurejeshaheshima katika kazi ni kuwaweka ndani japo kwa saa sita kwa kuwa wanajenga barabara chini ya kiwango."
mtanzania,januari 5,2011

the gentleman is at it again, cheap populist soft targets.
katika mikataba ya ujenzi inayotayarishwa na serikali, mkandarasi mzembe anavifungu vinavyombana kutekeleza kazi kwa viwango vinavyotakiwa.
Sasa hili la kuwaweka ndani wakandarasi ni la kushangaza!
Tunategemea dr magufuli aanza yeye kwa kuwaweka ndani wasimamizi na wakandarasi wa kilwa rd.kazi imefanywa chini ya viwango wakati wahandisi wa wizara walikuwepo na hata leo wapo, hawajafa.
Dr magufuli awaweke ndani hawa.
Sakata la mrema linaishaje, dr magufuli atayarishi lupango ya kumweka mrema wa tanroads, ama sivyo hataeleweka.
Msata-bagamoyo je?
Dr magufuli atayarishe selo ya mkandarasi aliyepewa kazi hiyo,takopa, wa kikorea ili tuweze kumwelewa.
Udhaifu wa mikataba mingi ya ujenzi msingi wake uko katika watayarishaji na wasimamizi wenyewe ndani ya wizara husika za ujenzi na halmashauri.
Suala la rushwa ndio usiseme.
Mchawi wa matatizo ya ujenzi iko huko huko mawizarani ikiwa ni pamoja na ni ukosefu wa usimamizi imara wa miradi yenyewe.
Zaidi ya yote namshauri dr magufuli kusoma mikataba ya ujenzi, kitu ambacho inaelekea hakielewi vema.

wewe umeandika thread kishabiki sana asa ulitakaje kwamba ni kosa kuwashitaki au?mwache afaye kazi me naona poa tu kuwashitaki.
 
Mkuu wa mkoa anamjua through senior engineer's reports ( if they are doing their jobs ) kila halmashauri ina mhandisi mshauri wa ujenzi sambamba na meneja wa mkoa wa tanroads mwenye dhamana ya kusimamia maendeleo ya barabara na miradi husika mkoani kwake

Kwa hiyo mkuu wa mkoa amuweke mkandarasi ndani kwa kupewa taarifa kuwa standards hazikufikiwa na meneja wa ukandarasi wa mkoa?

Anashindwa vipi kupewa taarifa kuwa kwenye mkataba hakuna kifungu kinachoruhusu kumuweka mtu ndani asipotimiza standards?
 
Watanzania bwana.... ati kuna kifungu kwenye mkataba kinasema wawekwe ndani?? leo ndio tunajua mikataba? ya dowans? ya radar? ya nyumba tunazopangisha siyoenda hata kunakohusika na kulipia kodi za mapato? ya gesti tunazokaa tukienda workshops na kuomba risiti ziongezewe bei??

tukibanwa sisi mikataba... ikibanwa serikali, poa sio??

Its a jungle law, Magufuli hana haja ya kutafuta sifa, kama ni sifa anazo kuliko waziri yoyote wa serikali ya awamu hii, tena zaidi ya rais wake na waziri mkuu wake

Gaijin and Lole... think about it

Hivi mnajua hawa makandarasi wanavyobaka rasilimali kwa kutumia ma-DED, DT., DC na wakandarasi wa wilaya wenye uchu wa mbwa??
 
Kwa hiyo mkuu wa mkoa amuweke mkandarasi ndani kwa kupewa taarifa kuwa standards hazikufikiwa na meneja wa ukandarasi wa mkoa?

Anashindwa vipi kupewa taarifa kuwa kwenye mkataba hakuna kifungu kinachoruhusu kumuweka mtu ndani asipotimiza standards?
the aim hapa ni accountability and nothing less G'
 
Kwa hiyo dawa ni KUKATA MAJANI badala ya MZIZI siyo?

Unaonaje akiwabana wasiwamizi wake wanaotoa hela, wanaotoa mikataba na wanaosimamia?

Kwani hao Wakandarasi wanakuja kuchota hizo hela kama akina LUKAZA pale EPA?

ACID, PULIZI. Unachoma nyavu za Wavuvi badala ya kukichoma Kiwanda kinachozitengeneza?

Kwa nini usiwapige marufuku Watengenezaji nyavu kuacha kutengeneza nyavu za namna hiyo?

Kwa nini unapotaka kwenda Kibaha, unaamua kupitia Vikindu, Kilwa .................. Kibaha?

Ukitaka kuwabana hao Wakandarasi, SI WANYIME TU HELA? Wanyang'anye kazi bila malipo.

Ngoja niamini kuwa "It's a Jungle Law".
Watanzania bwana.... ati kuna kifungu kwenye mkataba kinasema wawekwe ndani?? leo ndio tunajua mikataba? ya dowans? ya radar? ya nyumba tunazopangisha siyoenda hata kunakohusika na kulipia kodi za mapato? ya gesti tunazokaa tukienda workshops na kuomba risiti ziongezewe bei??

tukibanwa sisi mikataba... ikibanwa serikali, poa sio??

Its a jungle law, Magufuli hana haja ya kutafuta sifa, kama ni sifa anazo kuliko waziri yoyote wa serikali ya awamu hii, tena zaidi ya rais wake na waziri mkuu wake

Gaijin and Lole... think about it

Hivi mnajua hawa makandarasi wanavyobaka rasilimali kwa kutumia ma-DED, DT., DC na wakandarasi wa wilaya wenye uchu wa mbwa??
 
the aim hapa ni accountability and nothing less G'

Hapana mkuu

Kosa ni la tanroad na serikali kuandikiana mikataba mibovu na wakandarasi.
Kama hakuna clause ya kumbana mkandarasi kumaliza kazi on time kwa viwango vilivyowekwa tutamuweka ndani kwa kosa gani?

Sasa yeye anataka wachukuliwe hatua watu wasiochini yake wakati watenda makosa ni watu wake anawaacha?

Kwanini tunataka rule of law kama hatuwezi kuheshimu laws zilizopo?
 
Sikonge, Gaijin... nimewasoma but i still believe wa wilayani haswa wanajua kinachoendelea hasa baada ya decentralization... ZUNGUKA TU HALMASHAURI CHACHE UTANIAMBIA, MAANA KUNA MADARAJA HADI YA UDONGO

with all due respect naomba niwakubalie kwa shingo upande.... maana najua kama ni sheria basi nyingine yeye hana mkono kwani ziko local government na ndio maana akasema hayo.... zinazomhusu, yeye mwenyewe atashughulikia

One love G and sikonge
 
Hilo la kuwekana ndani litawezekana kama kutakuwa na kifungu cha namna hiyo ndani ya mkataba (which is imnposible under standard construction contracts).Tatizo la kazi kuwa chini ya viwango linatokana na rushwa. Mara nyingi wakandarasi wana omba zabuni kwa bei ya kawaida kabisa. tatizo linakuja kwa wasimamizi, watataka kitu kikubwa ili wampe kazi mkandarasi hata kama sifa zote zinazotakiwa anazo. Jamaa uwa wana demand pesa nyingi sana. Hivyo inapelekea mkandarasi kutumia hadi faida aliyotegemea apate.Kwa sababu ni biashara itambidi anunue materials ya kiwango cha chini na kufanya kazi chini ya kiwango ili hasipate hasara na kujikuta kafirisika.So tatizo kubwa ni rushwa na dawa yake si kuwekana ndani. Huyo mkuu wa wilaya ama mkoa anamgao wake kwa mkandarasi.
 
Is TANROADS now a section of the Ministry or an independent agency with its own Board? Jinsi mambo yanavyoendelea na huyu Mheshimiwa Waziri inaelekea sasa hii TANROADS imekuwa section directly under the Minister.
 
Nafikiri Magufuli amechanganyikiwa na hali aliyoikuta ya kiutendaji kwenye hiyo wizara so anajaribu kufanya mambo mengi kwa kipindi kifupi,tumpe muda ,si kazi rahisi kwake kuanza ku-deal na Mrema kama ilivyo rahisi kusema wandarasi wasiomaliza kazi kwa wakati wawekwe ndani.Atatulia tu,uzuri ana nia na dhamira ya kweli ya kufanya mabadiliko katika sekta hii muhimu ya ujenzi. Hayo ya mikataba mibovu ni kitu anachokifahamu sema mabadiliko ya vipengele vya mikataba yanachukua muda,naamini by the time anafika miaka miwili ofisini atakuwa ameshaongeza vipengele vya kuwabana zaidi wakandarasi na hao wanaosaini hiyo mikataba mibovu na hao wakandarasi.
 
Japokuwa mimi nina uchungu na nchi hii, ila sikubaliani na hatua za kienyeji kama vile nchi haina sheria... kwenye mkataba huo wa ujenzi kuna "sanctions" iwapo upande wowote utakiuka masharti ya mkataba, amao mara nyingi huwa ni fidia y fedha na adhabu zingine, sasa iweje Magufuli amweke lupango mkandarasi.. kosa gani amefanya la jinai.. of cousre la madai ila adhabu si kufungwa wala kuwekwa selo.. Tujadili kama watu wenye uelewa wa sheria ili tuweze kuwa na hoja zenye mantiki kuliko ushabiki... Nampuuza Magufuli kwa kauli hiyo... Peoples Power!!!​
 
Nadhani wakuu WAWILAYA na MIKOA, wanauwezo wa kumuweka mtu ndani au kumfukuza mtu yeyeyote maeneo yao ya utawala, na katib aipo kimya kwa hili!
NDIO MAAN TUNATAKA KATIBA MPYA!
 
Mingine hii ni mikakati tu ya kuingia masikioni mwa watz kwa ajili ya kujuliana mapema atakapogombea 2015...............fanya kazi magufuli na sio kuropoka kila siku lazzima uende na hatua si unajua uozo umeanzia kwa rais wako?...........inawezekana kabisa rais hakusupport ktk maamuzi yako
watch out?>
 
Back
Top Bottom