Magomeni: Basi lingine la UDART lagongwa

Magomeni: Basi lingine la UDART lagongwa

Hayo mabasi yawekewe ngao imara kwa mbele na nyuma ili kuyalinda na madereva wa Jiji ambao wengi wao hujifanya wana haraka kila wakati bila kujali sheria za usalama barabarani
 
Kuna tatizo la msingi hapa ambalo vyombo husika inabidi kudili nalo kimkakati haswa.Hili tatizo si tu kwa hii barabara za mwendo kasi bali kwa road zote hapa tanzania. Ni kuwa zaidi ya robo tatu ya madereva barabarani si madereva (wanajua kuendesha lakini wana ufahamu finyu sana wa sheria za barabarani)..jaribu tu kuangalia watu wanavyogombea kupita kwenye vipita shoto (keep lefts-sheria zake ziko wazi kabisa) kama vile jamaa wa sevilla walivyokuwa wanawagombea liverpool..ama wanaondesha double road mtu ana spidi ndogo kabisa lakini bado amebana upande wa kulia..ama wanaoingia barabara kubwa kutoka barabara ndogo bila kujali walioko barabara kuu wanakuja na spidi gani yeye anaingia kisha bila hata wasiwasi anatembea zake spidi ishirini (na pengine yuko bize na simu)..ama wanavyopita spidi kwenye vivuko vya waenda kwa miguu (zebra)....Hili ni tatizo pana sana ambalo linahitaji jeshi la polisi na taasisi husika kujipanga sawasawa
 
Ingewekwa faini pia ukileta ajali unawekwa ndani masaa hata 72 Kwanza halafu unakutana na faini yako, maana sasa wamezidi,
 
Yanakufa mapema sana haya magari, maskini ng'ombe wa maskini kweli hazai.
 
Inasikitisha sana kwa madereva wa kitanzania kutobadirika, hapo hapo ilipotokea ajali hiyo baada a kuondolewa hizo gari zilizopata ajali, jamaa mwingine pia aka_kunja (u turn) kuelekea kama yule wa awali alivofanya.

Bahati mbaya camera/simu ilikuwa mbali!!.
Huyo wa pili ilitakiwa abinywe balaa! mpuuzi sana
 
Tatizo hakuna elimu ya utumiaji barabara kwa wananchi not to mention questionable drivers katika umiliki wao wa leseni na uzingatiaji wa sheria za barabarani. This is a deep rooted problem wala sishangai.
Elimu gani unayoitaka wewe?!! Kila siku mnaelimishwa hakuna kukata kulia kwenye njia hizo hamsikii? Kuna alama kubwa tu,taa za kuwaongoza bado jitu linafanya uzembe kama huo mnasingizia hamjapewa elimu! Hebu tuache umbumbumbu jamani. Huu mradi hauna tatizo tatizo ni baadhi ya wabongo wako kama ng'ombe! Jitu utaikuta limevaa tai na suti unaweza kufikiri ni listaarabu kumbe hovyo kabisa afadhali ya ng'ombe wakichungwa wanatii mchungaji wao!
 
Nimepita pale na kujionea msururu wa mabasi hayo toka Kimara ukiwa umekwama pale maana barabara yao imezuiwa na basi lillilopata ajali.Kila raia aliyekuwa anapita pale alishikwa na hasira na huyu mwenye gari binafsi.
Mimi nadhani wangeachiwa watoto wa mbwa wa Magomeni pale wambebee hadi cylinder head atie akili pumbavu kabisa yule mwehu.
Imetengenezwa njia ya kuzunguuka pale,na mataa yapo na hizi basi zinakwenda taratibu na zina njia zake,unaigongaje kama sio akili za kisoda hizi?
Yaani wabongo hata chooni inabidi kuwawekea trafiki manake mtu anajisaidia pembeni na tundu la choo lipo!
Hii ngozi nyeusi hii,ngoja niishie hapa.
 
Kuna tatizo la msingi hapa ambalo vyombo husika inabidi kudili nalo kimkakati haswa.Hili tatizo si tu kwa hii barabara za mwendo kasi bali kwa road zote hapa tanzania. Ni kuwa zaidi ya robo tatu ya madereva barabarani si madereva (wanajua kuendesha lakini wana ufahamu finyu sana wa sheria za barabarani)..jaribu tu kuangalia watu wanavyogombea kupita kwenye vipita shoto (keep lefts-sheria zake ziko wazi kabisa) kama vile jamaa wa sevilla walivyokuwa wanawagombea liverpool..ama wanaondesha double road mtu ana spidi ndogo kabisa lakini bado amebana upande wa kulia..ama wanaoingia barabara kubwa kutoka barabara ndogo bila kujali walioko barabara kuu wanakuja na spidi gani yeye anaingia kisha bila hata wasiwasi anatembea zake spidi ishirini (na pengine yuko bize na simu)..ama wanavyopita spidi kwenye vivuko vya waenda kwa miguu (zebra)....Hili ni tatizo pana sana ambalo linahitaji jeshi la polisi na taasisi husika kujipanga sawasawa


Mwangalie huyo jamaa kwenye picha ndiyo typical Mmbongo yaani yeye kila kitu mataalmu tu sasa hapo utakuta anelezea jinsi mradi mzima ulivyokosewa wakati hata ukimuuliza hata akaundikie DART hawezi!

3f4fc0ba-8f81-4337-a1c9-da81d6202d6f-jpg.349247
 
mimi nadhani kuna changamoto kubwa sana kuhusu miundo mbinu na barabara ilivyotengenezwa....ukitokea kigogo kama unaenda kinondoni hakuna njia inayokuruhusu kwenda maeneo ya fire...sasa unapaswa kwenda kugeuza mbele ya magomeni hospitali au kuna eneo maeneo ya magomeni
si tatizo la madereva ila pia hakuna darasa lililotolewa kwa madereva maana miundo mbinu yetu mibovu hakuna njia mbadala ya kupita ukiwa mataa magomeni unataka kwenda maeneo ya muhimbili
Hebu acheni visingizio visivyo na kichwa wala miguu....Alama zipo ila mmezoea short cut, ukiambiwa zunguka huku unaona tabu unataka kukata kona au kugeuza hapo hapo uliposimama! Fuateni sheria acheni visingizio.
 
Wewe umesema kweli...kuchelewa kwake kutumia hizi njia kumezowesha watu vibaya...
Jana barabara ya Samora hubby nusu agongwe...mwenzie kasimama eti yeye ananambia huyu anasimama nini na basi limeshapita...anataka kukanyaga mafuta nikamwambia cheki upande wa pili...kwa akili yake alijua ile njia ya mwendo kasi ni one way na there is no way kukawa na gari nyingine kwa interval ndogo kiasi hicho.....kumbe limepita moja na la pili lilikuwa linaelekea the other side...na hakuna mataa bali alama ya simama...shiiida...


BUT haya mabasi yasijifanye treni...
Ingekuwa tractor wangegonga...?????
Kwenye makutano lazima nao waendeshe kwa tahadhari

Umetisha....!
 
Pole Mh. Raisi kuwaongoza watanzania. Inahitajika uvumilivu mkubwa. Nafikiri tuiboreshe elimu yetu ndiyo njia pekee ya kuweza kutubadilisha.
 
With time wataelewa tu, tuwape muda wananchi wa Dar es Salaam ni teknolojia mpya kwetu sote.

Wendawazimu / wazembe watakwepo tu, na tutaendelea kuona ajali nyingi...!

Si unaona hata kwenye vivuko vya reli ajali zinatokea sababu ya madereva wazembe kutokuchukua tahadhari?!

Ni muhimu kwa watakaosababisha ajali kupewa adhabu kali sana; labda itasaidia.
 
Elimu ,elimu,elimu naikumbuka kauli ya mgombea urais uchaguzi ulopita toka upinzani we real need it more than fly over tunazotaka kuzijenga hizo ndio zitakuwa kasheshe heri tuwekeze kwenye elimu kwanza LA sivyo hayo mabasi yarudishwe yalipotoka hizo barabara zigeuzwe reli tuagize Yale matreni daladala watu wateheshimu hizo njia
 
We ni mpumbavu na ndio mana unaona uo ni upumbavu. Ila wenye akili wanaona hizo ni changamoto kwa mradi mpya kama huo.
Wapumbavu ni nyinyi mnaleta uzembe wa wazi mnaita changamoto. Mngekuwa na akili mngevunja sheria hovyo hovyo, ni upumbavu unawasumbua ila mtanyooka tu.
 
Back
Top Bottom