Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,346
- 26,138
- Thread starter
- #41
Kingine naskia sio wachoyo huitana Kula pamoja
Ni kweli. Hawagombani kama ndege wengine wakati wa kula. Wanapenda kula mtama na kunde
Kingine naskia sio wachoyo huitana Kula pamoja
Mimi nimesikia njiwa ni ndege wa baraka sana kiasi kwamba
kama una mikosi au nuksi kubwa kubwa huwezi kuwafuga
hapa nazungumzia watu kama wauaji
au wachawi sugu nasikia njiwa hawakai majumbani mwao
au watu wenye kufanya taboo kama kutembea mtu na mzazi wake na kadhalika
Mkuu,umenena mambo ya kweli. Nimejionea kwa miaka 6
Sijawahi kujaribu kumfunga barua apeleke Tu na I wish nifanye hiyo maana wanasema kua eti ukishamfunga unamuonesha na picha ya yule unaempelekea barua na ukimwambia usiondoke had akujibu akifika huko haondoki had apewe majib arudishe hii sijawah hats ishuhudia na sinaa hakika if so
Kuanzia mwaka 1994,nilipokuwa darasa la nne, hadi mwaka 2000 nilipokuwa kidato cha tatu, nilikuwa nafuga njiwa. Nilifanikiwa kuwa na njiwa takribani 2000. Kilichofanya nisiendelee kufuga ni kuhamia kwangu Bweni nikiwa kidato cha tatu.Nyumbani hakukuwa na muangalizi mbadala kwangu.
Kwa miaka 6 ya ufugaji wa njiwa, nimepata mafunzo mengi sana. Nitashiriki nanyi katika mafunzo hayo kutokana na nilichokiona na kukizoea.
Kwanza, njiwa wana wivu. Dume la njiwa haliruhusu kabisa jike lake kufuatwa au kuvutiwa na dume lingine. Wivu huongezeka mno wakati jike anapokaribia kutaga. Dume husika humtinga jike popote aendapo na kumfukuza ili aelekee hasa tunduni. Wivu wa hali ya juu.
Pili, njiwa wana mapenzi, ikiwemo huba (intimacy) na uaminifu.Njiwa hugawana wawili wawili-jike na dume kwa kila kundi. Ni kama ndoa hivi. Hapo,kila mmoja huwa na huyo huyo tu. Hata pale jike au dume fulani linapokosekana,anayebakia hapati mwingine hadi pale ambapo upungufu utajitokeza mahali pengine au mpya kuletwa. Hii ina maana kuwa,kama dume ni moja na majike ni mawili au madume mawili na jike ni moja, hakutakuwa na mapenzi yoyote.
Pia, njiwa 'hula denda' kabla ya kupandana. Denda husaidia kuamsha hisia za mwenza. Ya kwamba, njiwa huandaana kabla ya 'majambo'.
Tatu, njiwa husikitika. Panapotokea msiba, njiwa wote husimama kwa mguu mmoja kama alama ya huzuni na masikitiko. Siku hiyo,mapenzi na kula husimama kwa muda.Ilikuwa ikinipasa 'kuwaambia' msiba husika pale ili kuwarudisha kawaida. Kama taarifa haitolewi,wote huruka na kupotea pindi mwili wa marehemu unapotolewa ndani.
Nne, njiwa wana uelewa mkubwa. Huikariri mbinja ya mfugaji. Mbinja ikibadilishwa,hawaji. Hii hutumika kuwaita ili waje kula. Kwa kufurahi kwao,njiwa waweza kutua mabegani,kichwani na viganjani huku wakijidai kwa furaha. Wakati wa kula,njiwa hawapigani lakini kila mmoja hula kwa kasi kubwa na akitosheka huondoka kwenda kupumzika.
Tano, njiwa husaidiana.Hapa ni hasa jike na dume lake.Kusaidiana kwao hasa huanzia pale jike linapotaka kutaga. Ni mayai mawili tu. Wakati huo,dume humsaidia jike kumpelekea vijiti na manyoya kwa jike kutengeneza kiota ndani ya tundu rasmi lililotengenezwa. Halafu,dume na jike husaidia katika kulalia mayai yao.Hulalia kwa siku 21. Hufanya zamu. Tena,husaidiana katika kulisha makinda na kuyafunza kuruka na kadhalika.
Kiukweli,kupitia njiwa wangu nimejifunza mambo mengi. Mengine nitaandika siku nyingine. Wameniongezea vitu maishani. Asanteni njiwa wangu!
Ni kweli. Hawagombani kama ndege wengine wakati wa kula. Wanapenda kula mtama na kunde
Yeah nakubali njiwa wanapenda romance Sana nalishuhudia daily hili
Mimi nimesikia njiwa ni ndege wa baraka sana kiasi kwamba
kama una mikosi au nuksi kubwa kubwa huwezi kuwafuga
hapa nazungumzia watu kama wauaji
au wachawi sugu nasikia njiwa hawakai majumbani mwao
au watu wenye kufanya taboo kama kutembea mtu na mzazi wake na kadhalika
naomba kujua njiwa wanaliwa?????
Huwaambia kwa lugha ya Kiswahili tu kwa maneno-taarifa. Kwa mfano: "Jamani hapa kuna tatizo limetokea.Kuna msiba. Ndiyo maan kuna watu wengi na vilio.Msishangae wala kushtuka." Wakati wa kusema hivyo,ni wakati wa kuwapa chakula kwa pamoja ili waje wote mahali fulani
Hiyo nzuri iandikie then uitoe gazetini. Ji moja ya tafiti nzur ya kipekee. Unaweza kwenda mbali zaidi kuwachunguza na ikakutoa kimaishaKuanzia mwaka 1994,nilipokuwa darasa la nne, hadi mwaka 2000 nilipokuwa kidato cha tatu, nilikuwa nafuga njiwa. Nilifanikiwa kuwa na njiwa takribani 2000. Kilichofanya nisiendelee kufuga ni kuhamia kwangu Bweni nikiwa kidato cha tatu.Nyumbani hakukuwa na muangalizi mbadala kwangu.
Kwa miaka 6 ya ufugaji wa njiwa, nimepata mafunzo mengi sana. Nitashiriki nanyi katika mafunzo hayo kutokana na nilichokiona na kukizoea.
Kwanza, njiwa wana wivu. Dume la njiwa haliruhusu kabisa jike lake kufuatwa au kuvutiwa na dume lingine. Wivu huongezeka mno wakati jike anapokaribia kutaga. Dume husika humtinga jike popote aendapo na kumfukuza ili aelekee hasa tunduni. Wivu wa hali ya juu.
Pili, njiwa wana mapenzi, ikiwemo huba (intimacy) na uaminifu.Njiwa hugawana wawili wawili-jike na dume kwa kila kundi. Ni kama ndoa hivi. Hapo,kila mmoja huwa na huyo huyo tu. Hata pale jike au dume fulani linapokosekana,anayebakia hapati mwingine hadi pale ambapo upungufu utajitokeza mahali pengine au mpya kuletwa. Hii ina maana kuwa,kama dume ni moja na majike ni mawili au madume mawili na jike ni moja, hakutakuwa na mapenzi yoyote.
Pia, njiwa 'hula denda' kabla ya kupandana. Denda husaidia kuamsha hisia za mwenza. Ya kwamba, njiwa huandaana kabla ya 'majambo'.
Tatu, njiwa husikitika. Panapotokea msiba, njiwa wote husimama kwa mguu mmoja kama alama ya huzuni na masikitiko. Siku hiyo,mapenzi na kula husimama kwa muda.Ilikuwa ikinipasa 'kuwaambia' msiba husika pale ili kuwarudisha kawaida. Kama taarifa haitolewi,wote huruka na kupotea pindi mwili wa marehemu unapotolewa ndani.
Nne, njiwa wana uelewa mkubwa. Huikariri mbinja ya mfugaji. Mbinja ikibadilishwa,hawaji. Hii hutumika kuwaita ili waje kula. Kwa kufurahi kwao,njiwa waweza kutua mabegani,kichwani na viganjani huku wakijidai kwa furaha. Wakati wa kula,njiwa hawapigani lakini kila mmoja hula kwa kasi kubwa na akitosheka huondoka kwenda kupumzika.
Tano, njiwa husaidiana.Hapa ni hasa jike na dume lake.Kusaidiana kwao hasa huanzia pale jike linapotaka kutaga. Ni mayai mawili tu. Wakati huo,dume humsaidia jike kumpelekea vijiti na manyoya kwa jike kutengeneza kiota ndani ya tundu rasmi lililotengenezwa. Halafu,dume na jike husaidia katika kulalia mayai yao.Hulalia kwa siku 21. Hufanya zamu. Tena,husaidiana katika kulisha makinda na kuyafunza kuruka na kadhalika.
Kiukweli,kupitia njiwa wangu nimejifunza mambo mengi. Mengine nitaandika siku nyingine. Wameniongezea vitu maishani. Asanteni njiwa wangu!
Hiyo nzuri iandikie then uitoe gazetini. Ji moja ya tafiti nzur ya kipekee. Unaweza kwenda mbali zaidi kuwachunguza na ikakutoa kimaisha