Lole Gwakisa
JF-Expert Member
- Nov 5, 2008
- 4,728
- 2,259
Lisemwalo lipo, kama halipo laja.
Kuna tetesi kuwa baadhi ya mafisadi wana uhusiano wa karibu na uongozi wa juu wa CHADEMA.
Nukuu ya gazeti la Raia Mwema la leo linaeleza kwa undani jinsi vikao vya mafisadi vitakavyofanyika huko Arusha Pasaka hii.
Arusha ndiko wanatoka Dr Slaa na E Lowassa, sijui kama kuna uhusiano hapo!
Nape Nnauye alitonesha suala hili la uhusiano kwa mbali kati ya genge la mafisadi na CHADEMA, wakati akituhumu kuwa kuna magezeti, chama fulani na viongozi fulani wa dini wameanza kutumiwa(taarifa za kiintelijesia?).
Jamani pesa hiyo inatembea.
Ikija thibitika CHADEMA will have lost all credibility.
============
Kuna tetesi kuwa baadhi ya mafisadi wana uhusiano wa karibu na uongozi wa juu wa CHADEMA.
Nukuu ya gazeti la Raia Mwema la leo linaeleza kwa undani jinsi vikao vya mafisadi vitakavyofanyika huko Arusha Pasaka hii.
Arusha ndiko wanatoka Dr Slaa na E Lowassa, sijui kama kuna uhusiano hapo!
Nape Nnauye alitonesha suala hili la uhusiano kwa mbali kati ya genge la mafisadi na CHADEMA, wakati akituhumu kuwa kuna magezeti, chama fulani na viongozi fulani wa dini wameanza kutumiwa(taarifa za kiintelijesia?).
Jamani pesa hiyo inatembea.
Ikija thibitika CHADEMA will have lost all credibility.
============
Mafisadi wadandia CHADEMA kujiokoa
- Wajipendekeza upinzani kupenyeza ajenda
- Benno Malisa ajiunga rasmi kuwatetea
- Watukana viongozi wa juu wa CCM
BAADA ya mambo kuzidi kuwaelemea ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), watuhumiwa wa ufisadi sasa wameanza kwa nguvu kubwa kutaka ‘kudandia mgongo' wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ili kujinusuru na kutafuta kuungwa mkono na umma, KuliKoni limefahamishwa.
Habari kutoka kwa baadhi ya watu walio karibu na watuhumiwa hao na matukio ya hivi karibuni yanadhihirisha pasi shaka kwamba, watuhumiwa hao sasa wameanza kutumia umaarufu wa CHADEMA kutaka kupata kuungwa mkono na umma na pia kuitisha CCM iogope kuendelea kuchukua hatua dhidi yao.
Kwa mujibu wa habari hizo, mkakati wa mwanzo ulikuwa ni kuhakikisha kwamba CCM inapoteza kiti cha Ubunge jimbo la Igunga kilichoachwa wazi na Rostam Aziz, aliyelazimika kujivua gamba ili ionekane ni hasara kuwalazimisha wengine kujiondoa katika nafasi zao.
Baada ya kukwama Igunga imeelezwa kwamba hatua inayofuata sasa ni kuwashambulia na kuwahujumu viongozi wa juu wa CCM na watu walio karibu nao huku wakizidi kujisogeza karibu na Chadema kwa kuwasifia, lakini wakipenyeza ajenda zao za kutetea mafisadi na miradi yao.
"Baada ya kushindwa kuzuia ushindi wa CCM Igunga ili kuonesha kwamba dhana ya kujivua gamba ina madhara kwa chama, sasa wameanza kujionesha wazi wazi kuwa wanaunga mkono Chadema ili wananchi wawaunge mkono pia na kuwatisha CCM waone kwamba watatoka CCM wakifuatwa na wafuasi wengi.
"Walifanya hujuma kubwa sana Igunga. Mchana walionekana wenzetu lakini usiku wanatuhujumu lakini hawakufanikiwa. Kuna wengine walidiriki hata kusaidia wapinzani kwa njia tofauti na wengine kuwaambia watu wao kutoichagua CCM na sasa wanaeneza propaganda kwamba CCM imechakachua kuhalalisha uovu wao," anasema mtoa habari wetu aliye karibu sana na mafisadi.
Imeelezwa kwamba watuhumiwa hao wamekuwa na mkakati wa muda mrefu wa kujiunga na vyama vya upinzani vyenye nguvu lakini baada ya Chadema kuzidi kupata wafuasi wengi, ndicho chama pekee wanachokiangalia kwa sasa japo hakuna dalili za kupokelewa huko kwa wakati huu.
KuliKoni limefahamishwa na mmoja wa viongozi wa Chadema kwamba, hoja ya kuwapokea baadhi ya watuhumiwa wa ufisadi iliwahi kujitokeza lakini ilipata upinzani mkubwa kutoka kwa viongozi wa juu wa chama hicho, pamoja na kuwapo mawasiliano yasiyo rasmi ya baadhi ya wafuasi wa watuhumiwa hao na viongozi hao.
Tayari kuna taarifa kwamba viongozi wawili wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) wamekuwa na mazungumzo yasiyo rasmi na viongozi wa CHADEMA, lakini hakuna dalili zozote za kupokelewa huko hasa baada ya kubainika wazi kwamba wameanza kujiunga rasmi na kundi la watuhumiwa wa ufisadi bila kificho.
CHANZO: Gazeti la Kulikoni