Maendeleo ya Mgomo wa Madaktari na Mwitikio wa Serikali

kwani Dr, Mshahara wake ni kiasi gani?

Maana kama tunaambiwa hawafiki hata 2000, ina maana serikali ina uwezo wa kuwalipa hata 7m per month bila shida.

7,000,000 x 2000 x12 = 168,000,000,000 kwa mwaka.
 
Hoja zako hazina mshiko, nimesema madaktari walitakiwa tokea mwanzo waeleze tatizo lao ni maslahi siyo kila mara kugeuka kama vinyonga; walianza na interns na sasa maslahi bora. Pia wanashinikiza masuala yaliyo nje ya uwezo wao: KUMTAKA BLANDINA, DR. DEO NA DR. NKYA WATUMULIWE! hata siku moja serikali iliyopewa dhamana na watz kwa kura nyingi haiwezi kufuata matakwa ya kila kundi ndani ya jamii
Kumbe ni wewe wasalimie bagamoyo.
 
kikwete asicheze na afya zetu ameshatuchezea sana na suala la umeme katika hili hatukubali kamwe waalimu amewazungusha hajawalipa richmond kawalipa huu si ujinga?
 
:lol:safi sana madaktari.....bigup!,endelezeni mgomo,imekuwa ni kawaida kwa hii serikali ya Tanzania kufanya mabadiliko kwa kushindikizwa,by the way pia unadhalau sana fani za watu,wkt shule yenyewe inabana...c sawa kabisa daktari kulipwa 700,000/=hiki ni kipimo pia kuona serikali unawajali vp wananchi wake...je wataleta wale madaktari wao wa jeshi?
MADAKTARI wametangaza rasmi kuanza mgomo katika hospitali zote za rufaa na vituo mbalimbali vya afya nchini kote hadi hapo madai yao yatakaposhughulikiwa na Serikali. Pia wamepitisha azimio la kumtaka Rais Jakaya Kikwete kuifumua na kuiunda upya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa kuwaondoa kwenye nyadhifa zao Waziri Dk Haji Mponda na Naibu wake, Dk Lucy Nkya kutokana na kile wanachodai kuwa ni kudhalilisha taaluma yao.

Dk Uliomboka pia aliwataja Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Blandina Nyoni na Mganga Mkuu wa Serikali, Dk Deo Mtasiwa kwamba wanapaswa kuwajibishwa na Rais. Akitangaza mgomo huo, Dar es Salaam jana Mwenyekiti wa Kamati ya Muda ya Jumuiya ya Madaktari hao, Dk Stephene Ulimboka alisema hatua hiyo inalenga kupata ufumbuzi wa madai waliyotoa kwa muda mrefu na kuongeza kwamba, leo wanatarajia kukutana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.


Dk Ulimboka alitaja baadhi ya madai yao kuwa ni kuwawekea mazingira bora ya kazi madaktari kwa kupeleka vifaa vya kazi hospitalini na kwenye vituo vya afya, kuboresha malipo ya posho na kuwapatia sitahili zote wanataalamu hao. Hata hivyo, tafauti na ilivyokuwa awali, kikao cha jana ambacho kilikuwa cha majumuisho, kilitumika pia kupokea ripoti ya mikutano iliyokuwa ikiongozwa na Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) na kupokea majukumu ya kuongoza harakati hizo.


“Kuanzia leo tunatangaza kuwa madaktari wote wanaoguswa na hili kote nchini kuacha kufanya kazi hadi hapo Serikali itakapotekeleza madai yetu, tunataka Serikali iboreshe mazingira ya kutolea huduma za afya, ili kumwezesha daktari kumpatia huduma mgonjwa katika kiwango kinachostahili,” alisema Dk Ulimboka.

Alitaja madai mengine matatu ambayo kamati anayoiongoza inasimamia kuhakikisha yanatekelezwa kuwa ni pamoja na madaktari kurejeshewa nyumba za kuishi kama inavyoelekezwa kwenye ‘Standard order’ ya Serikali, ambayo inasema daktari atapatiwa nyumba ya kuishi na Serikali na kama sivyo atapatiwa asimilia 30 ya mshahara.

Alisema kipengele hicho kiliondolewa kinyemela bila wao kushirikisha wala kuelezwa sababu za kuondolewa kwake, jambo linalowaongezea ugumu wa maisha na kuwafanya wadharaulike. Madai mengine yalihusu nyongeza za mishahara, ambayo alisema kumekuwa na ugumu wa kutekeleza suala hilo kila mara hadi wanapofanya mgomo.

“Mwaka 2005 wakati tunaanza kazi, mshahara wa daktari ulikuwa unafikia Sh124, 000, lakini baada ya mgomo ndipo ukapandishwa hadi kufikia karibu ya laki 700,000 sisi tunataka suala hili lirekebishwe na nyongeza yake isisubiri shinikizo,” alisema.

Madai mengine ni malipo kwa madaktari pindi wanapofanya kazi katika mazingira hatarishi na kupendekeza walipwe asimilia 30 ya mshahara wao, posho wakati wa kazi ya ziada ambayo kwa sasa wanalipwa asimilia 10 ya mshahara wao. Kuhusu mshahara, alisema yapo mapendekezo ambayo alisema wataitaarifu Serikali watakapokutana na viongozi wake.Madaktari hao leo wanatarajia kuendelea na mkutano wao katika ukumbi wa Don Bosco.

Rais wa MAT, Dk Namala Mkopi alisema alikabidhi majukumu kwa kamati iliyoundwa na wanachama baada ya kuonekana kuwa hadi sasa Serikali imekuwa ikiwazungusha. “Wanachama wamesema hapo mlipofikia tunashukuru mmejitahidi vya kutosha na sasa tunaomba mtukabidhi majukumu ili shughuli hii iweze kusimamiwa na kamati ya madaktari,” alisema Dk Mkopi.

Hatua hiyo imelenga kuongeza wigo wa washiriki ambao watawahusisha madaktari wasio wanachama wa MAT na wafanyakazi wengine katika sekta hiyo ya afya.

Mwananchi

 
Ni mwendo wa migomo tu, serkal gan inakosa usikivu, posho za wbunge zinaongezwa fasta lkn matabibu wanapgwa danadana.
 
Huyu Blandina Nyoni sijui yukoje, na pengine najiuliza kwa nini wanawake wakishika madaraka ya juu huwa na kiburi sana?

huyo ana kiburi tangu akiwa mhasibu mkuu wa serikali....nakumbuka kumuona katika TV wakati huo akimshambulia Utouh baada ya CAG kutoa Audit Report yake ambayo ilionyesha kuwa serikali kuu ni miongoni mwa sehemu ambazo fedha zetu walipa kodi zimekuwa zikipotea bila kujulikana.
 
Hivi hawa Madoc wanagoma kumtibu nani anae wasikiliza?? kwasababu wanaemgomea ni mgonjwa ambae hakuwaaajiri kazi . sasa basi wangeshauriana na Madoc wa India wagome wanakotibiwa wakubwa wanpoumwa malaria 2 au wanapokwenda kwa chekup.

Endeleeni kugoma mpaka wahusika watambue kua fani Muhimu ni ya udactari Hata wakikataa watambue hilo na sisi wananchi tuunge mkono kuihoji serikali kua kodi zetu zinakwenda wapi kama hatutibiwi . :A S embarassed:
 
Sijawahi kusikia Wabunge wakilalamikia serikali kucheleweshewa malipo au kutosikilizwa madai ya nyongeza zao za mishahara, posho na malupulupu mengine. Mihimili mingine ni malalamiko kila kukicha na haki hawaipati bila migomo na maandamano.

Hivi chakula cha watumishi hawa wa mihimili mitatu kinapikwa vyungu viwili tofauti au ni chungu kile kille kimoja?

Kama chungu ni kile kile kwa nini mpakuaji awe na upendeleo wa kujasa sahani ya wabunge hadi ifurike na wengine kuwatilia kijiko kimoja kinachoishia kuamsha tu hamu ya chakula bila shibe?
 
Yaani hawa madaktari nawafagilia kwa msimamo wao. Ila wakilegeza huo msimamo wao huo watakuwa ndio the last cadre kujidhalilisha beyond imaginable boundaries. Msiwe kama walimu ambao kila uchao hawajui destiny yao,onyesheni kuwa mnamaanisha mnachokiongea na kukidai.

@NDYOKO kama unafuatila historia madaktari tumefanya hivi mara kadahaa 95 Meghji akajiururu,2005 H.mwinyi alitufuata uumbini saa tano ya usiku na mishahara ikapandishwa kwa cdre zote za serikali ukianzia na afya cha muhimu tunaomba sapoti yenu ndugu zetu kwani at the end madai yetu nimadai ya watumishii wa umma na mwishowe ni heri kwa mwananchi wa kawaida
 
Oooh...madai ya madaktari ni ya msingi...sina shaka hata kidogo...kila jambo waliloliainisha katika ''hati yao ya mgomo" ni la msingi na halistahili kupuuzwa...lakini chonde matabibu,wanaoumia si wanasiasa...si Bi Blandina so far hata mafua atapelekwa India...Naandika kwa uchungu mkubwa kwa bado hata week mbili hazijakatika tokea mke wa rafiki yangu apoteze mtoto baada ya kukosa uangalizi stahiki kutokana na sakata la Muhimbili...kumbukeni kiapo chenu (mlokwisha kua kazini) na Ethics kwa mlio vyuoni katika tasnia ya utabibu!
 
Serikali yetu imezoea mabavu tu haina jambo lingine sijui tunaelekea wapi???.... mm hainijii akilini mtu unaalikwa kwenye shughuli waandaji wamekualika halafu unasema huwezi kuja kwenye huo ukumbi labda ukimbi flani!! hivi mtu akialikwa harusini huwa anachagua ukumbi ama anafuata ukumbi wa sherehe.

Mama Nkya kubali kuwa umechemka kwani ulipoletewa barua ya mwaliko yenyekuonyesha pahali pa tukio halafu ukaja pindisha dk za mwisho wakati ulisha kubali mwaliko kweli hainiingi akilini. Umekiri wizara yako imepokea barua, watu wamejianda wamekaa wanasubiri halafu unakuja eti huwezi kwenda huko wao wakuuate ww kwa sababu unazozijua mwenyewe.... watu 3 ama 4 ndio wanaosababishahii kero. Sie walala hoi tumezoea na hatuna sehemu ya kukimbilia kwenye matibabu zaidi ya hizi hospital zetu za ndani, lakini nyie viongozi checkup zenu za matibabu SouthAfrica,UK,India.

Mtanzania wakawaida hadi aje apewe kibali cha kwenda nje ya nchi kwa matibabu ni shughuli wengine hadi mauti inawakuta kwa ukiritimba wa wizara, kweli inasikitisha sana unamgonjwa yuko hoi matibabu hapa imeshindikana ukipewa kibali na dokta cha kumpeleka india mgonjwa ukifika serikalini (wizarani) unaambiwa hakuna hela lakini ngoja viongozi aanguke tu kwa kujikwaa dakika india saa hiyo pesa imetoka wapi??? viongozi wote huwa hawasubirishi kama wanalala hoi ni kwasababu gani???

Mgonjwa akifikishwa nje lawama zinamwangukia daktari aliemtibu wakati kosa sio lake la kumchelewesha mgonjwa.... mfano mzuri yule kijana wa ze komedi amesota muhimbili muda gani hadi amekuja kupelekwa india hali ni mbaya sana wakati angewaishwa mapema kijana wa watu ungekuta kesha pona anaendelea na kazi zake lakini mmemuweka muhimbili miezi kwa miezi kilasiku ugonjwa unakuwa uanasambaa mnategemea nini???

Hongereni Madaktari kwani mmedharauliwa vya kutosha, serikali kazi kutunyonya wao wakiugua hata ndege wanakodi wanakimbilia india. Hadi kieleweke safari hii walianza Kenya, sasa zamu ya Tanzania tukimaliza sie Uganda!:poa
 
Hoja zako hazina mshiko, nimesema madaktari walitakiwa tokea mwanzo waeleze tatizo lao ni maslahi siyo kila mara kugeuka kama vinyonga; walianza na interns na sasa maslahi bora. Pia wanashinikiza masuala yaliyo nje ya uwezo wao: KUMTAKA BLANDINA, DR. DEO NA DR. NKYA WATUMULIWE! hata siku moja serikali iliyopewa dhamana na watz kwa kura nyingi haiwezi kufuata matakwa ya kila kundi ndani ya jamii

kura nyingi za MKONO WA MUNGU,
 
Nini kinaendelea mawodini, tuambieni watumia mitishamba
 
Bado siamini kama masrahi ya madaktari wanayolipwa sasa hayatoshi,mimi naamni madaktari mmesahau kuwa kazi yenu siyo kazi pekee hapa tanzania na kwamba hakuna serikali ambayo itawabagua watumishi wake.

Mmekiri wenyewe kwamba mwaka 2005 mlikuwa mnaloipwa 124,000 leo mnalipwa 700,000 kwanza nampongeza jk na nawataka mfahamu kuwa kuomba nyongeza kwa kujilinganisha na wanasiasa ni ujinga, kama mnataka posho za siasa nendeni mkagombee, dunia nzima posho za wanasiasa ziko juu na watumishi wanalipwa kwa scales zao kulingana na policy.


Wewe ni kanyasumu et au kanya nini?Anyway
Thamani yakoo waijua wewe madaktari wanaijua thamani yao na kazi yao ni si kwamba eti hawajali maslahi ya wananchi lakini anayewajibika kuhudumia wananchi ni Serikali
  • kupata risk allowance ni haki yetu kwani mazingira yetu yanatisha na wewe hapo unayaogopa hata nikikualika kazini kwangu utakimbia ila mie na uhakika ukinialika kazini kwako nitapiga tu kazi
  • kulipwa hiyo posho ni haki yetu na imeandikwa kwenye miongozo ya serikali lakini hawataki kutulipa tunafanya kazi masaa 36 unalipwa 10000/= yaaani shilingi mia mbili 277.8 kwa saa hii ni haki kweli.kwa hiyo nikikaa masaa nane kama waheshimiwa nitalipwa 277 x 8=2222.22/=
  • Nyumba ni haki yetu twapaswa kulipwa.....kama ilivyoandikwa kwenye miongozo na inabadilishwa na watu kadhaa tu walafi kwanza.
  • Mishahara wa kunitosha ili niweze kuhudumia wagonjwa/wateja wangu ni muhimi ili nipate muda wa kusoma na niweze kuwajali wagonjwa wangu vizuri kabisa.
 
Jamani naomba niulize huyu Blandina nyoni kasomea hii professional ya udaktari? au kapewa kama katabia kao hawa jamaa.

Blandina Nyoni ni Certified Public Accountant, Aliwahi kuwa Mhasibu Mkuu wa Serikali kwa hiyo akina Kikwete wamempeleka akatumia uzoefu huo Pale wizara ya afya.
 
Hakuna mgomaji hapo,tishia nyau tu.
Mbona nimepita rufaa mbeya na nimepewa huduma au mgomo ni
kwa baadhi ya siku tu?

Premium member nafikiri utakuwa na balance disorder kwa jinsi kichwa chako ambavyo hakituliagi
MRH aka Mbeya referall hospital nenda kesho ukajionee ni kweli hawajaanza kazi
 
Back
Top Bottom