Maendeleo ya Mgomo wa Madaktari na Mwitikio wa Serikali

Madaktari wakigoma na walimu wakigoma sijui kama tutakuwa na product ya baadaye
 
Huduma zinatolewa...lakini si kama kawaida. katika kila kitengo kwatika hospitali hizo wameachwa madaktari wachache kuhudumia wagonjwa wa dharura (emergency)...clinic zote leo zimefungwa Temeke, Amana, Ilala, na Muhimbili ( pamoja na MOI na Ocean Road). Kwa kifupi mgomo umeanza japo taratibu lakini mpaka kesho huduma nyingi zitakuwa zimefreeze.

Kama unadhani utani nenda sasa hivi pale Don Bosco uone kuna madaktari wangapi wapo pale kwa mkutano tangu asubuhi, na huko mikoani leo jioni hii wanaitisha vikao, tayari Bugando, Mount Meru, Mbeya Referral na Mbeya Regional wameshaconfirm kufanya vikao jioni hii kujiunga na mgomo...hali itakuwa mbaya siku chache zijazo.

Kwa kuongezea tu, Dodoma kikao kimeshakwisha na mgomo umeshaanza. Kesho ni vikao vingine vinaendelea
 
Huduma zinatolewa...lakini si kama kawaida. katika kila kitengo kwatika hospitali hizo wameachwa madaktari wachache kuhudumia wagonjwa wa dharura (emergency)...clinic zote leo zimefungwa Temeke, Amana, Ilala, na Muhimbili ( pamoja na MOI na Ocean Road). Kwa kifupi mgomo umeanza japo taratibu lakini mpaka kesho huduma nyingi zitakuwa zimefreeze.

Kama unadhani utani nenda sasa hivi pale Don Bosco uone kuna madaktari wangapi wapo pale kwa mkutano tangu asubuhi, na huko mikoani leo jioni hii wanaitisha vikao, tayari Bugando, Mount Meru, Mbeya Referral na Mbeya Regional wameshaconfirm kufanya vikao jioni hii kujiunga na mgomo...hali itakuwa mbaya siku chache zijazo.
  • All the best colleagues....this is what we want to see....gomeni haswa haswa pasi na kikomo mpaka watawala wawasikilize....kumbukeni haki hutaftwa.......safari hii kuweni kitu kimoja msichoke.....nice to see Dr.Ulimboka is in....last time kumsikia ni kwenye ule mgomo wa 2006 ambako kuna ma dr wengi walitaabika sana baada ya mgomo ule...i hope this time mtasimama kidete ili kupata tija ya mgomo...we support you guys....mi baada ya 2006 niliacha tiba nikaingia kwenye research and development(R&D)kwasababu tu kuondokana na hizi kero za serikali yetu hii..
  • Kwasababu serikali hii inaonyesha kutowajali professionals wake kwa kiasi kikubwa huku wakishabikia wapuuzi,wezi wa mali za umma na wapiga siasa feki, ni wakati muafaka sasa kwa nchi hii nao professionals wa ngazi zote wasimame sasa na kuhesabiwa kwa kudai haki zao zinazoporwa na walafi wachache kwenye utawala huu.Ni wakati wa madaktari wooote nchini kugoma kwa hakika kwani ni wao ambao wanaweza kuwa organized kimsimamo kwenye kudai haki zao.Nasema wagome madaktari haswa wale walioko kwenye hospitali zote za rufaa nchini ambako huduma muhimu hazitaenda bila wao kuwepo .Wasimame wagome haswa maana wamezidi kudharauliwa na watawala....Nchi hii migomo huwa inaishia kuumizana kwa kuwa mara nyingi watu wanasalitiana na pia vyama vyao havikai nao kuwapa support.....mara zote migomo tunayoona inaleta mabadiliko duniani ni ile inayokuwa pasi na kikomo mpaka shida zinapopatiwa majibu.....huu ndio msingi wa mgomo, lakini hapa tz watu wanagoma kikondoo (tunaona kwa waalimu,wanafunzi etc etc...).....wanatishiwa nyau then wanafarakana na kuwapa watawala ushindi......hii si migomo....mkiamua kugoma gomeni haswa.......hii ni sacrifice yaani(mnatakiwa kuwa sacrificial lambs)....unaweka nyanga zote pembeni unaitafuta haki.......hapa tz sijaona migomo ya namna hii........chondechonde madaktari......na wataalam wengine watafuata maana ni professionals wengi nchi hii ambao wanataabika na utawala huu........wengi hawasemi kwa kuwa hawana jinsi lakini professionals tz hawana thamani mbele ya watawala...wenye kuthaminiwa nchi hii ni mafisadi na wanasiasa feki wanaocheza ngoma ya watawala......time to wake up.....kumbukeni JK alitukana wafanyakazi kabla ya uchaguzi uliopita...akionyesha dhairi namna gani hajali wafanyakazi nchi hii......
 
@NDYOKO kama unafuatila historia madaktari tumefanya hivi mara kadahaa 95 Meghji akajiururu,2005 H.mwinyi alitufuata uumbini saa tano ya usiku na mishahara ikapandishwa kwa cdre zote za serikali ukianzia na afya cha muhimu tunaomba sapoti yenu ndugu zetu kwani at the end madai yetu nimadai ya watumishii wa umma na mwishowe ni heri kwa mwananchi wa kawaida

mimi imani yangu ni ndogo sana kama mtaweza kugoma!!hiyo miaka unayotaja kuwa mlifanikiwa mlikuwa mnategeshea kwenye miaka ya uchaguzi mkuu,mwaka huu hakuna uchaguzi mkuu naamini kuwa mtazuka na kauli kuwa mnawaonea huruma wagonjwa na kurudi mzigoni,ila madaktari mlikuwa na uwezo kuitikisa serikali mpaka wakatuheshimu watumishi na tungeepuka kuitwa mbayuwayu.
 
Mhhh, hivi watawala wapo? wanataka mpaka watu wangapi wafe? maana kama kufa kuna watu wamesha kufa haijaripotiwa tu. Kama tulidhani Tanzania ni Kisima cha amani, nasikitika sana kuwa tunu hiyo ndiyo hiyoo inaishia zake. Subirini mgomo mwingine toka association nyingine muhimu soon. Ila tu funga kazi itakuwa ya hawa Machinga watakapoamua kuingia barabarani na kutoa hasira zao. Subirini muone.
 
madaktari kazeni buti hivyo hiyo wala msidanganyike kama wanaweza kuwalipa wakina mrema na wakina wasira wanaolala bunge sembuse nyinyi msikubali hata kidogo
 
MADAKTARI wametangaza rasmi kuanza mgomo katika hospitali zote za rufaa na vituo mbalimbali vya afya nchini kote hadi hapo madai yao yatakaposhughulikiwa na Serikali. Pia wamepitisha azimio la kumtaka Rais Jakaya Kikwete kuifumua na kuiunda upya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa kuwaondoa kwenye nyadhifa zao Waziri Dk Haji Mponda na Naibu wake, Dk Lucy Nkya kutokana na kile wanachodai kuwa ni kudhalilisha taaluma yao.

Dk Uliomboka pia aliwataja Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Blandina Nyoni na Mganga Mkuu wa Serikali, Dk Deo Mtasiwa kwamba wanapaswa kuwajibishwa na Rais. Akitangaza mgomo huo, Dar es Salaam jana Mwenyekiti wa Kamati ya Muda ya Jumuiya ya Madaktari hao, Dk Stephene Ulimboka alisema hatua hiyo inalenga kupata ufumbuzi wa madai waliyotoa kwa muda mrefu na kuongeza kwamba, leo wanatarajia kukutana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.


Dk Ulimboka alitaja baadhi ya madai yao kuwa ni kuwawekea mazingira bora ya kazi madaktari kwa kupeleka vifaa vya kazi hospitalini na kwenye vituo vya afya, kuboresha malipo ya posho na kuwapatia sitahili zote wanataalamu hao. Hata hivyo, tafauti na ilivyokuwa awali, kikao cha jana ambacho kilikuwa cha majumuisho, kilitumika pia kupokea ripoti ya mikutano iliyokuwa ikiongozwa na Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) na kupokea majukumu ya kuongoza harakati hizo.


“Kuanzia leo tunatangaza kuwa madaktari wote wanaoguswa na hili kote nchini kuacha kufanya kazi hadi hapo Serikali itakapotekeleza madai yetu, tunataka Serikali iboreshe mazingira ya kutolea huduma za afya, ili kumwezesha daktari kumpatia huduma mgonjwa katika kiwango kinachostahili,” alisema Dk Ulimboka.

Alitaja madai mengine matatu ambayo kamati anayoiongoza inasimamia kuhakikisha yanatekelezwa kuwa ni pamoja na madaktari kurejeshewa nyumba za kuishi kama inavyoelekezwa kwenye ‘Standard order’ ya Serikali, ambayo inasema daktari atapatiwa nyumba ya kuishi na Serikali na kama sivyo atapatiwa asimilia 30 ya mshahara.

Alisema kipengele hicho kiliondolewa kinyemela bila wao kushirikisha wala kuelezwa sababu za kuondolewa kwake, jambo linalowaongezea ugumu wa maisha na kuwafanya wadharaulike. Madai mengine yalihusu nyongeza za mishahara, ambayo alisema kumekuwa na ugumu wa kutekeleza suala hilo kila mara hadi wanapofanya mgomo.

“Mwaka 2005 wakati tunaanza kazi, mshahara wa daktari ulikuwa unafikia Sh124, 000, lakini baada ya mgomo ndipo ukapandishwa hadi kufikia karibu ya laki 700,000 sisi tunataka suala hili lirekebishwe na nyongeza yake isisubiri shinikizo,” alisema.

Madai mengine ni malipo kwa madaktari pindi wanapofanya kazi katika mazingira hatarishi na kupendekeza walipwe asimilia 30 ya mshahara wao, posho wakati wa kazi ya ziada ambayo kwa sasa wanalipwa asimilia 10 ya mshahara wao. Kuhusu mshahara, alisema yapo mapendekezo ambayo alisema wataitaarifu Serikali watakapokutana na viongozi wake.Madaktari hao leo wanatarajia kuendelea na mkutano wao katika ukumbi wa Don Bosco.

Rais wa MAT, Dk Namala Mkopi alisema alikabidhi majukumu kwa kamati iliyoundwa na wanachama baada ya kuonekana kuwa hadi sasa Serikali imekuwa ikiwazungusha. “Wanachama wamesema hapo mlipofikia tunashukuru mmejitahidi vya kutosha na sasa tunaomba mtukabidhi majukumu ili shughuli hii iweze kusimamiwa na kamati ya madaktari,” alisema Dk Mkopi.

Hatua hiyo imelenga kuongeza wigo wa washiriki ambao watawahusisha madaktari wasio wanachama wa MAT na wafanyakazi wengine katika sekta hiyo ya afya.

Mwananchi

Siyo sahihi kugoma kutibu wagonjwa kisa madai. Binadamu yoyote anaunga mkono daktari kugoma kutibu mgonjwa kisa madai hana tofauti na gaidi. Ni muuaji huyo. Hivi ni wafanyakazi wangapi wanafanyakazi bila posho? Daktari analipwa Tsh. 700000(laki saba) na posho ya asilimia 10, wakati huo huo kuna mtu analipwa Tsh. elfu themanini(80,000/=) na wote wanahitaji kula, wanasomesha n.k. Hakika unyeti wa kazi zao madaktari mimi hainishawishi niunge mkono watende dhambi ya kuua. Maana huo ni unyama. Hivi jeshi letu likisema linagoma patatosha kweli? au wao wana mishahara mikubwa kuliko Madaktari? au Jeshi siyo nyeti kuliko daktari?. Sasa wakitaka walipwe posho nyingi si ni wazi kwamba hawatapata hata wagonjwa wa kutibu kwa vile tayari watakuwa wameshakufa kwa njaa baada ya fedha zote kuelekezwa kwao? Najua wengi watasuta mtazamo wangu ila kweli utabaki pale pale kwamba hawa Madaktari wanagoma siyo kwamba hawaridhiki na kile wanacholipwa , bali ni kiburi tu cha kutaka kuonesha kwamba wao ndiyo wameshikilia uhai wetu na kwa maana hiyo wanaweza kufanya wapendavyo. Hii kwa mujibu maandiko ya vitabu vitakatibu ni kiburi, majivuno na kwa maana hiyo Shetani ameshatawala mioyo yao. Watanzania tuzidi kuomba shetani asichukue nafasi yake.
 
Mie naona sawa tu, maana hata kabla hawajagoma mlalahoi ilikuwa ishu kupata huduma pale muhimbili na hosp. nyingine za rufaa
 
Mbona kuna mahali nilisoma kuwa Maintern waliofukuzwa Muhimbili ni zaidi ya 1900. Sasa kama wanaweza kuwa intern wote hao ambao ni miaka miwili tu inakuwaje kwa miaka 50 ya uhuru bado tuna madaktari 2000 tu???

ilikuwa 194 mkuu na sio 1900
by the way intern waliofukuzwa walikuwa jumla ya 229 ikijumuisha na cadre zingine kama nursing,pharamacists, na wateknolijia wa maabara
 
This is the noble profession ucfananishe na walimu. Mgomo lazima uwe na hatua ndefu, manake unahusisha maisha ya watu. Anyway asante kwa hiyo challenge, tunaanza rasmi.
 
hebu wekeni facts basi, tusiwe tunapiga gumzo la sokoni, we need facts here, so that, information can reliable.
Afadhali umeliona hilo. Tunafanya ushabiki hata kwenye uhai wa watu. Hata kama Serikali ingekuwa na makosa kiasi gani mimi sisubutu kuunga mkono na kushabikia mgomo wa madaktari. Lipi la muhimu kwanza, Maslahi ya Daktari au uhai wa wagonjwa?.
 
Ninawashangaa sana wanaosuport huu mgomo...hawajui what is going to happen to them in the next few minutes, assume unapata ajali, unafikishwa MOI unakuta hamna huduma...sijui utamlaumu nani!!
Chamuhimu ni madaktari wakae na wahusika(serikali) wasolve matatizo yao. Naamini wataafikiana.
 
Afadhali umeliona hilo. Tunafanya ushabiki hata kwenye uhai wa watu. Hata kama Serikali ingekuwa na makosa kiasi gani mimi sisubutu kuunga mkono na kushabikia mgomo wa madaktari. Lipi la muhimu kwanza, Maslahi ya Daktari au uhai wa wagonjwa?.

vyote muhimu,daktari na mgonjwa
 
Afadhali umeliona hilo. Tunafanya ushabiki hata kwenye uhai wa watu. Hata kama Serikali ingekuwa na makosa kiasi gani mimi sisubutu kuunga mkono na kushabikia mgomo wa madaktari. Lipi la muhimu kwanza, Maslahi ya Daktari au uhai wa wagonjwa?.

utamsaidiaje mgonjwa wakati huna uhakika wakupata chakula na nyie mkiombwa hela mnajifanya ooh mnatuomba rushwa wagonjwa ni wagonjwa na madaktari ni madaktari inapofikia muda wakumpa haki yake mpe sio unamzungusha mie naunga mkono ili la mgomo na wanufaike na magonjwa yatapungua..

RIP TZ..
 
Ninawashangaa sana wanaosuport huu mgomo...hawajui what is going to happen to them in the next few minutes, assume unapata ajali, unafikishwa MOI unakuta hamna huduma...sijui utamlaumu nani!!
Chamuhimu ni madaktari wakae na wahusika(serikali) wasolve matatizo yao. Naamini wataafikiana.

mkuu rejao inaonekana kabisa walishakaa nao wakaona hawasikilizwi hamna mtu anaekurupuka tu na kuanza kufanya mgomo na migomo mingi huwa inatokana na kutokusikilizana wakati wa makubaliano..
 
Ninawashangaa sana wanaosuport huu mgomo...hawajui what is going to happen to them in the next few minutes, assume unapata ajali, unafikishwa MOI unakuta hamna huduma...sijui utamlaumu nani!!
Chamuhimu ni madaktari wakae na wahusika(serikali) wasolve matatizo yao. Naamini wataafikiana.

safi mkuu! leo naona una mawazo safi sana, serikali inatakiwa kukaa na hao jamaa wasiendekeze ubabe, wanaoumia ni mama, dada au ahta wadogo zetu
 
Afadhali umeliona hilo. Tunafanya ushabiki hata kwenye uhai wa watu. Hata kama Serikali ingekuwa na makosa kiasi gani mimi sisubutu kuunga mkono na kushabikia mgomo wa madaktari. Lipi la muhimu kwanza, Maslahi ya Daktari au uhai wa wagonjwa?.

Maslahi ya wabunge!
 
Back
Top Bottom