Maendeleo ya China yaliletwa na Katiba Mpya?

Maendeleo ya China yaliletwa na Katiba Mpya?

Mawazo duni sana. China walishafanya ukombozi wa fikra kwa kila raia.Wamepitia vipindi ambavyo sisi hatujafkia. Kutetea udikteta kwa kujilinganisha na China ni uzuzu. Usifundishe watu ujinga.
 
Hatuji ila tutasema. Maendeleo ya China yameletwa na uongozi bora. Maendeleo ya Rwanda yameletwa na uongozi bora. Mwalimu alisema: "Ili tuendelee tunahitaji watu siasa safi na uongozi bora." Hakusema na katiba mpya. Maendeleo ya Tanzania yataletwa na uongozi bora. Watu wakiuunga mkono uongozi wa Awamu ya 5, kama walivyounga mkono uongozi wa awamu zote tutapata maendeleo. Tunaona itihada za Raisi wa awamu ya 5 katika kuleta uongozi bora nchini.Bial shaka hatua za kuelekea kupata maendeleo zimekwisha anza kuonekana.

usiolijua ni kwamba siasa bora na uongozi ulio bora unaletwa na katiba iliyo bora
 
Katiba haileti maendeleo, lakini ni kwa namna gani Katiba mpya itazuia maendeleo unayoyaongelea? Ni kubadili tu maandishi na kupunguza nguvu kwenye taasisi moja na kuongeza kwenye taasisi nyingine. Labda sababu iwe si kipaumbele na haipo kwenye ilani ya chama tawala kwa sasa. Kama jinsi ambavyo Katiba haihusiki na kuleta maendeleo hivyo hivyo haizuii hayo maendeleo kuja. Maendeleo yanaletwa na Watz tena wa kawaida, Wachapakazi na Walipa Kodi. Katiba hata tukiibadili Watz Wachapakazi na Walipa kodi wataendelea kufanya majukumu yao kama kawaida.

chief kuna mahusiano makubwa kati ya katiba bora na maendeleo!. Marekani ndyo taifa tajiri duniani lkn ukiangalia siri ya mafanikio yao, utagundua ubora wa katiba yao umechangia pakubwa . katiba inayosisitiza nchi kwanza hlf maslahi ya mtu mmoja mmoja ndyo yanafuata sio huku bongo rais kapewa madaraka makubwa mpk anaamua kujenga airport kwao ambayo ni useless huku wanafunzi wanasomea nje kwa kukosa madarasa
 
Hatuji ila tutasema. Maendeleo ya China yameletwa na uongozi bora. Maendeleo ya Rwanda yameletwa na uongozi bora. Mwalimu alisema: "Ili tuendelee tunahitaji watu siasa safi na uongozi bora." Hakusema na katiba mpya. Maendeleo ya Tanzania yataletwa na uongozi bora. Watu wakiuunga mkono uongozi wa Awamu ya 5, kama walivyounga mkono uongozi wa awamu zote tutapata maendeleo. Tunaona itihada za Raisi wa awamu ya 5 katika kuleta uongozi bora nchini.Bial shaka hatua za kuelekea kupata maendeleo zimekwisha anza kuonekana.
Rwanda wameendelea?
 
Hilo sio taifa la kutolea mfano. Ni taifa la kihuni halina profesa hata mmoja mpaka sasa. Lina wahuni tu magaragaja wenye wanaosoma mpaka MBA na kuishia kutengeneza marembo ya wanawake na watoto
 
August,
China ilikuwa na ina chama kimoja mpaka sasa. Wakati Tanzania kwa sasa ina katiba inayotambua vyama vingi.

China ilifanya "Mapinduzi ya Kitamaduni" 1966-1976 badala ya kuleta vyama vingi baada ya kuona Wazee wa Kikomunisti China wameishiwa 'pumzi' ya kuleta Mapinduzi ya kifikra waweze kuwa nchi ya viwanda na uchumi mkubwa.

CCM walishiwa 'pumzi' na kuamua kuleta mfumo wa vyama vingi 1992 kikatiba Ili kukaribisha fikra na pumzi mpya. Ikiwa kweli CCM wanajiamini wafute mfumo wa vyama vingi na kuitupilia mbali katiba ya Kidemokrasia.

Tujiulize je CCM ina uwezo wa kuleta fikra mpya ktk vichwa vya watanzania kuondokana na mfano fikra kuwa kiwanda ni vyerehani vinne, elimu yetu ifumuliwe upya tuweze kujitegemea kwa kuleta mapinduzi ktk kilimo cha kisasa (Kilimo Kwanza) na viwanda vikubwa vya kufua chuma, kucheketa aluminium, Dhahabu, kuchonga Vito, viwanda vya Pamba / nguo n.k

Nini kilipelekea China kuleta Mapinduzi ya kifikra / tamaduni 1966 -1976 :

What were the four olds in the Cultural Revolution?
The Four Olds or the Four Old Things (simplified Chinese: 四旧; traditional Chinese: 四舊; pinyin: sì jiù) were Old Customs, Old Culture, Old Habits, and Old Ideas. One of the stated goals of the Cultural Revolution in the People's Republic of China was to bring an end to the Four Olds.

1911-1959
Mao had toured China and concluded that the Chinese people were capable of anything and the two primary tasks that he felt they should target was industry and agriculture. Mao announced a second Five Year Plan to last from 1958 to 1963. This plan was called the Great Leap Forward.

The Great Leap Forward planned to develop agriculture and industry. Mao believed that both had to grow to allow the other to grow. Industry could only prosper if the work force was well fed, while the agricultural workers needed industry to produce the modern tools needed for modernisation. To allow for this, China was reformed into a series of communes. After the catastrophic failures of the Great Leap Forward Mao Zedong withdrew from active rule and left Liu Shaoqi, Zhou Enlai and Deng Xiaoping Deng Xiaoping and the Transformation of China — Ezra F. Vogel | Harvard University Press to guide the economy to recovery (1981- to-date)


Ezra Vogel: The Transformation of China

Deng Xiaoping: the leader who shaped contemporary China. Gelber Prize winner Ezra Vogel sits down with Steve Paikin to discuss China under Deng Xiaoping

Source:The Agenda with Steve Paikin


 
Hatuji ila tutasema. Maendeleo ya China yameletwa na uongozi bora. Maendeleo ya Rwanda yameletwa na uongozi bora. Mwalimu alisema: "Ili tuendelee tunahitaji watu siasa safi na uongozi bora." Hakusema na katiba mpya. Maendeleo ya Tanzania yataletwa na uongozi bora. Watu wakiuunga mkono uongozi wa Awamu ya 5, kama walivyounga mkono uongozi wa awamu zote tutapata maendeleo. Tunaona itihada za Raisi wa awamu ya 5 katika kuleta uongozi bora nchini.Bial shaka hatua za kuelekea kupata maendeleo zimekwisha anza kuonekana.
uongozi gani boe=ra wa kumiminiana marisasi na kutekana?uongozi wa kishamba lazima upingwe kwa nguvu zote.
 
Kama hujui kitu bora unyamaze unajidhalilisha. Hivi unalinganishaje Tanzania na China? Alafu mbona hutaki kwenda deep kwenye economic theory ujue what was behind China's rapid success?
 
Kumekuwepo na kelele kiasi toka kwa baadhi ya Watu ambao wanataka kufunganisha maendeleo ya Nchi yetu na Katiba Mpya au kwa kifupi maendeleo yanaendana na Katiba wanazofikiria wao zitawapa ''fursa''
Kwa mfano ndani ya KKKT tumeshihudia migogoro kadha sasa sijui wao Hiyo katiba mpya wataianzisha lini?? Na kuna viongozi wa Kiroho ambao utajiri wao unatokana na kuwadhulumu waumini wao kwa njia moja au nyingine ndio Maana hutakuta vitabu vyao vya mahesabu kuwa wazi zaidi ya kuwa somea waumini wao taarifa wanazo taka wao.
Ukija kwenye vyama vya siasa hadithi ni Hiyo Hiyo wakati wao wenyewe demokrasia wanayo ipigia kelele hawaienzi.
Ukija kwenye Suala la Maendeleo mfano china na mabadiliko Yao ya kiuchumi tunaona wame weza kufanya hivyo bila vyama vingi Bali kwa kuimarisha mifumo Yao ya kiutendaji wakati urusi walikwenda na Glasnot matokeo yake sote tunayajua Gorbachev akakosa nchi na Yeltsin na ulevi wake Ndio aka tawala nchi , matokeo yake nchi ilipojitambua wakamleta Putin ambaye Yupo madarakani kwa miongo miwili sasa.
Ukija hizo nchi za ulaya iwe Germany ya Hitler na wengineo tuangalie walivyo piga hatua za maendeleo ilikuwa kwa sababu ya katiba mpya au demokrasia au lilikuwa ni suala la uzalishaji na usimamiaji wa itikadi inayolenga ktk maendeleo.
Mimi nionavyo tupate maendeleo kwanza Ndio tutaweza kuweka hizo rangi zingine kulemba maendeleo yetu na sio kulemba kitu ambacho hatuna.
Ndiyo, katiba mpya imewasaidia China kwenye maendeleo yao. Kwani maendeleo ya China yameanza kuwa recognized miaka ipi?

Kuanzia mwaka 1911, wachina wamekuwa wakibadili katiba ama kuifanyia amendments(recently mwaka huu 2018)

Hadi sasa, wameshafanya hivyo mara 12. Mwaka wa 1954, ndipo wali adapt constitution ya kwanza ya “People’s Republic of China”, ambayo ndiyo iliwapeleka officially kwenye mfumo wa communism.

Kwa maana nyingine, hii ni katiba ya 12 kwa wachina toka mwaka 1911.

Mkuu usijiunge kwenye propaganda na kuazisha threads nyepesi nyepesi...njoo na facts.
 
usilinganinshe China na Tanzania kwa sababu zifuatazo

1) China hakuna wajinga kama bongo
2) level ya maendeleo kijamii na kielimu ni tofauti kabisa
3)China hakuna dubwasha linaloitwa ccm
4) Katiba yao sio mbovu kama yenu vile vile raisi wao haamkia asubuhi na kutoa matamko au kukirupuka kwenda kujenga airport bush kwao
5)raisi hateui watu hovyo hovyo hasa wananchi wakionesha kutokumkubali mfano bashite wenu
Mengine waweza ongezea maana unayajua sema unaleta uhayawani

Yaani kwa upupwu huo endelea tu kulia na kujipiga vibao vya usoni pia..
Usisshau kuendelea kujifunza kuacha uvivu na lugha mbovu.
 
Kwaio maendeleo yataletwa na bombadier, fly over, wakati unasigina katiba iliyopo
Hivi unaelewa kuwa hata wakati wa kukuwa kwa mtoto tumboni mwa mama yake, mfumo wa mwanzo mwanzo kabisa kuundwa ni ule wa "transport" (circulatory ystem).

Hivi wewe na akili yako unafikiri ni kwanini wakati wa world War 2 mataifa mengi jirani yalipigwa na Ujerumani?

Na baada ya vita Dwight Eisenhower, Rais wa 34 Marekani alifanya nini?

Hitler alijenga autobahn ambayo ukiachana na matumizi ya kawaida ilisaidia sana ku mobilize wanajeshi, vyakula na vifaa vya kivita kwa urahisi kabisa.

Rais Eisenhower ambaye alikuwa vitani wakati ule alishangazwa na mabarabara yale na jinsi yalivyotumika kifanisi vitani. Aliporudi na kuwa Rais alijenga Interstate and defence highway system. Ambayo imesaidia sana kuimarisha uchumi wa Marekani.

Msipende kubisha vitu msivyo vielewa Rais Magufuli anajitahidi mara mia kuliko hao watatu waliopita.
 
Though sitaki kuamini,kweli hujui kuwa Tanzania tuna MTU anaitwa rais kwa kuwa katiba yetu ya 1977 inatoa cheo hicho? Sasa huyo kiongozi bora na siasa safi unavipataje kama hauna katiba bora? Jamani sometimes tufikirie na kutanda kama watu wenye akili

Niliyemibu alizungumzia "katiba mpya" ndiyo kigezo. Hata ukipewa katiba mpya kama masuala muhimu hayapo ni bure tu. Kama itapitiliza ni bure pia. angejadili yanayopungua katika utawala bora ayainishe sio kusema tu "Katiba Mpya". Nilimnukuu Mwalimu kwa sababu yeye alitaja dhima ya utawala bora kwa kuanisiha vipengele muhimu ambapo katiba sasa ikija itaviingiza. Haitanguli katiba inatangulia dhana na mahitaji ndiyo yanapewa vifungu husika. Ndiyo maana yangu.
 
Ukiona gari bovu na kila mtu anashuka, kama kuna anaelalamika basi ameacha mzigo wake mle.
Mmm. Kwa aibu nitakujibu dada.

Sasa wakati "mnaubutua wa miundi" (nadhani umenielewa) halafu gari bovu limetengemaa na linamipita, mtasemaje?

Mtalisimasha mpande au ndio basi tena, DUNIA SIMAMA NISHUKE?
 
Hatuji ila tutasema. Maendeleo ya China yameletwa na uongozi bora. Maendeleo ya Rwanda yameletwa na uongozi bora. Mwalimu alisema: "Ili tuendelee tunahitaji watu siasa safi na uongozi bora." Hakusema na katiba mpya. Maendeleo ya Tanzania yataletwa na uongozi bora. Watu wakiuunga mkono uongozi wa Awamu ya 5, kama walivyounga mkono uongozi wa awamu zote tutapata maendeleo. Tunaona itihada za Raisi wa awamu ya 5 katika kuleta uongozi bora nchini.Bial shaka hatua za kuelekea kupata maendeleo zimekwisha anza kuonekana.
Siasa safi za kuua watu na kuminya demokrasia, siasa safi za kuiba kura, siasa safi za kuweka makada kuanzia kwenye tume mpaka wasimamizi, siasa safi za kutwangwa risasi pale unapokosolewa, acheni hizo hizo, siasa safi kwa kuwapa upendeleo mtu hata darasa la 7 hujui kamaliza shule gani, wengine unawatimua, siasa safi fanyeni kitu kwa haki kama mtaona mtu akilalamika, kuna mengi tu ya kusema ambayo yanaleta hasira, halafu yoote hayo hamyaoni, nitaomba yawakute ndio ujue hizi ni siasa safi
 
usiolijua ni kwamba siasa bora na uongozi ulio bora unaletwa na katiba iliyo bora
Ninachosema mimi ni kuwa inatangulia dhamira ya utawala na uongozi bora ndipo katiba inatengenezwa sio kudai tu katiba mpya pasipo kujua kwa hakika nini unahitaji katika katiba hiyo. Katiba peke yake haikamilishi utawala bora. Yapo mambo mengi ikiwemo dhamira njema ya wananchi. Kama wananchi watauchukia uongozi kwa kuuchukia tu hata wasione mazuri ya uongozi huo hata katiba ya aina gani ije wataipinga tu. Tumeyaona hayo katika nchi nyingi. Rwanda wananchi wake wameiona dhamira njema ya uongozi uliopo na wameungana na kuiunga mkono kwa nguvu na nchi inakwenda. Katiba iliyobadilishwa majuzi imetokana na dhamira ya wananchi. Tunaona nchi nyingi sana zinafuata mwelekeo huo. China wamefanya hilo na nchi nyingine. Dhamira njema ya watu inaweza kuleta katiba nzuri sana itakayolingana na matakwa yao. Tunadai katiba mpya, sawa lakini dhamira yetu sisi wananchi ni ipi? Kenya walidai katiba mpya wakaipata. Hata hiyo baada ya muda wameiona ina mapungufu makubwa na wameanza kufikiri kurekebisha maeneo fulani fulani. Hii inaleta swali katika dhamira waliokuwa nayo wakati wa kudai katiba mpya. Hiyo ndiyo maana yangu.
 
Pimbi sana wewe!! Rwanda wameendelea?
Nitukane lakini kila mtu anakubali ya kuwa ukilinganisha Rwanda ya 1994 na ya sasa ipo tofauti kubwa sana ya kimaendeleo. Mengi yameandikwa juu ya maendeleo ya kiuchumi ya Rwanda na vyombo husika wewe nishambulie tu lakini huo ndio ukweli. Hawajafika mahala fulani lakini wanpiga hatua.
 
Mmm. Kwa aibu nitakujibu dada.

Sasa wakati "mnaubutua wa miundi" (nadhani umenielewa) halafu gari bovu limetengemaa na linamipita, mtasemaje?

Mtalisimasha mpande au ndio basi tena, DUNIA SIMAMA NISHUKE?
Nimecheka sana
 
Back
Top Bottom