Maendeleo ya China yaliletwa na Katiba Mpya?

Maendeleo ya China yaliletwa na Katiba Mpya?

August

Platinum Member
Joined
Jun 18, 2007
Posts
10,882
Reaction score
6,977
Kumekuwepo na kelele kiasi toka kwa baadhi ya Watu ambao wanataka kufunganisha maendeleo ya Nchi yetu na Katiba Mpya au kwa kifupi maendeleo yanaendana na Katiba wanazofikiria wao zitawapa ''fursa''

Kwa mfano ndani ya KKKT tumeshihudia migogoro kadha sasa sijui wao Hiyo katiba mpya wataianzisha lini?

Na kuna viongozi wa Kiroho ambao utajiri wao unatokana na kuwadhulumu waumini wao kwa njia moja au nyingine ndio Maana hutakuta vitabu vyao vya mahesabu kuwa wazi zaidi ya kuwa somea waumini wao taarifa wanazo taka wao.

Ukija kwenye vyama vya siasa hadithi ni Hiyo Hiyo wakati wao wenyewe demokrasia wanayo ipigia kelele hawaienzi.

Ukija kwenye Suala la Maendeleo mfano china na mabadiliko Yao ya kiuchumi tunaona wame weza kufanya hivyo bila vyama vingi Bali kwa kuimarisha mifumo Yao ya kiutendaji wakati urusi walikwenda na Glasnot matokeo yake sote tunayajua Gorbachev akakosa nchi na Yeltsin na ulevi wake Ndio aka tawala nchi , matokeo yake nchi ilipojitambua wakamleta Putin ambaye Yupo madarakani kwa miongo miwili sasa.

Ukija hizo nchi za ulaya iwe Germany ya Hitler na wengineo tuangalie walivyo piga hatua za maendeleo ilikuwa kwa sababu ya katiba mpya au demokrasia au lilikuwa ni suala la uzalishaji na usimamiaji wa itikadi inayolenga ktk maendeleo.

Mimi nionavyo tupate maendeleo kwanza Ndio tutaweza kuweka hizo rangi zingine kulemba maendeleo yetu na sio kulemba kitu ambacho hatuna.
 
Ngoja waje

Hatuji ila tutasema. Maendeleo ya China yameletwa na uongozi bora. Maendeleo ya Rwanda yameletwa na uongozi bora. Mwalimu alisema: "Ili tuendelee tunahitaji watu siasa safi na uongozi bora." Hakusema na katiba mpya. Maendeleo ya Tanzania yataletwa na uongozi bora. Watu wakiuunga mkono uongozi wa Awamu ya 5, kama walivyounga mkono uongozi wa awamu zote tutapata maendeleo. Tunaona itihada za Raisi wa awamu ya 5 katika kuleta uongozi bora nchini.Bial shaka hatua za kuelekea kupata maendeleo zimekwisha anza kuonekana.
 
Wewe wasema ndio sera zenu Ndio Maana hamtaki mabadiliko ndani ya nyumba zenu au vyama vyenu. Akitawala fulani hakuna demokrasia lakini akiwepo Yule wa darasa la saba la zamani basi uwepo wake ni demokrasia tosha.
Waraka wa Maaskofu naona hautwaacha watu salama. Watu naona matumbo yamechafuka. Chooni kutwa mara 21. Na bado mtaharisha mpaka utumbo mkubwa
 
Mkuu kwani katiba ni nini? Na kama katiba si muhimu nini maana ya kuendelea na hata hii tuliyonayo ya 1977? Kama katiba si muhimu why usiwashauri wanaccm wakaitupilia mbali katiba ya ccm ili wabaki na ilani tu? Tatizo kubwa la watanzania hasa wanaccm tunajilinganisha na mataifa mengine kwa mambo mabaya tu ili kuhalalisha ujinga wetu.right nguvu tunayoitumia kujilinganisha na wao kuhalalisha ujinga na upuuzi wetu tungetumia nguvu hiyo hiyo kujilinganisha hata katika mambo mazuri,Tanzania ingekuwa mbigu ya waafrica waliowengi
 
Unadhani kila dikteta anaweza kuleta maendeleo? Maendeleo ya China yanaletwa na vitu vingi ikiwemo ujuzi wa wananchi na kujituma katika kazi kwa watu. Serikali ilichukua jitihada za makusudi kuwekeza kwa watu kwa kuwapa elimu bora, kuweka mazingira bora ya uzalishaji,urahisi wa kupata mitaji kupitia benki, n.k. hayo ndiyo. Yaliyoleta maendeleo China. Hapa kwetu hata vipaumbele vya taifa havijulikani.

Tunahitaji katiba mpya ili wananchi wawe na uwezo wa kuwajibisha viongozi wanapishindwa kutelekeza matakwa ya wananchi. Kwa sasa kile anachoamua Rais ndicho kinatekelezwa na kuweka pembeni mipango yote iliyokuwepo. Tulikuwa na " Big Results Now" badala ya kuboresha, imepigwa chini kabisa. Tulikuwa na "kilimo kwanza" nayo imekufa kifo cha mende. Sasa hivi haijulikani hata ni falsafa ipi inayotuongoza.

Ni mambo ya " amri" tu. Katiba mpya ndiyo suluhisho.Wenzio Wachina walishaamua karibia miongo mitatu iliyopita kuhusu taifa lao liendeshweje kiuchumi. Kiongozi anayekuja anajua cha kufanya bila hata kuangalia katiba.
 
Hatuji ila tutasema. Maendeleo ya China yameletwa na uongozi bora. Maendeleo ya Rwanda yameletwa na uongozi bora. Mwalimu alisema: "Ili tuendelee tunahitaji watu siasa safi na uongozi bora." Hakusema na katiba mpya. Maendeleo ya Tanzania yataletwa na uongozi bora. Watu wakiuunga mkono uongozi wa Awamu ya 5, kama walivyounga mkono uongozi wa awamu zote tutapata maendeleo. Tunaona itihada za Raisi wa awamu ya 5 katika kuleta uongozi bora nchini.Bial shaka hatua za kuelekea kupata maendeleo zimekwisha anza kuonekana.
Nafikiri wanalilia SIASA SAFI
 
Kiongozi tunahitaji katiba bora ili tufikie malengo yetu kama nchi. Nchi haiwezi kuongozwa na utashi wa viongozi bika katiba . Bila shaka umeshuhudia mfumo wa Elimu unavyoyumbishwa kila awamu na mipango yake. Nini malengo ya Taifa? He kuna mwendelezo chanya wa viongozi wanaobadilisha madaraka? Je vipi ukuwaji wa democrasia. Watu wako huru kutoa maoni yao. Kwanini mchakati wa katiba uliazishwa na Mstaafu Raisi Jk. Bila katiba bora hakuna maendeleo endelevu na ni mwanzo wa serikali za kiimla
 
Yawezekana wananchi wa China hawakuitaka,Je,hapa kwetu wananchi wanaitaka?,sio kila kitu kinafananishwa!
Au unataka kutuambia kwamba yaliletwa na kupiga watu risasi?
 
Mtoa mada unafaham ama unajua kwa nn katiba ya zamani iliachwa na kutungwa ya mwaka 1977!? Ambayo tuko nayo sasa na bado tumeona tunapaswa kuachana nayo ili iwepo nyingine???
 
Back
Top Bottom