Baba V
JF-Expert Member
- Dec 29, 2010
- 19,479
- 9,550
Hivi inakuwaje unakutana na demu ambaye sio mtu wako wala hakuwahi kuwa mtu wako ila mnafahamiana fresh tu... Lakini unakuta baada ya muda mrefu wa kutokuwasiliana siku ukijichenga tu ukampigia au ukamtumia sms badala ya jibu unalotarajia utasikia "nikopeshe laki na nusu nina shida nayo ntakurudishia!"... Au siku hiyo unaitwa "dear nina shida na elfu hamsini ya salon"... Sasa unabaki unashangaa mazoea hayo yameanzia wapi!!? Na kwanini mpaka ukimtafuta tu ndio anatangaza shida zake?? Mbona ukiwa kimya hakutafuti?? Girls u need to change... Shida zenu zisiwadhalilishe!! Mdau unasemaje kuhusu hili!!?
Mie nilikuwa najiuliza kuwa kuna chuo cha "mizinga" wanapitia siku hizi au ndo hali ya maisha imekuwa tight sana. Unaweza ukapigwa mzinga hadi ukasema hiki nini..!? c.c Bishanga
Last edited by a moderator: