Madaktari waipiga changa la macho serikali

Madaktari waipiga changa la macho serikali

figganigga

Platinum Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
27,643
Reaction score
62,567
Wakati serikali ikikimbilia kuzuia mgomo mahakama kuu ya kazi, madaktari wanashangaa.
Serikali imeweka zuio la mgomo wa madaktari wa chama cha madaktari MART wakati madaktari wanafanya mgomo kupitia jumuia ya madaktari chini ya Uongozi wa Stephen Olimboka.
Naibu mwanasheria mkuu bwana Masaju katika chl10 kasema wao wanachotambua ni chama cha madaktari kilicho sajiliwa hivyo vyama vingine havitambuliki.
kaongeza pia ambaye atakiuka sheria ya mahakama atashitakiwa na awale watakao sababisha vifo. Mia
 
kwani mahakama itawafanya nini madaktari wote wakiamua kugoma?
 
ngoja tuone Punda anavyolazmishwa kunywa maji

Hapa Punda anaweza akawa Pinda (serikali inalazimishwa kulipa ... ) au ni madaktari (madaktari wanalazimishwa kufanya kazi ....) au ?
 
Tuache kusapoti u jinga na u huni unaofanywa na hawa jamaa....Hiyo kamati imesajiliwa wapi?? Kwahili sijawahi kuunga na wala sitoliunga mkono....Ninyi shabikieni lakini athari zitakazowapata mama ana baba zenu wakiwamo bibi na babu zenu ambao hamuishi nao ndo mtajua.....hata kama tunadhani tunaikomoa CCM na serekali..nadhani strategy hii ni mbovu na haifai na wala haitatufikisha popote....Nakaribisha matusi na kejeli kama ilivyo kawaida ya baadhi ya wana JF ambao hatutaki kusikia second opinion....
 
Kiongozi wa serikali yetu ni dhaifu matokeo yake serikali anayoiongoza imekuwa dhaifu. Ushahidi wa udhaifu huu ni pamoja na namna inavyotatua matatizo makubwa ya nchi kama hili la madaktari. Sikuamini nilipomsikia waziri mkuu anasema serikali imelipeleka swala la madaktari mahakamani.
 
Tuache kusapoti u jinga na u huni unaofanywa na hawa jamaa....Hiyo kamati imesajiliwa wapi?? Kwahili sijawahi kuunga na wala sitoliunga mkono....Ninyi shabikieni lakini athari zitakazowapata mama ana baba zenu wakiwamo bibi na babu zenu ambao hamuishi nao ndo mtajua.....hata kama tunadhani tunaikomoa CCM na serekali..nadhani strategy hii ni mbovu na haifai na wala haitatufikisha popote....Nakaribisha matusi na kejeli kama ilivyo kawaida ya baadhi ya wana JF ambao hatutaki kusikia second opinion....

hawa watu wanaathirika even madaktar wapo kazini
 
hawa watu wanaathirika even madaktar wapo kazini

Uko sahihi kabisa.....pata picha kila kitu kitakapokuwa kimesimama.....

Pili je, tunamuadhibu nani hapo?? serekali? Kwa maana ya nani?Kikwete Pinda au hussein Mwinyi wa wategemezi wao??.....
 
Je serikali ITADHIBITISHA VIPI watu waliopangiwa KUFA siku za mgomo na MUNGU ndio kapanga? maana hata madaktari wakiowepo vifo vipo bali kwa wastani....
 
Uko sahihi kabisa.....pata picha kila kitu kitakapokuwa kimesimama.....

Pili je, tunamuadhibu nani hapo?? serekali? Kwa maana ya nani?Kikwete Pinda au hussein Mwinyi wa wategemezi wao??.....
wafundishe watz kufanya wanachopaswa kufanya, kutimiza wajibu wao! si sahihi madaktari kulalamikia maslahi yao, sisi wananchi na hao unaowatetea tulipaswa kuilazimisha serikali iwajali madaktari wanaotutibu, kumbuka kazi yao ni ngumu, hata pale ndugu wa mgonjwa hawaruhusiwi kumgusa ndugu yao madaktari lazima wamhudumie! unayajua haya? km unaujua ukweli huu huwezi kuwalaumu madaktari kwa kile wanachofanya sasa, wamelazimika kufanya hivyo.
 
Kumpiga chura teke ni kumuongezea kasi,kila siku Serikali inavyozi kuwakandamiza wananchi wake ktk mambo tofauti ndivyo inavyojirahisishia kuondoka madarakani.
 
Tuache kusapoti u jinga na u huni unaofanywa na hawa jamaa....Hiyo kamati imesajiliwa wapi?? Kwahili sijawahi kuunga na wala sitoliunga mkono....Ninyi shabikieni lakini athari zitakazowapata mama ana baba zenu wakiwamo bibi na babu zenu ambao hamuishi nao ndo mtajua.....hata kama tunadhani tunaikomoa CCM na serekali..nadhani strategy hii ni mbovu na haifai na wala haitatufikisha popote....Nakaribisha matusi na kejeli kama ilivyo kawaida ya baadhi ya wana JF ambao hatutaki kusikia second opinion....

Mkuu mbona unakimbilia kujihami hivyo?
Hivi unafikiri wagonjwa sasa hivi mahospitalini hawapati madhara hata kama hakuna mgomo? Ulipata soma au kusikia madai ya madaktari? Utaona wanachodai siyo maslahi yao tu.
Tutake tusitake hii serikali yetu ni ya kisanii sana. Hivi kama kungekuwa na mgomo.
Tatizo lipo kwa serikali yenye mawazo yale yale ya kutatua matatizo. Hivi mahakama ikizuia, inaweza kuwalazimisha madoctor kufanya upasuaji?
Serikali na mahakama zake vichwa maji tu.
 
Je serikali ITADHIBITISHA VIPI watu waliopangiwa KUFA siku za mgomo na MUNGU ndio kapanga? maana hata madaktari wakiowepo vifo vipo bali kwa wastani....

Tunazungumzia Vifo vinavyosababishwa kwa makusudi na Serikali sababu mvutano ulio hapa ni kati ya Serikali(inayopaswa kuwajibika kwa wananchi)na madaktari wanaotakiwa kutekeleza majukumu yao.
 
wafundishe watz kufanya wanachopaswa kufanya, kutimiza wajibu wao! si sahihi madaktari kulalamikia maslahi yao, sisi wananchi na hao unaowatetea tulipaswa kuilazimisha serikali iwajali madaktari wanaotutibu, kumbuka kazi yao ni ngumu, hata pale ndugu wa mgonjwa hawaruhusiwi kumgusa ndugu yao madaktari lazima wamhudumie! unayajua haya? km unaujua ukweli huu huwezi kuwalaumu madaktari kwa kile wanachofanya sasa, wamelazimika kufanya hivyo.
Watumie vizuri nafasi yao ya kupiga kura ili wachague serekali makini itakayotumia vizuri rasilimali tulizojaliwa ili wafanyakaze wote walipwe vizuri..

Ambacho sikubaliani nacho hapa ni kushabikia matendo yatakayopelekea madhara kwa wasioukuwa na hatia kwa sababu tu tunataka kuiadhibu serekali ambayo to my opinion haiathiriki katika hili...
 
Hivi wananchi hatuwezi kuishitaki Serikali Kama vifo vitatokea?Kwa mfano sisi wananchi tumeshatimiza jukumu letu kwa kulipa kodi ya Serikali na kila siku tunaendelea kulipa kodi ya moja kwa moja kwa ununuzi Wa mahitaji yetu ya kila siku(unga/sukari/mafuta/sababuni/mchele/n.k.),sasa vipi kwa upande wa pili wa Serikali kuwajibika kwetu sisi wananchi kwa kutupatia Huduma bora na salama?
 
Mimi nimetembelea hospitali ya mkoa wa Dodoma. Kwa kweli hali ni mbaya sana kwasababu huduma inayoendelea ni ya usafishaji vidonda tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom