Madaktari waipiga changa la macho serikali

Mkuu mbona unakimbilia kujihami hivyo?
Hivi unafikiri wagonjwa sasa hivi mahospitalini hawapati madhara hata kama hakuna mgomo? Ulipata soma au kusikia madai ya madaktari? Utaona wanachodai siyo maslahi yao tu.
Tutake tusitake hii serikali yetu ni ya kisanii sana. Hivi kama kungekuwa na mgomo.
Tatizo lipo kwa serikali yenye mawazo yale yale ya kutatua matatizo. Hivi mahakama ikizuia, inaweza kuwalazimisha madoctor kufanya upasuaji?
Serikali na mahakama zake vichwa maji tu.
Najaribu tu mkuu kuforecast situation itakavyokuwa..haswa kwa wanyonge wa nchi hii
 
nilimsikia kiongozi mmoja wa madaktari akilalamika kuwa kuna vitendea kazi havistahili kutumika kwa wagonjwa, kuna uhaba pia wa vitendea kazi kitu kinachopelekea kazi hiyo kuwa ngumu mno.
pia wanalalamika hata baadhi ya wagonjwa kukosa vitanda mahospitalini na kupelekea wakati mgumu kwa madaktari wanaowahudumia wagonjwa hao hAsa wanapohitaji kuwafanyia vipimo inalazimika daktari kupiga magoti au hata kuchutama ili kumpima mgonjwa,
Kuna ya msingi mengi pia ambayo inabidi kutuliza kichwa ili kuyaelewa na si kukurupuka tu na kudhani kuwa jamaa wanachotaka ni kuongezwa mshahara.

Pia swala la kudai eti madaktari wakigoma watakaoteseka ni Baba zetu, Mama zetu, babu na Bibi zetu, ama ndugu zetu wengine hiyo ni kauli ya kipumbavu na ni ya mtu aliyekosa akili.

Kauli kama hizo zilitamba sana miaka ya 94, 95 pindi tulipokuwa tunaingia kwenye mfumo wa vyama vingi. Baadhi ya wana CCM waliokuwa wakipiga kampeni majukwaani waliropoka wazi kuwa eti tukichagua upinzani basi tunakaribisha vita.

Ishu ni kuwa hakuna aliyezaliwa ili aje kuwa mlinzi wa hii Dunia.
So kama kufa basi kila mtu atakufa, no matter madokta watagoma au madokta watakuwa kazini.
 
Watumie vizuri nafasi yao ya kupiga kura ili wachague serekali makini itakayotumia vizuri rasilimali tulizojaliwa ili wafanyakaze wote walipwe vizuri..

Ambacho sikubaliani nacho hapa ni kushabikia matendo yatakayopelekea madhara kwa wasioukuwa na hatia kwa sababu tu tunataka kuiadhibu serekali ambayo to my opinion haiathiriki katika hili...

Kama unaweza kuona ushabiki unaofanywa sasa kushabikia mgomo wa madaktari, mbona hukuuona ushabiki wa unaowatetea wakati wa uchaguzi? waache walipe gharama ya maamuzi yao ya kishabiki!
 
Hivi wananchi hatuwezi kuishitaki Serikali Kama vifo vitatokea?Kwa mfano sisi wananchi tumeshatimiza jukumu letu kwa kulipa kodi ya Serikali na kila siku tunaendelea kulipa kodi ya moja kwa moja kwa ununuzi Wa mahitaji yetu ya kila siku(unga/sukari/mafuta/sababuni/mchele/n.k.),sasa vipi kwa upande wa pili wa Serikali kuwajibika kwetu sisi wananchi kwa kutupatia Huduma bora na salama?

Sio tu tunaweza mkuu Ciril, pia ni haki yetu kuandamana kuzidai haki hizo zinazoambatana na huduma za afya, hatimaye kukiadhibu kwa kukifuta chama kinachowadharau wananchi ikibidi kuleni nyasi lakini lazima ndege ya rais inumuliwe this time wameongeza ukali wa adhabu kufeni, hatuongezi mishahara ya medical doctors kwani mishahara ya wabunge bado haitoshi, posho za wakurugenzi wateule wa jk ndio kipaumbele
 
Last edited by a moderator:
Mi nafikiri tatizo si madaktari, tatizo ni wanasiasa, fikiria wakati wengine wanajiongezea miposho ya safari tena za nje, madaktari wanapunjwa kwa kazi ngumu wanayoifanya, Jamani hii taaluma si ya kubeza. Mi nilipenda sana kuwa daktari, lakini nilipofika muhimbili pale, wiki mbili za kwanza tu nikaona pagumu hapa, huyooo nikatimkia Mzumbe nikapiga BBA yangu.
Wakati si tunapiga shule miaka 3, hawa jamaa wanapiga 5, halafu tunawazidi na maslahi kwa kupiga kwetu domo. hii si sawa, wagome tu serikali iwe sikivu. walazimishwe kusikiliza

Bungeni.jpg



cheki kama hawa jamaa hapa wanasinzia tu, halafu wanakula maposho kibao ya m.a.t.a.k.o
 
Uko sahihi kabisa.....pata picha kila kitu kitakapokuwa kimesimama.....

Pili je, tunamuadhibu nani hapo?? serekali? Kwa maana ya nani?Kikwete Pinda au hussein Mwinyi wa wategemezi wao??.....

Selikari ninani?
 
Kama unaweza kuona ushabiki unaofanywa sasa kushabikia mgomo wa madaktari, mbona hukuuona ushabiki wa unaowatetea wakati wa uchaguzi? waache walipe gharama ya maamuzi yao ya kishabiki!

Gharama/adhabu ya uhai ni kubwa mno haswa unapochanganya wanaohusika na wasiohusika....mimi na wewe tu wazima sas lakini unatoka kueleke morogoro njiani linatokea la kutokea ndipo utakapoelewa ninachokisimamia
 
Sio tu tunaweza mkuu Ciril, pia ni haki yetu kuandamana kuzidai haki hizo zinazoambatana na huduma za afya, hatimaye kukiadhibu kwa kukifuta chama kinachowadharau wananchi [/color=red]ikibidi kuleni nyasi lakini lazima ndege ya rais inumuliwe[/color] this time wameongeza ukali wa adhabu [/color=red]kufeni, hatuongezi mishahara ya medical doctors kwani mishahara ya wabunge bado haitoshi, posho za wakurugenzi wateule wa jk ndio kipaumbele[/color]

Tuko pamoja Mkuu! Badala ya sisi wanachi kuwalalamika madaktari ambao kimsingi madai yao yana hoja, ni wajibu wetu kuidai serikali tunayoilipa kodi huduma nzuri ya afya! Hatuna mkataba na wadaktari bali na serikali!
 
Mi nafikiri tatizo si madaktari, tatizo ni wanasiasa, fikiria wakati wengine wanajiongezea miposho ya safari tena za nje, madaktari wanapunjwa kwa kazi ngumu wanayoifanya, Jamani hii taaluma si ya kubeza. Mi nilipenda sana kuwa daktari, lakini nilipofika muhimbili pale, wiki mbili za kwanza tu nikaona pagumu hapa, huyooo nikatimkia Mzumbe nikapiga BBA yangu.
Wakati si tunapiga shule miaka 3, hawa jamaa wanapiga 5, halafu tunawazidi na maslahi kwa kupiga kwetu domo. hii si sawa, wagome tu serikali iwe sikivu. walazimishwe kusikiliza

View attachment 57264



cheki kama hawa jamaa hapa wanasinzia tu, halafu wanakula maposho kibao ya m.a.t.a.k.o

Mkuu nafikiri nyakati hizi ambapo vijana wengi wamepiga shule ni muhimu kupigania kupinga hii trend iliyojengwa karibuni - kwamba siasa na wanasiasa wanathaminiwa na kutuzwa kuliko elimu+wenye elimu zao walizosotea kwa viwango mbalimbali!! Tumekuwa Taifa lisilo na dira ya vipaumbele!
 
wafundishe watz kufanya wanachopaswa kufanya, kutimiza wajibu wao! si sahihi madaktari kulalamikia maslahi yao, sisi wananchi na hao unaowatetea tulipaswa kuilazimisha serikali iwajali madaktari wanaotutibu, kumbuka kazi yao ni ngumu, hata pale ndugu wa mgonjwa hawaruhusiwi kumgusa ndugu yao madaktari lazima wamhudumie! unayajua haya? km unaujua ukweli huu huwezi kuwalaumu madaktari kwa kile wanachofanya sasa, wamelazimika kufanya hivyo.
Wacha utani! unamaana kazi ya madaktari ni ngumu kuliko ya wabunge wanaojadili bajeti na kuipitisha kwa kishindo?
 
Mi ninachoshangaa ni kwa serikali kukimbilia mahakamani, hivi hawana hoja ya msingi na yenye nguvu ya kyuongea na madaktari? Kama ni wa kweli na hakuna hila ndani ya serikali kweli hawana maelezo yenye mashiko ya kuweza kuwafanya madaktari kuelewa? Matisho ni ya nini? Umewahi kuona mzazi badala ya kukaa chini na mwanae ampe maelezo ya kutosha yeye anakimbilia mahakamani ili asaidiwe hii ni hatari. Kwani lazima muwepo nyie madarakani? Kama mmeshindwa si muwaachie na wengine wenye uwezo watuongoze? Hii si sawa, halafu mnakimbilia kusema eti wanainchi waonewe huruma mbona nyie hamuwaonei huruma?
 
mkirua umewahi kwenda hospitali hizi kubwa ukaona wagonjwa wanalala chini?huduma zote wanapatiwa wakiwa hapohapo chini na hao madaktari na wauguzi!kazi inakuwa ngumu hasa mgojwa anapokuwa hajiwezi kabisa,atatakiwa ageuzwe kila baada ya saa mbili ktk mazingira hayo madaktari wamechoka,mtu anakaa kwenye kiti anajizungusha plus kiyoyozi halafu wanaleta dharau!waweke mazingira mazuri ya kufanyia kazi waone nani atawakumbuka!SERIKALI NA CHAMA CHAKE WAMEACHWA NA MUNGU SASA WANAJIUA WENYEWE!
 
Mimi nadhani wanaosema nchi haina hela yakuwatendea haki wananchi wake niviongozi waliowekwa nawanchi 2010,Sasa migomo kama hii nielimu tosha kwamba hawa waliowapa tisheti navitenge na elfu mbili zanauli wameamua kuwatoa nyie wanachi kafara wao waneemeke!Na kwahili 2015 hawa wananchi wenye serikali hawatarudia makosa!Maana somo wanalofunzwa sasa linaghara tena inayoumiza mno!Dr's kama tumeamua tusirudi nyuma mpaka haki itendeke.
 
mmh! Uzalendo ni kwa Madaktari tu! Mbona wabunge hamuonyeshi uzalendo wenu? Tena kwa kutoa wazo tu, la kuhamasisha kwamba kila kaya ichangie jero, au uanzishwe mfuko wa madaktari kama mlivyo changamkia mfuko wa jimbo kwa wabunge? ili pesa zitakazo patikana ziende kwenye kuhudumia madaktari, kama mnaona mkipunguza mazagazaga yenu kuhudumia afya ya mpiga kura wako ni noma!
 
Tuache kusapoti u jinga na u huni unaofanywa na hawa jamaa....Hiyo kamati imesajiliwa wapi?? Kwahili sijawahi kuunga na wala sitoliunga mkono....Ninyi shabikieni lakini athari zitakazowapata mama ana baba zenu wakiwamo bibi na babu zenu ambao hamuishi nao ndo mtajua.....hata kama tunadhani tunaikomoa CCM na serekali..nadhani strategy hii ni mbovu na haifai na wala haitatufikisha popote....Nakaribisha matusi na kejeli kama ilivyo kawaida ya baadhi ya wana JF ambao hatutaki kusikia second opinion....
Naungana nawe kwa hili, ni mbaya wananchi kusapoti huu mgomo, ni vizuri tukajadili au kujenga mijadala itakayoleta suluhu nzuri pasipo kuleta athari mbaya jamii hasa wale ambao maskini. Mimi na hawa wengine ambao wako huku JF huenda tuna uwezo wa kwenda Hindu Mandal, Aga Khan na kwenine... lakini kuna ambao hizi hospitali za serikali ni mkombozi wao. Tunavyoshabikia huu mgomo utokee tunadhani nani ambaye ataathirika!!!! Ni watanzania hawahawa ambao hata humu JF hawapo. Yes it's true that kuna uzembe mkubwa wa serikali lakini hatuwezi kusema Doctoros wagome!
 
Back
Top Bottom