Zamani ilikuwa mpaka mgonjwa atoe ridhaa, ikaonekana wagonjwa wengi wanakataa
Sioni ni kwa sababu gani daktari alazimishe consent simply because a patient will make a decision you don't disagree with. Otherwise, hiyo itakuwa ni duress kama siyo undue influence.
...baadae ikawa kila mgonjwa anayelazwa kwenye teaching hospital, automatically unakuwa umetoa ridhaa ya kutumika kufundishia..
Kwanza, unaposema university hospital unamaanisha university hospital zote duniani au ni zile za Tanzania tuu?
Pili, kama ni Tanzania, unaweza kutupa hiyo sheria au guideline inayohalalisha automatic consent kwenye university hospital kama Muhimbili? This will help a lot.
Tatu, kuna aina mbili za consent: explicit consent na implied consent. Explicit consent ni pale mgonjwa anapompa daktari specific permission to do something. Explicit consent inaweza kuwa ya mdomo au ya maandishi.
Implied consent ni pale mgonjwa anapoonyesha ridhaa yake indirectly, kwa mfano, kwa kuleta prescription ili umpe dawa. This is not a lesser form of consent but it is only valid if the patient knows and understands what they are consenting to.
Hii automatic consent inatoka wapi? Najua sometimes hasa wakati wa emergency treatment, kunaweza kuwa na automated informed consent kutokana na hali mbaya ya mgonjwa au kutokuwepo kwa mtu wa karibu kutoa explicit consent. Lakini mgonjwa ana capacity ya kutoa consent lakini analazimishwa kutoa consent automatically?
OK, let's assume pia kuna "automatic consent". Sheria inasema wazi kuwa ili consent iwe valid, lazima anayetoa awe na capacity ya kuitoa, lazima awe amefanya hivyo kwa hiari yake mwenyewe bila kulazimishwa na mtu yoyote, lazima awe amepewa "sufficient, balanced information" ili kumwezesha kufanya an informed decision, na pia ni lazima awe na uwezo wa kujua na kupima maelezo aliyopewa kabla ya kutoa ridhaa yake.
Sasa nyie kama madaktari mna-ensure vipi kuwa mgonjwa anajua kuwa hosipitali anayoenda ni university hosipital na kwamba consent yake ya kutumika katika kufundishia itakuwa obtained automatically? Hivi mgonjwa wa kawaida atajuaje hii ni teaching hospital na ile siyo kama hatapewa maelezo kabla?
Cha tatu, haikupaswa ninyi kuwepo wakati mwalimu anafundisha wanafunzi wake kwa mgonjwa wenu...kwa sababu atawaonyesha technic mbali mbali za kuexamine na kufukia conclusion na wanafunzi watajaribu..hili linahitaji 'privacy', kwa hiyo hata ninyi hamkuwa na heshima kwa mgonjwa wenu kwa kuwepo hapo karibu hivyo mkiangalia na kusikiliza wakati mgonjwa yuko na madaktari wake. Mimi naona ethical breach kwa pande zote mbili.
Wangejuaje kuwa hawakupaswa kuwepo pale wakati mwalimu anafundisha? Nani alikuwa na majukumu ya kuwaeleza kuwa hawakupaswa kuwa pale? Who led them to breach the ethics? Unaona jinsi tatizo moja linavyozaa tatizo lingine? Kutokuomba prior consent, kumesababisha breach of confidentiality.
Kama mgonjwa angekuwa ametaharifiwa kabla kuwa atatumika kufundishia basi angekuwa na fursa ya kuamua kama ndugu zake wawepo pale wakati anatumika kufindishia. In fact, daktari alikuwa na duty ya kumwuliza mgonjwa kama angetaka ndugu zake wandelee kuwepo wakati anatumika kufundishia.
Kwa hiyo hapo sidhani kama kuna "contributory negligence" kwa upande wa ndugu zake. Daktari alikuwa na duty ya ku-seek consent, hakufanya hivyo. Alikuwa na duty ya ku-maintain confidentiality, hakufanya hivyo. Hata kama kuna "automatic consent" sidhani kama ina dispense the duty of confidentiality automatically. Does it?