Madaktari wa Muhimbili: This is unprofessional....!

Madaktari wa Muhimbili: This is unprofessional....!

Yaani ndugu yangu wewe ni mgumu kuelewa,hata Muhimbili kama utaki kufundishiwa toa taarifa kwa uongozi,sio kusumbua madaktari wodini,ili ni teaching hospital,ukikataa kufundishiwa hamia IPPM na matibabu yako hayataathirika na kitu chochote.Unasoma articl alafu huzielewi,lakini tatizo sio field yako but unakomaa tu,wewe kweli mkomavu inaeelekea sura yako imukunjana njoo tukufanyie plastic surgery

Mkuu naona huko tunakoelekea,tunaweza tusifike... Matusi tena?!
Unahisi madaktari wote(wa TZ) wana mtazamo kama wako,huh?

Mimi siamini kama mtu anaweza kujua kila jambo,ila naamini ni busara kujifunza kutoka kwa wengine. Mimi ninaamini ZeMarcopolo lazima atakuwa ni daktari kutokana na michango yake humu JF ingawa siamini kama yupo hapa nyumbani.Kwa hiyo kusema hiyo sio field yake,sidhani kama ni sahihi.Anyway,hayo niwaachie ninyi wawili..

Hapa kuna malalamiko yametolewa,fine.Ila ni ya upande mmoja.. Hatujapata kusikia upande wa pili unasemaje.Kwa hulka ya kawaida ya kibinadamu kila mtu anapojieleza ni kawaida kabisa kuvutia kwake.. Tutaamaini vipi kama kila alichosema kina ukweli kwa kiasi gani? Mimi sijui.

Sina hakika kama wewe ni daktari au medical student/intern/resident doctor,whatsoever.. Nataka nikuulize kitu,je wakati wa kuchukua maelezo ya mgonjwa au kumfanyia physical examination,unaomba concert yake? Na ikiwa ndivyo,what for? What if mgonjwa akikubali ukachukua history yake vizuri,ila akakataa kumfanyia physical examination?

Anyway mimi nadhani pande zote zinatakiwa kutimiza wajibu wake.Madaktari wafanye kazi kwa ethics na sisi ndugu wa wagonjwa tutimize wajibu wetu.Lakini pia tukubali kwamba mazingira ya hospitali zetu nayo yanachangia sana kukandamiza haki za wagonjwa.Kwenye mjadala huu sijaona hata mtu mmoja akicomplain kuhusu mgonjwa 'X' kusikiliza siri ya tatizo la mgonjwa 'Y'.. Hii pia sio ethical.

Siku zote tusi ni baya ikiwa umetukanwa mbele za watu! Ndivyo na hili jambo ninavyolichukulia.Hapa tatizo sio kwamba dr.ametoa kauli hiyo mbele za wanafunzi.. ni kwa sababu dr.amesema mbele ya wagonjwa,na relatives waliokuwepo pale.Vipi kwa mfano kama mgonjwa angekuwa kwenye chumba cha peke yake na huyu ndugu yetu naye asingekuwapo? Vyoyote tukakavyojadili hapa,pamoja na kwamba wahudumu wetu nao wana mapungufu yao,ila hata mazingira ya kufanyia kazi nayo ni kikwazo kikubwa ktk kumaintain siri za wagonjwa.

Mimi nadhani,ili tupate competent doctors tunahitaji wapate mafunzo ya kutosha..tunahitaji wagonjwa wengi wa kujifunzia..elimu itolewe kwa watu wetu ili waone umuhimu wa kutumika kujifunzia..kwenye mafunzo ya udaktari models ni binadamu..Ndio maana kuna maiti nyingi zilizohifadhiwa kwa ajili ya kujifunzia,sio midoli(ingawa kwa nchi nyingine wanatumia midoli,lakini ni kwa level za chini tu)..tunatakiwa kujifunza kujitolea kutumika kwa ajili ya vizazi vijavyo..Kwa nchi nyingine(walipoelimika),watu wanajitolea miili na viungo vyao kutumika ktk vituo vya utafiti na medical schools pindi wanapokuwa wamefariki. Kwa hapa kwetu ni tofauti sana ndio maana hata tuna upungufu wa damu ktk vituo vyetu,kwa kuwa watu hawako tayari kujitolea kuchangia damu..

Kuhusu kutimuliwa kwa mgonjwa anapokuwa amekataa kutumika kujifunzia,sina hakika sana maana sijawahi kutibiwa muhimbili..ila kwingine nilikopita hiyo sijaona kwa mfano KCMC hiyo haipo.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu inaonekana huijui Muhimbili na pia hujasoma maelezo yangu ukaelewa, bali umekurupuka..
Hii Muhimbili unayoijua ndiyo inayoongoza kwa wagonjwa kufa vifo vinavyoweza kuzuilika. Hili nitalizungumzia siku nyingine lakini kwa sasa hebu kwanza pitia hiki nilichoandika, halafu nitaendelea kujibu hoja zako nyingine...

Sikatai mgonjwa kutumika kufundishia wanafunzi, hawa ni ndio madaktari wetu wa kesho wakajifunzie wapi. Lakini pale dakatari anapowaambia wanafunzi wake kwamba huyu mgonjwa aliyeko mbele yao yuko katika TERMINAL STAGE huku wanaomuuguza wakiwa karibu na hata mgonjwa mwenyewe akisikia, huu ni uuaji. Daktari huyo aliendelea kuwaonyesha wanafunzi wake dalili zinazothibitisha kuwa mgonjwa wetu yuko kwenye terminal stage.

Kitu ambacho madaktari wale walikuwa hawakijui ni kwamba mke wangu pamoja na dada yake ni wauguzi by professional na wanazijua hizo terminology vizuri sana. Sasa iweje waropoke hivyo bila kuangalia walioko karibu. kitendo hicho kilifanyika muda wa kuona wagonjwa na nadhani ndio walikuwa wanamalizia round.
Tumelazimika kumchukua mgonjwa wetu kwa ajili ya kuangalia ustaaarabu mwingine.

Kwanza nakanusha mgonjwa au ndugu wa karibu kushirikishwa kabla ya mgonjwa wetu kutumika kufundishia, hilo halikufanyika. Pili si kweli kwamba mgonjwa wetu alikuwa yuko kwenye Terminal Stage kama yule daktari alivyotaka kuwaaminisha wanafunzi wake na kama hii ndiyo aina ya ufundishaji wa matatibu wetu, haiyumkini ndio sababu ya kuongezeka kwa vifo vingi vinavyoweza kuzuilika katika hospitali zetu.... ninavyoandika hapa mgonjwa wetu yuko nyumbani na ana afya njema kuliko alivyokuwa amelazwa pale Muhimbili. Tulimpeleka akiwa anatembea tukamrudisha akiwa hawezi hata kunyanyua mguu, lakini kutokana na juhudi za wanaye tumeendelea kumhudumia akiwa nyumbani na sasa anaweza kutoka nje na kuzungumza na wajukuu zake... Tatizo hapa sio kukataa kukubali ukweli kwamba mgonjwa wetu yuko kwenye Terminal Stage, Mimi ninapinga namna ujumbe ulivyofikishwa na hili lilifanyika muda wa kuangalia wagonjwa, nadhani walichelewa kumaliza darasa na hivyo mke wangu na shemeji yangu wakawakuta wakiendelea na darasa bila kung'amua uwepo wao yule daktari aliropoka hayo maneno.... Napinga kabisa mgonjwa wetu hakuwa kwenye hiyo stage bali walitaka kum-maliza ili somo likamilike........

sasa kama ndugu zako ni manesi walikuwa wanajua hata status ya mgonjwa kwa nini walimpeleka coz i was expecting hawa ndo watusaidie counseling, na hakuna mgonjwa atakayefundishiwa bila ridhaa yake, pia kama ni wakati wa round hao ndugu zako walikuwa wanatafuta nini coz kwa Muhimbili hata muuguzaji haruhusiwi kulala wodin hata kama mgonjwa amezidiwa namna gani, pia wakati wa ward round hii ni routine lazima ipitwe na huku changanyikeni wanapita madaktari wengi hivyo lazima wajadiliane na hapa kwenye ward round hakuna consent hapa coz daily routine. Lakini kama Dr atakuja kufundisha apart from round time lazima aombe consent. Jua taratibu za hospital na pia kama uliona ndugu yako hajafanyiwa fair ungeenda pale kwenye dirisha la malalamiko ili utoe dukuduku yako na uelezwe utaratibu coz kulalamika hapa hakukusaidii hata kidogo zaidi unaoneka si mstaarabu, much know which u do not know.
 
Imenikuta juzi pale Regency Hospital namweleza daktari jinsi navyoumwa, mwisho akaishia kuandika kwenye file yangu eti "nilikuwa na hamu ya kutalii hospitali" kha! nimegundua hiyo baada ya kwenda kwa dr mwingine alipoamua kufanya marejeo.
 
Mleta mada anazungumzia mambo yanayotokea kwenye dunia ya tatu wewe unakimbilia kuGoogle unatuletea mambo ya kwenye dunia ya kwanza.

Akili zako zipo sawa kweli wewe?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
Hongera Kwako Mwenye akili zilizokuwa sawa na kwa kuchangia Jambo ambalo hujalielewa.
Hata mambo yanatokea Dunia ya Nane au ya kumi,hayo yanayoendelea katika hiyo sekta ya Afya hayakubaliki na hayatakubalika KAMWE.
Tatizo kwenye jamii zetu kuna watu Kama wewe unayeweza kutoa TAKATAKA nyumbani Kwako na kuzitupa katikati ya barabara kwa kuwa akili na fikra zako zinakutuma uko Dunia ya tatu na kuwa mchafu ni sawa na sio wajibu wako kuweka Mazingira safi.

Hizo Ethics hazitofautiana sana na Ethics za Utabibu Ulimwengu mzima.
Human anatomy system ni ile ile kwa Binadamu wa Dunia ya kwanza mpaka Dunia ya Tisa unayoijua wewe. Kwa hiyo Kama Mgonjwa yuko Dunia ya tatu Kama unavyoeleza hairuhusu kwa Madaktari na wauguzi kumpa huduma duni na za hali ya chini. Hizo Principle za Medical Ethics zinajieleza zenyewe...najua ukweli umeupata.

Usije hapa na hoja zako DHAIFU kutaka kupotosha umma. Kama umezoea kushabikia Mpira au vyama vya Siasa endelea huko huko. Hapa inahusiana na Afya za Watanzania na inasikitisha kuona kwamba kuna Watu Kama wewe unaleta ushabiki wa kijiweni bila kujenga hoja inayoweza kukusaidia Wewe,familia yako na ndugu zako ili kuondokana na kero zinazotupata Watanzania kila siku. Au wewe unatibiwa Apollo na familia yako!!??? Mwisho wenu unakuja,tunaheshimiana tu na Tanzania hii ni yetu wote kila mtu ana fursa na HAKI sawa. Mimi nachangia hoja hii Kama Mtanzania wa kawaida ambaye natibiwa Muhimbili na familia yangu na huwa nakutana na karaha Kama hizi.
 
Pia kuna tatizo kwa mtoa mada? Wewe muda round unafanya nini wodini au ndo ujuaji wenyewe? Na je kama yupo kwenye terminal ulitaka awbmbie vp? Maana una waka tu? Ndio wewe ni mropokaji? Na hujui taratibu vingenfvyo kama kusema tfrminal ndo tatizo we ungetafuta private rums atibiwf e huko
 
Kumbe haukuwepo...ningekua mimi,daktari asingekwepa kupata kofi kali sana la usoni!!!:boink:
 
Hongera Kwako Mwenye akili zilizokuwa sawa na kwa kuchangia Jambo ambalo hujalielewa.
Hata mambo yanatokea Dunia ya Nane au ya kumi,hayo yanayoendelea katika hiyo sekta ya Afya hayakubaliki na hayatakubalika KAMWE.
Tatizo kwenye jamii zetu kuna watu Kama wewe unayeweza kutoa TAKATAKA nyumbani Kwako na kuzitupa katikati ya barabara kwa kuwa akili na fikra zako zinakutuma uko Dunia ya tatu na kuwa mchafu ni sawa na sio wajibu wako kuweka Mazingira safi.

Hizo Ethics hazitofautiana sana na Ethics za Utabibu Ulimwengu mzima.
Human anatomy system ni ile ile kwa Binadamu wa Dunia ya kwanza mpaka Dunia ya Tisa unayoijua wewe. Kwa hiyo Kama Mgonjwa yuko Dunia ya tatu Kama unavyoeleza hairuhusu kwa Madaktari na wauguzi kumpa huduma duni na za hali ya chini. Hizo Principle za Medical Ethics zinajieleza zenyewe...najua ukweli umeupata.

Usije hapa na hoja zako DHAIFU kutaka kupotosha umma. Kama umezoea kushabikia Mpira au vyama vya Siasa endelea huko huko. Hapa inahusiana na Afya za Watanzania na inasikitisha kuona kwamba kuna Watu Kama wewe unaleta ushabiki wa kijiweni bila kujenga hoja inayoweza kukusaidia Wewe,familia yako na ndugu zako ili kuondokana na kero zinazotupata Watanzania kila siku. Au wewe unatibiwa Apollo na familia yako!!??? Mwisho wenu unakuja,tunaheshimiana tu na Tanzania hii ni yetu wote kila mtu ana fursa na HAKI sawa. Mimi nachangia hoja hii Kama Mtanzania wa kawaida ambaye natibiwa Muhimbili na familia yangu na huwa nakutana na karaha Kama hizi.

Nine Inch Nails - Head Like A Hole - YouTube
 
Mama mkwe wangu alilazwa Muhimbili kwa wiki moja, lakini jana nililazimika kumtoa kutokana na kile nilichokishuhudia pale. Pamoja na vituko vingi tu tulivyoviona kutoka kwa manesi wa ward ya Mwaisela, lakini nisingependa kuzungumzia hayo kwa kuwa si mageni masikioni mwa wengi. Tulimpeleka mgonjwa wetu kufanyiwa uchunguzi zaidi kutokana na kuwa na complication nyingi nadhani ni kutokana na uzee (mkwe wangu ana miaka 70 hivi sasa)

Tulipofika pale alichukuliwa vipimo vyote ikiwapo x-ray, tatizo lilikuwa ni pale madaktari wanapopita round kuona wagonjwa. kwanza walikuwa wamemgeuza mama mkwe wangu kama vile ni darasa la kufundishia wanafunzi, kila daktari alikuwa anafika na wanafunzi wake na kufungua darasa. Cha kushangaza walikuwa wameyakalia majibu ya mgonjwa wetu huku wakiendelea kumuweka pale kama mtu wa kufundishia wanafunzi.

Sikatai mgonjwa kutumika kufundishia wanafunzi, hawa ni ndio madaktari wetu wa kesho wakajifunzie wapi. Lakini pale dakatari anapowaambia wanafunzi wake kwamba huyu mgonjwa aliyeko mbele yao yuko katika TERMINAL STAGE huku wanaomuuguza wakiwa karibu na hata mgonjwa mwenyewe akisikia, huu ni uuaji. Daktari huyo aliendelea kuwaonyesha wanafunzi wake dalili zinazothibitisha kuwa mgonjwa wetu yuko kwenye terminal stage.

Kitu ambacho madaktari wale walikuwa hawakijui ni kwamba mke wangu pamoja na dada yake ni wauguzi by professional na wanazijua hizo terminology vizuri sana. Sasa iweje waropoke hivyo bila kuangalia walioko karibu. kitendo hicho kilifanyika muda wa kuona wagonjwa na nadhani ndio walikuwa wanamalizia round.
Tumelazimika kumchukua mgonjwa wetu kwa ajili ya kuangalia ustaaarabu mwingine.

pole ndugu. Hata mimi mama yangu aliwahi kugeuzwa darasa pale Amana Hospital. Mbaya zaidi tukaambiwa tusubiri nje hadi wamalize 'darasa' lao.
 
Imenikuta juzi pale Regency Hospital namweleza daktari jinsi navyoumwa, mwisho akaishia kuandika kwenye file yangu eti "nilikuwa na hamu ya kutalii hospitali" kha! nimegundua hiyo baada ya kwenda kwa dr mwingine alipoamua kufanya marejeo.
Pole sana mkuu,
Ndio maana mimi binafsi nafikiri imefika muda wa kuufumua muundo wa Afya na kuunda upya na pia kuundwa sheria ambazo zitamlinda mgonjwa na Daktari. Pengine hii italeta umakini na weledi kwenye sekta ya Afya.
Mara nyingi sana bahati au naweza kuwa Bold na kusema uzembe unaosababisha Wananchi kupoteza maisha,halafu hakuna hatua zozote za kisheria zinachukuliwa...kwa mfano Issue ya Mgonjwa wa mguu kufanyiwa upasuaji wa kichwa na mgonjwa wa kichwa kupasuliwa mguu.
Watoto wachanga wengi wanapoteza maisha kutokana na kuchomwa vibaya sindano za chanjo. Mambo inabidi yabadilike ndugu zangu.

Suala la Afya ya binadamu sio Jambo la mchezo.
 
Tafuta wakili, nenda mahakami ukawashitaki. Sheria hairuhusu kutoa siri ya mgonjwa. Ni wajinga, mbona watu wanaishi mpaka 100+

kutoa siri kwa nani?students, nurses are part of medical team so no breach of confidentiality. ila alitakiwa awe amemuambia mgonjwa kabla ya kutamka mbele ya watu wengi. hii habari ina walakini kidogo, madaktari wapite round na kuwe na ndugu ngumu kumeza
 
Katika hili,ukimwondoa mgonjwa ambaye alihitaji kupata huduma stahiki..

Wengine wote kila mmoja mapungufu yake.

Kuanzia:
Mtoa mada-ambaye (kwanza hatuna hakika ni kwa kiasi gani kuna ukweli ktk maelezo yake),ameshindwa kutoa malamiko mahali panapohusika ili kusaidia kukomesha tabia kama hii.
Daktari-ambaye (kama ni kweli) alishindwa kutambua mazingira/na utaratibu mzuri wa kutoa kauli hiyo,
Hao ndugu waliokuwepo wakati huo-waliposhindwa kutumia busara kupisha raundi ifanyike kwa utaratibu,matokeo yake wameishi kuumia roho tu,na kukosa ustahimilivu.
Sisi wachangia mada-ambao wengine wanatukana,kulumbana na kujadili bila kujali ni kwa kiasi gani hii habari ina ukweli.
Sekta/wizara ya afya-kuruhusu wagonjwa kujazana katika wards na kupelekea kukosekana privacy kwa wagonjwa.
 
Katika hili,ukimwondoa mgonjwa ambaye alihitaji kupata huduma stahiki..

Wengine wote kila mmoja mapungufu yake.

Kuanzia:
Mtoa mada-ambaye (kwanza hatuna hakika ni kwa kiasi gani kuna ukweli ktk maelezo yake),ameshindwa kutoa malamiko mahali panapohusika ili kusaidia kukomesha tabia kama hii.
Daktari-ambaye (kama ni kweli) alishindwa kutambua mazingira/na utaratibu mzuri wa kutoa kauli hiyo,
Hao ndugu waliokuwepo wakati huo-waliposhindwa kutumia busara kupisha raundi ifanyike kwa utaratibu,matokeo yake wameishi kuumia roho tu,na kukosa ustahimilivu.
Sisi wachangia mada-ambao wengine wanatukana,kulumbana na kujadili bila kujali ni kwa kiasi gani hii habari ina ukweli.
Sekta/wizara ya afya-kuruhusu wagonjwa kujazana katika wards na kupelekea kukosekana privacy kwa wagonjwa.

Hahahahahahahahahaha hii imenifurahisha sana.
Kwa hiyo kiujumla ni kwamba wote tuliohusika kwa namna moja au nyingine tumechemsha.
Katika hali kama hiyo kilichobaki ni kufuta ukurasa mzima na kuanza upya tu.

Ila jokes aside, daktari aliyesema hospitali ina haki ya kumfukuza mgonjwa aliyekataa kutumika kufundishia anatakiwa kurudi tena kwenye darasa la ethics...
 
Kama ndio hivyo basi yamefanyika makosa makubwa haya:

1. Kutokumpa mgonjwa opportunity ya kuopt out kutumika katika kufundisha wanafunzi. Hii ni haki ya mgonjwa kuamua kama yuko tayari kutumiwa kimasomo au la.

2. Mgonjwa kutojulishwa taarifa ya hali yake mapema. Majibu ya mgonjwa yakipatikana tu ni wajibu wa daktari kumjulihsa mgonjwa juu ya majibu hayo mapema iwezekanavyo.

3. Kupita round na wanafunzi mbele ya ndugu za mgonjwa. Kunaweza kuwa na mambo ambayo mgonjwa hataki ndugu zake wajue. Kuzungumza kuhusu afya ya mgonjwa mbele ya watu ambao si wahudumu wa afya wanaomhudumia ni kosa la kimaadili unless mgonjwa mwenyewe atoe ruhusu.

4.Kutoa taarifa mpya kwa watu wengine (wanafunzi) mbele ya mgonjwa bila kumshirikisha mgonjwa.

Watanzania huwa tunapenda sana kukesha tukiwalaumu wanasiasa, lakini inatakiwa ifike mahali tujiangalie kila mmoja katika kazi yake, je anaifanya kwa ufanisi???
kumbe ZeMarcopolo ni msomi kuliko nchemba na nape!!kwa nini wasikupe kile kitengo ukafanya siasa za kisomi!!!
 
Mtambuzi pole sana, wanaacha kumkomoa Kikwete na CCM yake, wanatukomoa sisi ambao hatuna uwezo hata wa kulipia hospitali kama ya Aga Khan.
Waganga wa kienyeji nao feki ile mbaya,
waombeaji nao wamekuwa magumashi ile mbaya.
Sijui tukimbilie wapi ili tupone.
Na wakati huohuo kila tunachokula na tunywacho tunaambiwa eti ni sumu.
Duhh

yameanzia wapi ndugu yangu mbona ni mropokaji wewe na hao madaktari kunatofati gani
 
Last edited by a moderator:
Pole sana for such a sad experience; but what did you can expect from an obsolete; decadent system!

Nilipata shida sana KCMC majuzi; daktari kamuandikia mtoto wangu sindano 20 za christapen kwa siku 5; manesi wanalazimisha kumdunga sindano 48!!

Mifumo yote ya huduma za jamii imeoza na hakuna kitu kinachoitwa serikali hapo juu kinachofanya lolote isipokuwa knee jack reactions!! na hatua za zima moto; yatapita tuu!

Elimu - Unda tume juu ya tume; yatapita tuu;
Afya - Walimboke yatapita tuu;
Maji - Zima hoja za wapinzani yatapita tuu;
Mikopo ya wanafunzi - Polisi piga mabomu; yatapita tuu;
Wafanyakazi - Kawashtaki mahakamani usiku usiku; yatapita tuu;
Vyombo vya habari vikiyaibua madudu ya serikali - funga gazeti na redio hiyo; yatapita tuu;
Kelele zikizidi anatumwa Jack Zoka - washughulikie hao; yatapita tuu
 
Poleni sana, lakini kwa ucunguzi nliowahi kuufanya (ingawa sio wa kitaalamu) nimegundua kwamba hapa Tanzania unaweza kuambiwa unaumwa ugonjwa fulani lakini kumbe sio kweli,na pia unaweza kuambiwa ugonjwa umefika stage flani kumbe sio kweli cha msingi ni kwenda hosp zaidi ya moja ili kuweza kupata ukweli kwamba unaumwa nini na uko kwenye stage ipi (kitu ambacho ni kibaya na kinapoteza muda na pesa)... kitendo walichokifanya kwa kweli sio kizuri hata kama mgonjwa alikuwa anajua anaumwa nini na yuko stage ipi... nijuavyo mimi hawaruhusiwi kutangaza ishu zozote za mgonjwa... wao wangemuona mgonjwa then wangerudi class na somo likaendela huko...shida nyingine ni kwamba hakuna pa kuwashtaki.... pole sana mungu atamsaidia mgonjwa atapata nafuu
 
Pole sana mtambuzi,lakini tatizo letu wabongo tunapenda kudanganywa mgonjwa akiambiwa ukweli hatupendi.Pili muhimbili ni hospitali ya kufundishia,kwahiyo huwezi kwepa mgonjwa wako kutumika kama kitabu.

of course inauma kuambiwa uko kwenye terminal stage lakini ndo ukweli wenyewe sema tu namna ya kuuwasilisha. Zemarcopolo tuongee yanayofanyika kwetu, sijawahi ona hizo fomu na sijui kama zipo. Aafu katika utaratibu wa kawaida, new case inakuwa admitted na md5 au intern atakayepresent kwa specialist kwa ajili ya shule sisi wote tumepita hivyo. Bila hivyo shule tungetoa wapi? Theory? Ndo maana intern wanaotoka bongo wanajiamini kwa wanayoyafanya with less supervision kwani wana exposure ya wagonjwa ya kutosha. Pia kuna case ambazo ni rare but you would wish your medical students to see kabla hawajaenda kukutana nazo mtaani wakauwa watu! All in all pole kwa mtambuzi lakini kwenye kufundishana tuvumiliane kwani wagonjwa ndo teaching material zetu.
 
Pia kuna tatizo kwa mtoa mada? Wewe muda round unafanya nini wodini au ndo ujuaji wenyewe? Na je kama yupo kwenye terminal ulitaka awbmbie vp? Maana una waka tu? Ndio wewe ni mropokaji? Na hujui taratibu vingenfvyo kama kusema tfrminal ndo tatizo we ungetafuta private rums atibiwf e huko

Nadhani hukusoma hapo kwenye bold............

QUOTE=Mtambuzi;5785884]Kitu ambacho madaktari wale walikuwa hawakijui ni kwamba mke wangu pamoja na dada yake ni wauguzi by professional na wanazijua hizo terminology vizuri sana. Sasa iweje waropoke hivyo bila kuangalia walioko karibu. kitendo hicho kilifanyika muda wa kuona wagonjwa na nadhani ndio walikuwa wanamalizia round.
Tumelazimika kumchukua mgonjwa wetu kwa ajili ya kuangalia ustaaarabu mwingine.
[/QUOTE]
 
Mama mkwe wangu alilazwa Muhimbili kwa wiki moja, lakini jana nililazimika kumtoa kutokana na kile nilichokishuhudia pale. Pamoja na vituko vingi tu tulivyoviona kutoka kwa manesi wa ward ya Mwaisela, lakini nisingependa kuzungumzia hayo kwa kuwa si mageni masikioni mwa wengi. Tulimpeleka mgonjwa wetu kufanyiwa uchunguzi zaidi kutokana na kuwa na complication nyingi nadhani ni kutokana na uzee (mkwe wangu ana miaka 70 hivi sasa)

Tulipofika pale alichukuliwa vipimo vyote ikiwapo x-ray, tatizo lilikuwa ni pale madaktari wanapopita round kuona wagonjwa. kwanza walikuwa wamemgeuza mama mkwe wangu kama vile ni darasa la kufundishia wanafunzi, kila daktari alikuwa anafika na wanafunzi wake na kufungua darasa. Cha kushangaza walikuwa wameyakalia majibu ya mgonjwa wetu huku wakiendelea kumuweka pale kama mtu wa kufundishia wanafunzi.

Sikatai mgonjwa kutumika kufundishia wanafunzi, hawa ni ndio madaktari wetu wa kesho wakajifunzie wapi. Lakini pale dakatari anapowaambia wanafunzi wake kwamba huyu mgonjwa aliyeko mbele yao yuko katika TERMINAL STAGE huku wanaomuuguza wakiwa karibu na hata mgonjwa mwenyewe akisikia, huu ni uuaji. Daktari huyo aliendelea kuwaonyesha wanafunzi wake dalili zinazothibitisha kuwa mgonjwa wetu yuko kwenye terminal stage.

Kitu ambacho madaktari wale walikuwa hawakijui ni kwamba mke wangu pamoja na dada yake ni wauguzi by professional na wanazijua hizo terminology vizuri sana. Sasa iweje waropoke hivyo bila kuangalia walioko karibu. kitendo hicho kilifanyika muda wa kuona wagonjwa na nadhani ndio walikuwa wanamalizia round.
Tumelazimika kumchukua mgonjwa wetu kwa ajili ya kuangalia ustaaarabu mwingine.

Pole sana mkuu.


Ukweli mgonjwa kutumika kufundishia si swala baya ila kuwepo na ruhusa ya mgonjwa. Na kwa uzoefu wangu mara nyingi mgonjwa huombwa kwa mdomo na hakuna form yoyote, na akikataa haitakiwi kumlazimisha. Na kama hakuombwa si sawa ila mgonjwa ana haki ya kusema No. Kingine ni kwamba taarifa za mgonjwa ni siri ya mgonjwa na daktari/madaktari. Kwa hao wanafunzi kujua hilo si tatizo ila ni vema Daktari kuwa mwangalifu taarifa isiwafikie watu wengine isipokuwa kwa ridhaa ya mgonjwa. Ni vizuri daktari kujitahidi kulingana na mazingira.



Lakini katika hili hebu niambieni mnadhani wodi hizo kweli zipo standard? Kuna privacy pale Muhimbili kwa wodi za kawaida? Kwa hiyo ni kujitahidi kuwa makini.

Tatu inavyopaswa kuwa (ideal kwa hapa kwetu) mgonjwa huyo alihitaji kujua hilo (yaani yupo kwenye terminal stage) na kufanyiwa death preparation. Hiyo ni kwa mujibu wa standard/ideal. Kwa jamii yetu hii huwa siioni, hatuna utaratibu wa kufanya hivyo na hata jamii zetu hazipokei vizuri, mi niliwahi jaribu; badala yake mgonjwa anakuona wewe mbaya, japo ni kitu kizuri tu. Mimi nina observation nyingine, Hivi kumbe Wauguzi wa Tanzania hawajui dalili za terminal stage? Sikutegemea kushtuka kiasi hicho kwa wife na sister. Tusaidiane, tuwekane sawa tunapokosea...


Privacy bado ni tatizo lakini pia wakati mwingine hata lugha... Hebu nisaidieni Terminal stage kwa kiswahili inakuwaje na itapokelewaje?
 
Back
Top Bottom