Madai: Aliyemuweka Mbongo rehani akamatwa!

Madai: Aliyemuweka Mbongo rehani akamatwa!

mtoto wa nani mkuu funguka tutakuchangia m 7
Siyo maarufu sana,Ila mbona bond wako wabongo wengi tu huko......Ila Hyo mtoto wa nini ni habari lakini bado kudhibitishwa....
Mfano akida alivyowekwa bond huko Pk,juma alienda naye n'a juma akamwambia akida kuwa inabidi abaki ili aje n'a mzigo mwingine kwani wao kwanza inabidi watangulie n'a mzigo wa kwanza ndiyo akida akabaki mazimaaa.....
Huyu juma ashawaweka bond ndg yake wa kwanza anaitwa hoza Ila alirudigi
 
Kwa maana hiyo Juma alishakuwa na kesi ya kukamatwa na unga kabla ya huyo aliyewekwa Bond kuonekana kwenye mitandao ya kijamii ??? Na kama hakukua na kesi hao polisi waliokamata huo unga sijui wa trilioni moja wameupeleka wapi ????


Unga wa trilioni moja halafu ki Bond chenyewe ni mwanadamu ? Tusidanganyane
Ahaa unajua watu wengine kudanganya hawajui. Huyo mfanya biashara (hata ya uhalali) atakayekubali bond ya Tz 1 trillion shs kwa uhai wa mtu ni nani? Nakuapia hata ukienda na wanao watatu wa kuwazaa hawatakupa mzigo!
 
Ahaa unajua watu wengine kudanganya hawajui. Huyo mfanya biashara (hata ya uhalali) atakayekubali bond ya Tz 1 trillion shs kwa uhai wa mtu ni nani? Nakuapia hata ukienda na wanao watatu wa kuwazaa hawatakupa mzigo!
Bank tu hapo vuka na nenda na kende zinaniginia kama bond uone hata kama mkopo wa milioni moja watakupa ,sembuse trilioni moja ,kila kitu ni maigizo tu yaani
 

Mtanzania aitwaye Juma (jina lake la pili tunalihifadhi kwa sababu maalum) anayedaiwa kumuweka rehani ughaibuni Mbongo mwenzake Adam Akida Mwinyimkuu, mkazi wa Magomeni Mapipa jijini Dar es Salaam ambaye ametekwa na kushikiliwa na watu wanaoaminika kuwa ni ‘Wazungu wa Unga’ , amekamatwa na polisi jijini Dar.


Uchunguzi wa kina uliofanywa na waandishi wetu wiki iliyopita umebaini kuwa, Juma alikamatwa na polisi mwishoni mwa wiki iliyopita Tegeta na anahojiwa kuhusiana na kutuhumiwa kumuweka dhamana kijana Adam kisha kumtelekeza ughaibuni huku ikidaiwa kuwa yeye alikuja na shehena ya unga.

Habari zinasema ili Adamu awe huru, Juma anatakiwa kupeleka fedha shilingi trilioni moja ambazo ni gharama ya unga aliopewa, huku akimfanya mwenzake huyo kuwa ‘bond’ ya mzigo huo haramu.

“Fedha anazodaiwa Juma ni nyingi ni shilingi trilioni moja. Ni kwamba mzigo wenyewe (unga) hakufanikiwa kuuza kwani alikamatwa na askari wakamnyang’anya na sasa sijui atafanya nini ili kumuokoa mwenzake aliye ughaibuni,” kilisema chanzo chetu.

Habari zaidi zinasema kuwa licha ya Juma kuwa korokoroni, baba wa Adamu mzee Akida Mwinyimkuu naye alishikiliwa kwa muda na polisi katikati ya wiki iliyopita lakini hakuwa na msaada wowote kwa vyombo vya dola.

“Mzee Akida alikamatwa na polisi lakini badala ya kusaidia akawa anapotosha ukweli. Yeye aliwaambia polisi kuwa mtoto wake Adam hakwenda Pakistani bali alikwenda Afrika Kusini na ndivyo anavyojua. Alipooneshwa video ya mwanaye akiwa chini ya ulinzi, alishangaa na hakuwa na la kusema,” kilisema chanzo chetu.

Kamanda wa Polisi wa Kikosi cha Kuzuia na Kupambana na Madawa ya Kulevya Tanzania, SACP Mihayo Msikhela (pichani) alipoulizwa na gazeti hili kuhusu kukamatwa kwa mzee Akida na Juma hakukiri wala kukataa.

“Unajua hili jambo bado lipo kwenye uchunguzi, hatuwezi kusema chochote hadi tumalize uchunguzi wetu lakini wote wanaotuhumiwa tunawasaka na tukiwakamata tutawahoji. Tukimaliza upelelezi wetu tutatoa taarifa kwa umma,” alisema kamanda huyo.
Aliyewekwa bond na mzungu wa unga ni ndugu kabisaa, Baba mkubwa na mdogo na ndio ata Baba wa kijana polisi kasema mwanae anajua yupo south Africa

Mwanzo aliwekwa bond mdogo wa uyo jamaa aliyekamatwa mda wake ukaisha akarudi bongo akajengewa nyumba bunju , kapewa na gari na pesa kama milion 30 hivi

Na hio pesa wanaodaiwa ya tillion sio kweli
Wanadaiwa kama dolla 100,000 tu
 
Aliyewekwa bond na mzungu wa unga ni ndugu kabisaa, Baba mkubwa na mdogo na ndio ata Baba wa kijana polisi kasema mwanae anajua yupo south Africa

Mwanzo aliwekwa bond mdogo wa uyo jamaa aliyekamatwa mda wake ukaisha akarudi bongo akajengewa nyumba bunju , kapewa na gari na pesa kama milion 30 hivi

Na hio pesa wanaodaiwa ya tillion sio kweli
Wanadaiwa kama dolla 100,000 tu
ahahaha sawa kiongozi bora
 
Aliyewekwa bond na mzungu wa unga ni ndugu kabisaa, Baba mkubwa na mdogo na ndio ata Baba wa kijana polisi kasema mwanae anajua yupo south Africa

Mwanzo aliwekwa bond mdogo wa uyo jamaa aliyekamatwa mda wake ukaisha akarudi bongo akajengewa nyumba bunju , kapewa na gari na pesa kama milion 30 hivi

Na hio pesa wanaodaiwa ya tillion sio kweli
Wanadaiwa kama dolla 100,000 tu
Asante sana kwa taarifa kwahiyo Adam Akida Mwinyimkuu alikuwa anapiga mahesabu ya kuuaga umasikini kwa njia ya mkato.
 
Aliyewekwa bond na mzungu wa unga ni ndugu kabisaa, Baba mkubwa na mdogo na ndio ata Baba wa kijana polisi kasema mwanae anajua yupo south Africa

Mwanzo aliwekwa bond mdogo wa uyo jamaa aliyekamatwa mda wake ukaisha akarudi bongo akajengewa nyumba bunju , kapewa na gari na pesa kama milion 30 hivi

Na hio pesa wanaodaiwa ya tillion sio kweli
Wanadaiwa kama dolla 100,000 tu
Kumbe ni michezo yao.....hahahaaa watu wanapenda miteremko aisee nadhani hata kugegedwa wanagegedwa
 
.....teh hee hee...skonyo hizi!
..ingekuwa kweli anadaiwa trillion 1 hata panya asingesalimika kwenye ukoo wa huyo Juma hadi hao polisi 'waliomnyang'anya' mzigo!
...
 
Mtanzania aitwaye Juma (jina lake la pili tunalihifadhi kwa sababu maalum) anayedaiwa kumuweka rehani ughaibuni Mbongo mwenzake Adam Akida Mwinyimkuu, mkazi wa Magomeni Mapipa jijini Dar es Salaam ambaye ametekwa na kushikiliwa na watu wanaoaminika kuwa ni ‘Wazungu wa Unga’ , amekamatwa na polisi jijini Dar.

“Fedha anazodaiwa Juma ni nyingi ni shilingi trilioni moja. Ni kwamba mzigo wenyewe (unga) hakufanikiwa kuuza kwani alikamatwa na askari wakamnyang’anya na sasa sijui atafanya nini ili kumuokoa mwenzake aliye ughaibuni,” kilisema chanzo chetu.

Yaani huyo Juma alikamatwa na askari akiwa na mzigo wa unga wa trilioni moja, halafu wakamwachia na kuja kumkamata tena baada ya kupata habari kwamba alimweka mtu rehani?

Sikujua ukikamatwa na Polisi na mzigo wa unga wa trilioni moja unaachiwa kirahisi namna hiyo.

Na hao watu walimpa unga wa trlioni moja? Na hiyo meli iliyosafirisha mzigo wa trilioni moja Juma aliikodi wapi? Ikaingia bandrini ina contaner kama mia moja za unga sivyo?

Unanikumbusha ile hadithi ya "mtaani kwetu kuna mbuzi mkubwa akichinjwa kijiji kizima kinapata nyama. Jamaa akajibu na mie mtaani kwetu limetengenezwa sufuria kubwa kijiji chenu chote kinaweza kuingia ndani. Jamaa wa kwanza akasema, dah, hiyo hadithi ya uongo! Akajibiwa, sufuria lilitengenezwa walipomuona huyo mbuzi wa kijijini kwenu!
 
Hata namna ya utesaji wa huyo mbongo ni usanii mtupu , mtu anateswa anaonekana kanona kabisa yupo kwenye sofa la maana hapo .. halafu wanampiga kizanzibar hao magaidi wenyewe !! usanii mtupu ,
 
ktk vitu nisivyopenda ni kusikia '"jina tunalihifadhi"" ndio kuficha kwenyewe wahalifu..
 
kumbe ni vijisenti tu hivyo..
Mzee atasaidia
 
Alikamatwa Na Shehena Ya Unga Akanyang'anywa Na Sasa Yuko Tegeta
 
Back
Top Bottom