Konzo Ikweta
JF-Expert Member
- Oct 3, 2013
- 745
- 1,504
RAIS WA MADAGASCAR ATANGAZA KUWA MADAGASCAR IMEGUNDUA TIBA YA CORONA: WHO YAPINGA VIKALI DAWA HIYO
Wakati wanasayansi duniani wakihangaika kupata chanjo na tiba ya virusi vya corona, Rais wa Madagascar Andry Rajoelina amezindua dawa ya mitishamba inayotibu' COVID-19.
Hata hivyo Shirika la Afya Duniani (WHO) na Marekani wamepinga vikali tiba hiyo ya COVID-19 baada ya Rais Rajoelina kutangaza dawa hiyo. WHO na Marekani imeitaka Madagascar kukoma kuendelea na matumizi ya dawa hiyo mara moja na endapo itakaidi kuacha matumizi ya dawa hiyo huenda Shirika hilo la Afya Duniani na Marekani zikalazimika kutoipatia msaada zaidi wa kupambana na janga la Corona.
Taasisi ya taifa ya tiba nchini Madagascar (Anamem) pia imepinga matumizi ya dawa hiyo inayoelezewa na Rais Andry Rajoelina kama yenye uwezo wa kuzuia na kuponyesha corona.
Taasisi hiyo imesema kuwa mitishamba inaweza kudhuru afya ya mtu kwani "hakuna ushahidi wa ufanisi wake kisayansi".
Mmea huo unatarajiwa kutolewa bure kwa watu wenye uwezekano mkubwa wa kuathiriwa na na virusi vya corona.
Ikizinduliwa kwa jina Covid-Organics, dawa hiyo imetengenezwa kutoka kwa mmea artemisia (pakanga) ambao ni mojawapo ya miti ambayo huchanganywa pamoja na mimea mingine ya Madagascar kama tiba ya ugonjwa wa Malaria. Mmea huo ni tiba maarufu ya malaria nchini Madagascar na kwa muda mrefu umetumika kutibu malaria kwa mafanikio makubwa.
Dawa hiyo imepakiwa kwenye chupa na kutangazwa kama chai ya miti shamba baada ya kujaribiwa kwa watu 20 kwa kipindi cha wiki tatu, katibu wa Rais Lova Hasinirina Ranoromaro ameiambia BBC.
Baada ya janga la Corona kutangazwa duniani, Rais aliwataka watafiti kuja na tiba ambayo kwa bahati nzuri 'waliipata kwamuda muafaka'.
"Vipimo vimefanyika na tayari wagonjwa wawili wa COVID-19 wamekwishapona kutokana na tiba hii," Bwana Rajoelina alisema katika uzinduzi wa Covid-Organics uliofanyika katika taasisi ya utafiti ya Madagascar- Malagasy Institute of Applied Research (Imra), ambayo ndiyo iliyotengeneza dawa hiyo ya mitishamba.
"Kinywaji cha dawa hii ya mitishamba huonesha matokeo katika kipindi siku saba," alisema Rais huyo mwenye umri wa miaka 45, ambaye aliwataka watu kuitumia kama hatua ya kujikinga na kujitibu ugonjwa wa corona.
Dkt Charles Andrianjara, Mkurugenzi mkuu wa taasisi ya utafiti ya Imra, anaafiki kuwa Covid-Organics inapaswa kutumiwa kama kinga.
Lakini alijihadhari zaidi kuzungumzia zaidi juu ya matumizi ya dawa hiyo kama tiba, lakini akasema kwamba uchunguzi wa kimatibabu umeonyesha "dalili ya ufanisi wake kama tiba", shirika la habari la AFP lilimnukuu akisema.
Kisiwa hicho cha Bahari ya Hindi kimekwisharekodi hadi sasa wagonjwa 121 wa virusi vya corona, na hakuna vifo kutokana na ugonjwa huo hadi sasa.
WHO YAPINGA DAWA HIYO, YASEMA 'HAKUNA NJIA ZA MKATO'
Ikizungungumzia uzinduzi wa Covid-Organics, WHO imeambia BBC kwamba shirika hilo la dunia halishauri "matibabu ya kibinafsi ya dawa zozote... kama njia ya kinga au tiba ya Covid-19."
Lilirejelea kauli za mkuu wa WHO Tedros Adhanom Ghebreyesus ambaye ni raia wa Ethiopia kwamba "hakuna njia za mkato" za kutafuta dawa ya kupambana na virusi vya corona. Majaribio ya kimataifa yanaendelea kupata tiba yenye ufanisi , WHO iliongeza.
Sent using Jamii Forums mobile app
Wakati wanasayansi duniani wakihangaika kupata chanjo na tiba ya virusi vya corona, Rais wa Madagascar Andry Rajoelina amezindua dawa ya mitishamba inayotibu' COVID-19.
Hata hivyo Shirika la Afya Duniani (WHO) na Marekani wamepinga vikali tiba hiyo ya COVID-19 baada ya Rais Rajoelina kutangaza dawa hiyo. WHO na Marekani imeitaka Madagascar kukoma kuendelea na matumizi ya dawa hiyo mara moja na endapo itakaidi kuacha matumizi ya dawa hiyo huenda Shirika hilo la Afya Duniani na Marekani zikalazimika kutoipatia msaada zaidi wa kupambana na janga la Corona.
Taasisi ya taifa ya tiba nchini Madagascar (Anamem) pia imepinga matumizi ya dawa hiyo inayoelezewa na Rais Andry Rajoelina kama yenye uwezo wa kuzuia na kuponyesha corona.
Taasisi hiyo imesema kuwa mitishamba inaweza kudhuru afya ya mtu kwani "hakuna ushahidi wa ufanisi wake kisayansi".
Mmea huo unatarajiwa kutolewa bure kwa watu wenye uwezekano mkubwa wa kuathiriwa na na virusi vya corona.
Ikizinduliwa kwa jina Covid-Organics, dawa hiyo imetengenezwa kutoka kwa mmea artemisia (pakanga) ambao ni mojawapo ya miti ambayo huchanganywa pamoja na mimea mingine ya Madagascar kama tiba ya ugonjwa wa Malaria. Mmea huo ni tiba maarufu ya malaria nchini Madagascar na kwa muda mrefu umetumika kutibu malaria kwa mafanikio makubwa.
Dawa hiyo imepakiwa kwenye chupa na kutangazwa kama chai ya miti shamba baada ya kujaribiwa kwa watu 20 kwa kipindi cha wiki tatu, katibu wa Rais Lova Hasinirina Ranoromaro ameiambia BBC.
Baada ya janga la Corona kutangazwa duniani, Rais aliwataka watafiti kuja na tiba ambayo kwa bahati nzuri 'waliipata kwamuda muafaka'.
"Vipimo vimefanyika na tayari wagonjwa wawili wa COVID-19 wamekwishapona kutokana na tiba hii," Bwana Rajoelina alisema katika uzinduzi wa Covid-Organics uliofanyika katika taasisi ya utafiti ya Madagascar- Malagasy Institute of Applied Research (Imra), ambayo ndiyo iliyotengeneza dawa hiyo ya mitishamba.
"Kinywaji cha dawa hii ya mitishamba huonesha matokeo katika kipindi siku saba," alisema Rais huyo mwenye umri wa miaka 45, ambaye aliwataka watu kuitumia kama hatua ya kujikinga na kujitibu ugonjwa wa corona.
Dkt Charles Andrianjara, Mkurugenzi mkuu wa taasisi ya utafiti ya Imra, anaafiki kuwa Covid-Organics inapaswa kutumiwa kama kinga.
Lakini alijihadhari zaidi kuzungumzia zaidi juu ya matumizi ya dawa hiyo kama tiba, lakini akasema kwamba uchunguzi wa kimatibabu umeonyesha "dalili ya ufanisi wake kama tiba", shirika la habari la AFP lilimnukuu akisema.
Kisiwa hicho cha Bahari ya Hindi kimekwisharekodi hadi sasa wagonjwa 121 wa virusi vya corona, na hakuna vifo kutokana na ugonjwa huo hadi sasa.
WHO YAPINGA DAWA HIYO, YASEMA 'HAKUNA NJIA ZA MKATO'
Ikizungungumzia uzinduzi wa Covid-Organics, WHO imeambia BBC kwamba shirika hilo la dunia halishauri "matibabu ya kibinafsi ya dawa zozote... kama njia ya kinga au tiba ya Covid-19."
Lilirejelea kauli za mkuu wa WHO Tedros Adhanom Ghebreyesus ambaye ni raia wa Ethiopia kwamba "hakuna njia za mkato" za kutafuta dawa ya kupambana na virusi vya corona. Majaribio ya kimataifa yanaendelea kupata tiba yenye ufanisi , WHO iliongeza.
Sent using Jamii Forums mobile app