Mada maalum ya ndege toka FB

Mada maalum ya ndege toka FB

Alexander Mamonov, raia wa Urusi mwenye umri wa miaka 62 anayeishi Florida, amepatikana na hatia nchini Marekani kwa makosa 12 yanayohusiana na kusafirisha kwa siri vipuri vya ndege vya thamani ya zaidi ya $900,000 kwenda Urusi, kinyume na vikwazo vya kiuchumi.

Uamuzi huo umetolewa na mahakama ya jimbo la Florida baada ya kubainika kuwa alishirikiana na mwenzake, Ignat Vakorin (ambaye bado anasakwa), kuisaidia kampuni ya ndege ya serikali ya Urusi ya Aeroflot kupata vifaa vya ndege vya Kimarekani

Mtandao huo uliwadanganya wasambazaji wa Marekani kuwa vifaa hivyo vilipelekwa UAE na Uchina wakati halisi vikienda Urusi kwa ajili ya shirika la Aeroflot, huku hukumu yake ikipangwa kutolewa Novemba 20, 2026.
 
Baada ya miaka saba ya maumivu, kusubiri, na vita vikali vya kisheria ng'ambo ya bahari, hatimaye familia 32 za Kenya zilizopoteza wapendwa wao katika ajali ya ndege ya Ethiopian Airlines (ET302) zimepata afueni ya kisheria.

Kampuni ya utengenezaji wa ndege ya Boeing itatoa jumla ya dola milioni 87.36, zaidi ya shilingi za kitanzania bilioni 230, kama malipo mapya ya fidia kwa familia hizo zilizoathirika ambapo Kenya ina idadi kubwa ya wahanga katika ajali hiyo.

Katika mpango huu mpya, kila familia inatarajiwa kupokea dola milioni 2.73, ambayo sawa na shilingi za Kitanzania bilioni 7.17

Ajali hiyo ya kihistoria ilitokea mnamo Machi 10, 2019, ambapo ndege hiyo ilianguka dakika 06 tu baada ya kupaa kutoka Addis Ababa kuelekea jijini Nairobi.

Tukio hilo liligharimu maisha ya watu wote 157 waliokuwemo ndani, huku Kenya ikipoteza raia wengi zaidi kuliko nchi nyingine yoyote kati ya mataifa 30 yaliyohusika.

Ingawa hakuna kiasi cha fedha kinachoweza kurudisha uhai wa waliopotea, ushindi huu katika mahakama za Marekani umekuja baada ya Boeing kupatikana na hatia ya kuwapotosha wadhibiti wa usalama wa anga, hatua iliyozipa familia hizo hadhi ya kisheria kama waathiriwa wa uhalifu wa jinai na kufungua njia ya kupata haki yao.
1788174340479.jpg
 
Mwanamuziki Diamond Platnumz amerejea nchini Tanzania kutoka Kigali, Rwanda kwa kutumia ndege binafsi (private jet) baada ya kukamilisha onyesho lake kubwa kwenye tamasha la Friends of Amstel Experience lililofanyika viwanja vya BK Arena.

Diamond aliondoka Tanzania kwa staili ya kipekee akishuka kwenye gari la kifahari aina ya Rolls-Royce na kupanda moja kwa moja ndege hiyo binafsi iliyomfikisha Kigali akiwa na timu yake ya wasafi.

Ndani ya ndege hiyo, walionekana kufurahia huduma za kiwango cha juu wakati wa safari zote mbili.

Baada ya kutikisa jukwaa usiku wa kuamkia Jumapili akisindikizwa na mastaa kama Bruce Melodie na Nel Ngabo, alionekana tena uwanja wa ndege akipanda jet hiyo kurejea nyumbani.
1788201833226.jpg
 
Back
Top Bottom