Mada maalum ya ndege toka FB

Mada maalum ya ndege toka FB

Kiwanja cha Ndege cha Mtemere kilichopo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Nyerere mkoani Pwani kusini mwa Tanzania kimefanyiwa maboresho makubwa ya miundombinu na sasa kina uwezo wa kupokea ndege zaidi na kwa usalama mwaka mzima.

Uwanja huu ndio mlango mkuu wa anga kwa watalii wanaofika Nyerere kwa ndege kutoka Dar es Salaam, Zanzibar na Arusha.

Katika maboresho hayo hivi karibuni, njia ya kurukia na kutua ndege yenye urefu wa kilomita 1.8 imewekewa teknolojia mpya ya Lami yenye polima "Hard Polymer Surface"

Teknolojia hiyo imetumia rangi ya udongo mwekundu ili kuendana na mazingira ya asili ya hifadhi na pia kuzuia uchafuzi. Faida nyingine ni kuimarisha udongo ili ndege ziweze kutua na kuruka salama katika majira yote, ikiwemo kipindi cha masika ambacho hapo awali uwanja ulifungwa kutokana na matope.

Pamoja na njia kuu ya ndege, uwanja umeongezeewa barabara ya usalama yenye urefu wa mita 300, eneo la kusimama dharura la mita 60, na eneo wazi la usalama la mita 300.

Kwa sasa maboresho hayo yameruhusu uwanja kupokea ndege ndogo na za ukubwa wa kati zenye uwezo wa kubeba hadi abiria 100. Katika hatua hiyo, hivi karibuni uwanja umepokea ndege ya aina ya Dash-8-300 kutoka shirika la ndege la Air Tanzania.

Maboresho haya yanatarajiwa kuongeza urahisi wa usafiri wa watalii kwenda Nyerere na kuifanya hifadhi hiyo kuwa kivutio kinachopatikana kwa urahisi zaidi wakati wote wa mwaka.

1787322705896.jpg
 
Taja kaulimbiu au Wito unaokuvutia zaidi kutoka katika mashirika haya ya ndege:

Air Congo - "𝙏𝙝𝙚 𝙃𝙤𝙥𝙚 𝙤𝙛 𝘼𝙛𝙧𝙞𝙘𝙖"
RwandAir - "𝙁𝙡𝙮 𝙩𝙝𝙚 𝙙𝙧𝙚𝙖𝙢 𝙤𝙛 𝘼𝙛𝙧𝙞𝙘𝙖"
Kenya Airways - "𝙏𝙝𝙚 𝙥𝙧𝙞𝙙𝙚 𝙤𝙛 𝘼𝙛𝙧𝙞𝙘𝙖"
Air Tanzania - "𝙒𝙞𝙣𝙜𝙨 𝙤𝙛 𝙆𝙞𝙡𝙞𝙢𝙖𝙣𝙟𝙖𝙧𝙤"
Ethiopian Airlines - "𝙏𝙝𝙚 𝙣𝙚𝙬 𝙨𝙥𝙞𝙧𝙞𝙩 𝙤𝙛 𝘼𝙛𝙧𝙞𝙘𝙖"
Uganda Airlines - "𝙁𝙡𝙮 𝙩𝙝𝙚 𝘾𝙧𝙖𝙣𝙚 𝙩𝙤 𝙩𝙝𝙚 𝙋𝙚𝙖𝙧𝙡 𝙤𝙛 𝘼𝙛𝙧𝙞𝙘𝙖"
1787330712628.jpg
 
Shirika la ndege la Jambojet litarejesha safari zake za kila siku kati ya Nairobi na Entebbe kuanzia Oktoba 1, 2026, baada ya kusitisha huduma hiyo kwa muda wa miaka sita.

Hatua hii inalenga kukidhi mahitaji yanayokua ya usafiri, utalii, na biashara katika ukanda wa Afrika Mashariki, ambapo huduma hiyo itajumuisha usafirishaji wa abiria pamoja na mizigo.

Safari hizo zitatumia ndege aina ya De Havilland Canada Dash 8-400, na safari hiyo inatarajiwa kuchukua takriban saa moja na dakika 15.

Nauli ya kwenda upande mmoja itaanza karibu Dola 170 za Kimarekani, ambayo ni takriban Shilingi za Kenya 22,000.

Aidha, abiria wanaotokea Uganda watapata fursa ya kuunganisha safari zao kuelekea maeneo mbalimbali ya pwani ya Kenya kama Mombasa, Diani, Malindi, na Lamu kupitia mtandao wa ndani wa Jambojet.

Shirika hilo linakadiria kusafirisha takriban abiria 300,000 kati ya nchi hizo mbili ifikapo mwishoni mwa mwaka 2026.
1787474674153.jpg
 
Ushirikiano wa kihistoria kati ya Urusi na China katika kuunda ndege kubwa ya abiria ya CR929 ulisambaratika rasmi kutokana na mgongano mkubwa wa kimkakati, vikwazo vya kimataifa, na kutosimama upande mmoja kimaslahi.

Mradi huo uliolenga kutoa ushindani dhidi ya kampuni kubwa za Boeing na Airbus ulianza kuingia doa kufuatia vita vya Ukraine mwaka 2022, vilivyosababisha Urusi kuwekewa vikwazo vikali vya kiuchumi.

China, kupitia kampuni yake ya COMAC, ilihofia kuwa kuendelea kushirikiana karibu na Urusi kungeweka rehani uwezekano wa ndege hiyo kukubalika kimataifa na kupata vipuri muhimu kutoka nchi za Magharibi.

Tofauti kubwa ya kifikra ilijitokeza kwenye uteuzi wa teknolojia, ambapo China ilitaka kutumia injini na mifumo ya kisasa kutoka kampuni za Kimagharibi kama General Electric ili kurahisisha mauzo ya nje, wakati Urusi ilishikilia msimamo wa kutumia teknolojia zao za ndani ili kujikinga na shinikizo za kisiasa.

Mbali na hayo, nchi hizi mbili zilishindwa kukubaliana kiwango cha ugawaji wa faida na masoko, huku kukiwa na mzozo wa chini kwa chini wa kutoaminiana kiufundi ambapo Urusi ilisita kukabidhi siri zake kuu za kihandisi na muundo wa ndege kwa China.

Hatimaye, ushirikiano huo ulivunjika na kuifanya China kuondoa herufi "R" iliyowakilisha Urusi na kuupa mradi huo jina jipya la C929 (Awali C-929) ikiendelea nayo peke yake, huku Urusi ikijitenga na kuelekeza nguvu zake zote katika kufanya marekebisho ya ndani kwenye mradi wake wa ndege ya MC-21 kwa kutumia injini na vifaa vya asilimia mia moja vya nyumbani.
1787476674339.jpg
 
Back
Top Bottom