Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 360,781
- 830,929
- Thread starter
- #741
Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar (ZAA) imetoa ufafanuzi kuhusu madai ya wizi wa mizigo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume (AAKIA), katika taarifa yake iliyotolewa mnamo tarehe 11 Februari 2026.
Mkurugenzi Mkuu wa ZAA, Ndugu Seif Abdalla Juma, amekanusha madai hayo na kusisitiza kuwa si sahihi.
Uchunguzi wa kina uliofanyika na kamati maalumu iliyoundwa na ZAA, haikupata ushahidi wa moja kwa moja unaothibitisha kuwepo kwa vitendo vya wizi wa mizigo ndani ya uwanja huo ambapo mizigo mingi iliyokuwa imefunguliwa au kuharibika ilibainika kuwa ilifanyika kabla ya kuwasili Zanzibar.
ZAA imechukua hatua za ziada za usalama, ikiwemo kumtaka mtoa huduma ardhini (ground handler) kuweka kamera maalum ndani ya ndege na kuwapatia wapakuzi wa mizigo kamera maalum za kuvaa mwilini (Body Cam).
Mamlaka inawahimiza wananchi na wasafiri kuzingatia taratibu za kiusalama na kuepuka kusambaza taarifa ambazo hazijathibitishwa.
Mkurugenzi Mkuu wa ZAA, Ndugu Seif Abdalla Juma, amekanusha madai hayo na kusisitiza kuwa si sahihi.
Uchunguzi wa kina uliofanyika na kamati maalumu iliyoundwa na ZAA, haikupata ushahidi wa moja kwa moja unaothibitisha kuwepo kwa vitendo vya wizi wa mizigo ndani ya uwanja huo ambapo mizigo mingi iliyokuwa imefunguliwa au kuharibika ilibainika kuwa ilifanyika kabla ya kuwasili Zanzibar.
ZAA imechukua hatua za ziada za usalama, ikiwemo kumtaka mtoa huduma ardhini (ground handler) kuweka kamera maalum ndani ya ndege na kuwapatia wapakuzi wa mizigo kamera maalum za kuvaa mwilini (Body Cam).
Mamlaka inawahimiza wananchi na wasafiri kuzingatia taratibu za kiusalama na kuepuka kusambaza taarifa ambazo hazijathibitishwa.