Azriel "Al" Blackman "Blackie" ni fundi wa ndege maarufu aliyefanya kazi takribani miaka 80 katika sekta ya usafiri wa anga na kustaafu akiwa na umri wa miaka 96 mwaka 2022.
Alizaliwa mnamo mwaka 1926, New York, na alianza kazi yake na shirika la ndege la American Airlines mwaka 1942 akiwa na umri wa miaka 16.
Blackie alifanya kazi kwenye aina mbalimbali za ndege za sasa na zamani, kuanzia Sikorsky flying Boats hadi Boeing 777.
Blackman alitambuliwa na kitabu cha Guinness World Records kama mfanyakazi (mechanics) wa muda mrefu zaidi wa sekta ya usafiri wa anga.
Lakini pia alikuwa na heshima ya muda wa kazi kwani alipangiwa kuanza kazi saa 5 asubuhi, lakini mara nyingi alikuwa anafika ofsini kabla ya saa 3 asubuhi.
Alikuwa mmoja wa wafanyakazi wa kwanza kufika kazini, na pia mshauri mzuri kwa mafundi vijana.
Shirika la American Airlines iliheshimu uwepo wake kwa kuweka jina lake kwenye ndege ya Boeing 777.
Pia, alipewa heshima ya kupanda ndege ya zamani ya DC-3 na kutembezwa juu ya jiji la New York.
Mwaka 2017, shirika la ndege la American Airlines, ilichora picha yake kwenye ukuta wa karakana ya ndege (Hangar).
Blackman aliendelea kufanya kazi hadi umri wa miaka 96 mnamo 2022, na aliendelea kuwa mshahuri wa mafundi vijana.
Blackman anasema, "Unapopenda kazi, haiwi kazi".
Kauli hii inaonyesha jinsi alivyokuwa na ari na kujitolea kwa kazi yake.
Hadi kufikia mwishoni mwa 2025, ripoti za maoni mtandaoni zilionyesha Azriel "Al" Blackman kuwa alikuwa amestaafu na anakaribia siku yake ya kuzaliwa ya miaka 100 mnamo Agosti 2025.