Mabraza wa Kariakoo na dili zao

TUNAVUKA MPAKA NA KUINGIA DRC!!!!!
Basi wenyeji wetu wakatuletea ugali na samaki tukala...baada ya hapo tukafunga funga mabegi yetu madogo ya mgongoni!!
Kumbuka tulikua porini nje kabisa ya mji mdogo wa Miduha......pale tulipokua ni kilimani maana ukishuka kidogo tu unaingia DRC kwenye misitu na mapori kati ya mji wa Bukavu na Uvira uelekeo kuelekea mji wa Kitenge,ambapo ndio starting point ya kuanzia tour yetu ya kutazama fursa.
Sasa wale wadau wetu wakatugongea mlango"""Hey bana tanganyika mko kwa fuasi tuondoke bayemba bayemba"""""
Ndagara akawajibu""""Nzala bayemba bayemba tuko kwa fuasi"""""
Wakatupokea mabegi yetu na tukatoka nje ya nyumba na kushuka chini kilimani mpaka chini kabisa..
Daaaah na msimu wa mvua ulikua ndio umeanza maana niliambiwa kule DRC kwenye misitu mvua inanyesha miezi kumi kwa mwaka mzima sasa sijui ni ukweli ila mimi nilikuta mvua kubwa tu kwa siku zoote nilizokaa misituni kati ya Burundi na DRC.
Waongozaji wetu walikua watu watano....watatu walikua na silaha na wawili walibeba mabegi yetu na mizigo yao.
Wote walivalia kiraia kama sisi na ilikua saa tano kasoro asubuhi ila kulikua na ukungu mkubwa kwa sababu ya mvua.
CHANGAMOTO YA KWANZA:
Pale tu tulipofika kule chini kilimani kabla harujatembea umbali mrefu ili kuingia aridhi ya DRC tulikutana na kundi kubwa la asikari wa jeshi la Burundi wakiwa katika doria ya mpaka wao dhidi ya waasi wa kitusi wa kirundi waliojificha kwenye misitu ua DRC hasa kutokea jimbo la Kivu kusini.
Muongoza msafara akatoa ishara tusimame na kulala chini kwenye majani na tutulie tuli......!!!Wao walikua hawatuoni ila sisi tunawachora tu walipokua wanapita kichakani kwa mstari mmoja ulionyoooka huku wengineo vichwani wakiwa wamebeba masufuria na madumu na silaha na kuni wanaongozana kuelekea destination ya doria yao.Sisi pale chini tumelala tuliiii....mpaka wakapita wote na idadi yao ni kama 150 hivi na ushehe.
Walipopita basi sisi hao tukainuka na kuvukia upande wa DRC na kuendelea na safari yetu.
Kumbuka tunapitia pori kwa pori na hakuna barabara zaidi ya kukata majani ya miti na mapanga na kuvuka mabwawa ya maji yaliyosababishwa na mvua zinazonyesha mwanzo huu wa mwaka.
Baaada ya masaa matatu au manne kutokea pale mpakani tukafika sehemu ya kijiji kinaitwa Punge na wakazi wa pale ni wa kabila moja na wale waongozaji wetu...na hapo ni katikati ya Uvira na Bukavu katika uelekeo wa kuelekea mji wa Kitenge.
CHANGAMOTO YA PILI:
Wakati ndio tumefika nje ya nyumba ambayo ndio tunatakiwa tupumzike pale Punge ghafla tukasikia mlio ya miluzi na wenyeji wetu wakatuchukua haraka kutukimbiza kwenye mashimo yaliyokua katikati ya ua wa ile nyumba na kwa juu wameweka mawe makubwa ya kusagia unga wa mihogo.
Ndani ya yale mashimo ni kama mahandaki kumeifadhiwa magunia ya mihogo mikavu kwenye vichanja vilivyojengewa humo humo shimoni kwa utaalamu wa ngazi kwa ngazi......na yale mashimo ni marefu futi sita kwa tisa kama sikosei hivi....kwa juu ndio wameweka vifuniko vya majani na mawe ya kusagia ili kupata unga wa mihogo.
Nilikuja kujua baadae kua wanafanya vile ili kutunza akiba zao za chakula dhidi ya wezi na waasi na wanajeshi wa vikosi vya serikali ya DRC.
Tukaingia mle ndani haraka sisi wote watu saba.
Ila kuna matundu madogo madogo kwa juu unaweza kuchungulia nje....mara nasikia milio ya magari na viatu vya watu vinakimbia kimbia.....nikainuka kuchungulia na kuona pale juu uwanjani zimepaki landcruser za kijeshi kama tano na wanajeshi wameshuka na kuanza kukagua kagua nyumba za pale kijijini na kuzungumza na wanakijiji afu baadae wakaondoka.
Baada ya mda nikasikia mluzi tena na wakaja watu wakatoa lile jiwe kwa juu,afu wakatuwekea ngazi tukatoka taratibu mpaka nje.
Tukapelekwa mpaka kwenye ile nyumba ya mwanzo tukaingia ndani....tukakaa chini tumechoka kweli na hiyo ilikua mida ya saa kumi kasoro.
Hapo tukapumzika kidogo na tukapatiwa uji wa mihogo afu safari ikaendelea mida ya saa moja jioni.....hapo kila mtu na tochi yake mkononi ila haturuhisiwi kuziwasha mpaka kiongozi wa msafara atoe ruksa....sababu kuwasha taa usiku ni hatari sana hasa msituni.
CHANGAMOTO YA TATU:
Tulipotembea umbali mrefu mpaka saa nne za usiku tukaamua tupumzike katika eneo ambalo ni kambi ya waasi wa KIBANGU BANGU waliyokua wameitelekeza baada ya kushindwa na vikosi vya majeshi ya FARDC na kukimbia.
Kambi yenyewe ni vibanda vilivyovunjika na majani yameota kila mahali maana kambi ilikua imetelekezwa mda mrefu.
Tukachagua vibanda vyenye nafuu kidogo tukajiegesha tujipumzishe.
Mda hata hatujatulia kidogo tukaanza kusikia mlio ya risasi kwa mbali......basi fasta fasta wale waongozaji wetu wakatutoa eneo lile na kuingia pembeni kwenye misitu ile na kutupandisha juu ya miti na rochi zote zikazimwa tukabaki tunaisikilizia ile milio ya risasi.
Milio ile ghafla ikakoma afu kujawa kimya sana na tukaanza kusikia vishindo vya watu wanaokuja kwa kukimbia na kumbe ni Wabangu bangu militia,s wamerudi kuchungulia kambi yao waliyoitelekeza.
Na kiasili Wabangu bangu na Makemba Bunene ni maadui wa jadi kwa sababu wote ni wezi wa madini na wanatafuta kumiliki maeneo na kuisumbua serikali ya DRC.
Mara zikaanza risasi kulia kuja ule upande wetu ila zinapita kwa chini....ni usiku unaona cheche na kusikia matawi ya miti mifupi inakatika tu....kwa mda wa dakika tatu afu kukawa kimya kwa mda wa nusu saa......mara ukasikika mluzi tena na vishindo vya watu kuondoka eneo la kambi ile kwa kukimbia na kuimba nyimbo zao....kumbuka sisi tupo pale juu ya miti tunasikilizia.
Baadae wale waongozaji wetu wakatuambia huenda wale wabangu bangu walipata taarifa kua kambi yao imevamiwa tena na wanajeshi wa serikali wa FARDC kutoka Bukavu au Uvira au waasi wa kinyarwanda na....ndio maana wakaja kuwaharibia ila walipofika wakakuta kambi ni tupu ndio maana wakaondoka.....na waliowapa taarifa ni watu wao MBILIKIMO WA MSITUNI ambao walitufananisha na wanajeshi wa FARDC au waasi wa kinyarwanda.
Tulishuka pale juu ya miti taratibu na tukaendelea na safari yetu mpaka usiku wa manane ndio tukafika kijini kilichochangamka kiitwacha Zendi au Zendika sikumbuki vizuri na hapo ni eneo rafiki kwa waongozaji wetu,,,,tukapata nyumba ya nyasi ya kupumzika ambayo ndani yake mlikua ni kama ghala la vifaa ila tukatandika chini matandiko tukalala tumechoka balaa maana tumetembea masaa manne au matano bilia kupumzika afu ni usiku wenye baridi balaa.
Ili asubuhi tukiamka tuendelee kuitafuta KITENGE ambayo ndio starting point yetu ya kutazama fursa.
CHANGAMOTO YA NNE:
Mda wa alfajiri nikashitushwa na Ndagara aliesema dogo vaa vizuri tuondoke maana huku usijiachie kama nyumbani Tz.Fasta nikaweka vitu vyangu sawa na kutoka nje ya ile nyumba tuliyofikia.
Kumbe bhana kijiji kizima wana Zendi ni masoja na hakuna akina mama wala watoto bali wazee wa kazi....na kile kijiji ni kambi yao isiyo rasmi....afu wake na watoto wao wanawaficha porini au kwenye miji mikubwa mikubwa especially kwenye mji wa KITENGE.
Na taarifa zetu zoote walikua nazo kutuelezea sisi ni kama wadau ambao tunaweza kuwatafutia masoko ya uhakika ya kuuzia mawe yao nchini Kenya na Tanzania.
Basi wakaongea kibangu bangu pale na bro Ndagara afu tukapewa makoti ya kuzuia mvua.....tukaanza safari ile alifajiri pori kwa pori....kuutafuta mji wa KITENGE....!!
DRC bhana hakuna barabara za uhakika hasa kipindi cha mvua na hakuna usalama kabisa maeneo ya mashariki...maana ilikua tukitembea mara tusimame tuchunguze uelekeo....mara tujifiche wakija watu karibu yetu.
Kwahiyo mwendo wetu ulikua wa pole pole pori kwa pori afu mvua inanyesha na inakata.
CHANGAMOTO YA TANO:
Humo njiani tukielekea mji wa KITENGE tulifika sehemu ya milimani hivi,kuna uwanda mkubwa wa majani majani.Tulikuta vita kati ya waasi wa vikundi vidogo vidogo vya waasi walikua wamedhulimiana madini.
Ikabidi tutulie huku juu ya kilima huku wale waongozaji wetu wakitafuta njia salama ya kupita chini ya vile vilima.
Tatizo la waasi wanapigana kama watoto....mara wanakimbizana...mara wanasimama na kutukanana...mara wanaimbaimba na kukata mauno....mara wavute bangi....mara wapige risasi hewani......Basi ilikua tafarani......ilibidi tutulie kule juu ya kilima masaa matatu afu ndio tuangalie utaratibu wa kushuka chini ya vile vilima ili tuendelee mbele uelekeo wa mji wa KITENGE.
Hiyo ilikua inaelekea adhuhuri na tulikua hatujapumzika toka asubuhi ila kwa sababu ya mvua hakukua na jua kali mpaka mda huo.
ITAENDELEA.........!!!!!!!
 
NAENDELEA........!!!!
Nilikua kimya kidogo sababu nilikua kwa wabangubangu huko nafuatilia dili flani afu tukadakwa na masoja wahuni waliopinda balaa wa FARDC katika road block ya barabarani kati ya mji wa Lellwa na Kamombo wakitudhania sisi ni wahalifu tunawauzia silaha banyamulenge,silaha za kutokea Uganda au tunanunua madini ya vikundi vya waasi na kuyavusha ziwa Tanganyika mpaka Burundi.
Ikabidi tukae ngomeni.......mpaka pale wadau walipokuja kututolea dhamana
NAPOMAANISHA DHAMANA NI KWAMBA WADAU WALIVAMIA NGOME NA KUZICHAPA MCHANA KWEUPE WAKIDAI WANAWATAKA WASWAHILI WAO ESPECIALLY MIMI WALIEKUA WANANIITA KALULU MTOTO YA ZANZBAR NA LILIKUA SHAMBULIZI LA SUPRISE SO IKABIDI TUACHIWE HURU MAANA MASOJA WALIKIMBIA NA KUTELEKEZA KAMBI AMBAYO ILIKUA KAMA KITUO KIDOGO CHA KUKAGULIA MAGARI BARABARANI KATI YA MJI WA LWELLA NA KAMOMBO BASI WADAU WAKATUTOA KINGUVU SISI NA WASHIRIKA WAO WENGINE WALIOKAMATWA KIPINDI HICHO*
Ila wale manjagu wahuni wa FARDC walitupukutisha mzigo wote wa mawe tuliopewa kuupeleka BURUNDI kimagendo kwa kuuvusha ziwani....na mpaka mda huu nipo na ugomvi na MWANANGU NDAGARA....maana alidai mm nina roho nyepesi sana ndio maana wale wanoko wa FARDC wamechukua mawe yetu......SASA NIPO SEHEMU SALAMA NIMETULIA ngoja niwape story kidogo...!!!
Kuna braza wetu mmoja wa kuitwa. ""NDAGARA""" yeye amezaliwa katika mji mmoja wa mpakani mwa DRC na Burundi ambao unaitwa MIDUHA....anaishi Nairobi alikuja masikani na dili la kuchukua mawe kinyemela kutoka DRC na kuyavusha Burundi....afu baada ya hapo""YANAUZIKA BILA KUKATWA KODI""".
Braza akasema ni issue ya wiki tatu tu tunamaliza kila kitu....mchawi pesa ya mtaji tu...
Akasema ameshawapanga watu wake Burundi na DRC na mizigo wanayo.....kwahiyo ni sisi tu...twende MIDUHA au tumtumie hela amalize kila kitu.......TUKAPIGIANA HESABU ZINAHITAJIKA MILIONI 60 ZA KIBONGO.....KWA KUANZIA AMBAZO ZITAZAA MILIONI 314 KAMA MZIGO UKIVUSHWA SALAMA BURUNDI......!!!
Kama mnavyojua ndugu yenu napenda hela.....afu hapa nilipo nimepigika na mwaka ndio unaanza.....nikaona hii fursa ngoja nichungulie........
Kama kweli unaweka milioni 60 na unapata 314 ndani ya wiki tatu.....basi mchawi mtaji...ngoja mtaji utafutwe hata kwa kukopa.
Hapa town sisi watoto wa mjini hatuna hela.....ila hela ya kula sio issue na hela za kukopa sio issue wala kupata asset za kuweka bondi sio issue"""""MAANA TUNAAMINIKA""".
Unajua TANZANIA kuna watu wana hela ila kama hawakujui hawawezi kukukopesha sababu pesa nyingi zinapitia mlango wa nyuma kuingia mifukoni mwa watu....
Safari hii nikawacheki wahindi mabraza zangu wa migodini huko kwa wasukuma""BIG UP BRAZA PATEL""" ....nikampa mchongo wanikope hela afu bondi nawaachia gari na trekta la kulimia vikae yadi mpaka hela itakapoanza kurudi.
Tukahesabiana siku 60 bila riba
WANA FAMILIA HATUTOZANI RIBA
Hela ikapatikana ikawekwa kibindoni sehemu salama ambayo mimi niliyekopwa na mkopeshaji tunaijua afu ndio nikakaa mezani kusikiliza hilo dili.....maana lilivutia.
NDAGARA: Mpango upo hivi...ni kwamba kule DRC hasa maeneo ya KIVU KUSINI hasa miji ya LUBENGA,KASABA,MALUNGU,KAHOLOLO, KILEMBWE NA TULAMBO....kuna mawe ya kumwaga ni sisi kununua tu na kuyavushia ITARA au KAKAMBA na kuyauzia MIDUHA kwa wadau wa kununua mawe.....kila kitu kipo under control.....na biashara ikiwa nzuri tutahamishia makazi BUJUMBURA kwa mda ili tupige hela..!!!
MIMI: Mkuu hii dili unachosema nakuelewa ila sasa kuna risk kubwa...afu mtaji wakuanzia milioni 60 tena za kukopa ni mdogo mno,......afu hapo hatujaweka gharama za usafiri na mambo mengine ya kibiashara...
MIMI: Kwanini tusijipe wiki mbili twende kigoma afu tuvuke ziwa tuingie burundi then tufuatilie soko sisi wenyewe kwa kutazama na sio kuambiwa.....MAANA MANENO YA KUAMBIWA CHANGANYA NA YAKO.
NDAGARA: Dogo sikia unachosema mimi nakuelewa.....wewe tafuta milioni sitini ya mtaji wako na mimi nina pesa ya mtaji wangu milioni sitini.
Hatutoingia kwenye biashara mpaka tufanye uchunguzi....ili tuone maneno niliyoambiwa ni kweli....
Gharama za kwenda safari yetu ya kuchunguza nadhani itatugharimu milioni mbili za kitanzania kila mmoja......sababu kule Burundi mimi ni nyumbani....na nina wadau wengi kwahiyo kwa kule gharama hazitokuwepo.
*NDAGARA ALIPOSEMA WADAU ALIMAANISHA WAASI WA MSITUNI KULE KONGO AMBAO WANATAFUTA MASOKO MAZURI YA KUUZIA MADINI YAO....SABABU HAWATAKI KUWAUZIA WANYARWANDA NA WAGANDA WAKIDAI WANAWAPUNJA MGAO
NDAGARA alinificha mengi ili nimpe kampani ila niliyajua nilipofika BURUNDI na kukutana na wazee wa kazi.....!!!!
Kesho yake asubuhi
Ndagara katoka Nairobi kaja dar afu tukakaa chini na kupangiana mipango ya kwenda kuchungulia fursa na ikiwa nzuri tunajitosa hivyo hivyo kila mtu na mtaji wa kukopa....
Mimi nikamcheki braza PATEL na kumwambia zile siku 60 asizihesabu maana bado sijaanza hiyo biashara rasmi,na kama ni biashara ya uhakika nitamuingiza na yeye aongeze mtaji.....ngoja nikaichungulie kwanza.....na katika zile milioni 60....tutoe milioni mbili za safari afu zingine akae nazo kwanza mpaka mimi nikiona biashara ipoje ndio nimwambie.
Na zile bondi zangu arudishie wadau wangu wakae nazo zisikae yard tena,sababu biashara bado kuanza.
Mimi naingia kigoma mara moja....kisha navuka ziwa naingia Burundi kibishi kuchungulia fursa na kukutana na wadau wa huko.
Jamaa yangu Ndagara kanihakikishia hao wadau wana mizigo ya kutosha ila tatizo ni wanunuzi tu wa kimagendo wa kuaminika na wao.
Fasta nikakamata gari mpaka kahama....pale kahama nikakamata gari mpaka Nyakanazi.....pale Nyakanazi nikakamata gari mpaka Kakonko......Kibondo........Kasulu.... then nipo town Kigoma ....mji wenye kumbukumbu nyingi na mimi since 1996............!!!
Ndagara tunakutana Kigoma mjini mitaa ya Mwanga afu tunakaa chini kupanga mpango kazi wa kukutana na wadau wenye mzigo....na namna ya kuvuka ziwa kimya kimya mpaka upande wa Burundi.....either tushukie mji wa KABEZI au GITAZA .....kule juu Bujumbura wachawi wengi ni noma!!!!
KUMBUKA SIKUJUA WADAU KAMA NI WABABE WA VITA HUKO DRC WATU WALIOPINDA BALAA*
Kaa chonjo nije nikupe kilichoendelea huko maana vita wewe visikie tu ila usiombe vikukute....!!!
ITAENDELEA................!!!!
Daah kama movieee.wee mdau salute
 
INAENDELEA.................!!!!
NEAR KITENGE CITY....DRC:
Wale waasi baada ya kuacha kupigana,kila kikundi kikachukua njia yake kwenda uelekeo tofauti wa vile vilima vinavyotazama upande wa mji wa Uvira huku wakiimba nyimbo kwa kukimbia mchaka mchaka na kukata mauno.Kwakua sisi tulikua chini ya vile vilima na tulikua tunaenda uelekeo wa mji wa Kitenge hatukuweza kuonana nao sababu ya yale majani marefu na vichaka vile vilivyoshonanana mule msituni.....na hata kama tungeonana nao kwa mujibu wa wale waongozaji wetu.....basi kungechapika kati yao na waongozaji wetu namaanisha bana""BUNENE""
Na vile vikundi vya waasi vilivyokua vinapigana vyenyewe kwa vyenyewe ni makundi ya vijana wahuni,wavuta bangi na mihadarati mingine ya porini na walevi wa pombe za kienyeji ambao kazi yao kubwa ni kupora wanavijiji na kuwaibia na kubaka raia wasio na hatia.
Kwahiyo bana bunene wanawajua vizuri sana hao wahuni na ndio maana walisema tukikutana nao zitachapika
Mvua zikaanza kunyesha wakati tukitembea ule uwanda wa chini kuukaribia mji wa Kitenge,na kwa sababu ya mvua na mawingu tukashindwa kujua mda ule ni saa ngapi sababu simu hatukua nazo bali ni moja tu ya waongozaji tena ni ya satelite.Tuliacha simu zetu kule Burundi kwa sababu za kiusalama...na ukitaka kujua mda unawauliza waongozaji.
NILISAHAU KUSEMA KUA KULE DRC KUNA MAENEO HAKUNA MAWASILIANO YA SIMU ZA MIKONONI BALI SIMU ZA SATELITE TU.NA KUNA SEHEMU HAUTAKIWI KUA NA SIMU ZA MKONONI AU ZA SATELITE ILI KUEPUKA CHANGAMOTO ZA KIUSALAMA HASA UKIWA SEHEMU ZINAZOKALIWA NA VIKUNDI VYA WAASI NA MAGENGE YA WAHALIFU KWA WINGI NA MFANO MZURI NI JIMBO LA KIVU YA KASKAZININA KIVU YA KUSINI*******
Sasa zile mvua zilikua na changamoto ya matope na mule porini kujaa matope.....ila baadae nahisi ilikua jua linakaribia kuchwa.....wale waongozaji wetu wakatufikisha katika eneo la kambi ya msituni...wakaniambia hapa ni kambi ya wanyarwanda wa FDLR ambapo wanaishi wanawake na watoto kwa usalama...na kwamba wale waasi waliokua wanapigana kule vilimani hapa kwenye hii kambi hawawezi kusogea hapa sababu wanawachukulia FDLR kama washirika wao wa kijeshi dhidi ya vikundi vya waasi wa kitusi.....wao kwa wao wakishalewa tu na kuvuta mihadarati wanagombana na wanauana na wanaibiana ila hawawezi kuwaibia au kugombana na hawa wanyarwanda wa FDLR sababu wanawachukulia kama wageni wao na sio maadui.......naposema kambi namaanisha eneo la makazi ya watu zaidi ya mia nane.
Na wamekuepo pale zaidi ya miaka tisa huku wakipambana na waasi wa kitusi kwa nyakati tofauti na hii kambi ni kituo kimojawapo cha vituo vingi vya FDLR nchini DRC.
Humo kambini watu wanaendelea na maisha yao kama kawaida na kuna hadi vijito vinavyotiririka ambavyo baadhi vinatumiwa kama beach za watu kwenda kupumzika na kuogelea na sehemu zingine maalumu kwa ajili ya kuchukua maji ya matumizi ya nyumbani.
Kuna mabucha ya kienyeji nyama pori zinapatikana hadi nyama ya nyani na sokwe.
Kuna hospital ya kienyeji na kuna hoteli za kienyeji na masoko ya mbogamboga na matunda na nafaka na pia maduka ya nguo za mitumba na spesho yapo na watu wanaishi maisha yao kama kawaida bila bugudha yoyote ile.Pia kuna wanamgambo walinda usalama ambao wanasimamia mbadala wa polisi na kuna sehemu za kusalia hasa makanisa kanisa ya kipentekoste.Pia zipo sehemu za mafunzo ya madogo madogo ya kijeshi hasa kwa vijana waliovuka balehe pale kambini.....Na hii kambi ipo porini kweli kweli mbali kabisa na makazi ya watu ila kwenye muelekeo wa mji wa Kitenge.
Na wakazi wake wengi ni wanawake,wazee,watoto,na vijana wa makamo!!!
Wale waongozaji wetu wakatuambia kua bila kua na vibali vya wanyarwanda wa FDLR huwezi kupata access ya kuingia hii kambi,na hapa tutapumzika sisi maana ilikua jioni na ni siku ya tatu kimahesabu katika safari yetu.
Wao waongozaji wetu wataenda kwenye location zao afu watatufuata sisi pale kambini baada ya siku mbili ili tuingie mji wa Kitenge rasmi sasa kwa kwenda kuzitazama zile fursa na kuangalia sample za mizigo ya mawe.
Na kuweka mambo yao mengine sawa kwa ajili ya harakati zao za kibiashara kari ya DRC na BURUNDI
FDLR CAMP IN SOUTH KIVU DRC:
Hawa wadau waliokya wanatuongoza kuna vitu walikua wananishangaza ile mbaya kwa tabia zao za ajabu mda wote ambazo ni
1: WALIKUA HAWAONGEI LUGHA YOYOTE KWETU ZAIDI YA KISWAHILI.
2: WALIKUA HAWALI MPAKA SISI TULE KWANZA NA WAHAKIKISHE TUMESHIBA.
3: KULE PORINI TULIPOLALA JUU YA MITI...WAO MDA WOTE WALIKUA NA BUNDUKI ZAO MKONONI WANAFANYA DORIA.
4: WALIKUA WANAFANYA TUNAVYOTAKA SISI JAPOKUA WAO NDIO WALIKUA WENYEJI WETU...MFANO MZURI TUKIWAAMBIA TUMECHOKA BASI WANASIMAMA NA KUTUTENGENEZEA HEMA TUPUMZIKE WAO WANASHIKA DORIA.
5:WALIKUA MDA WOTE WANATRACK SIMU ZINGINE KUPITIA SIMU YAO YA MAWASILIANO YA SATELITE MPAKA TUNAFIKA KWENYE ILE KAMBI YA FDLR MULE MSITUNI
6: WALIKUA WANATUULIZIA SANA HALI YA MAISHA NJE YA DRC.
7: WALIKUA WANAPENDA SANA KISWAHILI CHANGU NA NIKIONGEA WANACHEEEKA.
8: WALIKUA WANAJUA KUHISI TATIZO MBELE AU KUHISIA UJIO WA WATU NA WANYAMA WADOGO WADOGO WA PORINI HASA CHATU NA NYOKA NA NDIO MAANA KUNA SEHEMU WALIKATAA TUSISIMAME AU KULALA AU KUPUMZIKA KUEPUSHA HATARI HIZO.....HASA WAKATI WA KUVUKA VIJITO NA MABWAWA YA MAJI YA MVUA.
9: WALIKUA FASTA KWENYE KUPIKA MAANA WALIKUA WATANO NA WATATU KATI YAO WAMEBEBA VIFAA VYA KUPIKIA KABISA....NDANI YA MASAA MAWILI UGALI TAYARI.......KUMBUKA CHAKULA NI UGALI NA NYAMA KAVU.
10: WALIKUA WAMEVAA KIRAIA NA JUU WAMEVAA MAKOTI YA MVUA ILI KUFICJA SILAHA ZAO ZA BUNDUKI NA VISU NA MAGAZINE NA SILAHA NYINGINE NDOGO NDOGO......KIUFUPI WALIKUA WAHALIFU HASWA AU WAASI HASWA.....NA NDIO MAANA KULE MWANZO WALITUFICHA NA WAO KUJIFICHA WANAJESHI WA FARDC WALIPOVAMIA KILE KIJIJI NA KUANZA KUKAGUA KAMA NILIVYOELEZEA KULE MWANZONI KWENYE CHANGAMOTO NAMBA MOJA.
KAMBINI MWA FDLR
Mle kambini tukakaribishwa na kamanda wa FDLR kama alivyojitambulisha kwa jina la KANALI NIKAMBONYIERA.
Yeye alikua anakaa sehemu ya juu kilimani na hii kambi ipo kwa chini na hili kufikia makazi yake ilibidi tupande kilima tena ambacho kimefunikwa na msitu wa miti mingi pande zote na ikumbukwe wakati huo bado mvua za rasharasha zilikua zinaendelea kunyesha ila zilikua zimepungua upepo na sio kama mwanzo,na tulikua tumelowa chapachapa na tumechoka balaaa...tulipoingia tu kwenye ofisi yake ambayo ni nyumba ya miti na mabati.........Tukaonyeshwa chumba tukaingia watu wote saba tukavua makoti yetu taliyolowana na mvua na tukabadilisha baadhi ya nguo na tukapewa vikombe vya uji tupoze njaa.
Baaadae akatuita kwenye chumba kingine ambacho kilikua ni kama sebule ya kupokelea wageni wake.
Na maongezi yetu ni haya.
KANALI NIKAMBONYIERA: Bandugu nyinyi ni bafanya biashara kwa fasi ya wapi????
NDAGARA: Fasi ya nairobi papaa ila nazaya miduha burundi pale.
KANALI NIKAMBONYIERA: Oooh oky mnasugusa magolidii au maalimasi au masilaha???
NDAGARA: Vyote tunasugusa papaaa ukitupa mafaranga na makonectee
KANALINI KAMBONYIERA: Ila kwa sasa mnasugusa nini na hao ba bunene???
NDAGARA: Kwa sasa tunasugusa magolidii na maalimasi na hao ba bunene.
Bana tumizigo tupo Kitenge tunaenda kwa fasi hiyo kututazama na tukikulungura tunafanya nao bezinee.
KANALI NIKAMBONYIERA: Batu bangu pale....hapana kua na shida na masojaa kama nyinyi.
KANALI NIKAMBONYIERA: Huyu kadogoo ni sentee yako???
NDAGARA: Ndio papaa anaitwa KALULU mtu ya Baswahili.
KANALI NIKAMBONYIERA:Aaaaaah aaaah,aaaaaaah.Hii ni mtu ya baswahili KALULU....karibu sana,karibu sana.
HUYU KANALI NIKAMBONYIERA WAKATI ANATUPOKEA ALIKUA AMELEWA NA NDIO MAANA MDA MWINGI ALIKUA ANAONGEA TU NA ALIKUA ANATAKA KUJIONYESHA KWA WENZAKE KUA YEYE NI MTU WA KUFAHAMIANA NA WATU WENGI MAANA NILIMSIKIA KWA KINYARWANDA CHANGU CHA KUUNGA UNGA ANAWAAMBIA WALE WASAIDIZI WAKE KUA SISI NI WAGENI WAKE MAALUMU KUTOKEA TANZANIA TUMEKUJA PALE KWA AJILI YAKE YEYE NA AKAWA ANAWAAMBIA KUA WASIJE WAKATUPA NYAMA ZA NYANI WASAIDIZI WAKE WAKAMJIBU SAWA AFANDE ILA KWA LUGHA YA KINYARWANDA HUKU WAKICHEEKA KUA BASWAHILI HABAJUI UTAMU WA NYAMA YA NYANI🤣🤣🤣.........BASI WAKAWA WANACHEKA NA KUMPONGEZA KWA KUMWAMBIA MKUU TUNAKUAMINIA UNAJUANA NA WATU WENGI NA SAFARI HII HATUTOISHIWA TENA STOCK YETU YA VIFAA NA SILAHA.......AKAWA ANAWAJIBU KWA KUCHEKA NA KUSEMA MDA SI MREFU WATAKUJA WAGENI WANGU WENGINE KUTOKEA ANGOLA NA ZAMBIA.......WAKAWA WANACHEKA HUKU HAWAJUI KUMBE MIMI NAELEWA WANACHOSEMA ILA NIMENYUTI TU SABABU HAYANIHUSU NA MIMI NI MTALII TU NIMEKUJA KUFUATILIA DILI ZANGU HUKU......HAPO ILIKUA IMEFIKIA WIKI SASA TOKA TANGU TUTOKE KIGOMA MJINI KULE NCHINI TANZANIA***********
Na pale kambini palikua pakubwa sana ila hatukuruhusiwa kuzunguka kwa mda wote tuliokaa pale huku tukiwasubiri wadau wetu.
Na maeneo yote tuliopelekwa yalikua ni maeneo ya kawaida niliyoyataja hapo juu wakati nikijaribu kuelezea mazingira ya kambi hiyo,ambayo ni makazi ya watu katikati ya msitu mkubwa huko jimbo la kivu ya kusini nchini DRC.
ITAENDELEA..............!!!!!
 
TUNAVUKA MPAKA NA KUINGIA DRC!!!!!
Basi wenyeji wetu wakatuletea ugali na samaki tukala...baada ya hapo tukafunga funga mabegi yetu madogo ya mgongoni!!
Kumbuka tulikua porini nje kabisa ya mji mdogo wa Miduha......pale tulipokua ni kilimani maana ukishuka kidogo tu unaingia DRC kwenye misitu na mapori kati ya mji wa Bukavu na Uvira uelekeo kuelekea mji wa Kitenge,ambapo ndio starting point ya kuanzia tour yetu ya kutazama fursa.
Sasa wale wadau wetu wakatugongea mlango"""Hey bana tanganyika mko kwa fuasi tuondoke bayemba bayemba"""""
Ndagara akawajibu""""Nzala bayemba bayemba tuko kwa fuasi"""""
Wakatupokea mabegi yetu na tukatoka nje ya nyumba na kushuka chini kilimani mpaka chini kabisa..
Daaaah na msimu wa mvua ulikua ndio umeanza maana niliambiwa kule DRC kwenye misitu mvua inanyesha miezi kumi kwa mwaka mzima sasa sijui ni ukweli ila mimi nilikuta mvua kubwa tu kwa siku zoote nilizokaa misituni kati ya Burundi na DRC.
Waongozaji wetu walikua watu watano....watatu walikua na silaha na wawili walibeba mabegi yetu na mizigo yao.
Wote walivalia kiraia kama sisi na ilikua saa tano kasoro asubuhi ila kulikua na ukungu mkubwa kwa sababu ya mvua.
CHANGAMOTO YA KWANZA:
Pale tu tulipofika kule chini kilimani kabla harujatembea umbali mrefu ili kuingia aridhi ya DRC tulikutana na kundi kubwa la asikari wa jeshi la Burundi wakiwa katika doria ya mpaka wao dhidi ya waasi wa kitusi wa kirundi waliojificha kwenye misitu ua DRC hasa kutokea jimbo la Kivu kusini.
Muongoza msafara akatoa ishara tusimame na kulala chini kwenye majani na tutulie tuli......!!!Wao walikua hawatuoni ila sisi tunawachora tu walipokua wanapita kichakani kwa mstari mmoja ulionyoooka huku wengineo vichwani wakiwa wamebeba masufuria na madumu na silaha na kuni wanaongozana kuelekea destination ya doria yao.Sisi pale chini tumelala tuliiii....mpaka wakapita wote na idadi yao ni kama 150 hivi na ushehe.
Walipopita basi sisi hao tukainuka na kuvukia upande wa DRC na kuendelea na safari yetu.
Kumbuka tunapitia pori kwa pori na hakuna barabara zaidi ya kukata majani ya miti na mapanga na kuvuka mabwawa ya maji yaliyosababishwa na mvua zinazonyesha mwanzo huu wa mwaka.
Baaada ya masaa matatu au manne kutokea pale mpakani tukafika sehemu ya kijiji kinaitwa Punge na wakazi wa pale ni wa kabila moja na wale waongozaji wetu...na hapo ni katikati ya Uvira na Bukavu katika uelekeo wa kuelekea mji wa Kitenge.
CHANGAMOTO YA PILI:
Wakati ndio tumefika nje ya nyumba ambayo ndio tunatakiwa tupumzike pale Punge ghafla tukasikia mlio ya miluzi na wenyeji wetu wakatuchukua haraka kutukimbiza kwenye mashimo yaliyokua katikati ya ua wa ile nyumba na kwa juu wameweka mawe makubwa ya kusagia unga wa mihogo.
Ndani ya yale mashimo ni kama mahandaki kumeifadhiwa magunia ya mihogo mikavu kwenye vichanja vilivyojengewa humo humo shimoni kwa utaalamu wa ngazi kwa ngazi......na yale mashimo ni marefu futi sita kwa tisa kama sikosei hivi....kwa juu ndio wameweka vifuniko vya majani na mawe ya kusagia ili kupata unga wa mihogo.
Nilikuja kujua baadae kua wanafanya vile ili kutunza akiba zao za chakula dhidi ya wezi na waasi na wanajeshi wa vikosi vya serikali ya DRC.
Tukaingia mle ndani haraka sisi wote watu saba.
Ila kuna matundu madogo madogo kwa juu unaweza kuchungulia nje....mara nasikia milio ya magari na viatu vya watu vinakimbia kimbia.....nikainuka kuchungulia na kuona pale juu uwanjani zimepaki landcruser za kijeshi kama tano na wanajeshi wameshuka na kuanza kukagua kagua nyumba za pale kijijini na kuzungumza na wanakijiji afu baadae wakaondoka.
Baada ya mda nikasikia mluzi tena na wakaja watu wakatoa lile jiwe kwa juu,afu wakatuwekea ngazi tukatoka taratibu mpaka nje.
Tukapelekwa mpaka kwenye ile nyumba ya mwanzo tukaingia ndani....tukakaa chini tumechoka kweli na hiyo ilikua mida ya saa kumi kasoro.
Hapo tukapumzika kidogo na tukapatiwa uji wa mihogo afu safari ikaendelea mida ya saa moja jioni.....hapo kila mtu na tochi yake mkononi ila haturuhisiwi kuziwasha mpaka kiongozi wa msafara atoe ruksa....sababu kuwasha taa usiku ni hatari sana hasa msituni.
CHANGAMOTO YA TATU:
Tulipotembea umbali mrefu mpaka saa nne za usiku tukaamua tupumzike katika eneo ambalo ni kambi ya waasi wa KIBANGU BANGU waliyokua wameitelekeza baada ya kushindwa na vikosi vya majeshi ya FARDC na kukimbia.
Kambi yenyewe ni vibanda vilivyovunjika na majani yameota kila mahali maana kambi ilikua imetelekezwa mda mrefu.
Tukachagua vibanda vyenye nafuu kidogo tukajiegesha tujipumzishe.
Mda hata hatujatulia kidogo tukaanza kusikia mlio ya risasi kwa mbali......basi fasta fasta wale waongozaji wetu wakatutoa eneo lile na kuingia pembeni kwenye misitu ile na kutupandisha juu ya miti na rochi zote zikazimwa tukabaki tunaisikilizia ile milio ya risasi.
Milio ile ghafla ikakoma afu kujawa kimya sana na tukaanza kusikia vishindo vya watu wanaokuja kwa kukimbia na kumbe ni Wabangu bangu militia,s wamerudi kuchungulia kambi yao waliyoitelekeza.
Na kiasili Wabangu bangu na Makemba Bunene ni maadui wa jadi kwa sababu wote ni wezi wa madini na wanatafuta kumiliki maeneo na kuisumbua serikali ya DRC.
Mara zikaanza risasi kulia kuja ule upande wetu ila zinapita kwa chini....ni usiku unaona cheche na kusikia matawi ya miti mifupi inakatika tu....kwa mda wa dakika tatu afu kukawa kimya kwa mda wa nusu saa......mara ukasikika mluzi tena na vishindo vya watu kuondoka eneo la kambi ile kwa kukimbia na kuimba nyimbo zao....kumbuka sisi tupo pale juu ya miti tunasikilizia.
Baadae wale waongozaji wetu wakatuambia huenda wale wabangu bangu walipata taarifa kua kambi yao imevamiwa tena na wanajeshi wa serikali wa FARDC kutoka Bukavu au Uvira au waasi wa kinyarwanda na....ndio maana wakaja kuwaharibia ila walipofika wakakuta kambi ni tupu ndio maana wakaondoka.....na waliowapa taarifa ni watu wao MBILIKIMO WA MSITUNI ambao walitufananisha na wanajeshi wa FARDC au waasi wa kinyarwanda.
Tulishuka pale juu ya miti taratibu na tukaendelea na safari yetu mpaka usiku wa manane ndio tukafika kijini kilichochangamka kiitwacha Zendi au Zendika sikumbuki vizuri na hapo ni eneo rafiki kwa waongozaji wetu,,,,tukapata nyumba ya nyasi ya kupumzika ambayo ndani yake mlikua ni kama ghala la vifaa ila tukatandika chini matandiko tukalala tumechoka balaa maana tumetembea masaa manne au matano bilia kupumzika afu ni usiku wenye baridi balaa.
Ili asubuhi tukiamka tuendelee kuitafuta KITENGE ambayo ndio starting point yetu ya kutazama fursa.
CHANGAMOTO YA NNE:
Mda wa alfajiri nikashitushwa na Ndagara aliesema dogo vaa vizuri tuondoke maana huku usijiachie kama nyumbani Tz.Fasta nikaweka vitu vyangu sawa na kutoka nje ya ile nyumba tuliyofikia.
Kumbe bhana kijiji kizima wana Zendi ni masoja na hakuna akina mama wala watoto bali wazee wa kazi....na kile kijiji ni kambi yao isiyo rasmi....afu wake na watoto wao wanawaficha porini au kwenye miji mikubwa mikubwa especially kwenye mji wa KITENGE.
Na taarifa zetu zoote walikua nazo kutuelezea sisi ni kama wadau ambao tunaweza kuwatafutia masoko ya uhakika ya kuuzia mawe yao nchini Kenya na Tanzania.
Basi wakaongea kibangu bangu pale na bro Ndagara afu tukapewa makoti ya kuzuia mvua.....tukaanza safari ile alifajiri pori kwa pori....kuutafuta mji wa KITENGE....!!
DRC bhana hakuna barabara za uhakika hasa kipindi cha mvua na hakuna usalama kabisa maeneo ya mashariki...maana ilikua tukitembea mara tusimame tuchunguze uelekeo....mara tujifiche wakija watu karibu yetu.
Kwahiyo mwendo wetu ulikua wa pole pole pori kwa pori afu mvua inanyesha na inakata.
CHANGAMOTO YA TANO:
Humo njiani tukielekea mji wa KITENGE tulifika sehemu ya milimani hivi,kuna uwanda mkubwa wa majani majani.Tulikuta vita kati ya waasi wa vikundi vidogo vidogo vya waasi walikua wamedhulimiana madini.
Ikabidi tutulie huku juu ya kilima huku wale waongozaji wetu wakitafuta njia salama ya kupita chini ya vile vilima.
Tatizo la waasi wanapigana kama watoto....mara wanakimbizana...mara wanasimama na kutukanana...mara wanaimbaimba na kukata mauno....mara wavute bangi....mara wapige risasi hewani......Basi ilikua tafarani......ilibidi tutulie kule juu ya kilima masaa matatu afu ndio tuangalie utaratibu wa kushuka chini ya vile vilima ili tuendelee mbele uelekeo wa mji wa KITENGE.
Hiyo ilikua inaelekea adhuhuri na tulikua hatujapumzika toka asubuhi ila kwa sababu ya mvua hakukua na jua kali mpaka mda huo.
ITAENDELEA.........!!!!!!!
Anko umenikumbusha mbali sana hivi wale kabila fulani hivi jina nimesahau,
Wakienda battle wanakata mauno balaa na vigoma vyao na firimbi kisha ndio wanalianzisha unawafahamu?
 
INAENDELEA......!!!!
Wakati tupo pale kambini kwa wale watu wa FDLR kuna vitu vilikua vinaendelea ambavyo vilikua vinatupa wasiwasi.......
Mfano kuna nyakati usiku tulikua tunasikia movement za watu ambao ni kama walikua wanahamisha vitu vizito hivi.Na hizi movement zilikua zinaweza kuchukua hata masaa matatu mpaka manne hivi.
Ni kama watu walikua wanahamisha vitu vizito hivi kuvipeleka msituni.
Nilikuja kujua baadae kua hizo zilikia ni movement za asikari wa waasi,waliokua wanaamisha silaha zao nzito nzito kukwepa zisiharibiwe na mizinga ya adui......kama kutatokea mashambulizi ya ghafla!!!!
Vile vile kitu kingine kilichokua kinanitia wasiwasi.....ni wale asikari waliokua pale kambini kulinda doria....kuanza tabia ya kutuelekeza namna ya kufungua na kufunga bastola....na namna ya kulenga shabaha kwa kutumia bastola.
Utawasikia wakisema""""BASWAHILI BASWAHILI MKUJE PETII TUBAONYESHE KUPIYA MASASI.
BASWAHILI BASWAHILI MKUYE MUONE TUNAVYOSUGUSA KAKOTII......!!!!Kakotii maana yake bastola.
Nikawa nawaza hawa jamaa labda wanatufundisja ili kama kikiwaka tuweze kujitetea.
Au walikua wanatufundisha kama tuwaone wajanja zaidi yetu.
Mpaka wanamaliza kunifundisha tayari nilikua nimeshasahau hiyo KAKOTII inafunguliwa na kufungwaje 🤣🤣🤣🤣
Cha ajabu jamaa walikua hawafugi ngombe wa maziwa wala wa nyama.
Nyama wanakula wanyama pori na maziwa hakuna kabisa......ila mboga mboga za majani na vitu vidogo vidogo.....wanalimalima mule mule kambini,na hali ya hewa ni mvua mvua na baridi kali hasa nyakati za jioni
******************************
RATIBA YAO YA CHAKULA
1:ASUBUHI.....Uji na magimbi au viazi na nyama choma ya pori
2:MCHANA.........Ugali wa dona na nyama pori za kuchomwa au samaki wakavu na kisamvu au maharagwe
3:USIKU............Chakula Kama cha mchana hakuna tofautina sikuwahi kula wali kule porini.
4:Mda wote matunda pori yapo ya kumwaga.....maana humo msituni yanaota maparachichi pori na matikiti pori na machungwa pori na matunda ya kawaida pia yapo yanaparikana yanauzwa kambini.......vile vile hakuna uhaba wa maji ya kunywa na kuoga,sababu kuna vijito vingi mno na mabwawa yanayotiririsha maji.
*************************
KULALA KAMBINI
Tulikua tunalala ndani ya hema.......afu choo kipo mbali kidogo....ila kuoga mnaoga porini tu sehemu ya wazi hakuna shida.Na sehemu tuliyokuepo ni juu kidogo kilimani ambapo ni karibu na makazi ya KANALI NIKAMBONYIERA.Sisi tulikua tunalala kwenye hema ambalo limezungushiwa fensi ya ukuta wa miti na nyasi.
Afu kule msituni ikifika saa moja tu kila kitu kinakua kimya zinabaki tu sauti za ndege na popo na wanyama wadogo wadogo tu.
*********************************
MAISHA YA WANAKAMBI
Mle kambini ni marufuku kua na simu kwa wakazi wote wa mule na hilo wameshazoea maana maisha yakikua yanaendelea kama kawaida.
Watoto wanacheza.......vilabu vya pombe vinafunguliwa.......masoko yapo wazi.........mabucha yapo wazi..........sehemu za ibada hasa makanisa ya kipentekoste yapo wazi.Na shughuli nyingine zinaendelea kama kawaida kwenye maisha yao ya kila siku ukimbizini........maana asilimia kubwa ya wale wakazi wa ile kambi,wamezaliwa ukimbizini DRC.....ni mazalia ya wale wahutu waliokimbia vita vya kimbari kule Rwanda 1994.
Baada ya kupumzika kwa takribani siku mbili.......basi mimi na ndugu yangu Ndagara tukaanza mikakati yetu ya kiujasiriamali.
MIMI :Bro unadhani hawa jamaa zetu watarudi mapema kuja hapa walipotuacha.
NDAGARA :Sina hakika ila tusubiri tuone jinsi itakavyokua.......na ni bora hata wachelewe kuja,ila wakija waje na mizigo ya kutosha.
MIMI :Bro unajua mimi nina mashaka na usalama wa hii kambi.......je vikosi vya kulinda amani ya SADC vikianza kurusha makombora na mizinga mpaka huku tutafanyaje....kumbuka haviitambui FDLR kama kundi rafiki.
NDAGARA :Acha uoga dogo maisha hayapo hivyo""komaaa"""
Basi mjadala wetu ukakomea hapo na tukaendelea kuvuta kimya na kutulia huku tukiwasubiria wenyeji wetu.
Mule kambini tulipata marafiki wengi,hasa akina mama na watoto......na tulikua kila tunapoenda watu wanatupokea kwa ukarimu mkubwa sana na upendo......hasa hasa wakijua sisi ni watanzania na ni wafanyabiashara wa kawaida na sio wanajeshi au waasi.
******Nilikuja kujua baadae kua kisa cha kutupenda watanzania kinatokana na ambavyo jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ) linatoa kichapo heavy kwa mahasimu wao......nazungumzia M23 na Banyamulenge na washirika wao
Baada ya siku kama tano hivi tukiwa mule kambini,basi tukaitwa na yule mkuu wao wa kambi KANALI NIKAMBONYIERA na safari hii alikua hajalewa pombe kabisa na hivyo tukafanya mazungumzo serious.
KIKAO CHETU :
Mada kubwa ilikua ni kama kweli sisi tuna uwezo wa kuuza madini ambayo wao wanayachimba.
Na pia kama tuna uwezo wa kuwapatia connection za wao kununua vifaa vya kijeshi na silaha.
Walitaka kujua kama sisi ni wanasiasa au tuna ushawishi kwa viongozi wa serikali za nchi zetu????
Walitaka kujua uwezo wetu kifedha pia
Na kubwa pia walitaka kujua sisi tuna mahusiano gani na wana BUNENE zaidi ya kuuziana madini ya almasi na dhahabu.
Walitaka kujihakikishia pia sisi sio wapelelezi wa maadui zao.
Pia walitaka tuwasaidie kuwatafsiria kwa kiswahili baadhi ya document zao zilizokua zimeandikwa kwa kingereza.
Pia walitaka tu kujenga urafiki na mazoea nao ili siku wakija kwetu,tuwasaidie hata kama ni kwa vitu vidogo vidogo,kama raia na sio wanajeshi.
Kwa kifupi Kanali NIKAMBONYIERA alikua mtu poa sana na kiukweli pale kambini tuliiishi kama tupo likizo ya utalii vile.
Ila pia tulizungumza mambo mengine pia kuhusu maisha na jinsi gani dunia inavyokwenda nje ya siasa,ukabila na vita na mizozo.
Yalikua ni maongezi ambayo almost yalichukua maasaa matatu na baada ya hapo tukaruhusiwa tuendelee na ratiba zetu za kawaida za kila siku.
Ratiba zenyewe ilikua kula na kuzunguka na kusubiri wenyeji wetu.
Ila kwa Ndagara yeye ilikua ni fursa ya kunywa pombe za kienyeji kila alipokua anapata nafasi.
Mda wote tuliokua pale kambini tuliishi vizuri sana na wenyeji wetu,wale skina mama na vijana na marafiki zetu wakubwa walikua watoto wadogo.
Bahati mbaya tu ile kambi ilikosa shule ya msingi na ndio kasoro kubwa.......niliyoiona ambapo wale watoto walikosa nafasi za kwenda darasani,sababu walikua porini mno na hakuna miji ya karibu karibu.
**********************
DAR ES SALAAM TANZANIA
Kumbe wakati sisi tumeondoka mimi na mwanangu Ndagara.....ila kila mmoja njia yake na tukakutania mjini Kigoma.
Huku nyuma maskani story zikaenea kua mimi nimeenda kupigana vita Ukraine.
Story zikawa kubwa mno kua nimeenda kua mamluki huko Ukraine.
Bas maskani nzima wakapagawa na wengine kuitamani hiyo fursa pia.Sasa wakinicheki kwenye social network,s nipo offline na kwenye njia kuu za mawasiliano sipatikani......Bas wakaamini kua dogo janja KAJILIPUA KAENDA UKRAINE sababu kapata dili tamu la hela.
Lakini walipokuja kuambiwa nilionekana napanga mikakati na yule bro mrundi Ndagara basi wakawa wanacheka na kusema dogo janja anaenda kumuingiza chaka mrundi wa watu huko Ukraine nipige hela
Basi story zikawa nyingi maskani kkoo,dogo janja kaenda ukraine,kaenda ukraine.
Ila wadau wengine wakawaambia tumemuona dogo akienda kahama kwa akina Patel na hajapanda ndege kuelekea Ukraine.
*******************
MIDUHA BURUNDI
Pale Miduha kumbe wenyeji wetu na ndugu zake Ndagara walikua wanasikilizia,kua hawa majamaa wakichelewa kurudi basi tutatuma watu kuwafuatilia na kujua hali zao.Maana pale Miduha tuliacha vitu vyetu na isitoshe hata Burundi tuliingia bila vibali na DRC tuliingia bika vibali,lengo likiwa ni kufanya mambo yetu kimya kimya na kurudi kimya kimya.Sababu mara nyingi kufuatilia na kujua biashara za magendo hakuhitaji mbwembwe mbwembwe na kugonga gonga mapasipoti.
Kwahiyo kumbe jamaa zetu wa pale Miduha walitaka kujua maendeleo yetu na kama tumefanikiwa kufika mjini......KITENGE....maaana hali ya usalama jimbo la kivu ya kusini sio ya kuaminika saana mda wote.
Wakati wao wana wasiwasi na sisi,kumbe sisi hatuna hata wasiwasi bali tunapambania mikakati yetu.
NDAGARA : Dogo hawa watu kama wakichelewa sana itatubidi,tuangalie utaratibu mwingine.Namaanisha wa sisi kurudi Miduha afu wao wenyewe ndio watatuletea mizigo tuikague.....nikiridhia ndio nitawasiliana na connection zangu za Nairobi.
Maana ilikua siku ya tano sasa na nikaona kama ndugu yangu NDAGARA uvumilivu unaaanza kumshinda sasa......maana aliniambia kua tatizo la DRC hakuchelewi kunuka....hivyo chelewa chelewa utakuta mwana sio wako wakati mwingine.
ITAENDELEA.............!!!!
 
Back
Top Bottom