Mabraza wa enzi hizo Dar kumbukumbu zangu

Nelson Jacob Kagame

JF-Expert Member
Dec 26, 2022
9,473
12,863
Kwanza kabla ya kuanza story...nitoe big up kwa IBRAH THE HUSTLER wa ukoo flan Mau Mau. Moja ya mabroo wenye roho nzuri sana..nje ya maisha ya mziki. Nitoe big up pia kwa home boi mwenye roho ya kipekee our lil homiez LANGA we cant forget you lil brother, its very sad you pass away mapema mno and very young. NAVIO anazo story nzuri kukuhusu little homie

Sasa tuendelee wadau. Miaka ya mid 80,s na 90,s na 2000,s tulibahatika kukutana na mabraza wenye roho nzuri waliotufungulia njia madogo.

Wakongwe wanakumbuka miaka ile tunatoka muhimbili tukifika pale tambaza wale mabraza wanatusimamisha na kutusia madogo tusome kwa bidii ili tufaulu mitihani ya darasa la saba.

Tambaza ndio kulikua na mabishoo wote wa kupiga pamba kalikali.....role model wetu wale mabraza waliokua wanarap kingereza wa enzi hizo nyimbo kumkopi MC HAMMER kabla ya DIPLOMAT🤣🤣🤣😂😂

Tukipita pale Aza boi, mabraza halafu masela kichizi wakiongozwa na braza aliekua anajiita JESHI....mchizi alikua anatokea block 41 kama sikosei kumbukumbu zangu za enzi hizo.

Wanatusimamisha na kuanza kutuuliza vipi masomo yanaendaje na tukifanikiwa kufaulu basi watafurahi kichizi maana sisi ni madogo janja tunaonekana tuna akili sana za darasani. Big up braza JESHI popote ulipo its been longtime.

Turudi kwenye mada wakurungwa...
Katika maisha miaka hiyo ya mid 80,s na 90,s na 2000,s.

Mabrother walikuwa na moyo wa kusaidia madogo na sisi tusutue...
Nawakumbuka wana kama.
MODO MKIA.
SHAGGY SLAY.
MPEMBA.
KOMANDO KIPENSI.
MAUZAUZA.
SHOKISHUGI.
MEDDY NYANGEMA.
BROTHER PEPE.
MWARABU KOKO.
ORIJINO YG.
MSELA MSEKWA.
CHIFU RUMANYIKA.
ZAYEED.
HUSSEIN BONGE

Hawa mabraza walikua na roho nzuri za kusaidia madogo tutoke...na machizi hatukusoma nao ila tulikutana nao ukubwani.

Mabraza wa dar walikua na ushirikiano kichizi mpaka hela ya passport wanakuchangia na ukikwama ughaibuni wanakupa ramani za kutokea.

NB: MABRAZA WA ARUSHA WALIKUA WABNAFSI HATA TULIPOKUTANA NAO UGHAIBUNI WALIKUA WANAFEKI LOVE KWA KUTUSAGIA WATOTO WA DAR NA SISI MADOGO TULIWACHUKULIA MAFEKI NIGGA UMAREKANI MWINGI AFU WANAFEKI LOVE. ILA PANDE ZETU ZA UGHAIBUNI WATU WA ARUSHA WALIKUA HAWAFIKI MAANA WATOTO WA UPTOWN DSM NAZUNGIMZIA KKOO NA TMK NA ILALA NA KINONDONI WALIKUA NA DILI NGUMU NA WANAENDA PANDE NGUMU ZA DUNIA....MFANO WAKATI MOGADISHU NA BEIRUT NA SANAA KUMECHAFUKA MADOGO JANJA KIBAO WALIKUA WANAKATIZA PANDE HIZO KWA SAFARI ZA MASHARIKI YA MBALI.

BEIRUT NDIO KILIKUA KIWANJA CHA NYUMBANI WATOTO WA DAR KIBAO HUKU NJE YA MJI VITA VINAENDELEA.
ILA UTASHANGAA NIMEMPA HAI IBRA THA HUSTLA.NI KWA SABABU HOMIEZ ANA ROHO NYEUPE SANA NJE YA MAISHA YA MZIKI.

NA ATAKUA AMERITHI TABIA ZA MABRAZA WOOTE WA UKOO FLANI MAU MAU KWA UPENDO WALIOTUONYESHA MADOGO JANJA HUKO UGHAIBUNI ENZI HIZO...90,S NA 2000,S.

BIG UP KWA IBRA THA HUSTLA NA WANAFAMILIA WOTE WA UKOO FLAN MAU MAU.

Turudi kwenye mada pale kkoo mitaa flan ya kidongo chekundu ilikua kama ni kilinge cha watoto wa mjini wenye ndoto kubwa kukutana. Mabraza wote waliokua wamerudi kutoka ughaibuni utawakuta pale kilingeni na kule juu posta ya zamani.

Mabraza walikua hawakunji wanakupa details zote kuhusu mitikasi iwe halali au haramu.

Ngoja niwazungumzie mabrother wachache.

MODO MKIA: Huyu brother alikua hakunji toka early 90,s anagawa ramani kwa wakulungwa na sisi tujitafute na maisha...Msela hakua na ubaguzi na ni braza tu wa kitaani ila kawapa wana michongo mingi na wengine aliwapiga tafu kielimu kuhusu ada...za elimu ya juu.

Siku zote alikua anasema kua watoto wa mjini tunajuana kwa vilemba. Ukitoka na wewe mtoe mwenzio watoto wa mjini hatukunjiani.

Braza alikua anatupa somo jinsi gani tucheze fair gemu sababu maisha ya jela udwanzi.

KOMANDO KIPENSI:
Huyu braza yeye alikua anadili na dili nyeusi ila braza wa ukweli katika kutoa ramani....baada ya kutoka italy akarudi tz kutulia ila ndio mzee wa dili zote nyeusi.

Alikua na love kwa madogo hakupi dili nyeusi za kukupoteza...alikua na msemo mmoja kua""Nguruwe sio haramu""..

Akimaanisha kua dili yoyote inapigwa kibaya kufeli.......mwana alikua hakunji na alitoa ramani kwenye vijiwe vya uptown kkoo madogo tujitafute.

SHOKISHUGI:
Braza alikua anatoa maujanja ya kuishi bila vibali ughaibuni...wapi pa kutokea na wapi pa kuingilia. Enzi hizo hakuna EU ukifika Athens ni vurugu tupu, sasa braza Shokishugi alikua tunakaa chini anatupa darasa jinsi gani tutaishi kimagumashi ughaibuni.

Braza alikua na ugomvi mmoja tu,,,,pale anapogundua hatuendi shule na harakati zote za kusafiri alituambia tutazianza baada ya kumaliza shule.

Lakini bro katuuzisha sana weed kitaa na sisi kwa love tulimsukumizia mazaga yake.

NYANGEMA:
Huyu alikua braza sailor asiye na vibali yaani mzamiaji.

Braza alikua anatutajia meli zote na kampuni miliki...na ruti zote alikua anatupa na jinsi ya kukwepa bandari tata na meli tata alikua anatoa somo na anafundisha kuogelea pia.
Braza alikuwa na love kwa madogo wa kitaa akitaka na sisi tujitafute ughaibuni.

MAUZAUZA:
Huyu bro alikua bingwa wa ndumba mzee wa kutupeleka engo zote za vilinge vya waataalamu wa nyota ili madogo tukizamia ughaibuni tusionwe na wenye roho mbaya.

Na tukifika kule ughaibuni tuwakaange wazungu ile mbaya ili dili zetu ziende...
Braza alikua na dawa ya kufungua kufuli za jela, anakuuzia ila anasema sharti ukaitumie nje ya bongo..🤣🤣😂😂
Braza alikuwa anatupa darasa kuhusu uchawi wa kizungu na jinsi ya kuutegua🤣🤣🤣.

MPEMBA:
Huyu bro pamoja na love alikuwa anatupa maujanja ya kupata mademu wa kizungu tuzae nao ili tupate uraia wa ughaibuni..Alikua anatupa darasa wazungu wanapenda nini na hawapendi nini...pia anatoa darasa kuhusu tabia za wajapani madogo tujiongeze.

SHAGGY SLAY:
Huyu alikua mshua mpanga mipango mingi mingi na alikua hakunji. Akitoka Yemen na mazagazaga kibao tunakutana kkoo anatuchorea ramani madogo tunafaidika.

Alikua anatusisitiza sana kuhusu elimu na alikua mkali sana tukizembea kusoma.

MABRAZA WOTE HAWA TULIKUTANA NAO KITAANI NA WALIKUA NA ROHO NZURI SANA HAWAKUNJI. NA DAR ENZI HIZO ILIKUA YA UJAMAA SANA....MABRAZA HAWAKUA NA PESA NYINGI ILA WALIKUA WATAFUTAJI NA WACHORA RAMANI WAZURI WA MITIKASI AFU HAWAKUNJII MADOGO JANJA MICHONGO.

MABRAZA TUNAWAKUMBUKA SANA KWA UPENDO ROHO NZURI NA KUTUVUMILIA MADOGO MAANA TULIKUA WASUMBUFU SANA AFU MUCH KNOW USOMI MWINGI 🤣🤣🤣😂.

Siku hizi dar imebadilika mabrother hawawapi tena ramani madogo.Na madogo wamekua masnichi sana hawachelewi kuunguza ramani za mitikasi.

Na kizazi cha sasa hv hapa dar,,madogo wazembe na wanapenda kulalamika badala ya kutafuta fursa..
Sisi tumepambana enzi za uchumi wa kufunga mikanda na hatukulalamika bali tulitafuta fursa katika hali tete..
Kupitia upendo wa mabraza ..
Wapo waliofanikiwa ughaibuni.
Wapo walioishia jela..
Wapo walioa ughaibuni.
Wapo waliopata ufadhili wa masomo.
Na sote tulijifunza kutoa ni moyo na sio utajiri.

NB: NYAKATI WAGA HAZIRUDI ILA TUNAWAKUMBUKA SANA WASHUA NA MABRAZA WA UPTOWN ENZI HIZO...!!!!!!
CODE ZIMEZINGATIWA.
 
Bishoo kim 😂🤣🤣🤣 na panki lake lililonyooka...Duuuh kitambo
Kim alikuwa mtu poa sana.

Alituunganisha vijana wa mjini wote kwenye mashindano ya ku rap. Basi ukimfuata kwake pale town anytime yuko mtu poa sana.

Hao vijana wa Tambaza waliokuwa wanarap enzi za MC Hammer kabla ya Diplomatz ndio sisi ila hatutaki kujulikana tu hapa.
 
Kim alikuwa mtu poa sana.

Alituunganisha vijana wa mjini wote kwenye mashindano ya ku rap. Basi ukimfuata kwake pale town anytime yuko mtu poa sana.

Hao vijana wa Tambaza waliokuwa wanarap enzi za MC Hammer kabla ya Diplomatz ndio sisi ila hatutaki kujulikana tu hapa.
Aaaaah bro kama ni nyie mlikua mnatuinspire madogo janja.....na raba zenu mtoni...
Afu mnatusisitiza tusome ili tuwe kama nyinyi...
Kama ni wewe big bro,,,bas nitakukumbuka tu...
 
Aaaaah bro kama ni nyie mlikua mnatuinspire madogo janja.....na raba zenu mtoni...
Afu mnatusisitiza tusome ili tuwe kama nyinyi...
Kama ni wewe big bro,,,bas nitakukumbuka tu...
Halafu mimi watoto wa Muhimbili nilikuwa nao poa sana kwa sababu mwenyewe nimetoka Muhimbili nikawa na ndoto za kwenda Tambaza, nikatimiza ndoto zangu vile vile nilivyotaka.

Kwa jivyo nilikuwa nawaambia mnaweza kutoka Muhimbili mkaja Tambaza kama mimi.
 
Kim alikuwa mtu poa sana.

Alituunganisha vijana wa mjini wote kwenye mashindano ya ku rap. Basi ukimfuata kwake pale town anytime yuko mtu poa sana.

Hao vijana wa Tambaza waliokuwa wanarap enzi za MC Hammer kabla ya Diplomatz ndio sisi ila hatutaki kujulikana tu hapa.
Bro mlikua watu poa sana kwa madogo.....mnatufundisha maisha na elimu pia.....nyinyi mnavuta vitu ila sisi mwiko kuvuta tukiwa maskani...
Mabraza mlikua mnafanya kopi za MC HAMMER mpaka mavazi.....Afu braza KIM na zile nguo zake bwanga za vitenge 😂🤣🤣🤣🤣 YO RAP BONAZA ZA ENZI HIZO
 
Back
Top Bottom