Enzi hiyo Sugu ndiyo anaingia mjini kakaribishwa na "Dar Young Mob".
Nakumbuka kuna siku nimekaa maskani Tambaza na Yusuf "Y-Thang" wa Kwanza Unit , alikuwa na kitabu cha Ben Carson kinaitwa "Gifted Hands".
Nikamuuliza, huyu Ben Carson ni nani? Akaniambia huyu ni daktari mmoja, surgeon bingwa Mmarekani mweusi, amekulia ghetto kapanda juu mpaka kawa daktati bingwa hospitali maarufu ya Johns Hopkins ya Baltimore Maryland.
Y-Thang hapo yuko A- Level anasoma PCB Tambaza, lakini anasoma mpaka nje ya box, ananiambia anataka kuwa daktari wa magonjwa ya wanawake.
Yani tangu zamani masela wanakaa maskani wanaongea vitu vya kulenga career goals, kusoma, na vitu kama hivyo.
View attachment 2856069