Mkulima na Mfugaji
JF-Expert Member
- Jul 26, 2013
- 1,013
- 1,634
Naomba nitoe ushuhuda wangu niliofanyiwa na mtu wangu wa karibu
Huyu kijana tulikua pamoja katika harakati za utafutaji
Nakumbuka mimi nilikua ni miongoni mwa watu tuliokua tunamiliki magheto vijijini yale magheto ya vijijini
Huyu kijana nilikua nalala nae kwenye Ghetto langu kwani tulikua tumeshibana sana
Baada ya harakati za shule na vyuo na ajira kuwa na changamoto mimi nikasalia kijijini mwenzangu alipata kazi mjini
Ila katika kuhangaika kuna jamaa aliniunganisha kwenye kampuni moja ya kilimo na mifugo ambao iko Dar
Ile kampuni ikataka nipeleke vyeti vyangu physical na wanione
Aisee jamaa wakwanza kumjulisha alikua ni yule jamaa yangu alietoka kijijini kwetu kwamba wiki ijayo nakuja kuna mchongo nafatilia naomba unipe hifadhi ya siku mbili tu hapo kwako,kwani nilijua jamaa ana Gheto na hakua na mke
Jamaa alionyesha kufurahi na kunihakikishia sehemu ya kulala ipo na hata kula ni juu yake hata nikikaa mwezi
Mimi nikamwambia wala kuhusu chakula asihofu nimejipanga kwa hizo siku mbili na mimi dar nitakaa siku mbili tu shida yangu ni sehemu ya kulala tu kwani bajeti yangu ni ndogo
Siku ya safari inafika jamaa namwambia kesho ndio ile safari jamaa akanitoa hofu na kusema hataenda kazini ili aje anipokee
Aisee huwezi amini kuanzia kibaha napiga simu hazipokelewi na message hazijibiwi
Nilichanganyikiwa mpaka abiria niliekaa nae jirani akaniuliza kwani una nini mwanangu alikua ni mama mtu mzima ikabidi nimuelezee mwanzo mpaka mwisho
Mimi nilikua natoka Tanga ila huyu mama alipandia gari segera ila ni mtu wa Arusha
Yule mama alichonambia kama asipopokea simu Twende nyumbani kwangu akipatikana atakuja kukuchukua
Huwezi amini mpaka naingia Ubungo simu ilikua haijibiwi
Yule mama nilenda nae kwake akanitambulisha kwa familia yake
Mpaka usiku jamaa nampigia simu hola ikabidi nikae kwa yule Mama mpaka nimalize shughuli zangu nikarudi kijijini nikiwa na hasira na jamaa
Narudi kijijini nakuta habari zimezagaa kwamba nilienda kuomba kukaa kwa jamaa na ndugu zake ndio walikua wanasambaza hivyo
Nilichoka
Huyu kijana tulikua pamoja katika harakati za utafutaji
Nakumbuka mimi nilikua ni miongoni mwa watu tuliokua tunamiliki magheto vijijini yale magheto ya vijijini
Huyu kijana nilikua nalala nae kwenye Ghetto langu kwani tulikua tumeshibana sana
Baada ya harakati za shule na vyuo na ajira kuwa na changamoto mimi nikasalia kijijini mwenzangu alipata kazi mjini
Ila katika kuhangaika kuna jamaa aliniunganisha kwenye kampuni moja ya kilimo na mifugo ambao iko Dar
Ile kampuni ikataka nipeleke vyeti vyangu physical na wanione
Aisee jamaa wakwanza kumjulisha alikua ni yule jamaa yangu alietoka kijijini kwetu kwamba wiki ijayo nakuja kuna mchongo nafatilia naomba unipe hifadhi ya siku mbili tu hapo kwako,kwani nilijua jamaa ana Gheto na hakua na mke
Jamaa alionyesha kufurahi na kunihakikishia sehemu ya kulala ipo na hata kula ni juu yake hata nikikaa mwezi
Mimi nikamwambia wala kuhusu chakula asihofu nimejipanga kwa hizo siku mbili na mimi dar nitakaa siku mbili tu shida yangu ni sehemu ya kulala tu kwani bajeti yangu ni ndogo
Siku ya safari inafika jamaa namwambia kesho ndio ile safari jamaa akanitoa hofu na kusema hataenda kazini ili aje anipokee
Aisee huwezi amini kuanzia kibaha napiga simu hazipokelewi na message hazijibiwi
Nilichanganyikiwa mpaka abiria niliekaa nae jirani akaniuliza kwani una nini mwanangu alikua ni mama mtu mzima ikabidi nimuelezee mwanzo mpaka mwisho
Mimi nilikua natoka Tanga ila huyu mama alipandia gari segera ila ni mtu wa Arusha
Yule mama alichonambia kama asipopokea simu Twende nyumbani kwangu akipatikana atakuja kukuchukua
Huwezi amini mpaka naingia Ubungo simu ilikua haijibiwi
Yule mama nilenda nae kwake akanitambulisha kwa familia yake
Mpaka usiku jamaa nampigia simu hola ikabidi nikae kwa yule Mama mpaka nimalize shughuli zangu nikarudi kijijini nikiwa na hasira na jamaa
Narudi kijijini nakuta habari zimezagaa kwamba nilienda kuomba kukaa kwa jamaa na ndugu zake ndio walikua wanasambaza hivyo
Nilichoka