Mabomu ya Machozi yatumika kuwasambazi wananchi pamoja na Wanafunzi Mjini Dodoma

muhosni

JF-Expert Member
Feb 12, 2011
1,108
152
Ni kuhusu kuhudhuria public hearing ya mswaada wa katiba

Wanaharakati wafunga barabara na kuendesha public hearing kuhusu mswada wa kuandika katiba mpya baada ya kukataliwa kuingia ukumbi wa msekwa

Bunge baadaye latangaza kwamba public hearing kundi la pili litaingia ukumbi wa msekwa leo saa tisa kutoa fursa kwa waliokosa nafasi asubuhi

Bunge latangaza kwamba Public hearing sasa itafanyika siku tatu mfululizo ukumbi wa Msekwa

Vyombo vya habari vyashindwa kurusha matangazo live kutoka Dodoma

Wanafunzi wamewazomea Chenge na Lukuvi na kuwaita mafisadi, haikuchukua muda wakaja FFU na kuanza kutembeza mabomu ya machozi

Baada ya kupigwa mabomu Wanaharakati, Wananchi, na Wanafunzi wamehamia Nyerere Square kuendelea na "Citizen Public Hearing"

Maoni yangu:
Serikali imewakosea wananchi waliotumia muda na gharama zao kufika dodoma na kuwakataza wasiingie ukumbini. Katazo halikuwa la kistaarabu bali ubabe na amri kama vile wananchi hao walikuwa wafungwa. Ilikuwa ni jukumu la serikali kuhakikisha inawapatia wananchi hao ukumbi mbadala kwa haraka na kuwabembeleza na kuwapeleka huko kwenye ukumbi mbadala. Serikali haikutenda haki kuwapiga mabomu.

Ni kama kusema kwamba serikali haikutaka maoni ya wananchi bali wananchi ndio wanaolazimisha kutoa maoni yao! Hii inatia shaka kama maoni ya wananchi kweli yatafanyiwa kazi, au ni kutimiza tu mchakato kwamba kabla ya sheria kupitishwa maoni ya wananchi yalikusanywa, bila kujali kama yaliingizwa kwenye mswada.
 
Madai ni kwamba watu ni wengi nafasi ndani haitoshi
 
Nipo hapa Dodoma, kuna watu kibao mlangoni wanaimba na kushangilia, hiyo public hearing inabagua watu, wanataka waingie watu wenye mawzo mgando tu sio watu wenye mawazo bora na wenye malengo mema kwa taifa letu.
 
Waacheni tu, wananchi walishasema aina ya mchakato unaotakiwa kufuatwa sasa kama wao hawtaki wafanye wanavyotaka na baada ya mkutano huu wananchi wataamua kinachotakiwa kufanyika, katiba sio mali ya CCM. sasa mchakato wanafanya kwa upendeleo kwa nini wasi wa ruhusu wananchi wakatoa maoni yao? huo ni uwizi
 
Aliozuiliwa kuingia bungeni wameamua kulala barabarani kuzuia magari yasipite. Wengi ni wanafunzi wa UDOM
 
Ni kuhusu kuhudhuria public hearing ya mswaada wa katiba

askari wa dizaini hiyo huwa nawafananisha na mbwa!! wanakubali kila kitu wanachoambiowa na mafisadi ili mradi tu wamepigiwa miluzi.

askari kama huyo ukienda kwenye nyumba anapoishi (kota) utakuta sebule imegawanywa mara mbili kwa kipande cha shuka: upande mmoja wanakaa wageni, upande mweingine analala binti yake. asubuhi akiwa anakwenda kukoga lazima apite alipolala binti yake huku amevaa kitaulo cha machinga ambacho hakikaushi maji.
 
Wameanza kujadili muswada wakiwa wamekaa barabarani. Waliokuwa wameruhusiwa kuingia bungeni sasa wako kwenye uzio wa bunge wanafuatilia public hearing inayoendelea barabarani!
 
huo ukumbi wa pius msekwa una uwezo mkubwa kiasi gani? hiyo kamati haikuweza kukisia tangu awali kuwa muitikio wa wananchi unaweza kuwa mkubwa na hivyo kuchagua mahali ambapo panaweza kukusanya watu wengi zaidi au walifanya makusudi?
inasikitisha sana!
 
Hizi tv za tz bomu kweli kweli. Wamejazana hapa na makamera yao muda mrefu lakini hakuna live coverage. Hata Star tv ambao wanatangaza live kutoka Dodoma hawaoneshi yanayojiri ukumbi wa bunge ambayo ni historia kubwa sana. Wananchi wameamua kufanya public hearing yao nje ya bunge barabarani baada ya kuzuiwa kuingia ndani
 
Demokrasia ina gharama zake!..................mimi jile nasema "ni kazi sana kutenda haki ukilinganisha na kutotenda haki, ni rahisi sana kutotenda haki na ukahalaisha kutotenda haki kuwa ndiyo haki iliyokuwa inatakiwa kutendwa"................
 
kwanini hawajatumia ukumbi wa CHIMWAGA UDOM na NKRUMAH UDSM hii ingesaidia watu wengi kushiriki hapo bungeni kuingia ni balaa hadi upite hizo security checks umeshasahau point zote sababu ya usumbufu wa askari na karimjee inaingiza watu wachache sana kweli naona nia ya kushirikisha watanzania wengi kwny mchakato wa katiba
 
Hata siku moja huwezi kusikia manung'uniko ,maandamano,vita na vurugu palipo na haki................kila kitu kinaanzia na haki kutotendeka basi mambo mengine ni blabla tu za wanasiasa....................kwa hiyo tusidanganyane...
 
Nawasikitikia sana hao jamaa wanaowafukuza wananchi walioalikwa kwa mbwembwe jana na Mh. Job Ndugai, naibu spika! Wanaweza wakawafukuza tena hadi nyerere square, area C au chako ni chako hapo ddm. Lakini watayafukuzia wapi mawazo yao? Hata huko ndani ya ukumbi sitashangaa watakaopewa nafasi ya kuzungumza wakawa ni akina Wasira, Combani, Makamba and the like. Ila haitasaidia kitu. Mawazo na fikra zetu ndio zitaamua mustakabali wa nchi yetu maana tumeshaamua kwamba HAKUNA KULALA HADI KIELEWEKE
 
Back
Top Bottom