Mabinti wa kibongo na Oman

Kujiuza ni uamuzi wa mtu .

Wakati mwingine siyo uamuzi bidada, nimesoma stori kibao za watu wanaodanganywa kwa staili hii, wakifika huko wananyang'anywa all travel documents na wanakuwa at the mercy ya alowapeleka huko, wanafanyishwa ngono kwa kwenda mbele, kazi ya kuchora hina indeed, wonders shall never cease, na alivyo bado mbichi atagenerate wateja wa kutosha, fursa zipo hata Tanzania azichangamkie siyo lazima awe nje ya nchi.
 
mkuu hiko kitu ndio hata sisi kinatutia wasiwasi ila rafiki yake anapinga vikali sana kauli hiyo

So unategemea rafiki yake awaunge mkono?mkimkanya asiposikia mwacheni inaweza kuwa heri, ila shari ikimkuta ajue mlimueleza uamuzi wenu, so the ball is in her basket, after all she is an adult
 
Sina maelezo mazuri ya kukupa ila naomba msimruhusu kwenda Oman mtampoteza utu na thamani yake, hicho kinachompeleka huko hata mkikomaa hapa bongo kinawezekana pia
 
Huyu rafiki yake kwanini msimzabe vibao na kumfukuza kukanyaga kwenu?Anaenda kumuuza huyo!!!
mkuu hiko kitu ndio hata sisi kinatutia wasiwasi ila rafiki yake anapinga vikali sana kauli hiyo
 
Kujiuza ni uamuzi wa mtu .

SIO KWELI kwa wanaopeleka nje ya nchi maana wanalazimishwa, akifika ananyang'anywa passport na nyaraka zote na kupelekwa katika night clubs au kufungiwa kwenye mandaguro, ambako analazimishwa kufanya mapenzi na mtu atakayemchagua nk.


kwa waliopo dsm/nchini ni hiari yao
 

ushauri wangu msikubali kuenda huko, nasikia wana kitu wanaita gerejei, yaani ni madanguro wa wasichana wa aina zote wanapatikana huko na watu wanaenda kuzini nao, mshaurini asome. toeni taarifa ya siri immigration wafuatilie maisha na tabia za huyo jamaa ikibidi wamuondoe haraka nchini. nina mashahaka na uadilifu wake, mtu wa omani, anachora hina, ndio anatumia kuendesha maisha yake.

mshaurini binti yenu asome haya mambo yapo atayakuta tu.
 
oman ni kati ya nchi masikini pia duniani wa tz wengi wanacnfuse wakidhan nchi zote za waarabu utajiri ni bwere re nchi kama oman, yemen ni maskini kama sisi tu!!! so care should be taken kuliko kukurupuka!!
 
halafu we mdada embu tumia akili kweli mtu akulipie gharama zote za kusafiri na document zote halafu akapate faida kwa ndugu yenu kupaka wateja hina? ni faida gani huyo mdada atapata kwa gharama hizo?
 
kweli hii kitu ni risk sana ila huyo mwenzie ndo humwambii kitu

Kwa umri mdogo na elimu ndogo ya ndugu yenu huyo anayemng'ang'ania anataka akamfanye mradi. Kama mnampenda ndugu yenu mfukuzeni huyo kuwadi 'faster'
 
kwa nn asimchumue mdogo wake aje amchukue rafiki yake,mi naishi nje ya nchi hao madada mfoni huku ulaya ni kujiuza kwenye club za usiku na kufanyishwa ngono na wanyama na kinyumenyu
e na hawana dila wanatamani kurudi tz lakin passport washachukuliwa
 
Acha ubwege wewe, aliyekuambia Oman kuna shortage ya wanawake wanaojua kuchora hina ni nani? Huyo anaenda kuuzwa. wenyewe kwa wenyewe waarabu hairuhusiwi Ukahaba, lakini kwa wageni ni 'halal'. Jaribu ku-google tu uone nduguyo anaenda kufanywa nini, mfukuze huyo kuwadi haraka sana!

Hii ndio akili ya mbunge mwanamke kuwait, sidhani itakuwa tofauti sana na Oman:

"A Kuwaiti woman who once ran for parliament has called for sex slavery to be legalised - and suggested that non-Muslim prisoners from war-torn countries would make suitable concubines.

Salwa al Mutairi argued buying a sex-slave would protect decent, devout and 'virile' Kuwaiti men from adultery because buying an imported sex partner would be tantamount to marriage."

Mutairi claimed: 'There was no shame in it and it is not haram' (forbidden) under Islamic Sharia law.'
source:sex slaves kuwait
 
kweli hii kitu ni risk sana ila huyo mwenzie ndo humwambii kitu

Maamuzi ni ya familia au huyo mwenzie?
Huyo mwenzie hana ndugu wanaosota akawapeleka wakatoke au anampenda zaidi huyo mdogo wako?
Familia kama haijaridhishwa iseme NO! Bint akijifanya haelewi mrudisheni kwa wazazi wake huyo mwenzie amfate huko,amgharamie safari na huyo mdogo wako akishafunzwa na ulimwengu atarudi tu maana mchuma janga hula na wa kwao!!!
 
Akili za mbayuwayu changanya na zako, sasa hivi anatoroka huyo kama mtaamua kumkalipia bila kumwambia madhara yake.
 
mwaka jana niliskia report ya bbc wakisema wasichana wengi wa kiafrika wanaoenda uarabuni kwa ahadi za kutaftiwa kazi wanaishia kuwa mahausgeli na wengine wanatumikishwa kingono...wengine kwa hiari yao wanajiuza maisha yanapokua magumu..
 
Akili za mbayuwayu changanya na zako, sasa hivi anatoroka huyo kama mtaamua kumkalipia bila kumwambia madhara yake.

thats why nkaja hapa nipate hizo points za kumuelimisha madhara hayo
 
mwaka jana niliskia report ya bbc wakisema wasichana wengi wa kiafrika wanaoenda uarabuni kwa ahadi za kutaftiwa kazi wanaishia kuwa mahausgeli na wengine wanatumikishwa kingono...wengine kwa hiari yao wanajiuza maisha yanapokua magumu..

well said!
 
Hakuna kitu bora Kama msimamo hasa kwenye Tatizo Kama hili ni vyema wakati mwingine Kama w.familia kuchukuwa uamuzi mgum kwa manufaa ya ndugu yenu Kama kweli huyo rafiki anataka kumsaidia nduguyo kwanin asianze kuwasaidia wa familia yake kwanza. Dat fend z bad influence to ha Madhara yatakayo mpata nyinyi ndio mtakuwa wahangaikaji mchuma janga hula na wakwao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…