Ni hivi Tabrett, msilete mchezo kabisa na hiyo kitu, aisee muwe wakali kabisa.Kataeni kwa nguvu zote na huyo rafiki yake piga marufuku asionekane hapo.Huko hakuna kingine zaidi ya kujiuza katika umri huo.Watu wanalia kila siku,hata humu kuna ushahidi.Kazi kwenu.
mwanangu yaani ukoo unakaa kudiscuss kijana wa miaka 20 afanye nini!utamaduni wetu wa kulea vijana hadi miaka 30 ndio wawe na maamuzi yao utatupeleka pabaya sana hasa kwenye ulimwengu huu wenye mengi! Kama hajitegemei kimaamuzi wazazi waamue tu!Maana anayetaka kwenda nae ni rika moja maana yake na yeye haaminiki kimaamuzi vile vile!muda mwingine maamuzi tunayofanya yanaakisi uwezo wetu wa kufikiri pia
tumejaribu kumuelekeza katika hilo rafikiye kang'ang'ana kua hakuna kabisa hiko kitu na kinapigwa marufuku huko wako strict kuliko hata huku bongo
Mkuu omani kuna mtoto wa dada yangu alipelekwa kama mfanyakazi wa kuuza duka alipofikishwa kaambiwa kuwa duka limeibiwa na hatimae kawa mfanyakazi wa ndani kateswa kama nini ikabidi siku moja kapiga simu kwa kuiba ndipo dada kaenda kumchukua kuna wengine wanateswa sana na kufukuzwa na waishia kuwa watu wa kujiuza na nauli hana ya kurudi
ni hayo tu mwambie asiende huyo hajui yaliyoko huko anaona sifa kuwa kafika sifa lakini maisha yake siyo salama mijitu ya huko bado inaamini kuwa utumwa duniani hauwezi kuisha kwa waafrika
hivi kwa nini achukuliwe akafanye kazi huko wakati na huko kuna watu kama huku ujue kuwa huyo anapelekwa kwa matumizi yasiyo halali
Mkuu,
kwa uzowefu wangu na muda ambao nimeishi UAE. Nimeshuhudia wadada toka
mataifa mbalimbali wakiteseka kwa kinyanyasika sana tena wenye umri mkubw kuliko huyo dogo wako. Hakuna haja ya kumruhu kuja UAE pasipo mpango nadhubuti.
Habari za asubuhi wanajamvi,wanafamilia tumejikuta katika njia panda baada ya mdogo wangu wa kike(mtoto wa bamdogo) anaishi na wazazi wangu kua rafiki yake ambae alikua Oman anafanya kazi katika salon ya kuchora hina amekuja kumchukua ili waondoke wote wakajiunge katika kazi hiyo.Wanafamilia wote hakuna anayeafiki hilo suala ila yeye ndio amekomaa na huyo rafiki yake anajaribu kutushawishi kua hakuna tatizo atakua katika mikono salama,sisi tunahofia maana binti ndio ana 20 yrs hana professional yoyote ni form four leaver tu.Wanajamvi najua humu kunawenye uzoefu na Oman katika hili naomba mnisaidie kunifunua macho kweli hili jambo liko salama kwa binti huyu?
Mkuu...nitakupa honest opinion yangu..nimekutana na dada zetu wa kiafrica wengi mchana wanafanya kazi za kibinadamu usiku wanajiuza..kiukweli kama hakuna muelekeo usimuache aende..mimi naishi dubai na hili nimeliona na naaapa mwanangu wa kike hatoenda nchi za watu kwa mshahara wa milioni au milioni mbili.
Mkuu inaweza kua kuna kupaka hina ila vishawishi ni vingi na maisha ni ghali sana...
Nikiwa kama mtanzania nakuomba muelezedogo wenu anachotaka kimbilia its not worthy it all.
Kujiuza ni uamuzi wa mtu .
Wasiwasi wetu ni kua je itakua kweli ni hina tu au ndo mwamvuli wa kufanyia ufirauni mwingine!
muda meingi e mazingira yatalazimu kufanya hivyo...Kujiuza ni uamuzi wa mtu .