Mabalozi watatu waliomsindikiza Tundu Lissu uwanja wa ndege wanatuma ujumbe gani kwa Serikali?

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Wakati Tundu Lissu akiondoka nchini kwenda Ubelgiji kwa matibabu leo, amesindikizwa na mabalozi watatu ambao ni balozi wa Marekani, Ujerumani na Ubelgiji.

Washirika hawa watatu kwa hakika upo ujumbe wanaoutuma kwa serikali ya Tanzania.

Baada tu ya Tundu Lissu kuondoka nchini salama, balozi wa Marekani kwenye ukurasa wake rasmi wa Twitter ameonyesha kufurahishwa na tukio hilo. Aidha anasema kuwa Tundu Lissu anaelekea Ubelgiji kwa matibabu. "Nimefurahi kuwa hatimaye Tundu Lissu ameondoka salama kwenda Ubelgiji" amesema balozi huyo.

Tundu Lissu alibebwa ndani ya gari ya balozi wa Ubelgiji na msafara wao ulipita njiani kuelekea uwanja wa ndege bila kizuizi chochote kile.
 
Hao si wamesindikiza mke wao sasa shida iko wapi,
Ya Lisu muachie Lisu na ya serikari waiachie serikari,
Misheni yao imefeli hivyo tunawachora tu.
Serikari ina mambo mengi ya kufanya hivyo haina muda na mtu anyesindikizwa na watu wake.
Hao mabalozi itafika siku wataondoka wataiacha tanzania moja.
 
Tundu Lissu alibebwa ndani ya gari ya balozi wa Ubelgiji na msafara wao ulipita njiani kuelekea uwanja wa ndege bila kizuizi chochote kile.
89CF0E4B-7D93-49E3-8C20-BD8A4C5DF26E.jpeg
 
Hao si wamesindikiza mke wao sasa shida iko wapi,
Ya Lisu muachie Lisu na ya serikari waiachie serikari,
Misheni yao imefeli hivyo tunawachora tu.
Serikari ina mambo mengi ya kufanya hivyo haina muda na mtu anyesindikizwa na watu wake.
Hao mabalozi itafika siku wataondoka wataiacha tanzania moja.
Mnajifariji sana.Mkshakosea
 
Back
Top Bottom