Mabadiliko ya katiba yanukia: Mahakama kuanzisha Supreme Court, jengo limeshajengwa Dodoma

chiembe

JF-Expert Member
May 16, 2015
12,012
20,685
Katika hotuba yake, Mtendaji Mkuu wa Mahakama ameelezea kwamba ujenzi wa jengo la supreme court unaendelea. Bila shaka muda wowote katiba itafanyiwa marekebisho ili kuijumuisha mahakama hii, ambayo itakuwa mahakama ya juu kabisa, kwa Sasa mahakama ya juu ni mahakama ya rufani(court of appeal).

Haya ni marekebisho madogo tu ya katiba ambayo hayahitaji fedha nyingi, hata wale wa upande wa pili hawataenda kuomba fedha kwa wafadhili ili kupiga maneno na kula kuku.
 
Fuatilia hotuba ya uzinduzi wa makao makuu ya mahakama, Dodoma, kutakuwa na supreme court-court of appeal-high court-resident magistrates court-district court -primary court, endelea kunywa uji hapo ufipa
Wewe ni kilaza, mahakama ya rufaa ndio supreme court kwa Tanzania.
 
Unaleta ushabiki wa kipumbavu,hoja ni kuanzishwa Kwa supreme court,hayo mengine yanatoka wapi?Huwa hoja zenu zinakosa mashiko bila kuwahusisha hao upande wa pili kama unavyowaita!
Grow up!!
Kunywa maji mwanangu
 
Kina
Kinachojengwa Dodoma sio Supreme Court bali ni The Judiciary Headquarter Building" . Jengo la Mahakama ambalo ndani yake kutakuwa na Mahama Kuu, Mahakama ya Rufaa na Mahakama ya Juu (Supreme Court). Jengo moja lakini litakuwa na hizo mahama zote 3 in ONE HOUSE. Usanifu umezingatia itifaki za uendeshaji wa kesi kwenye hizo mahakama, na mahusiano ya utendaji kazi (seniority) kwa kila ngazi husika. Nimetoa ufafanuzi kwa kuwa nimewahi kuona usanifu wa jengo lenyewe (Architectural Drawings)
 
Hakuna mahakama ya juu katika katiba au mfumo wa mahakama Tanzania. Mahakama ya mwisho au ya juu kabisa au supreme ni mahakama ya rufaa.
 
Afadhali umenisaidia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…