Wanabodi,
Kama ilivyo kawaida yetu, wewe kama mwana JF, be the first to know kuwa ujio wa Lawassa kujiunga Chadema, unaandamana na mambo mengi mazuri, moja kubwa ni kuhama kwa Makao Makuu ya Chadema kwenye kijumba cha kupangisha pale Mtaa wa Ufipa Kinondoni Dar es Salaam, hadi kwenye moja ya majumba yenye hadhi inayolingana na Edward Lowassa.
Hali hii ni kufuatia hali iliyojitokeza jana, wakati Edward Lowassa alipofika Makao Makuu ya Chadema, mtaa wa Ufipa, kwa ajili ya kuchukua fomu ya kugombea urais kupitia Chadema, kufuatia umati mkubwa wa wafuasi wa Chadema kufurika kwa wingi hali iliyoleta shida na kero mtaa mzima, kutokana na location ya ofisi hizo zilipo, zilionekana ni kama kichochoroni!. Na hapo hao waliojitokeza ni wafuasi tuu wa Chadema, bado tsunami ya wafuasi wa Lowassa hawajatia timu!, wakitia timu kama hali ilivyokuwa uwanja wa Sheikh Amri Abedi, then nyumba zote huo Mtaa wa Ufipa, zinahatari ya kubomolewa kwa makundi ya watu!.
Kumbe ile ofisi ya Makao Makuu ya Chadema pale Ufipa ni nyumba ya kupanga!. Ukipiga hesabu ya jumla ya ruzuku yote ambayo Chadema imeishalipwa, ingetosha sana kujenga jengo la hadhi na mahali penye hadhi, na kama ni kupanga, hakukuwa na sababu kupanga kwenye kijumba kama kile hadi sasa Chadema ni chama kikubwa!. Hali hii ya Chadema kuendelea kuwepo kwenye kajumba hako, ni kufuatia upangaji mbovu wa vipaumbele vyake, hivyo kupelekea matumizi mabovu ya ruzuku, hali iliyopelekea Chadema kukumbwa na ukata siku zote, na kulazikika kuendelea kupanga kwenye kajumba kale pale Uswahili au Uzwazi Ufipa kwenye kabarabara ka uchochoro madimbwi mwamzo mwisho!.
Kufuatia Lowassa kuwa ni tajiri mkubwa, mwenye hadhi ya hali ya juu, huku akimiliki majengo lukuki, yenye hadhi, kwenye maeneo ya maana 'prime areas', ujio wake utapelekea Ofisi za Chadema kuhama uchochoroni, na kuhamia kwenye jengo la maana litakalo endana na hadhi ya Lowassa na tena haswa kwa kuzingatia Chadema ndicho kinakwenda kugeuka Chama tawala!.
Mabadiliko hayo chanya sio tuu kwa Chadema kumiliki jengo lake lenyewe, pia Chadema itamiliki kituo chake cha Redio na Televisheni pamoja na magazeti yake yenyewe, kwa sababu Lawassa hapo alipo tayari anamiliki Redio na TV!, hivyo sasa vitatumiwa na Chadema kwa kuanzia wakati mchakato wa umiliki rasmi wa vyombo vyake yenyewe ukiendelea!.
Ama kweli mgeni njoo, mwenyeji apone!.
Hongera sana Lowassa!.
Hongera Chadema.
Ikulu 2015 ni ya UKAWA!.
Mungu Ibariki Tanzania.
Pasco
Source ya Taarifa hii ni observation yangu binafsi.[/QUOTE
Kwani ukubwa wa jengo unauhusiano gani na ufanisi? Utajiri wa Lowasa sio wa CHADEMA, unadhani amepokelewa kwa sababu ni tajiri?