Elections 2015 Mabadiliko Chanya ya Ujio wa Lowassa: CHADEMA Kuhama Ufipa!, Kuwa Makao Yake, Kituo cha TV na Redio!

Ukipiga hesabu ya jumla ya ruzuku yote ambayo Chadema imekuwa ikipokea, na kulinganisha ruzuku hiyo imefanyia nini, utakubaliana na mimi, kuwa fedha hiyo, ingetosha kabisa kujenga jengo jingine kwenye eneo la kutosha. Hali hii imetokana na upangaji mbovu wa vipaumbele vyake, hali iliyopelekea matumizi mabovu ya ruzuku, kama yalivyofafanuliwa kwenye ripoti ya CAG.

Mabadiliko hayo chanya sio tuu kwa Chadema kumiliki jengo lake lenyewe, pia Chadema itamiliki kituo chake cha Redio na Televisheni pamoja na magazeti yake yenyewe, kwa sababu Lawassa hapo alipo tayari anamiliki by proxy wa familia kubwa ya media, yenye vituo vya Redio, TV na magazeti lukuki!, hivyo sasa pia vitatumiwa kuisupport Chadema kwa kuanzia tuu, wakati mchakato wa umiliki rasmi wa vyombo vyake yenyewe ukiendelea!.

Paskali

NB. Japo Pakali ni mwanachama wa chama cha siasa, na ni kada wa Chama cha Mapinduzi CCM, huyu ni kada mzalendo wa kweli wa taifa hili kwa kutanguliza mbele maslahi ya taifa, kazi yangu ni to tell nothing but the truth, with objectivity, impartiality and balance from all sides!.
Kushindwa kurusha mahojiano ya maalimu Seif pale Clouds tv ni salamu tosha kwa wapinzani kuwa tunakoelekea haitakuwa rahisi tena viongozi wa upinzani kualikwa na vituo vya habari vinavyomilikiwa na wanaccm.

Ikumbukwe pale Clouds media Rostam Aziz aliwahi kufanya uwekezaji wake na hata magazeti yake ya Mtanzania yameacha kuandika propaganda za Chadema baada ya Lowassa kuondoka.

Ni swala la muda tu habari za Mbowe na wapinzani wengine tutazisoma kupitia Tanzania Daima tu na hapa Jf.

Kwanini Chadema hamkuliona hili na kuanzisha luninga yenu kama wale akina Mwamposya na Mwingira?.....ni sehemu ndogo sana ya ruzuku ingefanya kazi hii.

Maendeleo hayana vyama!
Mkuu johnthebaptist, kiukwelihoja yako hii ni hoja ya muhimu sana, Chadema wana tatizo kubwa la kutokuona mbali, myopia, hivyo wanashindwa kupanga vipaumbele vyake. Angalia jambo muhimu kama hili, mimi niliwashauri lini katika uzi huu.
P
 
Wanabodi,

Kama ilivyo kawaida yetu jf, wewe kama mwana JF, una pata ile kitu inaitwa the jf advantage to "be the first to know" kuwa Chadema kuhama kwa Makao Makuu yake toka kwenye kale kajumba kalichopo Mtaa wa Ufipa, Kinondoni Dar es Salaam, ambako hakuna hadhi ya makao makuu ya chama kikuu cha upinzani, yatahama kutoka hapo Mtaa wa Ufipa hadi kwenye eneo jingine lenye hadhi na nafasi zaidi ili angalau kufanania!.
Hatimaye

This is good news. japo imepita miaka 8 since anticipating, hatimaye imekuwa kweli.
Hongera sana Chadema.
P
 
Mabadiliko hayo chanya ya ujio wa Lowassa sio tuu kwa Chadema kumiliki jengo lake lenyewe, bali pia Chadema itamiliki media zake yenyewe kikiwepo kituo chake cha Redio na Televisheni pamoja na magazeti yake yenyewe, kwa sababu Lawassa hapo alipo tayari anamiliki by proxy, familia kubwa ya media, yenye vituo vya Redio, TV na magazeti lukuki!, hivyo sasa pia vitatumiwa kuisupport Chadema kwa kuanzia tuu, wakati mchakato wa umiliki rasmi wa vyombo vyake yenyewe ukiendelea!.

Paskali
Japo ujio huu haukuleta matokeo tarajiwa lakini tujitokeze kwa wingi ule ule wakati wa kumuaga kama tulivyompokea wakati wa kumkaribisha.

Naendelea na My Tribute to this fallen hero, Mwamba wa Kaskazini, kwa kujikumbusha baadhi ya mabandiko yangu kumhusu shujaa huyu mpaka siku atakapo pumzishwa kwenye makao yake ya milele, let's celebrate the life and the times of Edward Lowassa.

RIP Shujaa Laigwanani Comred Edward Ngoyai Ole Lowassa,
Umepigana vita vilivyo vitakatifu, imani umeilinda.
Bwana alileta
Bwana ametwaa,
Jina Lake Lihimidiwe!.

Paskali
 
Ukipiga hesabu ya jumla ya ruzuku yote ambayo Chadema imekuwa ikipokea, ukajumlisha na zile fedha za Sabodo alizoipa Chadema kujenga ofisi za makao makuu zenye hadhi, na kulinganisha ruzuku hiyo imekuwa ikifanyia nini, utakubaliana na mimi, kuwa fedha hiyo, ingetosha kabisa kujenga jengo jingine la maana na lenye hadhi kwenye eneo la kutosha.
Jamaa huyu mpaka anaondoka, hakuwahi kupewa mrejesho wa fedha zake Chadema!.

BILIONEA SABODO AFARIKI DUNIA..

Bilionea na Mchumi maarufu nchini, Mustafa Jaffer Sabodo amefariki Dunia leo alfajiri akiwa nyumbani kwakwe, Masaki jijini Dar es Salaam.

"Mzee amefariki leo alfajiri akiwa nyumbani. Taratibu za mazishi zinaendelea na atazikwa katika makaburi yaliyoko mtaa wa Bibi Titi Mohamedi karibu na CBE," amesema Danstan.

Marehemu Sabado alizaliwa mkoani Lindi na alikuwa akifanya biashara katika nchi za Ufaransa, India, Kenya, Sudan, Nigeria, Zimbabwe na Tanzania.

Atakumbukwa kwa mchango wake ulioanzisha Mwalimu Nyerere Foundation National Lottery alipotoa msaada wa Sh milioni 800. Alihusika katika utoaji wa misaada kadhaa iliyohusisha kilimo, ujenzi wa visima na kusaidia wenye uhitaji.
Sabodo atazikwa leo saa 4:30 usiku.
Inna Lillahi wa inna ilaihi raji'un.
“We surely belong to Allah and to Him we shall return”
"Sisi sote ni wa Mola, na kwake tutarejea".

Paskali pia anakuaga!.
RIP Jaffar Sabodo.
 P
 
Back
Top Bottom