Maaskovu Vs. Makamba na mgongano wa Arusha

Huelewi unachosoma kwenye Biblia kwa kusoma peke yake,ila kwa msaada wa Roho Mtakatifu!

Wengi wanaosoma na kuruka ruka ndo wanao chukua maneno kwa ajili ya manufaa yao binafsi (kuangusha wengine)
 
Kwani Bibilia ina watu fulani wa kuitumia? Na sio kwa watu na Mataifa yote?
Ndugu yangu zomba,
Biblia ni mkusanyiko wa vitabu, maandiko,barua, funuo mbalimbali zilizoandikwa na mitume na manabii kabla ya Yesu Kristo kuzaliwa(agano la kale) na baada ya Yesu Kristo kuzaliwa(agano jipya). Ni wazi kuwa vitabu vya agano la kale vilitumiwa na wayahudi kama muongozo wao wa kiroho na kisheria.
Vitabu vya Agano jipya viliandikwa na mitume na wafuasi wa mwanzo na wa baadae(kama Paulo) wa Yesu Kristo, ukatumiwa na kusanyiko la wafuasi hao hata baada ya Yesu kufufuka na kupaa mbinguni, na ukawa mwongozo na imani yao kama jamii ya wafuata imani,ambao wakaitwa wakristo(katika matendo ya mitume).

Kwa kuwa Yesu Kristo (kama binadamu) ana mizizi ktk uyahudi, na historia ya ukombozi imeanzia tangu Musa na manabii, wakristo wakajumuisha vitabu vya agano la kale na lile jipya ktk msingi wa imani yao ambao ni kitabu kinachojulikana kama Biblia.

Ni kweli kabisa kuwa Biblia ni kwaajili ya mataifa yote(ndio maana kimeitwa 'Habari njema kwa mataifa yote'), lakini haina maana kuwa mtu yeyote anaweza akakichezea,kupotosha au kukinajisi. Bila shaka hii itakuwa ni ufedhuli na itazua hasira hasa kwa wenye kukiheshimu na kukiamini(naamini ni kwasababu hiyohiyo waislamu waligadhibika Quran tukufu zilipo tishiwa kuchomwa moto huko Marekani au pale mtu alipochora katuni ya kumkebehi Mtume Muhamad S.A.W). Maaskofu walichomkataza Makamba sio kuitumia Biblia, bali kuitumia kuhalalisha uovu au kuleta kejeli katika mambo ya imani au mambo ya msingi katika maisha ya watu.
 
huelewi wewe??? amekemea kutumia biblia kuhalalisha uovu! wake na wenzake na si vinginevyo
 
Hivi Makamba anajua kusoma na kuandika, mimi nadhani huwa anahadithiwa na watu mbalimbali hivyo vifungu vya Bible halafu anakwenda mtaani kubwabwaja.............
 
Amekuwa mtu wa kunukuu vipengele vya kitabu hiki kitakatifu na kutumia tafsiri anayopenda yeye,
mathalani kwenye moja ya nukuu zake anazosema kuwa bibilia inawataka watu kutii mamlaka zilizo kuu.
Hivi huyu kibabu hajui kuwa utii bila kufikiri ni utumwa?naomba cv yake hapa waungwana
 
Rest in peace, makamba

416351085_b2f9159d44.jpg
 
Nasikia kile kitoto alichopachika mimba wakati akiwa mwalimu mkuu, kalikuwa kakristo. Alikuwa anatumia biblia kukatongoza!
 
- ukiona viongozi wa taifa wanaanza ku-quote biblia badala ya katiba ya jamhuri, katika kuhalalisha vitendo vya serikali maana yake ni moja tu kwamba hao viongozi na serikali nzima ni mufilisi, wanahitaji kuondolewa mara moja!

william.

tangu uanze ku-comment kwenye jf mr malecela, leo ndio umeongea point. Usije ukawa mnafuatisha baba lakini maana yeye alisema wazi kuwa yule tahaira wa kike aitwae chatanda amekosa adabu. Namkubali baba yako kuliko wewe anytime
 
Ndo hayo Maaskofu wanakukatazeni !!!kwa akili ndogo uliyo nayo kujua watu wa mataifa kwa biblical context wewe huwezi elewa!! waingereza wanasema hivi'' no research no right to speak mimi naongeza no right to comment''you cannot be an authority to everything when it comes to intelectual thinking be it science or religious!!! nimesoma majibu yako kuhusu malipo ya DOWANS ulionekana kujibu kila hoja mimi nikafikiri wewe ni lawyer tena aliye specialize ktk international businnes leo hii unataka kuwa theologist yaani unaweza kujibu Maaskofu kwa kutumia Biblia,I think that is pathetic you cannot know it all!! Makamba type!!! Maneno mengi akili kidogo , tafakari kabla ujasema na jiulize je do I have enough knowledge on the subject matter at hand, If not keep your mouth shut!! there is no harm!! and your will have done a great service to you as a person and your readers . It is simply some piece of advice that is if your brain is still intact.
Sorry if I offended you.

Very well said. Thank you
 
Zomba ni tatizo,U lack self determination and actualization.Pia katk cognative domain yako jaribu ku Scann labda kuna virus wameingia ama Unamtindio wa ubongo+mawazo.
 
Maaskofu wa madhehebu ya Kikristu mkoani Arusha wamemkemea Katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Yusuph Makamba, kwa kuitumia Biblia takatifu kuhalalisha uovu; wakamtaka aache tabia hiyo mara moja.

Maaskofu hao wakiongozwa na Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini Kati, Thomas Laizer, aliyezungumza kwa niaba wenzake katika mazishi ya wahanga wa maandamano ya Arusha, alisisitiza kwamba wataendelea “kuikosoa serikali na chama chochote kile pindi kinapokosea.”

Kauli ya Makamba iliyowakera maaskofu hao, na ambayo amekuwa akiirudia mara kwa mara, ni ile aliyotumia kuwakejeli kwa kunukuu maandiko matakatifu ya Kurani na Biblia akisema “tiini mamlaka iliyo kuu.” Walisema ufahamu wa Makamba ni finyu katika kutafsiri maana halisi ya neno hilo.

“Kama serikali wameamua kutuvunjia heshima, basi wasimame kwenye majukwaaa kutetea uovu wao, na sisi tutasimama kwa ajili ya kupinga uovu wao, tuone Mungu atamsikia nani” alisema Askofu Laizer.

''Maaskofu wamesikitishwa na kauli yake na pia kauli ya Katibu wa CCM mkoa wa Arusha, Mary Chatanda kuwataka kuvua majoho na kuingia katika siasa kwani ni kuwavunjia heshima,'' alisema askofu Laizer.

Source: Tanzania Daima

Kwa kweli nilitegemea kauli hii ya viongozi wa dini wa Kikristo kuitoa muda mrefu. Makamba amekuwa akiitumia Biblia vibaya, na kwa muda mrefu kumekuwa na manung'uniko kutoka kwa wakristo jinsi Makamba ambavyo amekuwa akiitumia Biblia kuhalalisha uovu wake na wa serikali. Anavyoitumia, hakuna tofauti na shetani alivyotaka kumshawishi Yesu pale aliposema, 'Jirushe kutoka kwenye mnara huu mpaka chini maana imeandikwa kuwa malaika wa mbinguni watakudaka', na Yesu alimwambia ondoka shetani wewe maana imeandikwa pia usimjaribu Bwana Mungu wako.

Makamba anasema kuwa imeandikwa katika Biblia kuwa heshimuni Mamlaka maana mamlaka hutoka kwa Mungu lakini hajui ni mamlaka gani ambazo tuliambiwa tuziheshimu, na hajui pia ni mamlaka zipi, zilizopatikana kwa namna gani ndizo zinazostahili kuheshimika na kutambuliwa kuwa zinatoka kwa Mungu. Makamba ni shetani Mkubwa anayeikufuru Biblia Takatifu kuitumia katika kutenda uovu. Mbona Makamba hazungumzii wajibu wa kiongozi kwa watu anaowaongoza kadiri ya mafundisho ya Biblia? Makamba siyo tu mbumbu wa Biblia lakini pia ni adui mkubwa wa ukristo kwa kuufanya ukristo na Biblia vionekane ni imani inayosimamia uonevu na uovu. Tunakushukuru sana Askofu Laizer.
 
Nadhani maaskofu wako right to some extent on this. Sio vema viongozi wa kisiasa kutumia vitabu vya dini kwa minaajili ya malengo ya kisiasa. Nadhani ni kuchanganya dini na siasa wanakokukemea kila siku. Ila na maaskofu kwa makusudi au vinginevyo wana selective memory. Mbona walikuwa hawamkemei Makamba huyu huyu wakati anawatukana wazee wa kiislamu kwa BIblia na Quran hizo hizo tena akiwa katika shughuli za kanisa? Mbona hawakumkemea Kilaini wakati alipotoa ufunuo fake kuwa JK ni chaguo la Mungu? Au Mungu kabadili mawazo sasa anamtaka Slaa? Na huyo Mungu kaamua ku-overlook "fornication" ya PHD (Cannon Law). Looks like that god is troubled these days!
 
Is there any reason kubishana na huyo Zomba (nahisi ingekua Zoba) jamani? Mwacheni apayuke akichoka atanyamaza...ni wa kumhurumia tu!
 
Ukweli n kwamba Biblia ni kitabu cha wote. Lakini "wote" hapa ina maana kuwa kinasema na kila mtu, sio kwamba kila mtu ana uwezo wa kuifafanua. Hata sheria za nchi ni kwa ajili ya wananchi wote, lakini sio wote wenye mamlaka ya kutafsiri sheria ila mahakama. Kufasiri Biblia ni taaluma kubwa inayosomewa, somo la kufasiri Biblia huitwa "HERMENEUTICS." Na watu hupata hata Phd kwa hilo. Sasa Makamba amesoma wapi theolojia? Kwa taarifa yako wanatheolojia humnyamazia tu, lakini hufanya makosa mengi katika kutafsiri kwake, mojawapo ni hilo andiko lililonukuliwa.


Thank. Kula tano
 
Ukweli n kwamba Biblia ni kitabu cha wote. Lakini "wote" hapa ina maana kuwa kinasema na kila mtu, sio kwamba kila mtu ana uwezo wa kuifafanua. Hata sheria za nchi ni kwa ajili ya wananchi wote, lakini sio wote wenye mamlaka ya kutafsiri sheria ila mahakama. Kufasiri Biblia ni taaluma kubwa inayosomewa, somo la kufasiri Biblia huitwa "HERMENEUTICS." Na watu hupata hata Phd kwa hilo. Sasa Makamba amesoma wapi theolojia? Kwa taarifa yako wanatheolojia humnyamazia tu, lakini hufanya makosa mengi katika kutafsiri kwake, mojawapo ni hilo andiko lililonukuliwa.


Thanks.
Well articulated ndugu.
 
Back
Top Bottom