Maaskovu Vs. Makamba na mgongano wa Arusha

Facts1

JF-Expert Member
Dec 23, 2009
307
28
Maaskofu wa madhehebu ya Kikristu mkoani Arusha wamemkemea Katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Yusuph Makamba, kwa kuitumia Biblia takatifu kuhalalisha uovu; wakamtaka aache tabia hiyo mara moja.

Maaskofu hao wakiongozwa na Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini Kati, Thomas Laizer, aliyezungumza kwa niaba wenzake katika mazishi ya wahanga wa maandamano ya Arusha, alisisitiza kwamba wataendelea "kuikosoa serikali na chama chochote kile pindi kinapokosea."


Kauli ya Makamba iliyowakera maaskofu hao, na ambayo amekuwa akiirudia mara kwa mara, ni ile aliyotumia kuwakejeli kwa kunukuu maandiko matakatifu ya Kurani na Biblia akisema "tiini mamlaka iliyo kuu." Walisema ufahamu wa Makamba ni finyu katika kutafsiri maana halisi ya neno hilo.


"Kama serikali wameamua kutuvunjia heshima, basi wasimame kwenye majukwaaa kutetea uovu wao, na sisi tutasimama kwa ajili ya kupinga uovu wao, tuone Mungu atamsikia nani" alisema Askofu Laizer.


''Maaskofu wamesikitishwa na kauli yake na pia kauli ya Katibu wa CCM mkoa wa Arusha, Mary Chatanda kuwataka kuvua majoho na kuingia katika siasa kwani ni kuwavunjia heshima,'' alisema askofu Laizer.


Source: Tanzania Daima
 
Kwani Bibilia ina watu fulani wa kuitumia? Na sio kwa watu na Mataifa yote?
 
samahani alikuwepo kiongozi wa kiislam ktk mazishi hayo alietoa hotuba?


Nimefuatilia post zako nyingi, naanza kuhisi una ugonjwa mbaya uitwao udininisms. nakusaidia dawa jaribu kutafuta vitabu vya falsafa unaweza kupata nafuu au ukapona kabisa maradhi hayo. pia unaweza kumwona A. Mihanjo (phD) kwa msaada zaidi.
 
wakristo, una swali lingine?


Kwani Wakiristo ndio kina nani? Slaa yumo? Mbowe yumo?

Na wapi kwenye Bibilia iliposema "hiki ni kitabu cha wakiristo"?

Ukishindwa kujibu, kaa kimya! SHUT UP.
 
Kwani Wakiristo ndio kina nani? Slaa yumo? Mbowe yumo?

Na wapi kwenye Bibilia iliposema "hiki ni kitabu cha wakiristo"?

Ukishindwa kujibu, kaa kimya! SHUT UP.
Umeshajibiwa ni cha wakristo una jingine.
 
Kwani Bibilia ina watu fulani wa kuitumia? Na sio kwa watu na Mataifa yote?

Ndo hayo Maaskofu wanakukatazeni !!!kwa akili ndogo uliyo nayo kujua watu wa mataifa kwa biblical context wewe huwezi elewa!! waingereza wanasema hivi'' no research no right to speak mimi naongeza no right to comment''you cannot be an authority to everything when it comes to intelectual thinking be it science or religious!!! nimesoma majibu yako kuhusu malipo ya DOWANS ulionekana kujibu kila hoja mimi nikafikiri wewe ni lawyer tena aliye specialize ktk international businnes leo hii unataka kuwa theologist yaani unaweza kujibu Maaskofu kwa kutumia Biblia,I think that is pathetic you cannot know it all!! Makamba type!!! Maneno mengi akili kidogo , tafakari kabla ujasema na jiulize je do I have enough knowledge on the subject matter at hand, If not keep your mouth shut!! there is no harm!! and your will have done a great service to you as a person and your readers . It is simply some piece of advice that is if your brain is still intact.
Sorry if I offended you.
 
Ndo hayo Maaskofu wanakukatazeni !!!kwa akili ndogo uliyo nayo kujua watu wa mataifa kwa biblical context wewe huwezi elewa!! waingereza wanasema hivi'' no research no right to speak mimi naongeza no right to comment''you cannot be an authority to everything when it comes to intelectual thinking be it science or religious!!! nimesoma majibu yako kuhusu malipo ya DOWANS ulionekana kujibu kila hoja mimi nikafikiri wewe ni lawyer tena aliye specialize ktk international businnes leo hii unataka kuwa theologist yaani unaweza kujibu Maaskofu kwa kutumia Biblia,I think that is pathetic you cannot know it all!! Makamba type!!! Maneno mengi akili kidogo , tafakari kabla ujasema na jiulize je do I have enough knowledge on the subject matter at hand, If not keep your mouth shut!! there is no harm!! and your will have done a great service to you as a person and your readers . It is simply some piece of advice that is if your brain is still intact.
Sorry if I offended you.

Akili yako kubwa lakini hujajibu hoja.
 
Kwani Wakiristo ndio kina nani? Slaa yumo? Mbowe yumo?

Na wapi kwenye Bibilia iliposema "hiki ni kitabu cha wakiristo"?

Ukishindwa kujibu, kaa kimya! SHUT UP.

Ukweli n kwamba Biblia ni kitabu cha wote. Lakini "wote" hapa ina maana kuwa kinasema na kila mtu, sio kwamba kila mtu ana uwezo wa kuifafanua. Hata sheria za nchi ni kwa ajili ya wananchi wote, lakini sio wote wenye mamlaka ya kutafsiri sheria ila mahakama. Kufasiri Biblia ni taaluma kubwa inayosomewa, somo la kufasiri Biblia huitwa "HERMENEUTICS." Na watu hupata hata Phd kwa hilo. Sasa Makamba amesoma wapi theolojia? Kwa taarifa yako wanatheolojia humnyamazia tu, lakini hufanya makosa mengi katika kutafsiri kwake, mojawapo ni hilo andiko lililonukuliwa.
 
Maaskofu wa madhehebu ya Kikristu mkoani Arusha wamemkemea Katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Yusuph Makamba, kwa kuitumia Biblia takatifu kuhalalisha uovu; wakamtaka aache tabia hiyo mara moja.
Source: Tanzania Daima

- Ukiona viongozi wa taifa wanaanza ku-quote Biblia badala ya Katiba ya Jamhuri, katika kuhalalisha vitendo vya serikali maana yake ni moja tu kwamba hao viongozi na serikali nzima ni mufilisi, wanahitaji kuondolewa mara moja!

William.
 
- Ukiona viongozi wa taifa wanaanza ku-quote Biblia badala ya Katiba ya Jamhuri, katika kuhalalisha vitendo vya serikali maana yake ni moja tu kwamba hao viongozi na serikali nzima ni mufilisi, wanahitaji kuondolewa mara moja!

William.
well said!!! manake hii ni laana
 
WeWe W. J. Malecela nilifikiri una akili sana kutokana na jina lako< kumbe una pumba kumzidi yule orijino, ambae alig'ania kugombea ubunge mpaka akakataliwa kwenye kura za maoni. Si angestaafu toka alivyoachishwa kazi na Nyerere? hana haya, hata huyo mkewe mpya kakubalika, kuliko yeye.
 
Sasa Chadema kinazidi kujidhihiisha kuwa na chama cha kidini na hasa Ukatoliki ambao kasomea Slaa, walikuwa wapi kulaani kwa nguvu watu wa Pemba walipouwa kipindi wanaandamana? sio hawa walithubutu kusema kuwa CUF inapaswa kulaumiwa kwa kukataa kutii amri ya Polis? na huyu Kikwete walisema ni chaguo la Mungu, iweje leo awe chaguo la shetani? au kwa sababu kaondoa memorandum of understanding?
 
WeWe W. J. Malecela nilifikiri una akili sana kutokana na jina lako< kumbe una pumba kumzidi yule orijino, ambae alig'ania kugombea ubunge mpaka akakataliwa kwenye kura za maoni. Si angestaafu toka alivyoachishwa kazi na Nyerere? hana haya, hata huyo mkewe mpya kakubalika, kuliko yeye.

changia mada acha kumshambulia mtu hapa
 
Back
Top Bottom