Maaskofu waipinga CHADEMA...

Maaskofu waipinga CHADEMA...

hao ni maaskofu!sisi waamini ni chadema damu!
Ni kweli maana Askofu anapiga kura moja kama waumini wake!
Hata kama kweli aliyasema hayo ni kwamba ALIKURUPUKA kama wanavyokurupuka MAGAMBA wengine...!
CHADEMA HAIANZISHI kikundi BALI INAKIIMARISHA kilichopo!
Na kama Askofu hakulijua hilo angaliuliza kabla hajatamka...
Viongozi wengine bwana, damu ya CCM itawatokea puani...
 
mimi nashangazwa na utetezi wa cdm eti kwa kua ccm wana green guard then nao lazima wawe na kikundi kama green guard, red brigade huku wanakiri kwamba green guard ni kikundi kinacho fanya matendo ya kigaidi, sasa kama tunacho hicho kimoja do we need kingine? cdm should do things differently! why copy everything from ccm? in the end we will have ccmcdm or cdmccm! why should we have two ccms? viongozi wa cdm are you real sure mtachukua dola 2015? mtanisamehe for asking the same question so frequently maana kila nikiangalia bado hamjui expectation za waTZ! you simply don't know or hamjui kushika dola ni nini. you don't show any political maturity while we are two years away from you entering to magogoni! we need to see the other part of you! hii ya kila siku matamko, maandamano. mabomu n.k.... inatosha!
 
/QUOTE]

biblia inasema toa kwanza boriti ndani ya jicho lako ndipo utakapoweza kuona kibanzi kwenye jicho la mwenzako.
kkkt ina migogoro mingi hasa dodoma na bado hawajaweza kuimaliza wakiweza kulisafisha kidogo tu ndipo aje kwenye ulingo wa siasa inaonekana lowasa kamuachia mshiko huyo askofu wa kichina
 
bidhaa za kichina zimeingia madhabahuni(askofu wa kichina huyo kachoka kusoma biblia amuulize aliyesema kikwete ni chaguo la mungu yuko wapi?
 
Ni kweli maana Askofu anapiga kura moja kama waumini wake!
Hata kama kweli aliyasema hayo ni kwamba ALIKURUPUKA kama wanavyokurupuka MAGAMBA wengine...!
CHADEMA HAIANZISHI kikundi BALI INAKIIMARISHA kilichopo!
Na kama Askofu hakulijua hilo angaliuliza kabla hajatamka...
Viongozi wengine bwana, damu ya CCM itawatokea puani...

Aache Kutuzuga huyu Malasusa...kwani nani hajui kuwa FJP ni political wing ya The Muslim Brotherhood.. Similarly...CHADEMA ni political wing ya KANISA. Hivyo wasituzuge hawa jamaa.

Kwemwale.
 
Kila tamko la CDM huwa na impact kubwa sana, maana naona issue hii imeingia hadi makanisani!! kweli chama dume hiki.

Haya Maaskofu mbona hamuwakemei CCM wayafute makambi yao? na je vitendo vyote ambavyo CDM imekuwa ikifanyiwa na Green Guards mbona hamjavitolea matamko yenye msisitizo?

Hivi kuna tatizo gani mimi na familia yangu tukianza mazoezi ya karete ili kujilinda wenyewe!! ; hivi self-defence ni kukiuka katiba ya nchi.
 
Hivi we Askofu kama kweli unaijua kweli na unafanya mapenz ya Mungu basi hata Green Guard ungeiona...
 
Maaskofu wametoa angalizo kwa vyama vyote,hawajataja vyama.
Ni juu ya serikali Kurejesha amani na usalama wa raia wake kwa kuacha upendeleo na kutenda haki kwa vyama vyote vya siasa.
Serikali pia inapaswa kuendana na mabadiliko ya mahitaji ya wananchi wake,sio kukinzana na mahitaji yao kwa kutumia nguvu.

Sent from my BlackBerry 9380 using JamiiForums
 
Kwa sampuli yetu ya viongozi wa dini hata Yesu akirudi ataanza kuwanyooshea kidole kama ilivyokuwa mafarisayo na wakuu wa makuhani,wanashindwa kutenda haki wanakalia maslai,tendeni haki bhana
 
Askofu KKKT atahadharisha uanzishwaji vikundi vya ulinzi

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Dodoma, Amon Kinyunyu, amesema kitendo cha viongozi wa vyama vya siasa ya kuamua kujianzishia vikundi vya ulinzi wa kujilinda kwenye vyama vyao, ni ishara tosha ya kuhatarisha amani ya Taifa.

Askofu Kinyunyu amesema viongozi wa siasa wanaoanzisha vikundi vya namna hiyo ni kuashiria jinsi gani walivyokosa heshima kwa Mungu na kwa mamlaka ya serikali ambayo ina ulinzi na usalama unaolinda nchi kwa ujumla.

Alitoa kauli hiyo wakati wa hafla ya uzinduzi wa miradi ya mifumo ya miundombinu ya watoto ikiwamo ya maji, madarasa na vyoo vya kisasa iliyodhaminiwa na shirika la Compassion International Tanzania kwa kushirikiana na washirika wenza kutoka kwenye Makanisa ya Huduma ya Mtoto iliyofanyika katika viwanja vya Kanisa la Tag Miyuji mjini hapa.

Askofu Kinyunyu alisema kitendo cha vyama hivyo kuanzisha vikundi vya kujilinda, ni ishara ya kuleta machafuko ya amani ya nchi.

Pia alisema kitendo hicho kitawafanya vijana waliopo katika vyama hivyo kuendelea kuchukiana badala ya kupendana.

Alisema viongozi wa kisiasa hawana budi kutambua kuwa kwa kuanzisha vikundi hivyo ni kuzidi kujenga uhasama mkubwa utakaoiumiza jamii isiyohusika wakiwamo watoto, wanawake, wazee na walemavu.

“Hapa wanatakiwa kujua kuwa kitendo hicho ni ishara tosha inayoashiria kuanzisha vita ambayo washirika wakubwa ni vijana tunaowategemea kushika madaraka mbalimbali ya kiserikali na ya kisiasa,” alisema.

Askofu Kinyunyu amewataka viongozi wa vyama vya siasa kuheshimu amani iliyopo iliyobarikiwa na Mungu tangu kuumbwa kwa ulimwengu.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Compassion Intenrational Tanzania (CIT) hapa nchini, Mchungaji Joseph Mayala, alisema kitendo hicho ni sasa na uwekezaji kwa vijana wawe na roho ya ukatili badala ya upendo na amani.


Source: Home

NB:

..Askofu Mkuu wa KKKT Malasusa naye ametoa kauli inayoelekea kuwananga CDM.

..soma hapa chini:Home

Hujaelewa maana unabwabwaja tu Soma kwenye wekundu, Askofu anasema Vyama hivyo, siyo kimoja ni wingi. Anamaanisha Green Guard,Red Brigade na BLue Guard na vingine.
 
NI upuuzi kutuambia maaskofu wanasema nini au masheikh wanasema nini, kama wanajambo wawaambie waumini wao huko makasani na misikitini. Kwanza siasa na dini, waache mara moja.
 
Asanteni maaskofu, msg sent ila sidhani kama itafanyiwa kazi na hawa watu maana vichwa vyao vigumu sana.

Mpe Hongera sana ila kama mtu wa Mungu na anayetakiwa kuwaongoza watu watende haki awaambie hao anaowapigia debe waachane na Green Guard badala ya kufuatilia Chadema. Viongozi wa dini inabidi wakemee vitendo viovu vinavyofanywa na serikali iliyopo madarakani ili haki itendeke na si kuvifuatilia vyama vya upinzani ambavyo nia yake ni kuikosoa serikali hasa kwa suala la haki. Hakuna amani bila haki, kama wameshindwa kuwakemea viongozi serikalini hawana budi kuachia ngazi makanisani. Waangalie mifano katika Biblia-Eliya na serikali ya Ahabu 1Wafalme 17:1 na kuendelea, soma pia kuhusu manabii wengine kama Elisha (Wafalme), Samweli dhidi ya Sauli, Nathani dhidi ya Daudi (2Samweli 12:1-13) n.k. Kazi ya kiongozi kanisani ni kuonya si tu upinzani hata serikali iliyopo madarakani-Aache uoga, asimamie haki.
 
Yaani wewe sasa naona unajipalia makaa ya moto unawasema watumishi wa mungu bila woga na hofu
kanisa lilianzishwa kabla ya green guard. Walipaswa kukemea green guard kwanza. Inashangaza maaskofu kutoa matamko yenye harufu zote kuwa wamepewa mlungula na kuambiwa 'semeni hivi'
 
chdema walianza kuuwa siku nyingi sana ila kwa sasa wanataka kuhalalalisha mauji yao .

ni vema watu wa mungu kuyakemea mashetani haya yasiote mizizi kwenye jamii zetu.
 
Ni bora amesema wazi kwani akikaa kimya yatakuja mengine bure yasiyotarajika
 
Kauli ya maskofu siyo ya chadema tuu ni ya vyama vyote kwani ccm c wana green guard, au c haramu kwao wao wakianzisha kikundi cha kujilinda
 
JokaKuu inaonekana unapenda saana segere, wap huyu askofu kaitaja CDM, amesema vyama vya siasa..UMBEA M'BAYA SAANA....
 
Last edited by a moderator:
Kwani yeye ndo nani..! Busara haikutumika..!
Kulikua na green guard,blue guard kusikia cdm na nafasi ya kuhubiri amepata
 
Back
Top Bottom