Maaskofu waipinga CHADEMA...

Maaskofu waipinga CHADEMA...

Lakini massage anaitoa hapa huyu Askofu sio kwa CHADEMA pekee
Hii massage inaunganisha vyama vyote vya siasa
sasa wewe jokakuu ulimaanisha nini kuweka CHADEMA kwenye title ya hii thread
hope watu wengine wameshakukosoa
 
Nimepiatia hii thread 96 % hakuweza kuisoma na kuinyanyambua
kwa ufupi anachokisema huyu askofu ni sawa
haku taja jina la chama chochote kama mleta maada alivyopotosha watu humu
na watu wamechangia moja kwa moja kwa sababu ya title
naomba ma great thinkers tusijiangushe au kuliangusha hili jukwaa
tusome na kuelewa kabla ya kuchangia
asanteni
 
Askofu KKKT atahadharisha uanzishwaji vikundi vya ulinzi

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Dodoma, Amon Kinyunyu, amesema kitendo cha viongozi wa vyama vya siasa ya kuamua kujianzishia vikundi vya ulinzi wa kujilinda kwenye vyama vyao, ni ishara tosha ya kuhatarisha amani ya Taifa.

Askofu Kinyunyu amesema viongozi wa siasa wanaoanzisha vikundi vya namna hiyo ni kuashiria jinsi gani walivyokosa heshima kwa Mungu na kwa mamlaka ya serikali ambayo ina ulinzi na usalama unaolinda nchi kwa ujumla.

Alitoa kauli hiyo wakati wa hafla ya uzinduzi wa miradi ya mifumo ya miundombinu ya watoto ikiwamo ya maji, madarasa na vyoo vya kisasa iliyodhaminiwa na shirika la Compassion International Tanzania kwa kushirikiana na washirika wenza kutoka kwenye Makanisa ya Huduma ya Mtoto iliyofanyika katika viwanja vya Kanisa la Tag Miyuji mjini hapa.

Askofu Kinyunyu alisema kitendo cha vyama hivyo kuanzisha vikundi vya kujilinda, ni ishara ya kuleta machafuko ya amani ya nchi.

Pia alisema kitendo hicho kitawafanya vijana waliopo katika vyama hivyo kuendelea kuchukiana badala ya kupendana.

Alisema viongozi wa kisiasa hawana budi kutambua kuwa kwa kuanzisha vikundi hivyo ni kuzidi kujenga uhasama mkubwa utakaoiumiza jamii isiyohusika wakiwamo watoto, wanawake, wazee na walemavu.

“Hapa wanatakiwa kujua kuwa kitendo hicho ni ishara tosha inayoashiria kuanzisha vita ambayo washirika wakubwa ni vijana tunaowategemea kushika madaraka mbalimbali ya kiserikali na ya kisiasa,” alisema.

Askofu Kinyunyu amewataka viongozi wa vyama vya siasa kuheshimu amani iliyopo iliyobarikiwa na Mungu tangu kuumbwa kwa ulimwengu.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Compassion Intenrational Tanzania (CIT) hapa nchini, Mchungaji Joseph Mayala, alisema kitendo hicho ni sasa na uwekezaji kwa vijana wawe na roho ya ukatili badala ya upendo na amani.


Source: Home

NB:

..Askofu Mkuu wa KKKT Malasusa naye ametoa kauli inayoelekea kuwananga CDM.

..soma hapa chini:Home

Mbatikiwe watumishi wa Mungu kukemea upuuzi wa chadema
 
Maaskofu wengine cyo mkuu unakumbuka yule w a town alieshiriki kudanganya umma kwenda loliondo akaja kufa ugonjwA wa aibu
 
Mwambieni huyo Askofu aende Lumumba akachukue Buku 7

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums

Lazima nikufungulie kesi ya madai!! Umenisababishia kicheko kilichopelekea maumivu makali ya mbavu!!!!
 
Hicho kikundi kipo.kwenye katiba ya Chadema.Viongozi wa dini wafanye tafiti badala ya kupotosha waumini wao

Usihangaike na maaskofu wa aina hiyo. Hao ni wale ambao wanapata buku 7. Hatuwaruhusu kutumia madhabahu kuhubiri vya kwao badala ya kumhubiri Kristu. Walituambia tuombee amani hatukukataa, ingawa hawataji kuwa amani ni tunda la haki. Huwezi kumnyima au kumnyang'anya mtu haki yake halafu umwambie apige makoti kuombea amani. huo ni uzandiki wa hali ya juu.
 
Alipinga RG peke yake au pia na ya ccm GG ambayo ilishafanya maofu nyingi ya kuonea watu? Pia angetakiwa aende mbali zaidi ktk udhaifu unaofanywa na jeshi la polisi kwa 7bu jeshi la polisi haifanyi jukumu lake la kulinda raia mbali ikitekeleza mauaji kupitia maagiza ya serikali ya ccm.
 
Uyu Askofu yupo pale dodoma na naibu waziri wa ujenzi mh luwenge eti ni mzee wa kanisa kila akisoma matangazo lazima atie uccm wake..acheni kutuzingua nyie maaskofu tushachoka na sisi sasa...aah
 
mh nitaomba radhi endapo wanajf watanithibitishia kuwa cdm ndicho chama cha kwanza tz kuwa na ulinzi wake cause mi nimeondokewa imani kwa maaskofu hawa
 
Maaskofu wanaoheshimika ni
1 catholic
2 Luther
3 Anglican.....
Hao wengine ni wa kimarekani!
Mtu ana elimu ya 4m4 nae anajiita Askofu
 
angeenda mbali zaid kuwa hataki kuwaona waamini wa chadema kanisani kwake kama hilo hajaongelea bas kawa manipulated.
 
Maaskofu wanaoheshimika ni
1 catholic
2 Luther
3 Anglican.....
Hao wengine ni wa kimarekani!
Mtu ana elimu ya 4m4 nae anajiita Askofu
Mkuu hauko sawa sijui uko bar gani kwa sasa naona usha zigonga.
 
Back
Top Bottom