La Generale
Senior Member
- Sep 2, 2012
- 135
- 14
ahubiri watu waache umalaya na kuuza unga co kuingilia mambo ya msingi ambayo hayamuhusu....anaingia kichwakichwa...hawa ndo waliowah kusema za..fu n chaguo la MUNGU
Ok guys, here is a little bit of what has taken place out here between today and last Saturday.
View attachment 98324View attachment 98313View attachment 98315View attachment 98318View attachment 98321
Askofu KKKT atahadharisha uanzishwaji vikundi vya ulinzi
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Dodoma, Amon Kinyunyu, amesema kitendo cha viongozi wa vyama vya siasa ya kuamua kujianzishia vikundi vya ulinzi wa kujilinda kwenye vyama vyao, ni ishara tosha ya kuhatarisha amani ya Taifa.
Askofu Kinyunyu amesema viongozi wa siasa wanaoanzisha vikundi vya namna hiyo ni kuashiria jinsi gani walivyokosa heshima kwa Mungu na kwa mamlaka ya serikali ambayo ina ulinzi na usalama unaolinda nchi kwa ujumla.
Alitoa kauli hiyo wakati wa hafla ya uzinduzi wa miradi ya mifumo ya miundombinu ya watoto ikiwamo ya maji, madarasa na vyoo vya kisasa iliyodhaminiwa na shirika la Compassion International Tanzania kwa kushirikiana na washirika wenza kutoka kwenye Makanisa ya Huduma ya Mtoto iliyofanyika katika viwanja vya Kanisa la Tag Miyuji mjini hapa.
Askofu Kinyunyu alisema kitendo cha vyama hivyo kuanzisha vikundi vya kujilinda, ni ishara ya kuleta machafuko ya amani ya nchi.
Pia alisema kitendo hicho kitawafanya vijana waliopo katika vyama hivyo kuendelea kuchukiana badala ya kupendana.
Alisema viongozi wa kisiasa hawana budi kutambua kuwa kwa kuanzisha vikundi hivyo ni kuzidi kujenga uhasama mkubwa utakaoiumiza jamii isiyohusika wakiwamo watoto, wanawake, wazee na walemavu.
"Hapa wanatakiwa kujua kuwa kitendo hicho ni ishara tosha inayoashiria kuanzisha vita ambayo washirika wakubwa ni vijana tunaowategemea kushika madaraka mbalimbali ya kiserikali na ya kisiasa," alisema.
Askofu Kinyunyu amewataka viongozi wa vyama vya siasa kuheshimu amani iliyopo iliyobarikiwa na Mungu tangu kuumbwa kwa ulimwengu.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Compassion Intenrational Tanzania (CIT) hapa nchini, Mchungaji Joseph Mayala, alisema kitendo hicho ni sasa na uwekezaji kwa vijana wawe na roho ya ukatili badala ya upendo na amani.
Source: Home
NB:
..Askofu Mkuu wa KKKT Malasusa naye ametoa kauli inayoelekea kuwananga CDM.
..soma hapa chini:Home
wakati Cuf wanaanzisha blue guard Kadinal Pengo alijitokeza na kulaani vikali kuwa ni jambo litahatarisha amani,
tangu vijana wake wa chadema waseme wana andaa kambi za red guard yupo kimya kama hayupo
nawapongeza maaskofu wa KKKT kwa kua fair walipinga kwa CUF na sasa wamepinga kwa CHADEMA .....ila nawalaumu kwa kutopinga green guard ya CCM.
sawa vyama vyote lakini baada ya kisikia red brigade ikingali vingine vilishakuwepo.ndio maana imani ya dini inashuka kila sikuHujaelewa maana unabwabwaja tu Soma kwenye wekundu, Askofu anasema Vyama hivyo, siyo kimoja ni wingi. Anamaanisha Green Guard,Red Brigade na BLue Guard na vingine.
JokaKuu inaonekana unapenda saana segere, wap huyu askofu kaitaja CDM, amesema vyama vya siasa..UMBEA M'BAYA SAANA....
Sijui kwanini wanashindwa kufanya kazi walioitiwa na kujiingiza kwenye siasa wasiyoiweza. Kama kweli wangekua wanaweza kufanya kazi zao vema nadhani nchini hata rushwa isingekuwepo. Hawa walikua wanatumiwa hata Enzi za Yesu na ndio maana walikemewa sana makuhani.Alitakiwa kwenda mbali zaidi ya hapo kama ameamua kuacha altare na kujiingiza kwenye siasa.
Alitakiwa avitaje vikundi kwa majina, vilianza lini, na vinayemtumikia ni nani!.
Ni ukosefu wa umakini kulaumu vikundi vya ulinzi huku akiacha vacuum ya ulinzi katika vyama, wakati anajua wazi yanayotendeka na walinzi rasmi-Polisi.
Huyu alitakiwa aombwe aongelee suala la Mwangosi kwanza, ndipo athubutu kulaani vikundi vya ulinzi.
Hapa ndiyo utajua mipaka ya kazi hizi inamaanisha nini!
Umenikumbusha nyuma kidogo ule mlipuko wa bomu uliotokea kanisani arusha Askofu Fulani hata sio jimbo lake kakurupuka sijui alipewa hela eti mlipuko sio wa kigaidi. Nilistuka sana ujue , nikajiuliza kwanini hakukaa kimya na kuachia wahusika wafanye kazi yao. Yaani aliniudhi nikaona hata police haina kazi tena kumbe askofu anawafahamu walipuaji. Sijui kanisa linaelekea wapi. Pia nakumbuka Enzi zile Lowasa aliposimama/stop uwaziri kulikua na slogan ya ufisadi mpaka makanisani , hata Rostam nakumbuka alitoa mchango wa fedha kwenye kanisa flani waumini wakaja juu hawataki fedha za mafisadi. Sasa hawa hawa leo kila kukicha wanapokea pesa za wale waliowapinga kipindi kile. Kiukweli binafsi inaniuma sana viongozi wa kanisa wanapojiingiza kwenye siasa kinafiki, ndio kinafiki kwanini hawasimamii haki.....mara nyingine nikiwasikiliza hawa maaskofu napata kichefuchefu....i hate these kinds of hypocritical church leaders.....wanachangia sana hawa kwa yanayotokea TZ ya leo.....maana wanaacha kufanya yale wanayotakiwa na kujiingiza nje ya mipaka ya majukumu yao.....ndio maana makanisa siku hizi yamekua kimbilio la wanasiasa wasaka madaraka....wanawahonga hawa maaskofu uchwara (kwa mtaji wa sadaka)ili kufanikisha hila zao.....its so sad yaani....
wazi kabisa...mimi nakwambia wanaoharibu nchi hii ni viongozi.....kwenye sekta zote.....ziwe za kisiasa...au hata kidini.....na raia wa TZ kwa kweli ni wavumilivu sana....maana kama raia wangekua na uwezo wa kusimamia maadili wengeweza....lakini unapomkuta kiongozi wa dini anasimama anaendekeza maswala ya kifisadi....au kujiingiza kwenye maswala ya siasa za maji taka....alafu hapo hapo anasimama na kujifanya kukemea..kwa kweli hata raia inawawia ngumu kujishughulisha na mapambano ya uchuro (mfano ufisadi)...maana wanajifunza na kuona kutoka kwa viongozi wao(wa kidini au kisiasa).....Watu siku hizi hawana role model leaders (wawe wa kisiasa...wawe wa kidini)...ni tatizo kubwa hili TZ.........Umenikumbusha nyuma kidogo ule mlipuko wa bomu uliotokea kanisani arusha Askofu Fulani hata sio jimbo lake kakurupuka sijui alipewa hela eti mlipuko sio wa kigaidi. Nilistuka sana ujue , nikajiuliza kwanini hakukaa kimya na kuachia wahusika wafanye kazi yao. Yaani aliniudhi nikaona hata police haina kazi tena kumbe askofu anawafahamu walipuaji. Sijui kanisa linaelekea wapi. Pia nakumbuka Enzi zile Lowasa aliposimama/stop uwaziri kulikua na slogan ya ufisadi mpaka makanisani , hata Rostam nakumbuka alitoa mchango wa fedha kwenye kanisa flani waumini wakaja juu hawataki fedha za mafisadi. Sasa hawa hawa leo kila kukicha wanapokea pesa za wale waliowapinga kipindi kile. Kiukweli binafsi inaniuma sana viongozi wa kanisa wanapojiingiza kwenye siasa kinafiki, ndio kinafiki kwanini hawasimamii haki
Pengine wanata wawe marais. Ukiisimamia haki utapewa heshima tuu hata kama wewe ni mpagani. Hawa viongozi wetu wa dini wanalewa heshima na unyenyekevu wanaopewa na waumini wao mpaka kujihsi wao ni miungu watu, nachukia unafiki.Watu wengine sijui nini mbona green guard ipo muda mrefu hawakuwahi kusema?tatizo la kuchanganya dini na siasa ni hatari kweli