Maaskofu waipinga CHADEMA...

Maaskofu waipinga CHADEMA...

wazi kabisa...mimi nakwambia wanaoharibu nchi hii ni viongozi.....kwenye sekta zote.....ziwe za kisiasa...au hata kidini.....na raia wa TZ kwa kweli ni wavumilivu sana....maana kama raia wangekua na uwezo wa kusimamia maadili wengeweza....lakini unapomkuta kiongozi wa dini anasimama anaendekeza maswala ya kifisadi....au kujiingiza kwenye maswala ya siasa za maji taka....alafu hapo hapo anasimama na kujifanya kukemea..kwa kweli hata raia inawawia ngumu kujishughulisha na mapambano ya uchuro (mfano ufisadi)...maana wanajifunza na kuona kutoka kwa viongozi wao(wa kidini au kisiasa).....Watu siku hizi hawana role model leaders (wawe wa kisiasa...wawe wa kidini)...ni tatizo kubwa hili TZ.........
Wana bahati sana wangeongoza kipindi cha agano la kale sijui kama wange-survive . Manake kipindi kile ukileta unafiki au kosa dogo tu kama alilofanya Musa basi adhabu pale pale. Na pia washukuru mno watz tuko poa sana wanatunyanyasa lkn aa tunamwachia Mungu. Tena na hawa viongozi wa dini wanaongoza kwa ufisadi unadhani ukikosa ada ya mtoto shule wanakusaidia hawa . Wanasahau kua kila jpili unatoaga sh 200 wewe na familia yako yote na bado michango ya jumuia . Tumewanyamazia tu wanadhani hatuelewi/ hatujui kama wanatunyonya na wameanzisha mara fungu la kumi n.k. Viongozi wa dini acheni siasa fanyeni kazi mliyoitiwa na kama mnataka kutetea wananchi basi simamieni haki
 
Askofu si nabii na si malaika kama wako neutral angemaliza kutoa maoni yake kuhusu huundwaji wa red briegad ya cdm angeshutumu hata green guard iliyoazishwa na chama cha ccm angeeleweka sana
 
Mmmh......kama kujilinda dhambi basi hiyo kali.Kwanini tunafunga milango tunapolala?.......nataka kujiunga jamani na hicho kikundi cha kujilinda.
 
Wana bahati sana wangeongoza kipindi cha agano la kale sijui kama wange-survive . Manake kipindi kile ukileta unafiki au kosa dogo tu kama alilofanya Musa basi adhabu pale pale. Na pia washukuru mno watz tuko poa sana wanatunyanyasa lkn aa tunamwachia Mungu. Tena na hawa viongozi wa dini wanaongoza kwa ufisadi unadhani ukikosa ada ya mtoto shule wanakusaidia hawa . Wanasahau kua kila jpili unatoaga sh 200 wewe na familia yako yote na bado michango ya jumuia . Tumewanyamazia tu wanadhani hatuelewi/ hatujui kama wanatunyonya na wameanzisha mara fungu la kumi n.k. Viongozi wa dini acheni siasa fanyeni kazi mliyoitiwa na kama mnataka kutetea wananchi basi simamieni haki
..watanzania ni raia wapole na wavumilivu sana...na ndio maana wanaonewa kwenye kila nyanja ya maisha yao....wamebaki kumwachia Mungu tu mambo.....utawasikia hata baadhi ya raia wadai haki siku hizi wanaposhindwa wanabaki kusema wanamwachia Mungu... maana wakisema wanaambiwa watapigwa....na wanapigwa haswa...inauma.....
 
Mmmh......kama kujilinda dhambi basi hiyo kali.Kwanini tunafunga milango tunapolala?.......nataka kujiunga jamani na hicho kikundi cha kujilinda.
..hao viongozi wa dini wenyewe kwenye taasisi zao na majumbani kwao wamejiwekea ulinzi mkali......tena siku hizi ambazo wao nao wanapigwa mabomu ndio kabisa.....leo wanakuja na kauli hizi za kinafiki....utawaelewaje hawa viongozi....kama si minafiki mikubwa.....
 
..hao viongozi wa dini wenyewe kwenye taasisi zao na majumbani kwao wamejiwekea ulinzi mkali......tena siku hizi ambazo wao nao wanapigwa mabomu ndio kabisa.....leo wanakuja na kauli hizi za kinafiki....utawaelewaje hawa viongozi....kama si minafiki mikubwa.....

Si ndo hapo sasa.......
 
..hao viongozi wa dini wenyewe kwenye taasisi zao na majumbani kwao wamejiwekea ulinzi mkali......tena siku hizi ambazo wao nao wanapigwa mabomu ndio kabisa.....leo wanakuja na kauli hizi za kinafiki....utawaelewaje hawa viongozi....kama si minafiki mikubwa.....
Tena bola na wao wanapigwa pengine watapata akili. Yaani mimi wamenitoka sijui ndio ujeuri umenizidi yaani hata niwaonapo siwanyenyekei kama zamani sanasana wananitia hasira tu
 
Askofu si nabii na si malaika kama wako neutral angemaliza kutoa maoni yake kuhusu huundwaji wa red briegad ya cdm angeshutumu hata green guard iliyoazishwa na chama cha ccm angeeleweka sana
Yap hata mimi ningemuona wa maana lkn yuko biased hivi ndio inayotia hasira
 
Gamba huyu Askofu!! Leo hii ndio anaona vikundi vya ulinzi vinahatarisha AMANI alikuwa wapi kutoa kauli iyo wakati CCM walipoanzisha GREEN GUARD?
 
Wakati green guard inapigiwa kelele mbona hamkusema?nawasifu sana Chadema,yaani mtego wao unazidi kunasa wanafiki wengi!
 
Mimi ni mkristo na ni muumini wa KKKT na ninasali usharika wa Arusha Mjini Kati lakini kwa maneno ya askofu huyu yananifanya niamini moja kwa moja askofu huyu katoka nje ya maagizo na maneno ya vitabu vitakatifu na kutekeleza mashinikizo ya wanasiasa ikiwamo ccm kwa maslahi binafsi.

Ombi langu kwa askofu huyu ni ajitathmini kwa mara nyingine na afanye toba ya kweli aepeke hukumu ya dhambi hii kubwa aliyoifanya ya kupotosha kondoo wa Mungu.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Exoud mamuya poleni na deni la ciridor spring mkuu. Maaskofu wengine ndio tabu ya watanzania
 
kwa moshi na arusha ni hao red brigade ni makundi ya majambazi wataongozwa magenge ya uhalifu ya uwizi wa magari na mauaji ya Lema yaliyokuwa yanatikisa miji hiyo
Askofu alisema nini
kuhusu haya nayo. Nauliza hivi kwa kuwa inaonekana umeandika kwa mlengo
fulani ambao una upendeleo. Nimeshindwa kujua kama hiyo Slant ni ya
Askofu? au ni ya Mwandishi. Kasema lipikuhusu Haya
 
Askofu KKKT atahadharisha uanzishwaji vikundi vya ulinzi

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Dodoma, Amon Kinyunyu, amesema kitendo cha viongozi wa vyama vya siasa ya kuamua kujianzishia vikundi vya ulinzi wa kujilinda kwenye vyama vyao, ni ishara tosha ya kuhatarisha amani ya Taifa.

Askofu Kinyunyu amesema viongozi wa siasa wanaoanzisha vikundi vya namna hiyo ni kuashiria jinsi gani walivyokosa heshima kwa Mungu na kwa mamlaka ya serikali ambayo ina ulinzi na usalama unaolinda nchi kwa ujumla.

Alitoa kauli hiyo wakati wa hafla ya uzinduzi wa miradi ya mifumo ya miundombinu ya watoto ikiwamo ya maji, madarasa na vyoo vya kisasa iliyodhaminiwa na shirika la Compassion International Tanzania kwa kushirikiana na washirika wenza kutoka kwenye Makanisa ya Huduma ya Mtoto iliyofanyika katika viwanja vya Kanisa la Tag Miyuji mjini hapa.

Askofu Kinyunyu alisema kitendo cha vyama hivyo kuanzisha vikundi vya kujilinda, ni ishara ya kuleta machafuko ya amani ya nchi.

Pia alisema kitendo hicho kitawafanya vijana waliopo katika vyama hivyo kuendelea kuchukiana badala ya kupendana.

Alisema viongozi wa kisiasa hawana budi kutambua kuwa kwa kuanzisha vikundi hivyo ni kuzidi kujenga uhasama mkubwa utakaoiumiza jamii isiyohusika wakiwamo watoto, wanawake, wazee na walemavu.

“Hapa wanatakiwa kujua kuwa kitendo hicho ni ishara tosha inayoashiria kuanzisha vita ambayo washirika wakubwa ni vijana tunaowategemea kushika madaraka mbalimbali ya kiserikali na ya kisiasa,” alisema.

Askofu Kinyunyu amewataka viongozi wa vyama vya siasa kuheshimu amani iliyopo iliyobarikiwa na Mungu tangu kuumbwa kwa ulimwengu.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Compassion Intenrational Tanzania (CIT) hapa nchini, Mchungaji Joseph Mayala, alisema kitendo hicho ni sasa na uwekezaji kwa vijana wawe na roho ya ukatili badala ya upendo na amani.


Source: Home

NB:

..Askofu Mkuu wa KKKT Malasusa naye ametoa kauli inayoelekea kuwananga CDM.

..soma hapa chini:Home

Mkuu sijui malengo yako lakini huwatendei haki "Maaskofu"! Hii uliyotoa hapa ni kauli binafsi ya "Askofu Amon Kinyunyu" na hujaonesha popote kwamba yeye ni "msemaji wa maaskofu"!!!
 
mimi nashangazwa na utetezi wa cdm eti kwa kua ccm wana green guard then nao lazima wawe na kikundi kama green guard, red brigade huku wanakiri kwamba green guard ni kikundi kinacho fanya matendo ya kigaidi, sasa kama tunacho hicho kimoja do we need kingine? Cdm should do things differently! Why copy everything from ccm? In the end we will have ccmcdm or cdmccm! Why should we have two ccms? Viongozi wa cdm are you real sure mtachukua dola 2015? Mtanisamehe for asking the same question so frequently maana kila nikiangalia bado hamjui expectation za watz! You simply don't know or hamjui kushika dola ni nini. You don't show any political maturity while we are two years away from you entering to magogoni!


vip babako yupo? Tunataka mlinzi wa ofis za cdm,huku zinavunjwa na nyaraka kuibwa! Huna aibu mjinga wewe,twende polis tuombe ulinz wa ofis? Chambua alichosema mbowe,red brigade ipo inaimarishwa kukabiliana na hila zenu.
 
kanisa lilianzishwa kabla ya green guard. walipaswa kukemea green guard kwanza. inashangaza maaskofu kutoa matamko yenye harufu zote kuwa wamepewa mlungula na kuambiwa 'semeni hivi'

Mimi naamini huu ni mwendelezo wa propaganda za wahuni - CCM!
Haiingii kabisa akilini huyo askofu akemee uanzishwaji wa vikundi vya kujihami dhidi ya hujuma zinazofanywa na CCM na washirika wao dhidi ya CHADEMA.
Hivi askofu huyo anaishi hapa nchini au ughaibuni? Ni kweli kabisa hafahamu CCM Ina Jeshi la kuteka, kutesa na kuua wote wenye mawazo tofauti na wao?
Hapa ndipo ninapoungana na mchangiaji mmoja aliyesema inawezekana Askofu huyo amehongwa na vibakauchumi hawa CCM ili kutoa tamko la namna hiyo, tamko linalofhalilisha hadhi yake.
Kama ni kukemea angefanya hivyo kwa CCM ambayo kwa miango kadhaa sasa ina Jeshi la kulinda uhalifu wao.
 

Attachments

  • ImageUploadedByJamiiForums1374268635.322842.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1374268635.322842.jpg
    81.6 KB · Views: 56
  • ImageUploadedByJamiiForums1374268674.807263.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1374268674.807263.jpg
    56.7 KB · Views: 51
  • ImageUploadedByJamiiForums1374268709.677697.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1374268709.677697.jpg
    57.6 KB · Views: 54
  • ImageUploadedByJamiiForums1374268741.688941.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1374268741.688941.jpg
    19.8 KB · Views: 50
  • ImageUploadedByJamiiForums1374268764.771291.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1374268764.771291.jpg
    34.1 KB · Views: 42
Back
Top Bottom