Kumbe watu wengine utaendelea kuwaona wana busara mpaka hapo watakapoongea kitu...
Mkuu hapa watu si wanaweka kila kitu wazi. Si uwataje tu?
Naona ndugu Gaijin umeegemea sana katika Udini na kushindwa kujadili hoja.Tamko likitolewa na Baraza la Maaskofu na tulichokipata toka gazeti hilo la majira ni story ya mwandishi(mhariri) na baadhi ya nukuu chache tu.Kumbuka kuwa kilichoandikwa sio tamko bali ni habari ambayo mhariri ametumia taaluma yake kuhakikisha kuwa habari yake hailaumu serikali wala CUF.
Katika paragraph ya sita serikali ililaumiwa na Maaskofu kwa kukiona chama cha CUF kama waasi na kulazimika kutumia jeshi la Polisi kuwaua.Ukisoma vizuri paragraph ya sita utagundua kuwa mhariri alitumia taaluma yake vizuri kuepuka uchochezi kati ya Maaskofu na Serikali pamoja na gazeti la Majira na serikali.Nanukuu paragraph ya 6
"Baraza pia limesema kuwa Watanzania wengi hawajajua mwelekeo wa demokrasia ya siasa za vyama vingi ambayo husababisha wengine kuona kuwa kutokukubaliana au kuhitilafiana katika jambo Fulani la kisiasa ni uasi au uadui"
Ukiichambua hii paragraph utajionea kabisa kuwa CUF hawakukubaliana na matokeo ya Urais wa Zanzibar wa Oktoba mwaka 2000.Kwa mtaji huo wakaanzisha maandamano huko Zanzibar na kwa hilo basi serikali wakawaona kuwa CUF ni maadui au ni waasi.Siku zote kukabiliana na waasi lazima utumie jeshi lako na lazima waasi wauawe na ndivyo ilivyotokea.
Kwa hiyo Gaijin lazima ufahamu kazi ya mhariri na kutofautisha Tamko na habari.Napenda kuhitimisha kuwa Maaskofu waliwalaumu serikali baada ya mauaji ya January 26 na 27,2001.Kama ushauri ungefuatwa na serikali basi mauaji ya Arusha yasinetokea
hitimisho;
a) Maaskofu walitoa tamko mwaka 2001.
b) Tamko hilo lilikemea kilichotokea.
Hoja ilikuwa maaskofu hakukemea. Safari hii wamekemea. Sasa hoja ya nyongeza ni kwa nini hawakukemea vikali. Sidhani kama hoja ya nyongeza ina mshiko kwa sasa. Cha msingi walikemea na wakshauri. Serikali haikusikiliza ushauri wao kwa hiyo safari hii wameikemea zaidi. Hata kama walikuwa upande wa serikali then basi kwa kitendo hicho kurudiwa wana kila sababu ya kutoitetea serikali zaidi. Tusubiri kama CUF watapigwa tena tuone kama maaskofu wataitea serikali. Lakini CUF na wao wapigwe kwa kuonewa sio wafanye ukaidi ili wapigwe wategemee kutetewa na maaskofu na watu wengine! Waandamane kuhusu Dowans tujiunge nao. Wakipigwa na maaskofu wakikaa kimya ukweli utajulikana!
Mkuu wewe ni mwanasheria na nina uhakika hata siku moja hautoweza kuwasilisha utetezi kama huu based on on extracts kama zile kwenye attachment. Bandiko hili linaonyesha kwamba an expression of sympathy rather than a condemnation ya mauaji yaliyotokea.
Gaijin ametanabaisha vizuri tu, bandiko hili linazidi kuwakaanga maaskofu.
Ila ni bora hii mijadala ya nani kafanya hivi, nani kasema vile, fulani akampinga ifungwe. Viongozi wote wa dini ni bora warudi kwenye nyumba zao za ibada na wakaliombee taifa hili amani na dhambi walizochangia kuzileta za ubaguzi, dharau na kejeli.
It was refreshing kusoma gazeti la Mwananchi wikiendi hii iliyopita ambapo viongozi wa dini hizi za Abraham waliungana kumetetea ajuza aliyekuwa anataka kuporwa ardhi yake na Halmashauri ya Njombe. Hii ilionesha jitihada za pamoja za kutetea wanyonge na kujenga social cohesion na sio kubomoa kama baadhi ya rhetoric za sasa zinavyohatarisha
Hivi mnambembeleza wanini mwacheni aendelee kuamini anavyoamini kwani atawafanya nini wakristo au atafanya nini, watu wakorofi wanaopenda maneno wako hivyo huwa hawaridhiki.Gaijin hapa jf tuliaminishwa kuwa maaskofu hawakutoa tamko. Sasa kesi imebadilika ni kuwa walitoa tamko jepesi. Unaona kuna mtu anajaribu kuilisha jamii sumu ili watu waone kuwa maaskofu wanafanya kazi ya kusahihisha maovu anapokuwepo kiongozi mwislamu lakini ikiwa ni mkristo wako kimya. Je huu ni ukweli?? Inawezekana ni kama wahalifu sugu wafanyavyo anakujeruhi halafu anakuwahi polisi.
Hujui maana ya tamko ina maana waislamu mliposema mnataka vyeo nusu kwa nusu lilikuwa onyo na kwa nani.Hilo siyo tamko/onyo ila niushauri ..hapo hamna tamko watoe tamko wakati kiongozi ni mwenzao lol thubutu tunawjua kwa unafiki
hitimisho;
a) Maaskofu walitoa tamko mwaka 2001.
b) Tamko hilo lilikemea kilichotokea.
Hoja ilikuwa maaskofu hakukemea. Safari hii wamekemea. Sasa hoja ya nyongeza ni kwa nini hawakukemea vikali. Sidhani kama hoja ya nyongeza ina mshiko kwa sasa. Cha msingi walikemea na wakshauri. Serikali haikusikiliza ushauri wao kwa hiyo safari hii wameikemea zaidi. Hata kama walikuwa upande wa serikali then basi kwa kitendo hicho kurudiwa wana kila sababu ya kutoitetea serikali zaidi. Tusubiri kama CUF watapigwa tena tuone kama maaskofu wataitea serikali. Lakini CUF na wao wapigwe kwa kuonewa sio wafanye ukaidi ili wapigwe wategemee kutetewa na maaskofu na watu wengine! Waandamane kuhusu Dowans tujiunge nao. Wakipigwa na maaskofu wakikaa kimya ukweli utajulikana!
je baada ya tamko hilo 2001 (jepesi kama baadhi ya watu wanavyotaka tuamini) kuna yoyote alitamka kuwa waache kujihusisha na siasa?
Hilo siyo tamko/onyo ila niushauri ..hapo hamna tamko watoe tamko wakati kiongozi ni mwenzao lol thubutu tunawjua kwa unafiki
Hivi mnambembeleza wanini mwacheni aendelee kuamini anavyoamini kwani atawafanya nini wakristo au atafanya nini, watu wakorofi wanaopenda maneno wako hivyo huwa hawaridhiki.
Huwa hamkosi cha kulalamika ukileta hili ukajibiwa unazusha hili. Tumeshawazoea nyie!