Hulka ya waafrika wengi ni familia kuzaa watoto wengi ambao wanaweza kuwa na timu kamili ya mpira wa miguu (first eleven), hayo ndiyo maendelo ambayo FaizaFoxy anayatetea. Malezi ya watoto hao na kuwaandaa kimaisha ndo kiinimacho, hoja ambayo wanashangaa wanafunzi wameigeuka serikali na kuwa na migomu kila kukicha papo hapo serikali kutoa utetezi dhaifu kwamba wanasiasa ndio wachochezi, kwani hao wanafunzi hawana akili haki gani hawatendewi na serikali?
Jedwali hilo halina mantiki ya maendeleo bali ni kuwavika watanzania kilemba cha ukoka. Unapoulizwa maswali ya msingi wa waliobobea katika nyanja za upembezi wa falsafa na utendaji wa uongozi kwa nini taifa tangu lina tatizo la umeme tangu upate uongozi, halafu kiongozi anajibu kwamba tumeongeza megawaiti kadhaa ambazo hazitoi umeme, na tena mnataka nieuke kuwa wingu ninyeshe mvua kujaza bwawa la Mtera ili tupate umeme, hili ni jibu linalotoka kwa kiongozi wa nchi mwenye uchungu na watu wake na FaizaFoxy anatetea kwa nguvu zote hadi mishipa kumtoka kichwani.