Maandamano ya kumlaani Spika Makinda

Maandamano ya kumlaani Spika Makinda

Tuko

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2010
Posts
11,180
Reaction score
7,355
Najua yapo mambo mengi ya kuandamana kwa sasa. Hata hivyo mi nadhani hili la bunge kuendeshwa ki-hovyo hovyo na Spika Makinda ni kubwa na jambo la hatari sana kwa maendeleo ya taifa letu. Nawashauri CHADEMA, na wote wanaokerwa na mama huyu, wafanye maandamano nchi nzima au sehemu kadhaa za nchi, kulaani uendeshaji mbovu wa bunge unaofanywa na spika. Ingawa najua haitafanya aondolewe madrakani, naamini itamoa msg, na itamfanya ajue kuwa anachokifanya bungeni kinawaudhi wengi. Mi nadhani kwa sasa anadhani kuwa hajashtukiwa kuwa anaendesha bunge visivyo, so akiona maelfu wameandamana kumlaani, atapata funzo fulani/

------------------------------------------------------------------------------------
------------------------------------------------------------------------------------

UPDATE

Nimefuatilia kwa karibu jinsi mama huyu anavyoendesha kikao cha bajeti, na ukisoma taarifa ya jinsi anavyomkingia kifua Pinda, naona bado haya maandamano hayaepukiki.
 
Hata wewe waweza anzisha hayo maandamano, tutakua nyuma yako.
 
Makinda ukiona adui yako ana lalamika basi ongeza zaidi kasi ya jambo hilo unalofanya! Mama Makinda endelea hivyo hivyo na msimamo wako huo!
 
saivi mtaanzisha kila kitu kuona nyuma yake kuna wajinga wangapi!
Mi sio moja wao
 
Najua yapo mambo mengi ya kuandamana kwa sasa. Hata hivyo mi nadhani hili la bunge kuendeshwa ki-hovyo hovyo na Spika Makinda ni kubwa na jambo la hatari sana kwa maendeleo ya taifa letu. Nawashauri CHADEMA, na wote wanaokerwa na mama huyu, wafanye maandamano nchi nzima au sehemu kadhaa za nchi, kulaani uendeshaji mbovu wa bunge unaofanywa na spika. Ingawa najua haitafanya aondolewe madrakani, naamini itamoa msg, na itamfanya ajue kuwa anachokifanya bungeni kinawaudhi wengi. Mi nadhani kwa sasa anadhani kuwa hajashtukiwa kuwa anaendesha bunge visivyo, so akiona maelfu wameandamana kumlaani, atapata funzo fulani/

Wanaounga mkono pendekezo hili waseme "Ndiyooooooooo"
Wanaopinga waseme "Siyoooooooooo"

Ahsante sana kwa kunisikiliza...

Taja madhambi yake kwanza ndio tuone kuna umuhimu wa kuandamana ama la. Pengine inawezekana kumwandikia barua tu na akaelewa kuliko maandamano
 
Anakula na kujaza vyoo tu,hana anachotusaidia 80% maskini wa taifa hili
 
Ninaunga mkono hoja.
Nafikiri nchi hii inahitaji maombi. Sehemu nyeti kama bunge mnamuweka mama anayechemka hivyo...asiyejiamini na kibaraka wa chama ni hatari sana kwa maendeleo ya taifa hili sio tu linaendelea, lakini kwa mtazamo wangu mimi limekoma kuendelea kwa muda mrefu.

Tutaendelea kuwa Highly indebted poor country kwa sababu uendeshaji wa mambo ya muhimu yanatawaliwa na miongozo ya maveterani wa chama ambao kwa ktumia science ndogo, uwezo wao wa kufikiria umeshakoma...wangepaswa kubaki nyumbani walee wajukuu.
 
Mwanamke mpumbavu huivunja nyumba yake kwa mikono yake mwenyewe mwache BINTI KINDA aivunje CCM kwa mikono yake mwenyewe
 
saivi mtaanzisha kila kitu kuona nyuma yake kuna wajinga wangapi!
Mi sio moja wao
wabunge wenyewe ndo waandamame sisi tutawapima wao hatukumchagua makinda tuliwachagua wabunge!
 
hao wabunge ndo watetezi wake, walimchagua wao na ndo mana wanalindana. Ikipigwa kura wanaomkataa watazidiwa na wanaomkubali. Sina hakika kama kuna mbunge hata mmoja wa CCM akiambiwa aandamane kumwondoa/kumpinga spika atafanya hivyo.
wabunge wenyewe ndo waandamame sisi tutawapima wao hatukumchagua makinda tuliwachagua wabunge!
 
naunga mkono hoja 7x70......atakayepinga basi ajipinge yeye na mtazamo wake kabla ya kuupinga wangu..naunga hoja kwa maslahi ya taifa na wala mimi sio mwanasiasa.....



Ninaunga mkono hoja.
Nafikiri nchi hii inahitaji maombi. Sehemu nyeti kama bunge mnamuweka mama anayechemka hivyo...asiyejiamini na kibaraka wa chama ni hatari sana kwa maendeleo ya taifa hili sio tu linaendelea, lakini kwa mtazamo wangu mimi limekoma kuendelea kwa muda mrefu.

Tutaendelea kuwa Highly indebted poor country kwa sababu uendeshaji wa mambo ya muhimu yanatawaliwa na miongozo ya maveterani wa chama ambao kwa ktumia science ndogo, uwezo wao wa kufikiria umeshakoma...wangepaswa kubaki nyumbani walee wajukuu.
 
soma hiyo habari utaelewa kwanini haya yanatokea

Menopause is a stage in life when a woman stops having her monthly period. It is a normal part of aging and marks the end of a woman's reproductive years. Menopause typically occurs in a woman's late 40s to early 50s.
What are the symptoms of menopause?

Early symptoms of menopause among others include
  • Emotional changes (irritability, mood swings, mild depression) :angry::frown:
  • Sleeplessness
 
Makinda ukiona adui yako ana lalamika basi ongeza zaidi kasi ya jambo hilo unalofanya! Mama Makinda endelea hivyo hivyo na msimamo wako huo!
Nahisi kama ulihusika kumtuma awe spika! Kwakuwa hasimamii sheria za bunge ila za waliomtuma
 
haina haja ya kuandamana inaonekana mama bado hajaiva vizuri tumpe muda hadi bunge lijalo atakuwa amepata experience zaidi
 
Huyu mama atakuja kuwa ni Kigingi cha sisiem maana waliomuweka hapo (mafisadi) wameanza kupambana na sisiem......cdm tuvute subira
 
Back
Top Bottom