Papa D
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 752
- 182
Unajua Tanzania sheria inasema kitu tofauti na mambo yanatendwa tofauti. Fikiria sheria inasema Chama cha Siasa kinapotaka kufanya mkutano au kuitisha maandamano kitoe taarifa kwa maandishi (siyo kuomba ruhusa) kwa kamanda mkuu wa polisi wa eneo husika katika muda usiopungua saa 48. Kama CDM wametoa taarifa kadiri ya matakwa ya sheria, na mpaka siku ya mkutano au maandamano inafika ndo polisi wanaibuka na taarifa za kiintelijensia, kasoro ipo kwa nani? Bahati mbaya kwa yale yaliyotokea Arusha, polisi hawakutoa kizuio kwa maandishi bali aliibuka mtu mwingine anayazuia kwa kutumia TV(siyo maandishi) na wala hakuwa kamanda wa polisi wa eneo husika. Hivyo, Tanzania bado mambo hayajakaa sawa.
Ndugu!!
Tambua jambo moja kwamba:- Dalili moja wapo ya umaskini ni watu kutofuata sheria. Kwa hivo sishangai kuona serikali yenyewe inavunja sheria kwani ni halali kwa nchi isiyopiga hatua kama tulivyo Tanzania!